Mila potofu hazina nafasi katika ukuaji wa uchumi

Mila potofu hazina nafasi katika ukuaji wa uchumi

Joined
Apr 9, 2022
Posts
66
Reaction score
32
IMG-20220916-WA0004.jpg
Mtandao wa Jinsia Tanzania (TGNP) umesema kuwa mila potofu hazina nafasi katika uchumi endelevu.

Akiendesha program kwa wadau mbalimbali waliofika kuchangia jana Dar es Salaam mmoja wa wawezeshaji wa mada Jane Msigita amesema uchumi jumuishi wa kaya baadhi ya wanawake wanaweza kuwa hawajui kile ambacho wanachangia hali inayopelekea mwisho wa siku wanakuwa hawatambuliki katika mchango wa kaya.

"Mila potofu hazichangii uchumi jumuishi hazina nafasi katika uchumi endelevu ," amesema Misigita.
IMG-20220916-WA0007.jpg


Msigita aliwataka wachangiaji kuchangia mada hiyo kwa upana kwa kulenga fursa za shughuli jumuishi katika jamii.

Aliongeza kusema kuwa katika kulenga shughuli hizo jumuishi ata katika sehemu nyingi za masoko shughuli nyingi zenye fursa zimekuwa zijifanywa na wanaume.

Naye afisa program mwandamizi mtandao wa jinsia Tanzania (TGNP) zainabu mmay amesema kuwa usawa wa jinsia,desturi,mitazamo,imani ni kikwazo pekee cha kufikia uchumi jumuishi na maisha endelevu.

Ameongeza kuwa pamoja na mambo hayo jamii imeelezwa kuna uwezekano wa maisha ya wanafamilia kama taasisi za kindoa kuishi vibaya na kusababisha malezi mabovu kwa watoto.
 
Back
Top Bottom