Misemo kama ya aina hii inafaa kufutwa

Misemo kama ya aina hii inafaa kufutwa

"Mficha uchi hazai" hii methali imesababisha dada zetu kuvaa nguo za ajabu ajabu ilimradi wasiwe wagumba.
Misingi ya misemo ya zamani ya wazee wetu ilikuwa ni kukumea maovu, kuamrisha mema, na ukiona misemo kama hii ujue inazungumziwa kwa munasaba wa ndoa kwa maana ya kuchelewa chelewa kwani wao hawakuamini juu ya watoto wa nje ya ndoa.
 
mkianza kuchukulia hii misemo kama ilivyo mtaumia sana, hakuna kitu ya kufutwa hapa kila msemo unaweza kudadavuliwa kwa namna yake au mazingira husika.
 
Sio lazima iwe hivyo, inawezekana ikawa ni kinyume chake, yaani inawezekana kwa kumpa huyo mtoto mchawi ikawa ndiyo easy access kwake kumdhuru (nimechukua literally).

Ninachotaka kusema ni kwamba; hiyo tamathali ni tata kitu kikishakuwa tata kitaleta utata ya nini kukuchukua???.

Misemo / methali lazima zijenge na kufundisha jamii hekima (philosophy) zisizokuwa tata na sio kupotosha, misemo/methali ni sehemu ya lugha, sasa iweje tushike lugha potofu.

Ponder in that broder line.
Hapo mimi naona utata unauleta wew mtoa mada ila hiyo tungo sio tata.

Na utata wa tungo haimaanishi kuwa inapotosha jamii,naona unachanganya kuaminisha umma kuwa unachoamini ni sahihi.

Na ndio sababu haijawekwa maana moja kwa moja ili kila mtu atoe maana.leo ukiambiwa mtu ana mkono wa birika utahoji ni vipi mtu ana mkono uliojikunja,hutoishia hapo utahoji pia kuku anawezaje kutagia mibani....
 
"Mficha uchi hazai" hii methali imesababisha dada zetu kuvaa nguo za ajabu ajabu ilimradi wasiwe wagumba.
Hizi methali zote zina maana sana tu,,nadhani babu zetu wikuwa ni genus.. Hyo maana ya mficha uchi hazai sivyo Kama unavyofikiria wewe,, methali nyingi zinafanana ,,au zinapingana ili kukupa changamoto,,na zote zina maana,,mfano mficha uchi hazai,,na mficha maradhi kifo humuumbua,,zote ni maana moja,,kwamba ukificha tatizo mwisho wa siku ni tatizo kubwa zaidi,,au ukificha tatizo utasaidiwaje na wengine?eleza matatizo yako usaidiwe..hyo ndy maana,,unapaswa utafakari kwa kina maana hizi,,
 
Kabla hujaandika huu uzi ulitakiwa uwaulize Waswahili wanaitumiaje misemo hii. Uzi wako uneonyesha ni kwa namna gani hukijui unacho kiandika na hili ni tatizo kubwa. Mathalani msemo wa kwanza ulio unukuu, huwezi ukamkuta Mswahili anautumia bila kuzingatia muktadha wa hali,, muktadha wa hali ambao akiutumia msemo huo unaleta maana ya wazi kabisa, huo msemo wa pili, ndio daaah, uko wazi na kuwatahadharisha watu juu ya kutenda haki hata kwa mtu mnyonge wa namna gani,bali mpaka kwa mtu unaye mchukia.

Kwa ushauri wangu ni bora ututake radhi sisi Waswahili kisha uufute huu uzi.

Ahsante.


Niwatake radhi kwa kosa lipi??!!.

Kuongea kiswahili sio tiketi kwamba wajua kiswahili au wewe ni mswahili.

Misemo yenye maana katika lugha ni ile inayoakisi uhalisia wa jambo lenyewe, mfano ukisema; "Fimbo ya mbali haiui nyoka" maana yake fimbo iliyo jirani nawe ndio yakupasa uitumie kuuia nyoka kabla hujaenda kuchukua fimbo ya mbali, huo ndio uhalisia wa msemo/ methali hiyo, kitamathali unaweza kusema hivi; Fimbo ni mwanamume aliyekaribu (mahali anapoishi) na Nyoka ni mwanamke hivyo mwanaume aliyekaribu na mwanamke ndiye anayeweza "kupata mzigo" kuliko mwanamme aliyekuwepo mbali.

