Mirathi ya nyumba iliyojengwa na mjane yazua balaa; ukoo wa mume na ukoo wa mke wanaigombania

Mirathi ya nyumba iliyojengwa na mjane yazua balaa; ukoo wa mume na ukoo wa mke wanaigombania

FRESHMAN

JF-Expert Member
Joined
Sep 29, 2011
Posts
9,137
Reaction score
34,793
Habari wadau.

Kama mnavyojua suala la mirathi linavyotolewa macho hapa Tanzania.

Jirani kwetu kuna mama amefariki na kuacha nyumba nzuri tu na hajaacha mtoto hata mmoja.

Historia ya huyu mama (kabila mpogoro) mwaka 1991 aliolewa kwa ndoa ya kanisani na mume wake (kabila mchaga)

Baada ya kufunga ndoa walinunua kiwanja na mume wake na kuzaa mtoto mmoja wa kiume.

Mwaka 1994 mume wa huyu mama alifariki na kumuacha mke na mtoto mmoja wakiwa hai.

Taratibu za mirathi ya mume wake zilifanyika baada ya msiba. Mama na huyo mwanae wakapewa hiko kiwanja maeneo ya tegeta kikiwa kitupu hakijaanzwa ujenzi wowote.

Maisha yakaendelea. Mama huyu hakuolewa tena . Aliendelea kuishi na mwanae kwa kupanga nyumba ya NHC keko. Na mdogo mdogo akaanza ujenzi wa nyumba katika kiwanja walichoachiwa na mumewe.

Alijenga nyumba nzuri tu ya kisasa. Na zingine ndogo ndogo pembeni za kupangisha. Maana kiwanja kilikuwa kikubwa sana (maana enzi wananunua tegeta ilikuwa pori ardhi haina thamani miaka ya 90 muuzaji anakuuzia bonge la kiwanja kwa bei ndogoo)

Baada ya kumaliza ujenzi yeye na mwanae waliendelea kuishi nyumba ya NHC na kule tegeta walipojenga wakapangisha wapangaji kadhaa.

Mwaka 2015 mama alipata msiba mwingine wa kufiwa na mtoto wake huyo mmoja kwa ajali ya gari na hii ikamfanya mama kubaki peke yake bila mtoto wala mume.

Mama akaendelea kuishi mwenyewe mpaka na yeye mama alipofariki mwaka huu mwanzoni.

Mwili wa mama ulisafirishwa kwenda moshi kuzikwa walipozikwa mume wake na mwanae.

Shida imekuja kwenye nyumba zilizojengwa na huyo mama. Ukoo wa mume unasema ni mali zao. Na ukoo wa mke nao unasema ni mali zao maana zimejengwa kipindi mume wa huyo mama ameshafariki.

Wataalamu wa mirathi Kesi kama hii upande upi kati ya ukoo wa mume na ukoo wa mume una haki ya kurithi hizo mali za huyu mama.

Wazazi wa huyu mama wote wameshafariki pia.
 
Mimi sijui kabisa sheria lakini kuna maswali ya machache ya kujiuliza?
  1. je baada ya mume wa marehemu kufariki nini kiliamliwa kwenye miradhi
  2. kama mke alikubali kuwa mjane na atabaki kama mwanafamilia je wanafamilia walihusika vipi na malezi ya mtoto wa ndugu yao?
  3. mawasiliano yalikuwaje kati ya familia iliyooa na mjane wakati wa uhai wake?
  4. Je walikuwa na mchango wowote
na mengine mengi mwisho wa siku busara inaweza kutumika kwa familia zote mbili kugawana wakipata ratio ya 2:3
 
Wote hawana haki bali wanatakiwa kwenda mahakamani mali igawanywe kwa hao ndugu. Mahari aliyetoa alishafariki hivyo ndugu wa mume hawana haki ya kusingizia mahari,mjane harithiwi mkuu
mwanamke kama alilipiwa mahari hao ndugu wa mwanamke hawana wanachodai kwa upande huo alioolewa huyo mwanamke. wanachotaka kufanya hakina tofauti na wizi
 
Wote hawana haki bali wanatakiwa kwenda mahakamani mali igawanywe kwa hao ndugu. Mahari aliyetoa alishafariki hivyo ndugu wa mume hawana haki ya kusingizia mahari,mjane harithiwi mkuu

Alipozikiwa Huyo mjane ndio wanauhalali WA hizo Mali.
Mbona iko wazi kabisa.
Ingawaje ni busara Mali ikauzwa wakagawa kulingana na upendo walionao.

Mambo ya kugombea Mali ni Watu kutokujua mipaka Yao.
 
Uhalali upo sababu mume alitoa mahari na pia mwanae kazikwa hapo. Mfumo mnaoutetea ulishapitwa na wakati.
Alipozikiwa Huyo mjane ndio wanauhalali WA hizo Mali.
Mbona iko wazi kabisa.
Ingawaje ni busara Mali ikauzwa wakagawa kulingana na upendo walionao.

Mambo ya kugombea Mali ni Watu kutokujua mipaka Yao.
 
