Misemo kutokana na Vichwa vya Treni

Navyo vichwa vya treni vikaulizana kwa sauti ya chini je sisi ni yatima au tuna wazazi. Kwa pamoja vikajibu hatujui, tunahitaji kuundiwa tume iliyo tukuka
Makirikiri 3:5
 
Ndipo kuwani yule akamuuliza mtoto wa mfalme kwanini nyumbani kwako matokeo ya wanafunzi ni mabaya kiasi hiki?
Naye bila kupepesa macho akajibu kwa ujasiri akisema'je ni wapi dunia hii uliposhuhudia vita ya madawa ikimuacha mtu salama? Sileti Vyeti 10.1-7.
 
Hakika bavicha wakaandamana kila kona ya mji na kulisifu jina lake na adumu milele bwana wao kwa nehema zilizotukuta za vichwa vya treni.kibiti 3:4-9
 
Nao wakastaajabu ya Musa, vichwa vya treni viliposhuswa toka mawinguni. Wakaandaa sherehe wakatwaa mikate isiyotiwa makinikia na mvinyo wakala na kunywa.

Waraka wa pili wa Bashite kwa wanadarisalama 2: 23-27
 
Basi ukimya ukatawala pande zote za nchi na kustaajabu muujiza wa ujio wa vichwa vya treni, mara watumishi hewa wakaibuka toka buzwagi wakisema, eeeh bwana ni kwanini ulitufuta katika kitabu chako malisho ya kila mwezi.

Tazama sasa hao akina bwana mipango uliowaamini walivyokutenda mchana kweupe. Nchi hii haiendeshwi kwa kiki tu bali ujue na matumiz klachi.

Ndipo watoto waja wepesi nao wakasemezana taratibu, mkuu tupotezee nasi tukapige pindi kama ulivyowapotezea wana wa kolomije. Uhakiki endelevu. 0:0-0
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…