Miradi mikubwa inayojengwa kasi imepungua sana, huko mbeleni tutaambiwa gharama zimeongezeka mara dufu

Yaani Wizara yako ya UJENZI imepewa Budget ya 55% lkn unasema hadi sasa mmetekeleza 60%

Naanza kupata wasiwasi nawewe unahusika kwenye upigaji au unaimba story za Makaratasi.
Siko wizara ya ujenzi,ila Niko kwenye industry ya ujenzi.
 
Kila mradi wa serikali huwa inachelewa na gharama.lazima ziongezeke kwa sababu za riba.

Sio Kweli, gharama zinaongezeka kwa mradi kuchelewa kumalizika Kwa Muda uliopangwa kama wakandarasi hawalipwi fedha zao kufuatana na mkataba!! At the sama time serikali haiwaadhibu contractors ambao hawamalizi miradi kufuatana na mikataba hivyo gharama kuongezeka!!!
 
Sasa kama Serikali ikichelewa kulipa si ndio wanadai riba mda wa mradi ukiisha..

Kusema mkandarasi anachelewesha Kazi ni nadra kwa sababu ni hatari kwake zaidi kuliko kwa client..

Hakuna cha adhabu zaidi ya kukatwa pesa na kuvunja mkataba,na ukivunja mkataba unamlipa chake..

Yale makelele ambayo huwa wanapiga wanasiasa wakati hawajalipa pesa huwa ni upuuzi.
 
Kipofu siyo lazima uwe umetoboka macho!!!
 
Daktari wa Kemia angalitufikisha hadi 2025, basi miradi mikubwa ingaliweza kukamilika, ijapokuwa deni la taifa labda lingalifika hafi 150Tn huku tukiaminishwa kuwa bado ni himilivu.

Ijapokuwa nilikuwa sikubaliani naye katika masuala ya utawala bora, lakini kwa msimamo wake thabiti katika kusimamia rasilimali za taifa, hakika huyu alikuwa ni mzalendo wa kweli.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…