Mirathi kwa watoto nje ya Ndoa

Mirathi kwa watoto nje ya Ndoa

Dini ipi ya kikristo au Kiislamu

Lakini pia kama dini inatambua hivyo ni Kwanini sasa mahakama inaenda kinyume ilihali mahakama inatambua sheria za mila, sheria za kidini nk

Dini ya Kiislamu.
Mahakama za Tanzania hazitoi hukumu zake kwa kutegemea sheria za dini.
 
MAHAKAMA TANZANIA YASEMA HAKUNA MWANAHARAMU, ILA KUNA WAZAZI HARAMU TU.

Kuna hukumu-rejea ilitolewa tarehe 28/5/2020 na Mahakama Kuu ya Tanzania, Kanda ya Dar es Salaam kupitia Mh. Jaji Mlyambina.

Ni hukumu ya kesi ya mirathi no. 50 ya mwaka 2016 (ina maana kesi ilichukua miaka 4 kwisha).

Ishu ya msingi katika kesi hiyo ni kuna mume wa mtu alifariki bila ya kuacha wosia. Aliacha mke ambaye alikuwa amemuoa kwa ndoa ya kikristo na watoto wa ndoa hiyo, na wengine wa michepuko (nje ya ndoa).

Watoto wa nje ya ndoa wakaweka pingamizi la mirathi maana walikuwa wameenguliwa wasipate kitu na msimamizi wa mirathi hiyo ambaye ni mtoto wa ndoa.

Wakati wa uhai wake, marehemu alikuwa anawasomesha watoto hao (ambapo wengine tayari walikuwa ni watu wazima), vyeti vyao vya kuzaliwa vilikuwa na jina la marehemu kama baba mzazi, na alishawatambulisha kwa mama yake na ndugu zake wengine.

Mahakamani mama na dada wa marehemu walitoa ushahidi kwamba wanawatambua hao watoto kama watoto wa marehemu.

Upande wa wa kwenye ndoa walikataa DNA test kufanyika kupima kama hao ni watoto wa marehemu.

Katika hukumu yake, Mahakama ikatumia sheria zifuatazo:

1. Katiba ambayo inasema watu wote ni sawa
2. Sheria ya Mtoto kifungu cha 5 ambacho kinakataza kubagua watoto
3. Sheria ya Mtoto kifungu cha 10 ambacho kinampa mtoto haki ya "ku-enjoy" mali ya mzazi wake.
4. Mikataba ya kimataifa kuhusu haki za mtoto ambayo Tanzania imeridhia.

Katika majumuisho yake, Mahakama ikasema, "Watoto hawana hatia maana hawachagui kuzaliwa au kwamba watazaliwa wapi. Msemo wa "kitanda hakizai haramu" maana yake ni hakuna watoto haramu. Ila kuna wazazi haramu."

Kwa hiyo mama za watoto wa nje ndoa ndo wakatambuliwa kwamba ni wazazi haramu na hawastahili kurithi mali ya marehemu. Ila watoto wa nje ya ndoa wakaingizwa katika orodha ya warithi, ambayo ilijumuisha na mjane wa marehemu na mama wa marehemu.

Pia ikaonekana mtoto wa ndani ya ndoa kusimamia mirathi hiyo haitakuwa vyema, ikateua Kabidhi Wasii Mkuu (yaani serikali) awe msimamizi.

------------------------------
Kwa kuwa hii ni hukumu-rejea kwa sasa hii ndo tafsiri ya sheria nchini Tanzania, mpaka pale itakapoamuliwa vinginevyo na Mahakama ya Rufaa, au mpaka Bunge litakapotunga sheria tofauti na tafsiri hii ya mahakama.

Je wewe unaonaje? Mahakama iko sahihi, au tuendelee kufuata misimamo ya kidini ambayo inawabagua watoto wa nje ya ndoa na watoto wanaozaliwa kabla ya ndoa?

