Misa ya Mkapa: Nimeona tofauti kubwa kati ya maaskofu wa Katoliki na wale wa makanisa kama la Gwajima!



Mmh!
 
Ewe unayefahamu lakini kwa kusudi la kupotoa mafundisho ya Kristo na wewe unaamua kupotosha ili hali unajua na unaelewa. Inatakiwa uelewa huo sasa umgeukie Kristo, uache kujilisha upepo na mafundisho ya warumi yaliyo maagizo ya wanadamu.

Nimefurahi unajua hakika Yesu ndiye mwanzilishi wa Kanisa na ndiye mmiliki wa kanisa. Swali pekee ambalo umeshindwa kulijibu ni kanisa lipi? Badala utoe jibu sahihi unarudi kwenye upotofu wako, wa kudhani ni kanisa katoliki, ndilo kanisa aliloanzisha Kristo. Pole sana.

Yesu alisema ataanzisha kanisa na akaanzisha kanisa karne ya 1, miaka 30-33 tu. Mitume wake wale 11, jumlisha mmoja 1, walifanya kazi ndani ya karne hiyo moja, na waliuwawa kwa namna mbalimbali kwa sababu ya injili ya Kristo.

Kanisa la warumi(roman catholic) limeanza karne ya 4, miaka 300+ baada ya kanisa la Yesu kuanza na kufanya kazi. Kazi ya kulihudumia kanisa la Kristo ni mbiyo za kijiti, waliachiana kijiti nasi tunaachiana kijiti. Miaka 320 baada ya Kristo kuondoka, ndipo mfalme Augustino wa dola ya kirumi alipotangaza kulegeza mateso na unyanyasaji kwa wakristo. Naye aliikubali na kuwa mkristo.

Hata hivyo, Augustino hakukubali kubatizwa kama walivyobatizwa wakristo wengine, alikubali ukristo, lkn hakufuata kanuni za ukristo hasa ya kubatizwa. Alinyunyizwa, na ndio likawa pokeo jipya la ubatizo wa kunyunyiza. Hautopata popote kwenye biblia, ni Augustino ndo aliamua.

Hivyo, pamoja na Augustino kukubali kuwa Mkristo, ilimweya vigumu kuacha mila na desturi za kirumi. Ndipo hapo sasa walipo kaa mezani wakaanzisha taratibu rasmi za kirumi za kumwabudu Mungu. Taratibu zote hizo hutazipata kwenye biblia, ila waliamua wenyewe. Baadhi ni yafuatayo:-

1. Dini kuambatana na uongozi wa serikali.
2. Dini kuanzisha utawala na kumiliki njia za kiuchumi.
3. Tamaduni za kirumi kukopwa na kutumika kama taratibu za kanisa la Kristo. Mfano, sherehe za Krismas hutazipata popote kwenye biblia, ni mipango ya kirumi.
4. Wakaanzisha litrugia na makao makuu ya kanisa la kirumi. Kumbuka makao makuu ya kanisa la Yesu ni kule aliko Yesu, alienda kutuandalia makao.
5. Wakaanzisha sala za maria, rozari ambavyo hutaviona kwenye biblia. Wakati biblia inasema *"....mimi ndiyo njia kwelo na uzima...."* warumi wakaanzisha utaratibu wa kuomba kupitia kwa Maria.

Walipindua mengi sana, mengi mno.

Haya, ukisema ni wakatoliki wali assemble biblia, nikubaliane na wewe kisha nikuulize yafuatayo.

1. Kwa nini sasa wapingane nayo? Biblia inasema "...msiitwe baba nyie duniani, kwa kuwa baba yenu ni mmoja naye ndiye Mungu...". Kwa nini wakatoliki mnao mababa?

2. Kama wao ndo walitengeneza biblia, kwa nini watofautiane na 1Timoth 3ff? Ambayo inataja sifa anuawai za mtu kuwa askofu? Na nani alikuambia, kwa andiko lipi Mtume Petro aliitwa askofu? Umeona wapi? Kuna tofauti ya mtu kuwa mtume, mwalimu, mwinjilisti na kuwa askofu. Askofu ana vigezo vyake vinavyopimika.

3. Wakusanye maandiko lkn washindwe kuliishi neno la ubatizo? Petro alibatizwa kwa kuzamishwa na wanafunzi wote na Yesu mwenyewe, kwa nini warumi hamzamishi?

Jambo lingine nikukumbushe, kanisa ni moja nalo ni la Kristo. Ile kutaja la warumi maana yake limeanzishwa na kumilikiwa na warumi. Waanglican limeanzishwa na kumilikiwa na waanglicani. Sasa kulisambaza dunia nzima kanisa lao, haina maaana kuwa ndio umoja unaotajwa wa kanisa la Kristo. Wanasambaza la kwao, anglican la kwao, fpct la kwao, full gospel la kwao n.k.
 