Uhalali upo sababu mume alitoa mahari na pia mwanae kazikwa hapo. Mfumo mnaoutetea ulishapitwa na wakati.
Alipozikiwa Huyo mjane ndio wanauhalali WA hizo Mali.
Mbona iko wazi kabisa.
Ingawaje ni busara Mali ikauzwa wakagawa kulingana na upendo walionao.

Mambo ya kugombea Mali ni Watu kutokujua mipaka Yao.
 
Uhalali upo sababu mume alitoa mahari na pia mwanae kazikwa hapo. Mfumo mnaoutetea ulishapitwa na wakati.
Alipozikiwa Huyo mjane ndio wanauhalali WA hizo Mali.
Mbona iko wazi kabisa.
Ingawaje ni busara Mali ikauzwa wakagawa kulingana na upendo walionao.

Mambo ya kugombea Mali ni Watu kutokujua mipaka Yao.
 
Habari wadau.

Kama mnavyojua swala la mirathi linavyotolewa macho hapa Tanzania.

Jirani kwetu kuna mama amefariki na kuacha nyumba nzuri tu na hajaacha mtoto hata mmoja.

Historia ya huyu mama ( kabila mpogoro) mwaka 1991 aliolewa kwa ndoa ya kanisani na mume wake ( kabila mchaga)

Baada ya kufunga ndoa walinunua kiwanja na mume wake na kuzaa mtoto mmoja wa kiume.

Mwaka 1994 mume wa huyu mama alifariki na kumuacha mke na mtoto mmoja wakiwa hai.

Taratibu za mirathi ya mume wake zilifanyika baada ya msiba. Mama na huyo mwanae wakapewa hiko kiwanja maeneo ya tegeta kikiwa kitupu hakijaanzwa ujenzi wowote.

Maisha yakaendelea. Mama huyu hakuolewa tena . Aliendelea kuishi na mwanae kwa kupanga nyumba ya NHC keko. Na mdogo mdogo akaanza ujenzi wa nyumba katika kiwanja walichoachiwa na mumewe.

Alijenga nyumba nzuri tu ya kisasa. Na zingine ndogo ndogo pembeni za kupangisha. Maana kiwanja kilikuwa kikubwa sana ( maana enzi wananunua tegeta ilikuwa pori ardhi haina thamani miaka ya 90 muuzaji anakuuzia bonge la kiwanja kwa bei ndogoo..)

Baada ya kumaliza ujenzi yeye na mwanae waliendelea kuishi nyumba ya NHC na kule tegeta walipojenga wakapangisha wapangaji kadhaa.

Mwaka 2015 mama alipata msiba mwingine wa kufiwa na mtoto wake huyo mmoja kwa ajali ya gari na hii ikamfanya mama kubaki peke yake bila mtoto wala mume.

Mama akaendelea kuishi mwenyewe mpaka na yeye mama alipofariki mwaka huu mwanzoni.

Mwili wa mama ulisafirishwa kwenda moshi kuzikwa walipozikwa mume wake na mwanae.

Shida imekuja kwenye nyumba zilizojengwa na huyo mama. Ukoo wa mume unasema ni mali zao. Na ukoo wa mke nao unasema ni mali zao maana zimejengwa kipindi mume wa huyo mama ameshafariki.

Wataalamu wa mirathi Kesi kama hii upande upi kati ya ukoo wa mume na ukoo wa mume una haki ya kurithi hizo mali za huyu mama
Kwa mujibu wa sheria ya ndoa, mali inayopatikana KATIKA ndoa ni mali ya wanandoa-ni marital property. Hata mtu ujifanye unajenga kisirisiri. Ukifa ikajulikana hiyo nyumba au mali inakuwa ya mwenzako aliyebaki hai. Hata mkeo akihongwa ujue pesa au mali aliyohogwa ni yenu ninyi nyote wawili katika ndoa. Na mume wa mtu ukihonga ujue umemfanya hata mkeo akahonga😀

Kwa kesi ya huyu mama mali aliyopata baada ya mume kufa nadhani ni yake yeye peke yake, maana ndoa ilivunjwa na kifo, hivyo ndugu zake wana haki juu ya mali hiyo.
Ikiwa kuna mali walipata pamoja na mumewe, ni mali ya wanandoa....hivyo ndugu zao wote (nadhani hasa wazazi wao pande zote mbili) wana haki kwa mali hiyo kwa kuwahurumia tu wazazi wa marehemu mume maana alipokufa mali was transfered kwa mke.
 
Ni kwamba ndugu wa mume hawahusiki maana ndoa ilishavunjwa kwa sababu alishakufa mume..Mali zilishakuwa transfered kwa upande wa mke kama kiwanja ni Mali ya mke kwa kuachiwa na mumewe yeye akajenga bila msaada wa Mume alikuwa marehemu

Hao ndugu wa mume wanatokea wapi kama sio Tamaa?
Imagine huyo mama angekufa akiwa kaolewa na mtu mwingi izo Mali zingeenda hata kwa huyo Mume wake mpya..yule marehemu hana chake kwanza hakuacha nyumba.
 
Back
Top Bottom