Millioni 5 ninaweza kufanya biashara ipi?

Walnut Creek

JF-Expert Member
Joined
Mar 17, 2009
Posts
5,830
Reaction score
6,315
Wajameni nina 5M ninataka izunguke ilinipate japo pesa ya kulipia mtoto ada bila kubangaiza.
Msaada wenu wa mawazo nitauheshimu sana na kama nikifanikiwa na idea ya mtu baada ya miaka miwili au mitatu sitamsahau japo kwa zawadi ya shukurani.

Mwenzenu kwenye matatizo na raha.
 
Inategemea na sehemu ulipo:
(1)Binafsi ningekushauri ufungue duka la spare za pikipiki kwa mtaji huo almost utapata unit atleast kumi za vipuri mhimu kulingana na sehemu husika.
2) Jikite kwenye kilimo cha matikiti maji. Anza na ekari mbili kwa mtaji wa 2M. Ukitaka mchanganuo wa kilimo hiki nitakuelekeza hapahapa jukwaani.
 
Jaribu kuangalia pia uwezekano wa kufungua duka la nafaka za vyakula mbali mbali kaa vile mchele n.k. ambavyo unaagiza au unavifuata Dubai. Nimewahi kusikia hii nayo ina faida kubwa sana ila sina details.
 

Mkuu tuelekeze hapa tupo wengi
 
Jaribu kuangalia pia uwezekano wa kufungua duka la nafaka za vyakula mbali mbali kaa vile mchele n.k. ambavyo unaagiza au unavifuata Dubai. Nimewahi kusikia hii nayo ina faida kubwa sana ila sina details.

mkuu Nafaka Dubai, italipa kweli hii?..kumbuka kuna mchele mwingi na mtamu sa unatoka hapa nchini tena kwa bei nzuri!!
 
Waliokuwa wanazungumza hili nami nikiwepo walidai bei ya kule ni poa ukilinganisha na bei za nchini pamoja gharama za usafirishaji faida ni ya kutosha tu.

mkuu Nafaka Dubai, italipa kweli hii?..kumbuka kuna mchele mwingi na mtamu sa unatoka hapa nchini tena kwa bei nzuri!!
 
Jaribu kuangalia pia uwezekano wa kufungua duka la nafaka za vyakula mbali mbali kaa vile mchele n.k. ambavyo unaagiza au unavifuata Dubai. Nimewahi kusikia hii nayo ina faida kubwa sana ila sina details.
Haiwezekani we utakuwa mzee wa rivasi :A S 11: Mchele from Dubai to TZ. mhh!!!
 

mkuu Naomba tufahamishe juu ya kilimo cha matikiti.
 

Mkuu naona watu wengi sana wamejikita kwenye kuhamasisha kilimo cha tikiti lakini hawa zungumzii kuhusu upatikanaji wa soko lake.Vipi wewe una zungumziaje soko la tikiti? Ni la uhakika? Na je ni wapi lipo au kwako wewe huwa wanakuja kuchukua shambani?
 
mkuu Nafaka Dubai, italipa kweli hii?..kumbuka kuna mchele mwingi na mtamu sa unatoka hapa nchini tena kwa bei nzuri!!
kwenye biashara inawezekana mkuu. Haujaona kuna sukari,cement kuku nk vinatoka nje na vinauzwa hapa kwa bei poa zaidi!. Kuna jamaa yangu anachukua bia za Heineken South Africa analeta hapa tz na kuuza jumlajumla. Amesema pamoja na kulipia kodi zote bado anabaki na faida nzuri.
 
Waliokuwa wanazungumza hili nami nikiwepo walidai bei ya kule ni poa ukilinganisha na bei za nchini pamoja gharama za usafirishaji faida ni ya kutosha tu.

mh! Inamaana kule mavuno ni makubwa kuzidi huk.., au ni mchele wa kutengeneza huo mkuu?
 
Cjui upo wapi ndugu but tafiti bajaji kwa ulipo inauzwaje fany cost and benefit analysis kwa hela yako inaweza tosha ukipewa elfu 90 kwa wiki ci haba mkuu ni hayo tu kwa uzoefu wangu
 

Asante mkuu, nimependa idea ya vifaa ya pikipiki, nitafanya kautafiti juu hiyo biashara kwasababu na wasiwasi kama nitaweza kushindana na bei za wachina wa Kariakoo.
As for biashara ya tikiti maji, kama wachangiaji wengi walivyouliza hapo juu issue ni markets,
nina kama ekari 5 mkuranga tatizo sijui nilime zao gani lenye returns nzuri na gharama ndogo kulima.
 
Cjui upo wapi ndugu but tafiti bajaji kwa ulipo inauzwaje fany cost and benefit analysis kwa hela yako inaweza tosha ukipewa elfu 90 kwa wiki ci haba mkuu ni hayo tu kwa uzoefu wangu

Nashukuru. Biashara za vyombo vya usafiri zimenishinda ndugu yangu, nilikuwa na pick up ilileta faida kwa muda baadaye madereva wakaanza kuleta pesa ndogo na hicho kiduchu nilichopata kiliishia garage. Wewe kwa experience yako unadhani Bajaj itakuwa tofauti?
 
Jaribu kuangalia pia uwezekano wa kufungua duka la nafaka za vyakula mbali mbali kaa vile mchele n.k. ambavyo unaagiza au unavifuata Dubai. Nimewahi kusikia hii nayo ina faida kubwa sana ila sina details.

Ahsante kwa hii idea. Nakumbuka kuna wakati wafanyabiahsra wakubwa walikuwa wanaingiza mchele na kuuza kwa bei ya chini kuliko wa Ifakara kwa hiyo siwe kupuuzia.
 

Tofauti ipo kubwa sana kwani pickup ulikua unasubiri mzigo lakini bajaji tofauti yake ni kuwa ni kama daladala na wateja wengi sana cku izi bodaboda na tax zimekuwa overtaken na bajaji.

Watu mjini wanapendelea bajai sana kwani bei yake ni ndogo kwa abiria ukilinganisha na tax biashara ya vifaa vya pikipiki napata wasiwasi kwani kuna wengne ata hawasafiri bt wanaletewa mzigo walipo so kushndana nao ni ngumu.

Kwa wewe unaenza vilevile kama unainterest na kilimo jaribu vitunguu malolo mpakani mwa Irnga na dodoma huo mtaji unatosha kwa ekari chache vilevile jaribu kwenda mashambani kanunue mpunga kwa bei ndgo kama 50elfu kwa sasa sehemu nyingi then weka store mpaka miezi ya badae utauza marambili yake but kuwa update na soko pamoja na wapi watakua wanavuna ucjeingia loss mkuu.kila la kheri
 
mkuu mkuru...hiyo yakuhifadhi mazao na kuuza baadae itamliza mwenzio , kwanza atatumia mda kuhifadhi hela bila kuzalisha vilevle serikali haitabiliki ktk biashara ya mazao!!
 
Last edited by a moderator:
mkuu mkura...hiyo yakuhifadhi mazao na kuuza baadae itamliza mwenzio , kwanza atatumia mda kuhifadhi hela bila kuzalisha vilevle serikali haitabiliki ktk biashara ya mazao!!

Nakubaliana nawe mkuu alafu samahani ni Mkuru na si mkura najua ni typing error tu lakin nilikua najaribu tu kumpa mawazo tofauti kama ulivochangia mwenzangu yeye ndo mwenye pesa mwsho wa ciku mwamzi mkuu ni yeye lakn akhasante tupo pamoja
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…