Sasa tuje kwenye uhalisia wa msemo; Mpe mchawi alee mtoto, Swali wewe unaweza kumpa mchawi alee mtoto wako???!!.

Lazima ujue kwamba misemo/methali lazima kwanza zijengwe kwenye uhalisia ndipo baadaye zije tafsiri zingine, kama uhalisia ni hovyo basi msemo nao unakuwa wa hovyo na haufai kuwepo katika lugha ya watu wastaarabu wenye hekima, Kiswahili ni lugha ya watu wenye hekima.
 
Ni mambo ya kushangaza kuona watu na akili na busara zetu bado tunashikilia misemo isiyokuwa na maana bali kupotosha jamii, eti utasikia ikisemwa; "Mpe mchawi alee mwanao" au utasikia; "Mnyonge mnyongeni lakini mpeni haki yake".

Mchawi ni mtu mbaya sasa iweje umpe mwanao amlee?!--- je akimfundisha uchawi au akimlisha nyama za watu utamlaumu nani??-- kama neno mchawi ni tamathali kwanini tamathali hiyo inathibishwa na kitu kibaya?

Pia utasikia Mnyonge mnyongeni lakini apewe haki yake, sasa mtu kisha nyongwa (kawa marehemu) ni kwa vipi atapewa haki yake?--- au atapenyezewa akiwa kaburini?

Misemo mingine ilitungwa na Wahenga waliotoka kunywa Pombe na katika zama hizi za haifai kuendelea kutumika kwani inafanya jamii iamini ujinga kuwa ni busara na hekima.
Utasikua hata mtu mkubwa kabisa serikalini anasema wapinzania wanapaswa kuuwawa.
 
Ni mambo ya kushangaza kuona watu na akili na busara zetu bado tunashikilia misemo isiyokuwa na maana bali kupotosha jamii, eti utasikia ikisemwa; "Mpe mchawi alee mwanao" au utasikia; "Mnyonge mnyongeni lakini mpeni haki yake".

Mchawi ni mtu mbaya sasa iweje umpe mwanao amlee?!--- je akimfundisha uchawi au akimlisha nyama za watu utamlaumu nani??-- kama neno mchawi ni tamathali kwanini tamathali hiyo inathibishwa na kitu kibaya?

Pia utasikia Mnyonge mnyongeni lakini apewe haki yake, sasa mtu kisha nyongwa (kawa marehemu) ni kwa vipi atapewa haki yake?--- au atapenyezewa akiwa kaburini?

Misemo mingine ilitungwa na Wahenga waliotoka kunywa Pombe na katika zama hizi za haifai kuendelea kutumika kwani inafanya jamii iamini ujinga kuwa ni busara na hekima.
Mnyonge mnyongeni inatumiwa sana awamu inayojinasibu kutetea wanyonge. Wananyongwa mchana kweupe. Haki yao wataipata makaburini.
 
Utakuwa huzielewi maana za hizo methali/misemo. Tafuta maana yake halafu urudi hapa
 
Mchawi mpe mwana alee- katika jamii kama wengi mmekubaliana jambo mmoja mmemtambua anakubali kinafiki ndio afanywe kuwa kinara.

Mfano ; mmepanga kujitolea kuchimba mtaro mtaani mmoja mnamuona anakubali kinafiki , yy huyo ndo mnamkabidhi sululu.

Mnyonge ,mnyongeni lkn haki yake apewe!- jamii iache dhulma, mwanajamii bila kujali hadhi yake akikosa aadhibiwe, akiwa hana kosa apewe stahiki yake.

Wahenga hakuna walichoacha ! Misemo ya sasa ndo ya MATEJA.
 
Tamathali za semi ni lazima ziwe "conceivable".---- inatakiwa ziendane na hali halisi ya tungo mama.

