Mimi ni mwanabaiolojia na huu hapa ndio uthibitisho wa uhalali wa Mungu(2)

Mimi ni mwanabaiolojia na huu hapa ndio uthibitisho wa uhalali wa Mungu(2)

Ndio, sio sawa mtu kujitambulisha taaluma ya sayansi halafu aendelee kutoa hoja za kiroho. Ni kuchafua tawi husika. Bora atoe maoni yake binafsi na si kutaka kukuza uzito wa hoja kwa kuongezea sifa za taaluma anayodai kujikita. Kuanza kwa kujitambulisha mimi ni "fulani" ni kutaka kujipa mamlaka zaidi wakati hoja ni dhaifu. Jaribu kuelewa sio kurukia maneno tu.

Sawa, lakini mbona kama unamzushia hivi, sijaona sehemu hata moja Uhakika Bro alipotumia hoja za kiroho kuthibitisha hilo ulilodai, kwa comments nilizosoma nimeona akitumia hoja za kisayansi, kisaikolojia, kifalsafa na kiakili, hoja za kiimani kwake hazijanithibitikia moja kwa moja isipokuwa nazinusa kwa mbali mno, yaani tena mbali mno

Hoja dhaifu kwa upeo wako, kwa upeo wa wanasayansi wengine na yeye na mimi na wengine wengi tunaona zina nguvu ndo maana tumeamini

Nilielewa sana ndo maana nilikubania kwenye hiyo angle, mimi mshangao ulikuwa kwa nini ukane kwamba sicho ulichokuwa unapinga awali? Hilo tu, yaani kuna muda unakataa halafu kuna muda unakubali, kama mwanzo uligeuka, lakini naona sasa hivi umejibu wazi tena kwa kujiamini kwa kuanza na ndiyo, hivyo ndo inavyotakiwa, usiwe unakimbia kivuli chako
 
Kumbe we ni mtu wa kukariri... aliyekudanganya qualitative phenomenon haziwezi kuelezwa na takwimu ni nani? Unasikitisha. Everything can be quantified. Tusiende mbali, una mengi ya kujifunza.

Eti wa kukariri, mimi siyo wewe rafiki

Ulichokosoa umejifunga mwenyewe, qualitative phenomenon ukishai-quantify tu hiyo siyo qualitative tena ni quantitative [emoji4]

Ngoja nifungue darasa la takwimu kidogo!

Qualitative phenomenon ni zile phenomenon ambazo zinahusika na maelezo na zinaonekana kwa macho lakini hazipimiki 'numerically' kwa mfano: harufu, uzuri au jinsia. Unaweza kupima harufu kwa figure? Je unaweza kupima uzuri wa mtu kwa figure?

Ili kupima qualitative data inatakiwa uzifanyie coding "kuzipa geresho na value" (kwa mfano jinsia: 1= Me, 2 = Ke) kikategoria 'categorically'. Kitakwimu ukifanya hivyo hakuhesabiki kwamba umezipima qualities zenyewe kiuhalisia kama ambavyo unaweza kupima urefu wa mtu, coding: hii husaidia kwenye kufanya investigation tu lakini kitakwimu hakuhesabiki kwamba umezipima phenomenon halisi, na huku kufanya coding ndo kunahesabika ni kufanya quantification

Quantititative phenomenon ni phenomenon ambazo zinaonekana na zinapimika kwa namba 'quantity - numerically' kwa mfano uzito 'uzani', idadi ya watu na umbali

NB: Takwimu ni fani inayodili na numerical facts na figures. Qualitative phenomenon kiasili hazipo numerically hadi pale tu utakapozi-convert kwenda kwenye quantity

Hitimisho: Katika hali ya kawaida Takwimu haipimi qualitative aspects, hivyo ndo maana fani ya takwimu husema moja ya udhaifu wake ni kupuuzia phenomenon zenye sifa hiyo