Hukumu hii inapatikana hapa:[emoji116]

https://tanzlii.org/tz/judgment/hig...me-mwimbe-other-prob-admincause-no50-2016.pdf

Sent from my HUAWEI VNS-L31 using JamiiForums mobile app
Hii inaitwa mkanganyiko wa kisheria
 
Kwa hio?
Ibn zinaa maanake nini kwa kiswahili maarufu? Usilete hapa ubishi wenu wa kiwahabi right.
mtoto aliyetokana na zinaa ( wa kiume) ila hajaitwa wa haram, hiyo haramu ni matusi ya walimwengu
 
Mimi sio mtaalamu wa haya mambo ila kina rafiki yangu yeye na mme wake ni wakristo na mme kafariki mwaka juzi. Watoto wa mke wa ndoa ni wakubwa wote wana maisha yao halafu kuna kengine mme alizaa nje hat hajafika 10 years. Mme hakuacha wosia. Ila mahakama hawakumpa haki huyyu mtoto wa nje kwa kuwa mke wa ndoa ndio alikuwa main bread winner. Sana sana nyumba ya kijijini kwa baba ake ndio baba ake alijenga ikaamuliwa either iuzwe ili asomeshe au ipangishwe isaidie huyu mtoto wa nje. Lakini zile investments kubwa zote ni jasho la mke wa ndoa so watoto wake wanastahili kufaidi jasho la mama yao.
 
Dini ya Kiislamu.
Mahakama za Tanzania hazitoi hukumu zake kwa kutegemea sheria za dini.
Okey,
Sasa unakuta watoto wa nje wana miaka chini ya 18

Na watoto wa ndoa wako above 18

Kwenye mgao kama watoto wote wana haki pia sheria inaanglia umri watoto wenye umri mdogo watapewa zaidi, sasa kwa kesi hiyo hao watoto wa nje ambao wapo chini ya miaka 18 watapewa zaidi kuliko wa watoto wa ndoa hii imekaaje mkuu, yani kama pesa wawo wana mgao mkubwa kwenye hili mahakama wanalitekelezaje?
 
Mimi sio mtaalamu wa haya mambo ila kina rafiki yangu yeye na mme wake ni wakristo na mme kafariki mwaka juzi. Watoto wa mke wa ndoa ni wakubwa wote wana maisha yao halafu kuna kengine mme alizaa nje hat hajafika 10 years. Mme hakuacha wosia. Ila mahakama hawakumpa haki huyyu mtoto wa nje kwa kuwa mke wa ndoa ndio alikuwa main bread winner. Sana sana nyumba ya kijijini kwa baba ake ndio baba ake alijenga ikaamuliwa either iuzwe ili asomeshe au ipangishwe isaidie huyu mtoto wa nje. Lakini zile investments kubwa zote ni jasho la mke wa ndoa so watoto wake wanastahili kufaidi jasho la mama yao.
Safi sana umetoa mfano mzuri sana, hilo linawezekana ndiyo, na ndoa za kikristo zina masharti sana, kuna wakati mke wa ndoa wa marehemu ambae alifunga ndoa ya kikristo ya mke mmoja na mume mmoja yeye kama yeye anapewa usimamizi na kumiliki mali za mume wake kama kuna mtoto wa nje ni yeye akiamua kugawa au lahasha.
 
Ndiyo napitia sheria hapa mama watoto ili vimada wasije kukusumbua [emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787] [emoji1787] [emoji1787] [emoji1787] [emoji1787]
Wosia unasaidia sana, kuepusha mlolongo mrefu kama huu sasa
 
