Mimi na Ndugu yangu Gentamycine tunawatakia Simba Ushindi wa Kishindo

Mimi na Ndugu yangu Gentamycine tunawatakia Simba Ushindi wa Kishindo

TUKANA UONE

JF-Expert Member
Joined
Jan 3, 2018
Posts
2,345
Reaction score
6,970
Ukihitaji salamu subiri kwanza mechi ya kesho iishe!

Mimi TUKANA UONE a.k.a Mpiga lamination mbele na nyuma!

Pamoja na ndugu yangu na mtani wangu GENTAMYCINE a.k.a Mkunyubenga

Kwa Pamoja tunawatakia Timu ya Simba ushindi mnono hiyo kesho pale kwa Mkapa.Mimi kama shabiki wa mabingwa wa nchi na wana-fainalist wa Kombe la shirikisho pekee kutoka ukanda huu wa Afrika Mashariki,ninayofuraha kuona timu ya Simba a.k.a Makolo inacheza hiyo kesho katika mashindano mapya kabisa ya AFL (African Football League),ni matumaini yangu ya kwamba,timu ya Simba a.k.a Makolo wataibuka na ushindi mnono hiyo kesho.

Utani wangu utabaki kwenye ligu yetu ya ndani lakini linapokuja suala la michezo ya kimataifa ya kuiwakilisha nchi huwa naungana pamoja na wenzangu hata kama tunautani wa ngumi.

Naungana na ndugu yangu na mzee aliyeshindikana GENTAMYCINE a.k.a Mkunyubenga kuwatakia ushindi mnono hapo kesho!

Ndugu yangu Mkunyubenga kesho sitokuwepo mjini,ningeungana na wewe kuelekea uwanjani ila usijali nikitoka Dodoma nitakucheki uje uchukue ngawila ya chupa mbili za Wanzuki pamoja na msokoto wa Sativa!.

Pokeeni salami zangu

Ndimi TUKANA UONE a.k.a Mpiga lamination mbele na nyuma!.
 
[emoji23][emoji23][emoji23] dah!!
Nyie wanasimba mko wapi? Mnaitwa huku!!
 
Back
Top Bottom