Kama hujaelewa kamtafute Fisher
 
Kumbe we ni mtu wa kukariri... aliyekudanganya qualitative phenomenon haziwezi kuelezwa na takwimu ni nani? Unasikitisha. Everything can be quantified. Tusiende mbali, una mengi ya kujifunza.
Acha kukimbia mada, bado hujataja madhaifu ya fani ya sayansi. Ni kweli na mengi ya kujifunza kwani nayofahamu ni machache sana - yaani machache mno, kama leo nilikuwa napitia tena theory of everything, nimeongeza maarifa. Lakini si mimi tu, hata fani ya sayansi nayo ina mengi sana ya kujifunza [emoji2960]
 
Unachekesha sana. 100% ulizipimaje? Yaani wewe ni mshirikina wa aina zote kumbe... Imani zimekujaa. Ndio maana nikasema tuko parallel. Mitazamo yako ya kale sana.
Nilipimaje? Kwani uwepo wa wanadamu nimepimaje mbona nathibitisha uwepo wao kwa 100%? Nathibitisha uwepo wa mwanga kwa 100%, kipimo ni kule kuwepo kwa hiyo phenonemon tajwa

Kumbe kuamini uwepo wa uchawi ndo kuwa mshirikina "mchawi"? Eti hii nayo ni hoja kajenga [emoji848], ni sawa na kusema kuamini juu ya uwepo wa Mungu basi nawe ni sehemu ya Uungu au nawe ni Mungu, msishangae, ndo upeo wake ulivyomtuma

Sawa ngoja nikubali, sitakuwa wa kwanza, wapo wakina Dynamo Magician

Halafu hata nikisema nikomae na hilo neno tu peke yake, maana yake kilugha 'kiistilahi' na kiimani hutoboi

Acha ushamba na ulimbukeni, unafikiri eti usipoamini uwepo wa Mungu au uwepo wa uchawi ndo utaonekana wa kisasa - wa kileoleo [emoji23]
 
Inabidi uelewe consciousness ni kitendo sio kitu fulani stationary... observation yake inafanyika mubashara. Mfano kuelewa nini kinakuza imani kichwani mwako inabidi ufungwe sensa ukiwa unaomba, au kama huwa unakemea, kutoa ushuhuda nk.. kila sehemu kichwan hubadilika kulingana na tukio unalofanya au kuwaza. Mambo mengi tayari yanajulikana na mengine mengi yatajulikana. Ramani yote itakamilika. Ni suala la muda na si kwamba imeshindikana. Again, mtazamo wako wa kuegemea beyond scientific knowledge ni wa kale. Badilika, uachane na hizo imani zote potofu.

Akili ni kitendo? [emoji2960]
 
Hakuna mwanasayansi au mtu yoyote mwenye kujua kusoma na kuelewa atabisha kuhusu evolution. Hivi vitu vinavyotokea kila siku kudhihirisha kwamba viumbe vinabadilika kila wakati huyajui? Ina maana unaandika based on past experiences na sio dunia ya leo? Ibuka kutoka pango hilo ulilopo uungane na wenzio. Unless umeridhika na hizo imani zako za uongo. Eti mungu umtumainiae!
Huu utahira wa Darwin nimekwambia kajadiliane na wanafunzi wa darasa la kwanza D, tena wale wasio na mtaala wa Montessori, japo hata wao watakuona dishi limeyumba, mbona hunielewi
 
Hakuna mwanasayansi au mtu yoyote mwenye kujua kusoma na kuelewa atabisha kuhusu evolution. Hivi vitu vinavyotokea kila siku kudhihirisha kwamba viumbe vinabadilika kila wakati huyajui? Ina maana unaandika based on past experiences na sio dunia ya leo? Ibuka kutoka pango hilo ulilopo uungane na wenzio. Unless umeridhika na hizo imani zako za uongo. Eti mungu umtumainiae!
Eti hakuna wanasayansi wanaopinga evolution, hivi we jamaa maarifa yako huwa unaokotea wapi aisee?