Hivi kiuhalisia, wewe unaweza kumpa mchawi amlee mwanao??!, mchawi ni shetani iweje umkabidhi ili amlee??.

Hii inaweza kusababisha watu wengine nao walete tungo zao mfano; "Ukitaka kujua ubaya wa dhambi mfuate shetani". ---je tamathali kama hiyo inaingia akilini???.

Tafakari.
Kuna kipindi nilipotoka chuo na kurudi home mzee alisema maneno huku akinikabidhi duka lake ili niliendeshe

Mwanzo sikujua maana yake ila nilipoanza kushika shika viela vya pale zote zikawa zinaishia kwny anasa

Mzee alipoona hvy ilibidi nikabidhi funguo nikapauka sana

Kweli " MPE mchawi mwanao amlee"

Hapo duka ndio lilikua mtoto kwakua nilikua mchawi nikaa kuliroga..
 
Kuna kipindi nilipotoka chuo na kurudi home mzee alisema maneno huku akinikabidhi duka lake ili niliendeshe

Mwanzo sikujua maana yake ila nilipoanza kushika shika viela vya pale zote zikawa zinaishia kwny anasa

Mzee alipoona hvy ilibidi nikabidhi funguo nikapauka sana

Kweli " MPE mchawi mwanao amlee"

Hapo duka ndio lilikua mtoto kwakua nilikua mchawi nikaa kuliroga..


Hao wanaopinga wakisoma maelezo yako nadhani watanielewa. 🤣
 
Kama sikosei kuna tasnifu ya uzamili (Masters) iliyoandikwa na mwanafunzi wa chuo kikuu cha Osaka au Leiden (sikumbuki vizuri) kuhusu Methali za Kiswahili na Mabadiliko ya Sayansi na Teknolojia. Ukienda pale Mlimani unaweza kuibahatisha au ukigoogle pia waweza kuipata. Nitajaribu pia kuisaka na nikiipata nitaiweka hapa.

Misemo na methali ni sehemu ya lugha, na lugha ni sehemu ya jamii. Lugha ni kiumbe hai na huakisi maendeleo ya jamii husika katika uhalisia wake nayo hubadilika badilika kulingana na maendeleo hayo. Si jambo la ajabu basi kuona kuwa baadhi ya misemo, methali na nahau zikipigwa dafrau na maendeleo ya jamii husika na hulazimu ama kubadilishwa na jamii lugha au kuachwa kabisa. Ni jambo la kawaida katika lugha zote duniani.

Ni wazi methali kama pole pole ndiyo mwendo na haraka haraka haina baraka katika dunia ya sasa inabidi ziangaliwe kwa jicho jipya. Mambo ya aliye juu mngoje chini...mh! Kizazi cha sasa hakina muda wa kumngoja mtu mpaka ashuke mwenyewe bali kinamfuata huko huko na kumshusha kwa nguvu au kinampopoa mawe tu anashuka mwenyewe bila kupenda.

Na kabla ya kuzitolea kauli ya mwisho methali hizi, inabidi kwanza kuelewa vizuri muktadha na utamaduni zilimotumika na lengo kuu la kuanzishwa kwake. Ukiongea na wazee watakwambia hasa lengo la methali/misemo kama mnyonge mnyongeni lakini haki yake mpeni lilikuwa ni nini na ukijua mazingira halisi ya matumizi yake ndiyo utaona busara kuu iliyojificha katika methali hiyo; na nyinginezo.

Lugha, katika ujumla wake, ni tata mno na imebeba historia, mila, falsafa na utamaduni wa watu japo tunaichukulia kijuu juu tu...
Ndugu yangu asante sana. Maelezo yako yanaonyesha umebobea kwenye hii fani. Kwa kifupi yanaelimisha sana. Mimi nadhani misemo na methali nyingi hazipitwi na wakati (naomba nisieleke kuwa napinga kuna mingine inapitwa). Hebu tuchukulie msemo kama ''haraka haraka haina baraka''. Huu msemo haiuhimizi watu wasifanye mambo kwa haraka kama wengi wanavyodhani. Huu msemo unahimiza watu kuwa na ustahamilivu kwa mambo yanahitaji muda kufikia lengo lake. Unawataka watu wasifanye short-cut kwa mambo yanahitaji process ndefu ili kufikia lengo. Hata hiyo mifano aliyotoa mwanzisha thread bado ina mantiki na mafunzo mazuri tu kwa jamii. Ila naona jamaa yeye anatafsiri kama ilivyo ndiyo maana anaona haifai. Misemo ya kupiga vita ni kama hii ya wanasiasa wa siku hizi wanayosema eg ''mheshimiwa ukiona inakupendeza.........''.
 
