Mimi nauliza nini sababu ya kuficha ficha Expiry date kwenye bidhaa nyingi hapa Tanzania? Kwanini zinaandikwa wala hazieleweki nini sababu?

Mimi nauliza nini sababu ya kuficha ficha Expiry date kwenye bidhaa nyingi hapa Tanzania? Kwanini zinaandikwa wala hazieleweki nini sababu?

Pacha kwema. Long time asee.

Sema jamaa kaibua jambo ambalo hata mimi huwa linanitatiza sana sio bidhaa za Tanzania tu ni bidhaa zote. Kuipata Expiry Date/Best Before ni lazima mtu uhangaike sijui hawa watengenezaji kwanini huwa wanaficha sana hiki kitu.
Kweli kabisa pacha, kitambo! Mambo yalibana hapa kati aisee!

Yaah jamaa ana point kubwa sana kwenye huu uzi, vitu vina expire ila vinazunguka mtaani, na wenye mamlaka husika hawajali!

Juzi nimekutana na Blue Band zimebakisha Siku 15 zi Expire. Jamaa wanatembeza mitaani na kuuza Elf 2,500/=Tsh badala ya 7,000/=Tshs. Hawa jamaa wapo sehemu nyingi! Najua watu wengi wameshakutana nao na bado wanakutana nao mitaani!

Week iliopita nlipita Pharmacy fulani kumnunulia dawa Mzee wangu mmoja tunaefanya nae harakati za kutafuta maisha, tunaheshimiana nae sana mzee huyo, namchukulia kama mzazi wangu, ana matatizo ya mshipa mmoja wa moyo kuziba, basi nikampitishia kwake, nikasepa zangu home. Bila mimi kuzisoma expire date, yeye usiku kabla ya kuzitumia bahati akazisoma kumbe dawa zime Expire tokea January 2023. Akanipigia sim kuniuliza mwanangu mbona umeniletea Sumu badala ya dawa? Nikashtuka sana na kumuuliza kulikoni tena? Mbona sikuelewi?

Ndio akanielewesha zime expire, Dah!

Nikajiuliza maswali mengi sana, na kwabahati huwa natoa pesa zangu mfukoni kumnunulia dawa zake (Almost Elf 65 kwa dose moja), ingekua anatoa pesa zake basi angeweza kunifikiria nimeanza kumchezea mchezo mchafu au chochote.
 
Kweli kabisa pacha, kitambo! Mambo yalibana hapa kati aisee!

Yaah jamaa ana point kubwa sana kwenye huu uzi, vitu vina expire ila vinazunguka mtaani, na wenye mamlaka husika hawajali!

Juzi nimekutana na Blue Band zimebakisha Siku 15 zi Expire. Jamaa wanatembeza mitaani na kuuza Elf 2,500/=Tsh badala ya 7,000/=Tshs. Hawa jamaa wapo sehemu nyingi! Najua watu wengi wameshakutana nao na bado wanakutana nao mitaani!

Week iliopita nlipita Pharmacy fulani kumnunulia dawa za Mzee wangu mmoja tunaefanya nae harakati za kutafuta maisha, ana matatizo ya mshipa mmoja wa moyo kuziba, basi nikampitishia kwake. Bila mimi kuzisoma expire date, yeye bahati akazisoma kumbe dawa zime Expire tokea January 2023. Akaniulia mwanangu mbona umeniletea Sumu badala ya dawa? Nikashtuka sana na kumuuliza kulikoni tena? Mbona sikuelewi?

Ndio akanielewesha zime expire!

Nikajiuliza maswali mengi sana.
Mamlaka zetu tumewapa wauwaji. Juzi hapa nilisikiliza speech moja ya PLO Lumumba aliongelea hili jambo.

Kwamba mamlaka tumewapa watu wasiokuwa na huruma kwetu, watu wanafki. Wanaruhusu vitu kama hivyo dawa zilizo expire n.k lakini wanaita alichokifanya Hitler holocaust bila kujua wao nao wanafanya hicho hicho.

Tunawapa mamlaka wanatujengea miundombinu mibovu kila siku ajali zinaua watu, lakini wana blame genocide kwenye nchi nyingine bila kujua wao wenyewe wana commit genocides kila siku.
 
Noma juzi nimekunywa juice nikawa siewi ladha yake ndio nikaanza kutafuta mwisho wa matumizi bhana wewe nilitoka jasho hapo mwisho nikakuta imepita mda aisee, duka lipo mtaani sijakachaga tena duka lile.
Pole sana ndugu tuongeze umakini
 
Shida ya watanzania mnapenda ku conclude mambo bila ya kuwa na uhakika.

Expired date kwa bidhaa zinazo ifadhiwa kwenye makopo zinandikwa kwenye ubavu wa chupa au chini kwenye kitako


710b0110f9c1163098cb0e4a55bb86e8.jpg


images (10).jpeg



Hiyo hapo jju kwenye mfuniko sio tarehe ni product ID au Bach number. Hizi zinatumiwa na scaner na viwandani kujua product and kuzipanga. Zipo juu ya mfuniko kwa sababu za urahisi wa kuzi scan.