Maadam wanaendeleza mila na desturi za kirumi, hawapaswi kuitwa watumishi wa Kristo bali watumishi wa Rumi. Fahamu hilo
 
Acha upotoshaji katoliki ni kanisa linaloendesha mambo yake ovyo hovyo na wala hawana utaratibu wowote mzuri kama unavyodai
 
Kanisa Katoliki ni taasisi mambo yake ni ya kitaasisi tofauti na makanisa ya hao wahuni kama Gwajima
 
Nani kakudanganya kuwa Petro alikuwa papa wakwanza? Huo ni uongo na hakuna andiko linalosema hivyo.
 
Maadam wanaendeleza mila na desturi za kirumi, hawapaswi kuitwa watumishi wa Kristo bali watumishi wa Rumi. Fahamu hilo
Sina la kusema mkuu. Anaewaita ni Mungu alie juu, kwa kumtumikia kwa kufuata desturi za Vatcana au kwingineko,sina la kusema kabisa.
Ila itoshe tu kuwaheshimu kwa wao kuitikia wito wa "Alie juu"
 
Sina la kusema mkuu. Anaewaita ni Mungu alie juu, kwa kumtumikia kwa kufuata desturi za Vatcana au kwingineko,sina la kusema kabisa.
Ila itoshe tu kuwaheshimu kwa wao kuitikia wito wa "Alie juu"
Juu wapi mkuu? Vatcan ni juu? Asilimia 90 ya wanaylyafanya ni maagizo ya Vatican siyo juu. Hebu sona 1Timo 3, uone sifa za wanaoyafanya ya aliye juu
 
Ukiwakuta wana sali unaweza sema wanafukuza mwizi,kuna wengine haitoshi wao kabla ya kuombea wanaomba kipaza sauti,sasa sijajua shetani anaogopa kipaza sauti,yaani unaya treat maswala ya kiroho kwa kutumia njia za kimwili.

Yesu alikemea lakini si kwa style yao fujo tupu.
 
Na wewe nionyeshe andiko lisilosema hivyo [emoji23][emoji23][emoji23]
Andiko linalosemaje? Wewe ndo ulete andiko la Petro kuitwa papa. Halipo, ila lipo linalokataza ujinga huo wa kuitana baba mtakatifu.

Soma Mathayo 23:9 Wala msimwite mtu baba duniani; maana Baba yenu ni mmoja, aliye mbinguni. Wala msiitwe viongozi; maana kiongozi wenu ni mmoja naye ndiye Kristo.

Na kwa andiko hili ni uthibitisho wa hekaya zenu kuwa warumi ndio waliounganisha biblia, ilikuwaje wakakiuka andiko hilo?
 
Ndivyo mnavyojidanya mdogo wangu nilimwachia ziwa alitolewa pepo na padri bila hayo makelele yenu,kamshika kichwa kamwombea,kamwagia maji na alikuwa peke yake sisi tukiwa pembeni.

Mungi haitaji mbwembwe.
 
Uache utapeli wako mkuu. Wapi imeandikwa Peter ni Papa wa Kwanza? Wapi Petro alikabidhi huduma mtu mmoja na kumpa uongozi? Hivi nyie mnasoma biblia kweli?

Hebu soma Mathayo 23:9-12 halafu njoo tujadiliane tufute ujinga huo kwa pamoja

 
Juu wapi mkuu? Vatcan ni juu? Asilimia 90 ya wanaylyafanya ni maagizo ya Vatican siyo juu. Hebu sona 1Timo 3, uone sifa za wanaoyafanya ya aliye juu
Kwa misingi ya biblia, kuna mengi mazuri wanayofanya japo kwa kupungukiwa sifa ya kuwa wanandoa naomba nisitie neno hapa.
Ila itoshe kusema, "Yule mama aliekamatwa na mafarisayo akizini wakitaka apigwe mawe, Yesu hakumtia hukumuni japo alijua ametenda dhambi.

Principle aliyoitoa ni nenda usitende dhambi tena.

Kwa kuwa wajua wana nakisi ya kukidhi utimilifu wa maandiko, nikushauri uwatafute na kuwasaidie waijue kweli yote kibiblia na sio kufuata maelekezo ya Vatcana pekee.
 
Waliohoji maamuzi ya Vatican, siyo watawa tena. Mfanl Fr Nkwera hata huyu mwandishi Privatus Karugendo. Alihoji anakuwaje Padre ilo hali hana ndoa, leo anaendelea na ndoa yake japo ukatoliki bado umemzingira. Askofu Slaa aligundua hilo akajisalimisha kwa Mshumbusi lkn ukatoliki wa kufuata maagizo ya Vatican bado umemzinga.

Biblia iko wazi sana, haijatuficha jambo lolote ni sisi tu kukubali na kutii
 
[emoji3][emoji3] najaribu kufikilia paroko anavyokemea pepo kwa upole
"Toka pepoooo uende zakooo"
,,,[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…