Nakuchana wazi kwamba wapo wanasayansi wanaopinga hiyo nadharia totally, na wengi wao wanapinga hiyo nadharia partially, sasa kama wanasayansi ndo hivyo je wenzangu na mimi uliowataja hapo 'literacy' hao wapo lukuki! Halafu hata hivyo awali sikukosoa nadharia ya evolution kwa ujumla wake, nilikosoa utahira wa Darwinism ambao umepingwa karibu na wanasayansi wote. Nilikosoa hilo. Lakini kwa kuwa umenichokonoa ukitaka nipinge hata hiyo nadharia ya evolution kwa ujumla nitai-refute vilevile

Boona Mohammed kwenye moja ya mashairi yake alisema 'You must really come from apes with your monkey point of view"
 
Unadhani ni mimi tu?[emoji1787] iko hivi, imani uliyonayo wewe hapo sio kila mtu anaifata. Kimsingi kama una dini moja au dhehebu unalofata sijali lolote lile, tofauti yako na watu wasiofata ujinga wowote ni ndogo mno. Umekataa imani zote duniani ukabaki na hiyo moja wakati wengine tumeenda mbele zaidi kukataa zote pamoja na hiyo moja yako. Imani yako ni ujinga kama zingine zote. Tua zigo hilo!

Einstein yawezekana alikuwa deist. Wewe hapo ni theist. Kwa namna kubwa deism ni position ngumu kuhoji zaidi ya kwako wewe theism na mungu wako unayemtumainia. Tusiende mbali sana, kama Einstein alikuwa na imani so what? Unataka wote tufate imani kwa sababu ya mtaalamu mmoja? Tumia akili na ujenge hoja yenye mantiki.
Kwani hoja yako awali ilikuwa nini nilipokuthibitishia kwamba EINSTEIN alikuwa akiamini uwepo Mungu? Unapojibiwa unasahau kwamba hayo maelezo yalikuwa yakihusu swali au ufafanuzi fulani wa nyuma, badala yake unadandia hapohapo tena na kujifanya kuanzisha kitu kipya, kwani kilichokuwasha mpaka ukaniuliza nafahamu ni Mungu gani aliyedhaniwa kuwepo na Einstein kilikuwa nini? Ulikuwa na hoja gani ya kunieleza pale nisiyoifahamu? Na nililitolea maelezo mengi hilo swali kusudi ili kila sehemu utakayojifanya ndo hoja yako utakapoiwasilisha niwe nilishaigusia, na kama nilijua tu, hamna jipya ulilochangia hapo, nilieleza yote, kwani deism ni nini? Hiiiii, sikueleza kwamba Spinoza alikuwa mwanafalsafa? Sasa hapo hoja yako ni nini? Deism au Theism ni terminology tu za kutofautisha lakini hoja ni kwamba wote hao wanaamini uwepo wa Mungu
 
Unataka wote tufate imani kwa sababu ya mtaalamu mmoja?

Hapo unaona umeuliza swali la kunibananisha mwenyewe? Kwa faida yako rejea moja ya comments nilizokuwa na-share maarifa na Uhakika Bro uone nimetaja wanasayansi wangapi na wanafalsafa wangapi wanaoamini uwepo wa Mungu. Shabaha ya kukutajia hao ni kwa sababu ya upeo wako limbukeni, ulikuwa hujui kwamba wapo wanasayansi wakubwa wanaoamini uwepo wa Mungu, kwa kifupi ulikuwa unapinga, kukuthibitishia wapo ndo ikanilazimu nitaje baadhi yao, nilipotaja ndo ukashtuka - ukajifunza, ukazuga nawe ulikuwa unafahamu hilo, hoja zako za awali zikabaki zinakushangaa "gaka"!

