Milion 10 inatosha kuanzisha biashara ya Baa?

Milion 10 inatosha kuanzisha biashara ya Baa?

Milion 10 inatosha kuanzisha biashara ya Baa? Uzuri wa biashara hii unaweza fanya popote budget yangu ni mil 10 ambayo itajumuisha TV 3, friji, viti, meza, jiko, wafanyakazi 3 wa kuanzia, mziki mkubwa (sijui bei yake) ingependeza kama kuna watu wanafanya biashara waje watoe uzoefu wao.
Tuma nikuelekeze
 
Mkuu mimi nna Liquor Store nlianza kwa mtaji la 7Million. Kikubwa n Business Location tu
Huko nyuma nimeeleza pia, nimewahi ifanya hii biashara hamn kitu nisichokijua kuanzia mtaji wa vinywaji, jinsi ya kupata wahudumu, kuongeza mauzo,kuvutia wateja n.k... Mimi nilifungua na 6mil lakin haikuwa bar, baadae nikaongezea mapooltable na African slots Machines mkoani huko.
 
, 😂😂😂😂... Wanaweka chupa ya hennessy tupu au sio alf mteja akiiagiza????
Pombe kali ni hennesy peke yake??
Hennessy ikiwa tupu si inaonekana ni tupu.
Kama wewe ni mteja tu wa kawaida hizi mbishe huwezi kuelewa.

Ila bars za mjini ujanja mwingi. Ukiwa kolo utasubili upate hizo 50M ili ufungue bar uswekeni wakati wenzio hiyohiyo 10M anapiga kazi.
 
Ila ukifungua jithidi biashara yako iwe business oriented .

Maana biashara ya bar huwa hazichanui
 
Biashara haihitaji kuuliza uliza ata kama una laki unaweza fanya Biashara ukapata faida ukakuza Biashara , kama kuna kitu umewaza kufanya wewe fanya haraka mkuu.
umeongea vizuri sana huna baya hongera kwa mawazo chanya hata bilionea Mengi (R.I.P) aliwai kusema watu wengi wanafail kabla ya kuanza.
 
Samahani, unaonekana una kiburi na dharau na unapenda kubishana na hutaki ushauri!

Tuanzie hapa kwenye mziki 'heavy duty', hapa nilivyokuelewa unataka disco kwa kifupi unataka wenye bar wengine waufyate!

Chukua hiyo milioni kumi nenda nayo pale congo (Kariakoo) ulizia full package ya disco sound bei ya chini ni kiasi gani! Kitachobaki kafungulie bar!
Aiseeh[emoji23][emoji23]
 
Milion 10 inatosha kuanzisha biashara ya Baa? Uzuri wa biashara hii unaweza fanya popote budget yangu ni mil 10 ambayo itajumuisha TV 3, friji, viti, meza, jiko, wafanyakazi 3 wa kuanzia, mziki mkubwa (sijui bei yake) ingependeza kama kuna watu wanafanya biashara waje watoe uzoefu wao.
TV ni lazima uweke 3?
 
Back
Top Bottom