Mimi Nina tatizo Moja, nataka kuanzisha biashara ya genge la nyanya, vitunguuu, mboga mboga ila naogopa watanichukuliaje?

We unaviuza lkini?!
Hapana ila nawazaga tu
Sema hapa jirani pana mtu anauza namuona ana mzigo leo siku ya 3 nyanya ziko poa/viazi/ ndizi mbivu na mbichi
Nmegundua anachukua vitu vile safi haviharibiki haraka pia anachukua mali isiyoiva sana kama nyanya na viazi
Hakosi wateja mana ni vitu vinahitajika anauza na hayupo kwenye mzunguko mkubws ila anauza kakodi frem ya mtaani naona atakua analipa 50 hivi
 
Hio kazi Ina hela
zi m
 
Shukrani Kwa tag Mkuu

Japo nimechelewa kuona ila mtoa mada amepata michango mizuri sana kutoka Kwa wadau

Kwa kuongeza na kumtia moyo mtoa mada, asiwaze kwamba watu watamcheka

Bora wewe unataka kuanza biashara ya kuuza genge, umewahi kufikiri ingekuwa biashara ya kutembeza vitu barabarani ungeweza kweli?

Vipi ingekuwa kazi ya mamantile wanaotembeza vyakula kwenye site za Ujenzi, ungeweza kweli Bibie?

Kumbuka, Biblia inasisitiza kwamba
"Mtu yeyote asiyependa kufanya kazi, asile chakula.” 2 Wathesalonike 3:10
 
Mimi nina degree 2, nina kazi nimeajiriwa, nilikuwa nina maduka ya rejareja mtaani mawili kwa sasa niliyafunga sababu ya wizi wa vijana niliowaajiri. Katika maduka yote hayo mawili niliweka genge pia, kwa hivyo alfajiri nilikuwa nawahi kutoka naenda Ilala sokoni nanunua vitu vya gengeni kisha ndio naelekea kazini.

Hapo dukani pia tuliweka maandazi na tulikuwa tunayapika wenyewe, na ubuyu na karanga tulikuwa tunatengeza wenyewe..

endelea kuona aibu
 
Habari zenu ndugu zangu,

Mimi Nina tatizo Moja, nataka kuanzisha biashara ya genge la nyanya, vitunguuu, mboga mboga ila naona aibu kutoka na mazingira niliyopo na namna watu watanichukulia

Naombe ushauri wenu?
Endelea kuona aibu,mi mwenzio ni muajiriwa wa serikali tena jeshini,lakini nimenunua sim tank,mke wangu anauza maji,dumu sh 100/.
 
Maisha ukiyaelewa raha sana.. uyo unawaza atakuonaje usiku ikifka anakua ndan kwake anakula alichokitafuta bila kuwaza utamwonaje sa iyo ww huna kila ktu au umekula ujashiba kwasababu ya kutokua na pesa ya kutosha
 
Habari zenu ndugu zangu,

Mimi Nina tatizo Moja, nataka kuanzisha biashara ya genge la nyanya, vitunguuu, mboga mboga ila naona aibu kutoka na mazingira niliyopo na namna watu watanichukulia

Naombe ushauri wenu?
Watakuchukulia kàma wewe unavyowachukulia wenye hayo magenge.
 
Liweke tu kisasa jioni mataa kama yote.Utapiga hela vibaya mnooo.Kesho anza haraka.Simu moja tu tukutane Bank .Oiiii.
 
Kafungue biashara yako mbali na mazingira ulipo sasa. Huko utakapoenda Jitahidi kubadilisha muonekano wako, hakujui mtu humjui mtu ni kazi tu.


Haya sasa, leta kisingizio kingine.
Kama ni mazingira uliyokulia [Comfort zone], ni ngumu Sana, unahitaji zaidi ya ujasiri , ondoka comfort zone, Jiulize ukiondoka hapo utapoteza nini cha msingi .
Hapa ndio kwenye tatizo kubwa.
Na wengi hawawezi kuthubutu kutokana na sababu hizo hapo juu.
Ni wachache sana waliojaribu na kufanikiwa katika mazingira ya nyumbani (walikokulia).

Ile watanionaje au watanifikiriaje.....🤔 linafelisha na linaendelea kufelisha wengi mno katika suala zima la kujikwamua kiuchumi ili kujiletea maendeleo.
 
Sahihi kabisa Madame B
 
Habari zenu ndugu zangu,

Mimi Nina tatizo Moja, nataka kuanzisha biashara ya genge la nyanya, vitunguuu, mboga mboga ila naona aibu kutoka na mazingira niliyopo na namna watu watanichukulia

Naombe ushauri wenu?
Anzisha kisha ajiri mtu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…