Milioni 20: Wastani wa kiasi cha fedha ambacho mwanamuziki Diamond huingiza kwa siku

Milioni 20: Wastani wa kiasi cha fedha ambacho mwanamuziki Diamond huingiza kwa siku

mr gentleman

JF-Expert Member
Joined
Aug 1, 2012
Posts
3,222
Reaction score
4,689
Maneno mengi sana yamesemwa kuhusu kiasi cha fedha alichonacho Naseeb Abdul a.k.a Diamond Platnumz na vile vile unaweza kumuita Chibu Dangote au Baba Tiffah, na wengine kufikia hatua ya kusema anaweza kuwa ndiye msanii tajiri Afrika Mashariki kwa sasa.
Inasemekana kwamba, kwa kuangalia yote anayoyafanya msanii huyo unaweza kuwa na mwanga kiasi fulani wa kujua anaingiza kiasi gani.
Diamond Platnumz, kwa siku anaingiza wastani wa Shilingi milioni 20 za Kitanzania kutokana na kupakuliwa kwa nyimbo zake zilizoko kwenye mitandao: Kumbuka hii ni pembeni kabisa na shows anazofanya au malipo anayopokea kutoka kwenye makapuni anayoyafanyia matangazo kama Vodacom, Coca Cola, DSTV, Red Gold na NMB. Mpaka hapo utaamini sasa ule usemi wake wa siku zote kwamba muziki ni biashara! Na wasanii wengine hawana budi kumuiga Diamond Platnumz, wawe na wivu wa maendeleo na sio kutamani kumshusha alipo sasa.
Baadhi ya makampuni yanayofanya kazi na Diamond Platnumz:-


source swahilitimes. com
 
Mnajua nyie wapambe ndio mnawaingizaga watu mkenge...mkipiga mayowe namna hii TRA akija kutaka kodi manake hela zote hizi ni kipato na hivyo lazima alipie kodi..sasa afisa TRA akimzukia kwa ajili ya kodi..wakati mwingine unakuta ni uongo tu kama huu mnakimbia tena kuja kulalama humu humu...mil 20 kwa siku manake ni mil 140 kwa wiki atakua nanawazidi mastaa wengi wa EPL nmanake...
 
Kuna uongo mwingi hapa yaani diamond kila siku nyimbo zake zina download kila siku sawa Na video zake kila siku watu wanaangalia sawa yaani kama ni viewer milion 1 kila siku milion 1 anaingiza hela lakini sio kila siku sawa inategemea angekuwa anapata ela hiyo kila siku asingekuwa anafanya matangazo ya tomato
 
Vjana wanatoa mapov sana.... million ishirini ya Zimbabwe..
 
Tatizo la africa na tanzania hakuna uwazi huko majuu ukitaka kujua networth ni rahisi kwa sababu data zipo. Sasa figisu ni nyingi sana kiasi wengine wanahoji huyu msanii wetu biashara yake ni muziki tu? Maana wanaimba wengi ila pesa anaonekana kuwa nazo yeye. [HASHTAG]#inawezekana[/HASHTAG]
 
Million ishirin per day .... si mchezo.... Team chibu kazini....
 
Thubutu, hivi unadhan 20mil ni pesa ndogo kama alivyosema yule mama kuwa ni pesa ya mboga tu!?
 
Hakuna kitu kama hicho,we unadhani 20mil ni mchezo?basi itakuwa anamzidi mpaka pogba
 
Kuna uongo mwingi hapa yaani diamond kila siku nyimbo zake zina download kila siku sawa Na video zake kila siku watu wanaangalia sawa yaani kama ni viewer milion 1 kila siku milion 1 anaingiza hela lakini sio kila siku sawa inategemea angekuwa anapata ela hiyo kila siku asingekuwa anafanya matangazo ya tomato
umeambiwa hayo ni mapato yake "kwa wastani" sio fixed, yaani jumla gawanya kwa idadi ya siku, muwe mnaelewa kwanza kabla ya kucoment
 
Kuna uongo mwingi hapa yaani diamond kila siku nyimbo zake zina download kila siku sawa Na video zake kila siku watu wanaangalia sawa yaani kama ni viewer milion 1 kila siku milion 1 anaingiza hela lakini sio kila siku sawa inategemea angekuwa anapata ela hiyo kila siku asingekuwa anafanya matangazo ya tomato
Sijui unaelewa maana ya wastani? tuanzie hapo kwanza!
 
Back
Top Bottom