Umeshindwa kujibu kwanini Waislamu uwanyime haki ya ku-practice dini yao wakati katiba imewapa haki hiyo, hali kadhalika sheria ya mirathi inawapa hiyo haki. Na kwavile umeshindwa kujibu, better nikupuuze kwa sababu ibara ulizotaja hazijibu maswali niliyokuuliza!!!
Usichoelewa haki inayotajwa ibara ya 19 ya katiba ni uhuru wa kuabudu na kueneza dini na siyo haki ya kutumia dini yako kubagua wengine.Limitation ya haki ni pale haki yako inapoingilia haki ya mwingine na ku undermine serikali.Tunachojadili hapa siyo haki ya kuabudu ni haki ya kurithi.Unajaribu kuchanganya mada eti ile kesi ya Kenya yule bwana alikuwa mwisilamu jina.Yule alikuwa mwisilamu na ndo maana mirathi iliamuliwa na Kadhi.Kwakuwa kwa mujibu wa sheria ya kiislamu haiwezi kutumika kuamua hatima ya asiye muislamu,mama na watoto wake walienda mahakama kuu na kisha rufaa na wakapata haki kwa kuwa jurisdiction ilikuwa ni high court na sheria husika ni .Unaweza Succession Act na si Islamic law kwakuwa mama na watoto hawakuwa waislamu kudai mbona haitokei Sana Ni kwamba mtu akiishi dini yake ni ngumu kuzaa nje ya ndoa na kwa waislamu wanaruhusa ya kuongeza mke hivyo katika urithi watoto na mama zao kuwa halali mbele ya sheria ya kiislamu.Ikitokea tofauti sheria ya kidini inapoteza jurisdiction juu ya shauri husika.Acha kuchanganya haki ya kuabudu na haki ya kurithi.
 
Dini ya Kiislamu.
Mahakama za Tanzania hazitoi hukumu zake kwa kutegemea sheria za dini.
Shehe,kwenye ndoa,talaka,mirathi sheria ya kiislamu na kimila zinatumika lakini pale ambapo wahusika wote ni waislamu na wanaishi Kama waislamu na Kama sheria husika haikinzani na sheria za nchi na katiba yake.Zinapokiuka sheria za nchi ama wahusika wa kesi siyo si wa dini hiyo basi sheria ya dini inawekwa kando.
 
Mimi sio mtaalamu wa haya mambo ila kina rafiki yangu yeye na mme wake ni wakristo na mme kafariki mwaka juzi. Watoto wa mke wa ndoa ni wakubwa wote wana maisha yao halafu kuna kengine mme alizaa nje hat hajafika 10 years. Mme hakuacha wosia. Ila mahakama hawakumpa haki huyyu mtoto wa nje kwa kuwa mke wa ndoa ndio alikuwa main bread winner. Sana sana nyumba ya kijijini kwa baba ake ndio baba ake alijenga ikaamuliwa either iuzwe ili asomeshe au ipangishwe isaidie huyu mtoto wa nje. Lakini zile investments kubwa zote ni jasho la mke wa ndoa so watoto wake wanastahili kufaidi jasho la mama yao.
Hapa Ni sawa,Tanzania Kwanza hakuna mtoto haramu,kama Kuna sheria inamtaja mtu hivyo hiyo sheria na taratibu Ni unconstitutional.Katika kumiliki mali kwa wanandoa Kuna Mali binafsi na Mali ya pamoja,kwa kesi hiyo dogo alistahili kurithi kwa baba yake tu.
 
Shehe,kwenye ndoa,talaka,mirathi sheria ya kiislamu na kimila zinatumika lakini pale ambapo wahusika wote ni waislamu na wanaishi Kama waislamu na Kama sheria husika haikinzani na sheria za nchi na katiba yake.Zinapokiuka sheria za nchi ama wahusika wa kesi siyo si wa dini hiyo basi sheria ya dini inawekwa kando.

Asante kwa elimu ndugu[emoji1431]
 
Okey,
Sasa unakuta watoto wa nje wana miaka chini ya 18

Na watoto wa ndoa wako above 18

Kwenye mgao kama watoto wote wana haki pia sheria inaanglia umri watoto wenye umri mdogo watapewa zaidi, sasa kwa kesi hiyo hao watoto wa nje ambao wapo chini ya miaka 18 watapewa zaidi kuliko wa watoto wa ndoa hii imekaaje mkuu, yani kama pesa wawo wana mgao mkubwa kwenye hili mahakama wanalitekelezaje?

Ni hivi mkuu: mtoto aliezaliwa nje ya ndoa bila kujali umri wake harithi kabisa/chochote kwa baba yake na pia baba yake halazimiki kumhudumia. Anarithi tu kwa mama yake na ndie mwenye majukumu ya kumlea na kumtunza kwa kila kitu. Ama kuhusu mambo ya mahakama sijui.
 
Back
Top Bottom