Mitaala ya somo la Historia iliyositishwa ilijaa propaganda za kumsifu Magufuli kuwa ni kinara wa mabadiliko nchini

Status
Not open for further replies.
Katiba mpya hazizuzii kina Magufuli.

Kina Magufuli huwa hawafuati KATIBA.
Katiba ya Sasa inampa mamlaka rais kuingiza kichwa kwenye mifumo takriban yote huku wakituhadaa kuwa hatoingia mzima. Sasa wewe unaelewa Tembo akiingiza kichwa atashindwaje kuingia mzima akitaka?

Tunataka katiba ambayo kuna baadhi ya vitu hata kuvisogelea tunampiga stop achilia mbali hiyo nafasi ya kuingiza kichwa!

Vitu kama mahakama na bunge raisi anapaswa akae mbali navyo, asiwe na mkono wake mle tofauti na sasa ambapo yeye ni sehemu ya kwanza ya bunge na ukina kwenye mahakama yeye ndo bosi wa DPP na ndiye anayemteua, na anateua Majaji wote hadi mkuu wao yaani Jaji mkuu
 
Huu ni upotoshaji wa makusudi kabisa
Somo la historia lipo miaka nenda Ila halikuwa la lazima, kilichotaka kufanyika ni kuliweka hili somo kuwa la lazima Kama lilivyo somo la uraia civics/ general study
Wewe na nyiendio mnaopotosha sema ukweli wa unalofahamu ili usilofahamu ufahamishwe.Vinginevyo ni wale wale.
 
Reactions: Qwy
Katiba Bora inabalance mambo..Mfano Matendo ya magufuli yangeweza kupingwa na Mkurugenzi wa usalama wa taifa kama kungekuwa na katiba yenye checks and balance. Yaani matendi ya magufuli yalikuwa yakihatarisha usalama wa taifa letu hivyo asingepewa upenyo.
 
Hakijavuja hata kitabu kimoja kiwe sample huku mtaani au smartphone ya chanzo haina scanner
Bila hata kuona kitabu, namna amri ya kuanzishwa hili somo ilivyotolewa inaonyesha utaalam haukuzingatiwa. Mitaala ya masomo haianzishwi na kutayarishwa kwa gahafla namna hiyo. Inatakiwa kwanza ifanyike research na wataalam wa kuandaa mitaala wapewe muda ili kuandaa. Tulikuwa na rais kichaa.
 
Phd ya mashaka. Ndio maana baada ya kupata Urais Maprof wote wa udsm walipata vyeo. Ni kama alikuwa analipa fadhila
 
Si mara ya kwanza zimamoto imeleta hasara kubwa kupitia Taasisi ya Elimu Tanzania.

Taratibu zina faida zake
Na hao TET walishindwa kusimamia taaluma na sheria zao kuzuia mwendazake asiwapangie ??, ona sasa, shilingi ngapi zimepotea hapo ??
 
Hicho chanzo ni TET siyo TEA, isitoshe ni kwamba waandishi ndiyo walijipendekeza kuandika hizo sifa, wakati mwingine hata ibilisi anasingiziwa tu, Mwendazake hakuwapelekea TET cha kuandika wala kuwalazimisha wamuandike ila kuna kasumba imejengeka kwa wengi wa viongozi kutojitegemea kiakili isipokuwa mentality ya kujipendekeza
 
Kama ni Prof. kwelii alitakiwa kuonyesha msimamo tangu awali kulinda taaluma yake na kujitegemea kwa akili yake
 
Na Je, akizuiwa kuingia na akalazimisha kuingia mzima mtafanyaje ?

Africa tunajijua tulivyo mabingwa wa kukiuka kanuni na taratibu ndogo tulizojiwekea.

Katiba ngapi za Africa zina ukomo wa madarak, zinaheshimika ?

Kuna kubwa kuliko hilo ?
 
Jamani inatosha. Hiyo legacy ya JPM mnayojaribu kuiua mpaka kwa propaganda haiwezekani. Nasema tena haiwezekani. Kila mtu ana macho na ameona kilichotendeka katika awamu zote. Mnatumia nguvu kubwa sana.

Huyu mtu ameshakufa mwacheni apumzike kwa amani. Kumtoa kwenye mioyo ya watanzania narudia tena haiwezekani.

Sent from my SM-A730F using JamiiForums mobile app
 
Naanza kuelewa ni kwanini Mungu aliamua kufanya yake; fikiria hi elimu ingewafikia watoto/wajukuu zetu, imagine yaani!
Unataka kumuelewa Mungu utaweza? Mungu huyo huyo kamchukua Magufuli ila kamuacha Ibilisi hadi leo.
 
Status
Not open for further replies.
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…