Wapi nimetaka wote mfuate? Rejea kwenye hiyohiyo post niliyokudokeza utaona nilikiri kwamba wapo wanasayansi pia ambao ni atheist/agnostics, licha ya kwamba kwenye hili kundi sikuwataja kwa majina, ukihitaji majina yao nifahamishe nikutajie
 
Unataka wote tufate imani kwa sababu ya mtaalamu mmoja?

Kabla ya kuniuliza hilo swali ungejiuliza, kwani mimi nanufaika nini au nahasarika nini na wewe kutomuamini Mungu? Je ukimuamini mimi nitanufaika nini? Je kinyume chake?

Mustakabali wa maisha yako na ya kila mmoja wetu yapo mikononi mwake, sijakushikia maisha yako, jitambue

Halafu hata hivyo, hili si suala la kutaka au kutokutaka, kwani nikitaka huwa? Na nisipotaka pia hakiwi? We naje, mimi ni nyang'au kama wewe tu isipokuwa tofauti yetu kubwa ni moja tu, mmoja yupo kwenye nuru na mmoja yupo gizani, hajajua purpose ya haya maisha, anafikiri tupo duniani kucheza vikoba na kula manicha
 
Ndio, sio sawa mtu kujitambulisha taaluma ya sayansi halafu aendelee kutoa hoja za kiroho. Ni kuchafua tawi husika. Bora atoe maoni yake binafsi na si kutaka kukuza uzito wa hoja kwa kuongezea sifa za taaluma anayodai kujikita. Kuanza kwa kujitambulisha mimi ni "fulani" ni kutaka kujipa mamlaka zaidi wakati hoja ni dhaifu. Jaribu kuelewa sio kurukia maneno tu.
Kwamba unadhani nilitaka kutumia ujing.... I mean fallacy [hivi fallacy kwa kiswahili ni nini? au ndio ufala🤨!] ya ad hominem?

Hapana mimi nilitaka kutumia a biologist point of view kuitetea hoja ya kwamba imeonekana kila kinachoishi, kinaonekana kuishi kwa ajili ya wenzake na mfumo mzima kwa ujumla. Ndio maana tumeangalia point of view ya seli, viungo, mifumo, kiumbe mzima hadi jamii za viumbe na kuongezea magimba kwa juu na atomu kwa chini. Vyote vimeonekana kuwa na maana pale vinapoishi kwa ushirikiano na vyenye asili moja, pia na vyenye asili tofauti kwa ajili ya lengo fulani kubwa kuliko wao wote combined. Hivyo tu.
 
Reality ni Reality, eti kwani reality kwako ni nini? Kama kwangu au kwako au kwa yule ikiwa tofauti ndo itaifanya isiwe reality? Kuwa na ufahamu tofauti au wa kimakosa wa neno fulani hakuondoshi maana halisi ya neno
Reality, tumetoka kuiweka sawa nilipomjibu kwa post namba 225. Najua ameisoma na kuikubali na hajataka tu kuitolea majibu [nimechukulia silence means yes]

Tukiachana na pande tulizoshikilia [za God or no God] kuna kitu kimoja hapa natamani kila mmoja binafsi akichallenge kwa uelewa wake kwa kile anachoona ni sensible:

Hoja kuu: Tunauishi ukweli kulingana na tunachohisi ni kweli binafsi. Yaani mimi binafsi ninaushi ukweli ninaoujua binafsi kwamba ni ukweli na ndio iko hivyo. Na wewe binafsi unauishi uhalisia wako binafsi kutokana na unachokijua kuwa ni kweli wewe mwenyewe. Mambo ya relativity.

