Mitandaoni sio sehemu ya kujibizana na kila mtu

Mitandaoni sio sehemu ya kujibizana na kila mtu

Joined
Feb 2, 2024
Posts
23
Reaction score
104
Katika miaka kadhaa ambayo watanzania tumeizoea mitandao basi tunakutana na watu mbalimbali katika posts zao ama comments ambazo ukizisoma unaweza patwa na hasira kwa jinsi alivyoandika upuuzi.

1.Kuna hawa wanaoandika kuhusu siasa, kuunga mkono juhudi, kutukana wapinzani, kusifia mambo yasiyoeleweka. Sio lazima kujibizana nao.

2.Kuna hawa wadau wa michezo.
hapa kila mtu yupo na hisia zake, kuna watakaoanfika matusi, pumba, na kila aina ya upuuzi ili tu kujifurahisha kuhusu timu zao. Hapa ndio kabisa hakuna haja ya kujibu.

3.Mashabiki wa miziki.
Huwa nashangaa sana watu wanajibizana nini katika hili, watu wanaingia studio kufanya kazi zao za kujipatia riziki, lakini utakuta kuna watu mitandaoni wanatukana msanii husika kwamba eti "muda wako umeisha", "umechuja", na kauli nyingi kama hizo, tena hususani kwa hawa wadau wa vizazi vya diamond na alikiba. Hakuna haja ya kuwajibu.

Kitu ambacho wengi huwa tunakisahau tunapoingia mitandaoni ni kwamba huku tunakutana na watu wenye akili tofauti, ufahamu tofauti, umri tofauti, na hata watu waliokulia kwenye malezi tofauti, unaweza kumaliza nguvu zako ukaanza kujibizana na jitu ambalo hata mama yake mzazi lilimshinda kulielewa.
Anyway, TUJENGE TAIFA.
 
Siyo kujibishana bali ni kuelimishana,kuna mtu mfano hapa jukwaani unaona kabisa ana ujinga mwingi,na bahati nzuri mtu mjinga ukimuelimisha Kwa facts anabadilika.

Hapa nimezungumzia hasa wale praise teams za wanasiasa
This is so sure, ila kuna watu wana masikio ya chuma, hawabadiliki. Hivi ushawahi kutana na choicevariable kweli?
 
tukajibizanie wapi sasa..?
humuhumu tunatoana meno we mtu yupo nyakurunduma huko halafu analeta ujinga ujinga tunamlamba humuhumu! sasahivi hakuna kulaza damu jino kwa jino uking'ata hatupulizi tunakung'ata nawewe!
tena ukizingua hata wewe hatukulazii damu!.
 
Unaposema Kujibizana unakua una maanisha nini?
Kwenye social media mara nyingi hua kua kujadili jambo,sasa hapo kwenye kujadili ndio una maanisha kujibizana?

Kwa mentality hizo ni bora uache kabisa kuingia kwenye social media au usiwe interacted na watu hata huko vijiweni,huwezi kukwepa kila challenge kwenye maisha.
 
Katika miaka kadhaa ambayo watanzania tumeizoea mitandao basi tunakutana na watu mbalimbali katika posts zao ama comments ambazo ukizisoma unaweza patwa na hasira kwa jinsi alivyoandika upuuzi.

1.Kuna hawa wanaoandika kuhusu siasa, kuunga mkono juhudi, kutukana wapinzani, kusifia mambo yasiyoeleweka. Sio lazima kujibizana nao.

2.Kuna hawa wadau wa michezo.
hapa kila mtu yupo na hisia zake, kuna watakaoanfika matusi, pumba, na kila aina ya upuuzi ili tu kujifurahisha kuhusu timu zao. Hapa ndio kabisa hakuna haja ya kujibu.

3.Mashabiki wa miziki.
Huwa nashangaa sana watu wanajibizana nini katika hili, watu wanaingia studio kufanya kazi zao za kujipatia riziki, lakini utakuta kuna watu mitandaoni wanatukana msanii husika kwamba eti "muda wako umeisha", "umechuja", na kauli nyingi kama hizo, tena hususani kwa hawa wadau wa vizazi vya diamond na alikiba. Hakuna haja ya kuwajibu.

Kitu ambacho wengi huwa tunakisahau tunapoingia mitandaoni ni kwamba huku tunakutana na watu wenye akili tofauti, ufahamu tofauti, umri tofauti, na hata watu waliokulia kwenye malezi tofauti, unaweza kumaliza nguvu zako ukaanza kujibizana na jitu ambalo hata mama yake mzazi lilimshinda kulielewa.
Anyway, TUJENGE TAIFA.

Kweli kabisa kama kusoma magazeti ya mwashwambwa ni lazima ukatapike ndio urudi upya kusoma vingine, ni bora tu usifungue kwa ajili ya afya ya akili na ya mwili.
 
Mi ukiniletea ubishi niko tayari tubishane miaka hata 8
 
Back
Top Bottom