Mimi ni shabiki wa Yanga katika vitu sitamani vitokee ni Mgunda kurudi 5imba

MwananchiOG

JF-Expert Member
Joined
Apr 4, 2023
Posts
1,970
Reaction score
4,037

Huyu kocha ni mtu wa hatari sana, katika vitu nafurahishwa navyo ni pale ninapoona 5imba hawana mpango naye, Ila katika makocha wajuzi na hatari hususan kwa Ligi yetu ni Juma Mgunda a.k.a Mzee wa acha boli litembee, mzee wa pira biriani. Huyu jamaa akiachiwaga timu mfano pale alipofukuzwa Tinyo, alikichafua utadhani sio ile 5imba ya Tinyo๐Ÿ˜€ akamuibua Edwin Balua sijui kutoka wapi huko, hakupoteza hata mchezo mmoja, alituumiza sana vichwa ๐Ÿ˜€ hana woga sio juu,kati,mbele anakichafua tu!

Anajua sana kuwatumia wachezaji kulingana na weakness na strength zao, alafu sio kocha wa majina.Hawa ndiyo wale makocha unampatia pilipili na vitunguu unakuta ametengeneza kachumbari safi ๐Ÿ˜€

Wapinzani bado hawajalitambua hili, Jambo linalotufurahisha mno! Hata pale kikosi cha Taifa stars nina uhakika mchango wa mwamba ni mkubwa sana.
 
Unatoboa Siri tena Mzee๐Ÿ˜Ž๐Ÿ˜Ž.. Libakie moyoni c ndo tulikubalianaga wazee
 
Nachekea chinichini Simba ikijichanganya kumuachia timu huyu Mzee hata nusu msimu wanashika nafasi ya 7.
 
Ni KOCHA mzuri anayejua kupanga list na kuhamasisha wachezaji tatizo kubwa Hana plan B.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn moreโ€ฆ