Minyukano CCM: Ushauri wa bure kwa Bashiru na wenzako kokote kule mliko

Da labda kwanza tukupe pole mtoa mada , inawezekana kabisa hujui mengi ila Daktari kayakanyaga mwenyewe mwishoni kabisa kwa kuonyesha nia ya kuisigina katiba ili aurithi ufalme, yaani kama Mchonga angekuwa presidaa daktari saa hizi alitakiwa awe detention kama Shekh Jumbe. Mama ana dini kaona kiroho safi wampeleke mjengoni.

Hawa watu ni wakatili sana kuliko unavyojua na ungewajua hawatakiwa hata kutajwa manake jalali ndio ameamua kuwe na mabadiliko haya baada ya kuona nafsi katili za viumbe hawa.
 
Mwingine huu hapa:

View attachment 1772301

Ukihitaji mwingine sema. Kukuongezea mwingine "itapendeza zaidi." - Dr. Shika.
Si Udaku wa ki blog cha Dar Mpya? Na wanaomshutumu Bashiru wengi mambo yao hayakwenda. Na kale ka mnec kaka yake alikatwa kwenye kura za Maoni. Mimi sitetei waovu hata kidogo. Wamefurahi wapi, Vyombo vya habari Vikubwa na vyenye weredi si vingeripoti? Tuache Nongwa. Bashiru aliifanya kazi yake mpaka hayati alimpotoa kwenye Chama. Wizi wa Mali za Chama ulizidi mno. Mpaka Chama kilikuwa kinashindwa kulipa Mishahara ya wafanyakazi wake. Ni aibu. Tumelogwa na nani kuwachafua wale wanaofanya mageuzi katika taasisi mbali mbali?
 

Huu nao ni udaku wa Dar ipi?

 
bashiru ana roho mbaya sana, amenyanyasa sana watumishi wa CCM makao makuu, huku yeye anayejinasabu mjamaa akiwa anapenda rushwa
Wewe sasa ndio unafahamu, Tulidhani Karma itawashughulikia miaka ijayo, 2025 na kuendelea imekuwa mapema zaidi ya tulivyodhani.

Hahah sasa hivi watakuja tuwahudumie kama wanachama wengine tu. wanachama wa mkopo hawakupaswa kuwa viburi na wanyanyasaji vile.

KM na NKM-Bara walikuwa wakiamua tu kuwa huna uwezo wa kushika ofisi fulani basi kesho barua inakufuata, WAGENI waliokuwa wanaamua kwa midomo fulani hafai na wanamleta fulani kutoka mikoa ya mbali kushika hiyo nafasi.

Karma mkali sana, wameondolewa wote hakuna salia hata moja, Wabara tuache roho mbaya tukipata nafasi, mbona wenzetu wa visiwano hawapo hivyo?

Eti kuna mtu anasema blah blah Bashiru na Polepole hawajakomolewa na chochote sababu wamepelekwa bungeni, Hivi mnajua ni kwa kiasi gani walizipenda ofisi walikotolewa!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…