Mfano 1.a. Yule anayeamini ukweli wa maisha baada ya kifo basi akifa ataendelea kuishi katika namna sambamba na alivyoamini. Huyu ameamini katika uhai

1.b. Na yule aliyeamini kuwa hakuna lolote la ziada ukweli ni mnyama akifa kila kitu kinasambaratika na kuwa viinilishe kwa wanyama wengine basi akifa atapata sambamba na ukweli wake binafsi. Huyu ameamini katika kifo

Mfano 2.a Yule atakayeamini kuwa ukweli ni tunaishi katika mazingira ya hatari ya, wizi, uonevu, magonjwa na vita ni vitu vya maisha ya kawaida na vingi kuliko hali ya amani basi kila kitu chake kitaitikia kwa kujiweka mkao wa vita mbeleni. Atajikusanyia bima ya rasilimali nyingi zaidi physically. Na kimwili atajiwekea bima ya rasilimali muhimu kama mafuta[nishati] na protini kujiandaa na vita inayokuja.
Na ikitokea akaamini kuwa sio hatari tu bali tayari tumo katika vita, iwe ni kuchumi, kiroho, kisaikolojia, familia, kazini etc. Basi tutashuhudia akiwa na nishati ya kutosha mwilini ili apambane sasa hivi. Namaanisha sukari. Mfano wake ni bosi wa wastani[CEO] anayeongoza kampuni kubwa yenye faida kubwa na hatari kubwa zaidi ya kufilisika ni kwa nn wanakuwa na vitambi/sukari?

2.b. Kinyume chake atakuwa ni jamaa anayeamini kwamba tunaishi na watu wa amani na upendo zaidi kwamba wengi ni wa upendo kuliko wa vita na mimi. Basi huyu mwamba hata hajiandai na rasilimali zozote za kimali binafsi physically. Na hasahasa kimwili hajiandai kwa kujirundikia mafuta[nishati] wala maprotini mwilini. Mfano ni rastamani wa wastani mwenye imani ya kirasta kwa nini wanakuwaga wembamba?

Mfano wa kwanza tuachane nao kutokana na asili yake utatusumbua. Naomba muuchallenge huu mfano wa pili. Ila nahisi hapa naharibu uzi ngoja nikipata muda niuanzishie uzi wake. Ila nipeni challenge ili nijipange vizuri.
 
lakini ni kwanini Mungu akae mbali nasisi ambao ni viumbe wake.
 
Unataka nikurupuke kwa mshangao au butwaa nione uwepo wa kitu kisichokuwepo? Yaani kwa vile kuna mpangilio fulani uliowezesha kuwepo vitu fulani nilipuke tu kusema lazima mungu amefanya hivi. Huoni kasoro kwenye mtiririko huo wa mawazo?

Unaandika vitu vya uongo. Eti vinavyoshikika tu! Unaweza kushika sauti au mwanga? Be serious.

Mambo ya kutungatunga ni kujidanganya. "And let there be light" seriously?

Ukifika ukomo wa uelewa sema tu sijui. Usianze kukumbatia imani na maandiko ya watu wa kale(ambao umewazidi sana ufahamu wa mambo mengi). Ni uongo mtupu!

Unaanzaje kuangalia dunia na ulimwengu halafu uhoji nani kaumba? Sio lazima kitu kiumbwe ili kiwepo, kinaweza kutokea tu. Mara kwann tuko hapa? Sio lazima kuwe na nia yoyote ya sisi kuwepo hapa. Tukifa tunaenda wap? Sio lazima kuwe na maisha baada ya kufa. Unaweza kuweka "hakuna ushahidi" kwenye 'sio lazima'.


Mtazamo wako unatia mashaka mwanabailojia.
na pia mkuu mtu ambaye hajui ni mjinga, lakini asiyetaka kujua ni mpumbavu .kweli tunakumbatia maandiko ya kale kuhusu uwepo wa Mungu, nayo ni kwasababu tunataka kujua, ipi hasa ni kweli .lakini huoni kama wewe unayebisha usiyetaka kujua zaidi juu ya uwepo wa Mungu ni mpumbavu ?
 
lakini ni kwanini Mungu akae mbali nasisi ambao ni viumbe wake.
Unaweza kuichukulia hivyo kimwili zaidi kumpata yupo mbali, lakini kiroho yupo nasi tunaishi naye kila siku yupo mahali pote ni sisi tu kumtambua
 
Back
Top Bottom