Kabla hujaandika huu uzi ulitakiwa uwaulize Waswahili wanaitumiaje misemo hii. Uzi wako uneonyesha ni kwa namna gani hukijui unacho kiandika na hili ni tatizo kubwa. Mathalani msemo wa kwanza ulio unukuu, huwezi ukamkuta Mswahili anautumia bila kuzingatia muktadha wa hali,, muktadha wa hali ambao akiutumia msemo huo unaleta maana ya wazi kabisa, huo msemo wa pili, ndio daaah, uko wazi na kuwatahadharisha watu juu ya kutenda haki hata kwa mtu mnyonge wa namna gani,bali mpaka kwa mtu unaye mchukia.

Kwa ushauri wangu ni bora ututake radhi sisi Waswahili kisha uufute huu uzi.

Ahsante.
Asante sana sana kwa elimu. Mwanzisha thread yeye anaichukulia misemo kama ilivyo. Hivi siku hizi somo la lugha limeondolewa jamani?
 
"Mficha uchi hazai" hii methali imesababisha dada zetu kuvaa nguo za ajabu ajabu ilimradi wasiwe wagumba.
Hiyo ni tafsiri yako lakini msemo hauna nia ya kuhimiza watu wafanye ngono. Fasihi haifundishwi tena siku hizi?
 
Ndugu yangu asante sana. Maelezo yako yanaonyesha umebobea kwenye hii fani. Kwa kifupi yanaelimisha sana. Mimi nadhani misemo na methali nyingi hazipitwi na wakati (naomba nisieleke kuwa napinga kuna mingine inapitwa). Hebu tuchukulie msemo kama ''haraka haraka haina baraka''. Huu msemo haiuhimizi watu wasifanye mambo kwa haraka kama wengi wanavyodhani. Huu msemo unahimiza watu kuwa na ustahamilivu kwa mambo yanahitaji muda kufikia lengo lake. Unawataka watu wasifanye short-cut kwa mambo yanahitaji process ndefu ili kufikia lengo. Hata hiyo mifano aliyotoa mwanzisha thread bado ina mantiki na mafunzo mazuri tu kwa jamii. Ila naona jamaa yeye anatafsiri kama ilivyo ndiyo maana anaona haifai. Misemo ya kupiga vita ni kama hii ya wanasiasa wa siku hizi wanayosema eg ''mheshimiwa ukiona inakupendeza.........''.




Mkuu labda utakuwa hujanielewa vyema, nasema hivi; Msemo au methali kimsingi lazima kwanza iwe na maana ya moja kwa moja (literal sense) na baada ya hapo ndipo maana zingine hufuata, umetoa mfano wa; "Haraka haraka haina baraka" na ukatolea ufafanuzi na mimi naafiki ufafanuzi wako lakini maelezo yako yanaendana na uhalisia wa huo msemo yaani hakuna contradiction hapo na mimi sina shida na misemo ya aina hiyo ambayo uhalisia wake unaendana na tafsiri yake (intrepretation).

Shida ipo kwenye uhalisia wa; "Mpe mchawi amlee mwanao" je, tunaweza kupata tafsiri yake inayoendana na uhalisia wake?? (literal). Uhalisia ni kumpeleka mtoto wako kwa mchawi ili amlee, je unaweza??!.

Tafsiri na uhalisia ni muhimu vikubaliane/viendane ndipo msemo unakuwa na maana ya kimantiki.

Na huo ndio uzuri na utamu wa lugha, lugha ikiwa na maneno yasiyo na mantiki hiyo ni lugha mbovu.

