Mimi nilidhani mnawashtaki Wabelgiji ICC kwa 'Kumuua' Hayati Lumumba kumbe mlichoona cha Muhimu Kwenu ni kurudishwa tu Jino lake?

Mimi nilidhani mnawashtaki Wabelgiji ICC kwa 'Kumuua' Hayati Lumumba kumbe mlichoona cha Muhimu Kwenu ni kurudishwa tu Jino lake?

GENTAMYCINE

JF-Expert Member
Joined
Jul 13, 2013
Posts
60,660
Reaction score
121,325
Mamlaka ya Ubelgiji imekabidhi jino la kiongozi wa uhuru wa Congo Patrice Lumumba, kwa familia yake katika hafla iliyofanyika Brussels. Jino hilo ni sehemu pekee ya mabaki ya mwili wake ambayo inadhaniwa kuwa bado ipo baada ya kunyongwa na kisha mwili wake kuyeyushwa kwa tindikali mwaka 1961.

Chanzo: ITV Tanzania

Kwahiyo hilo Jino ndilo litawafanyeni Wakongo muwe na Amani na kupata Akili za Kujiongoza wenyewe kabisa? Kuna muda siwaelewi Waafrika Wenzangu kwani tunapenda sana Kuendekeza mambo ya Kipuuzi na yasiyo na Tija yoyote Kimantiki na Kimaendeleo.

Kumbe ndiyo maana nyie Wakongo mnachezea mno Vitasa kutoka kwa Rais Kagame na Rwanda na mnastahili sana.
 
Hakika ni upuuzi wa hali ya juu kushangilia kwa kupokea mabaki ya mwili(jino) badala ya kuchukua hatua zaidi kisheria, ambazo zingewafanya wabeligiji kuwajibika zaidi kwa familia ya Lumumba na Taifa la DRC kwa ujumla.
 
Mamlaka ya Ubelgiji imekabidhi jino la kiongozi wa uhuru wa Congo Patrice Lumumba, kwa familia yake katika hafla iliyofanyika Brussels. Jino hilo ni sehemu pekee ya mabaki ya mwili wake ambayo inadhaniwa kuwa bado ipo baada ya kunyongwa na kisha mwili wake kuyeyushwa kwa tindikali mwaka 1961.

Chanzo: ITV Tanzania

Kwahiyo hilo Jino ndilo litawafanyeni Wakongo muwe na Amani na kupata Akili za Kujiongoza wenyewe kabisa? Kuna muda siwaelewi Waafrika Wenzangu kwani tunapenda sana Kuendekeza mambo ya Kipuuzi na yasiyo na Tija yoyote Kimantiki na Kimaendeleo.

Kumbe ndiyo maana nyie Wakongo mnachezea mno Vitasa kutoka kwa Rais Kagame na Rwanda na mnastahili sana.
Loud and clear
 
Kuna kauli wanasemaga Mungu akupi vyote, Congo inakila kitu nchi inahitaji kuendelea kasoro watu wenye utashi, hilo halishangazi.
 
Back
Top Bottom