Pre GE2025 Miongoni mwa kosa kubwa watakalolifanya CCM ni kumpitisha Samia Hassan kuwa mgombea wa urais

Pre GE2025 Miongoni mwa kosa kubwa watakalolifanya CCM ni kumpitisha Samia Hassan kuwa mgombea wa urais

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
nyie tutol
Kwanza samia ajiulize mwenyewe kama sio kifo cha jpm yeye angekua na nafasi gani kua rais wa nchi hii. Kwa uhakika yeye hakua chaguo la jpm kumrithi. Hakufiti kiitikadi kwa Magufuli kwa sera yake iliyojikita kwenye misingi ya ujamaa ya kujali maslahi ya umma na kujali wanyonge. Mama wala hana ujasiri uadilifu na uzalendo uliyoipaisha tanzania chini ya Magufuli. Samia ajitambue tu kama rais kwa katiba. Uzalendo wake utaonekana kwa kulisaidia taifa kupata kiongozi ajaye aina ya Magufuli. Akifanya hivyo atakumbukwa kwa heshima kubwa.
nyie wajinga. yaani mnataka kutuaminisha kuwa kipindi cha Mzee magufuli tulikuwa tunaishi peponi. kumbe maisha yalikuwa magumu tu na ndoo tukaja na msemo "wavyuma vimekazaa" . Acheni hizo bwana mama ni mpambanaji tunaona sana mafanikio yake ndani ya miaka yake hii minne
 
Hili litakuwa ni kosa kubwa sana na hata kama watafanikiwa kushinda kiti cha urais basi itakuwa kwa mbinde sana tena kwa mabavu.

Tangu akalie kiti cha urais, kwa haraka haraka hapo ulipo ukiambiwa ni kipi cha maana alichokifanya jibu ni hakuna.

Zaidi na zaidi ni kuineemesha Zanzibar kupitia mgongo wetu. Mikopo kila kukicha cha ajabu pesa zinaelekezewa ZNZ na wanaolipa ni watanzania bara.

CCM wanachotakiwa kukifanya kama bado wanamuhitaji basi wamsimamishe kama makamo wa rais na nafasi ya kugombea urais wamchague mwengine.

Uchaguzi utakuwa mrahisi sana kwa wapinzani kama SSH atagombea kiti cha urais.
Sasa kama kweli Samia ni mwepesi kushindwa na upinzani, kwa nini uwashitue?

Si ungekaa kimya tu ili upinzani muje mushinde kwa kishindo!!

Yaani eti Capatain wa Yanga anaipangia Simba kipa wa kuwa golini!!!! Uliona wapi??????
 
Yule bibi ile kazi ya jikoni ndio anayoiweza
Kwahiyo niye ccm mulimuona anaiweza kazı ya umakamu wa rais lakini mifahamu hana şifa za kuwa rais? Au kazi yenu kupiga tu hamjali?

Hamkufahamu kuwa hata rais akisafiri nje ya nchi yeye ndo anakaimu? Achilia mbali rais akiwa “incapacitated or dead “?!
 
Back
Top Bottom