Tujenge Kiswahili chetu tusikibomoe.
 
Mkuu labda utakuwa hujanielewa vyema, nasema hivi; Msemo au methali kimsingi lazima kwanza iwe na maana ya moja kwa moja (literal sense) na baada ya hapo ndipo maana zingine hufuata, umetoa mfano wa; "Haraka haraka haina baraka" na ukatolea ufafanuzi na mimi naafiki ufafanuzi wako lakini maelezo yako yanaendana na uhalisia wa huo msemo yaani hakuna contradiction hapo na mimi sina shida na misemo ya aina hiyo ambayo uhalisia wake unaendana na tafsiri yake (intrepretation).

Shida ipo kwenye uhalisia wa; "Mpe mchawi amlee mwanao" je, tunaweza kupata tafsiri yake inayoendana na uhalisia wake?? (literal). Uhalisia ni kumpeleka mtoto wako kwa mchawi ili amlee, je unaweza??!.

Tafsiri na uhalisia ni muhimu vikubaliane/viendane ndipo msemo unakuwa na maana ya kimantiki.

Na huo ndio uzuri na utamu wa lugha, lugha ikiwa na maneno yasiyo na mantiki hiyo ni lugha mbovu.

Tujenge Kiswahili chetu tusikibomoe.
Asante sana. Una uelewa mpana sana kwenye hii fani.
 
Uzi mfupi**

Wachawi wanapatia changamoto nying wanapotaka kukuroga, kwanza inabidi atafute pesa ya kununulia Vifaa Vya kazi
Kununua Vifaa Vya kazi ni gharama kubwa na Muda mwingine itamlazimu kusafiri ata nje ya Mkoa ili akanunua kifaa icho cha kukurogea

Kwa mfano Kuna uchawi mwingine ili ufanyike mchawi ataitaji maji ya maiti
upatikanaji wa maji ya maiti ni mgumu sana,

Yani inabidi uwe na koneksheni ya kufa mtu ili upate maji ya maiti na maana muda mwingine unaweza uziwa maji feki
Kwaiyo katika hali kama iyo mchawi inabidi atoe pesa ndefu ili kufanikiwa

Mchawi ni mtu mbishi sana yana hakubali kushindwa kabisa
Kitu ambacho kinamuumiza sana mchawi ni pale anapotumia nguvu nying kukuroga alafu ww unaleta dharau

Yani yeye anapokuroga anataka kuona matokeo yani anataka kukuona umepaniki
Mchawi Anaskia raha sana pale anapoona kwamba umepaniki alafu umekimbilia kwa mganga

Changamoto kubwa kwa mchawi ni kuona kwamba badala ya kupaniki lakini ww ukamua kufanya ibada yan ukasimama na MUNGU
Mda mwingine mchawi inabidi akijifunze teknolojia ambayo itamsaidia kukuroga

Hapa inabid aende kozi iyo maalumu na inabidi alipie pesa kwa ajili ya kupata utaalamu
Upatikanaji wa Vifaa Vya kurogea imekuwa changamoto kubwa kwa Wachawi

Maana katika maduka ya kawaida ya asili havipatikani
Madalali wanaouza Vifaa Vya kurogea wamekuwa wakiwauzia wachaw Vifaa ivyo kwa bei juu sana

Kwa mfano mchawi ili aingie kwako lazima awe na testa ili aone kama kuna mtego au hamna
Testa ya kichawi inauzwa bei juu sana maana bila ya testa unaweza jikuta unaingia mtegoni

Kama ulishawai ona mchawi Kanasa juu ya bati au ameanguka basi jua uyo ameingia bila testa
Wachawi wanatumia pesa nyingi sana kununua Vifaa Vya kurogea pande za mahospitali na makaburini

Mara nyingine mchawi anajikuta anamadeni mengi sababu anataka afanikiwe kukuroga
Akishakuroga itambidi afatilie mara kwa mara maendeleo yako ili aone kama uchawi unafanya kazi

Muda mwingine inabidi afanye update yani kama vile Ana update windows

AsanteniView attachment 1495584
 
Back
Top Bottom