Ukujaribu ku scan hicho ulicho weka kitaleta kama hivi:

Mfano

Code:
TZS 574 AZAM
 
Shida ya watanzania mnapenda ku conclude mambo bila ya kuwa na uhakika.

Expired date kwa bidhaa zinazo ifadhiwa kwenye makopo zinandikwa kwenye ubavu wa chupa au chini kwenye kitako


View attachment 2671433

View attachment 2671434


Hiyo hapo jju kwenye mfuniko sio tarehe ni product ID au Bach number. Hizi zinatumiwa na scaner na viwandani kujua product and kuzipanga. Zipo juu ya mfuniko kwa sababu za urahisi wa kuzi scan.


Ukujaribu ku scan hicho ulicho weka kitaleta kama hivi:

Mfano

Code:
TZS 574 AZAM
Shida sio ya Watanzania.
Shida ipo kwa mamlaka na taasisi husika.
Ni lini TBS,TMDA,TFDA au taasisi nyingine yoyote inayohusika iliwahi kutoa elimu kwa Watanzania kuhusu hili jambo!!???
 
Niliwahi kwenda supermarket fulani dodoma ile ya alfa kununua sabuni ya kusuzia nguo ile ya maq ya maji..kumbe kwenye expire date wameweka kikaratasi cha price.SIO DAWA ZOTE ZIPO KWENYE MADUKA YA MADAWA!🧏[emoji2533]🧏[emoji2533]‍[emoji3601]

1 - Mazoezi ni dawa.
2 - Kufunga ni dawa.
3 - Chakula cha asili ni dawa.
4 - Kicheko ni dawa.
5 - Mboga na matunda ni dawa.
6 - Kupumzika na Usingizi wa kutosha ni dawa.
7 - Mwanga wa jua ni dawa.
8 - Kuwapenda wengine ni dawa
9 - Kujipenda ni dawa.
10 - Kuwa na moyo wa Shukrani ni dawa.
11 - Kuacha dhambi/kosa ni dawa.
12 - Kutafakari ni dawa.
13 - Kusoma na kujifunza Neno la Mungu ni dawa.
14 - Kula vizuri, kwa wakati na bila ziada ni dawa.
15 - Fikra sahihi ni dawa.
16 - Kumtegemea Mungu ni dawa
17 - Marafiki wazuri ni dawa.
18 - Kujisamehe na kusamehe wengine ni dawa.
19 - Kunywa maji mengi ni dawa.
20 - Moyo wenye amani ni dawa.
21- Kuvuta hewa safi ni dawa.
22 - Kuwa na kiasi katika kila jambo ni dawa

Ukinywa dawa hizi za kutosha , ni mara chache sana utahitaji zile za maduka ya dawa.
 
Hii ishu ni hatari haswa kwenye suala la bidhaa za vyakula !! Baadhi ya bidhaa aina hii unakuta zina Manufacturing na Expiry Date kweye katoni/boksi la nje (Outer Packaging) lakini kwenye Pakiti ya ndani (Inner/Immediate Packaging) hazina hizo indications. Mfano wa hili ni bidhaa aina ya BISKUTI ambazo nyingine wanapewa watoto kama zawadi mashuleni !!!
T-B-S Where are you !!!??
 
Naomba kuuliza kwa nini zile taarifa za bidhaa kuisha muda wake ‘expire date’ kwenye bidhaa nyingi huwa zinafichwa sana?

Yaani kuna bidhaa ile taarifa yake ya expire unaitafuta kwa shida au inaweka kwa namna ambayo haisomeki vizuri hasa kwa mtu mwenye shida ya macho.

Hii inapelekea watu wengi kutokuwa na nafasi nzuri ya kutoona vizuri tarehe husika kwa kuwa ili uione unahitaji kufanya ukaguzi vizuri, hili silo la kufumbia macho.

Ndio maana kuna bidhaa nyingi watu wananunua na kuzitumia licha ya kuwa zimeshapita muda wa matumizi kwa kuwa hawazioni.
 
Tbs,na tfd wameshaamua tusio wahusu tukafie mbele
 
Hiyo siyo expiring date. Hizo ni security numberau codes maalumu zinazowasaidia wazalishaji kutambua bidhaa zao, umeona hadi kuna QR code hapo. Manufacturing and expiring date utazitambua coz husa zinaanza na herufi Mfg, au manufacturing , exp. Au full expiring date. Zinaweza kuwa pembezoni mwa chupa au chini kutegemeana na muundo sa kifungashioo.
 
Hivi kwa mfano

View attachment 2671366

Naomba nisaidiwe kusoma hiyo expire date hapo kwenye picha

Na bidhaa za aina hii zipo nyingi yani expired date haieleweki kabisa utakuta imeandikwa ila huwezi kuielewa kabisa

Ni nini tatizo mbona bidhaa za nchi zingine zinasomeka vizuri kabisa tarehe ya kuzalishwa na mwisho wa kutumika vinaonekana na vipo wazi kabisa.

Hii nchi uhuni umezidi sana
Mi nadhani sababu ni wenye jukumu la kusimamia kujisahau na kuishi kwa mazowea.
 
Back
Top Bottom