Pole sana ndugu yangu, ndo ukubwa huo!!NasDaz,
..asante kwa mchango wako hapo juu.
..mimi bado naugulia kipigo tulichopata huku Tanganyika.
..kwa kweli siko sawasawa sasa hivi siwezi kuchangia ya Znz.
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Pole sana ndugu yangu, ndo ukubwa huo!!NasDaz,
..asante kwa mchango wako hapo juu.
..mimi bado naugulia kipigo tulichopata huku Tanganyika.
..kwa kweli siko sawasawa sasa hivi siwezi kuchangia ya Znz.
Tathmini ya uchaguzi mwaka huu ni ngumu sana.Hili la mbunge kuangukia chama kingine na rais chama kingine ni jambo la kawaida kabisa! Binafsi, sikumpigia Lowassa kwa sababu ambazo tayari nilishazieleza hapa jamvini lakini hata hivyo ubunge na udiwani nilipigia upinzani! Kuna bro wangu yeye ni mtu wa kawaida kabisa... I hope unanielewa namaanisha nini! Yeye nilipomuhoji akasema wazi kwamba Urais amempigia Magufuri lakini ubunge na udiwani akampigia mtu wa UKAWA!
Tukirudi kwenye matokeo kwa ujumla hapa tusisahau kwamba CHADEMA walitumia nguvu kubwa sana kujijenga Kanda ya Ziwa na kwa kweli walifanikiwa. Ukichukua mikoa 4 ya kanda ya ziwa; Mwanza, Geita, Simiyu na Shinyanga; watu ambao walijiandikisha walikuwa 3.8 million. Huu ni mtaji mkubwa sana kwa chama chochote. Hao watu 3.8 million ni sawa na waliojindikisha Arusha, Kilimanjaro, Mbeya na Manyara ambazo ndio nguzo za CHADEMA. Hata hivyo, Mbeya sio maeneo yote. Kwa bahati mbaya, kura za mikoa (hiyo 4) ambayo ni ngome ya CHADEMA zikawa dissolved na kura za ngome nyingine ya CHADEMA, yaani kutoka Kanda ya Ziwa ambao waliamua kumpigia kura mtu wa kwao! Kwahiyo investment ambayo CHADEMA waliifanya kwa miaka kadhaa ndani ya kanda ya ziwa ikapotea mara moja tu baada ya CCM kumpitisha mtu wa kanda ya ziwa. Kwa tabia za Kiafrika, ni ngumu sana watu waache kumpa kura za urais mtu wa kwao.
Ukiondoa hiyo mikoa 4, CHADEMA wangeweza kufurukuta tu Mara na kidogo Kagera lakini mikoa mingine yote ambayo ilibaki ilikuwa ni ngome ya CCM except for Dar es salaam at least kwa uchaguzi uliopita. Kwa bahati mbaya, kama unavyofahamu watu wa Dar es salaam kwa kujifanya wapo bize, nilipiga hesabu za haraka haraka na kukuta waliojitokeza kupiga kura ni around 55-57%!
Binafsi nilipokuja kuona kumbe Tabora, Tanga, Dodoma na Morogoro kwa ujumla wao wana wapiga kura wengi kuliko Arusha, Kilimanjaro, Manyara na Mbeya kwa ujumla wake tayari nikaona ugumu walionao UKAWA huku kanda ya ziwa ikiwa inatafuta nani wa kui-dissolve!
Hivyo basi, waliosaliti UKAWA ni watu wa kanda ya ziwa ambao waliamua kumpigia mtu wa kwao na Dar es salaam ambao hawakujitokeza kwa wingi!
Kuna gazeti la Tanzania nimelisoma jana (silikumbuki ni lipi) ambalo linazungumzia Kahama (wilaya) kuwa ndipo Uraisi ulifahamika. Kwa mujibu wa gazeti hili, Magufuli alipiga kura Jumapili akiwa nyumbani kwake Chato. Kesho yake akisafiri kwa barabara, msafara wake ulifika Kahama na mahitaji ya kuchimba dawa yakatokea. Waliposimama hapo Kahama, ilikuwa Jumatatu Oktoba 26 mida ya saa nne asubuhi.
Walipoondoka Chato, Magufuli alikuwa amekaa mbele na dereva kama kawaida. Walipokuwa wamesiama Kahama saa nne asubuhi, mfumo na mchakato wa msafara na usalama ukabadilika. Watu wa Usalama wakashika hatamu, Magufuli akahamia kiti cha nyuma, gari yake badala ya kuwa gari la mbele, ikawa gari la tatu katika msafara na kukawa na nyongeza ya magari ya usalama na ulinzi wake.
Protocol nzima ilibadilika walipofika Kahama na status ya Magufuli ilibadilika kutoka kuwa Mgombea na kuwa Mteule huku bado kura zikiwa zinahesabiwa, kujumuishwa na kukusanywa.
Je ni nani alikuwa na majibu yote ya Urais jumatatu ya Oktoba 26 saa nne asubuhi? ikiwa NEC na Lubuva jumatatu hiyo walitangaza majimbo 11 mengi yakiwa ya Zanzibar, kwa nini Protocol ilibadilishwa ghafla saa nne asubuhi na Matokeo rasmi yalianza kutangazwa tarkibani kuelekea jioni ya Jumatatu Oktoba 26?
Tuchemshe Bongo!
Hiki ni sawa na ile Ze Comedy nyingine ambapo Rais JK alioenekana kumpongeza Mteule na picha zikapigwa nyingi!Kuna gazeti la Tanzania nimelisoma jana (silikumbuki ni lipi) ambalo linazungumzia Kahama (wilaya) kuwa ndipo Uraisi ulifahamika. Kwa mujibu wa gazeti hili, Magufuli alipiga kura Jumapili akiwa nyumbani kwake Chato. Kesho yake akisafiri kwa barabara, msafara wake ulifika Kahama na mahitaji ya kuchimba dawa yakatokea. Waliposimama hapo Kahama, ilikuwa Jumatatu Oktoba 26 mida ya saa nne asubuhi.
Walipoondoka Chato, Magufuli alikuwa amekaa mbele na dereva kama kawaida. Walipokuwa wamesiama Kahama saa nne asubuhi, mfumo na mchakato wa msafara na usalama ukabadilika. Watu wa Usalama wakashika hatamu, Magufuli akahamia kiti cha nyuma, gari yake badala ya kuwa gari la mbele, ikawa gari la tatu katika msafara na kukawa na nyongeza ya magari ya usalama na ulinzi wake.
Protocol nzima ilibadilika walipofika Kahama na status ya Magufuli ilibadilika kutoka kuwa Mgombea na kuwa Mteule huku bado kura zikiwa zinahesabiwa, kujumuishwa na kukusanywa.
Je ni nani alikuwa na majibu yote ya Urais jumatatu ya Oktoba 26 saa nne asubuhi? ikiwa NEC na Lubuva jumatatu hiyo walitangaza majimbo 11 mengi yakiwa ya Zanzibar, kwa nini Protocol ilibadilishwa ghafla saa nne asubuhi na Matokeo rasmi yalianza kutangazwa tarkibani kuelekea jioni ya Jumatatu Oktoba 26?
Tuchemshe Bongo!
Come on Rev.
Let's keep it 100 here.
Was the outcome ever in doubt?
Mimi sikuwa na shaka lolote kwamba NEC ya CCM eti somehow ingeweza kumtangaza mgombea asiye wa CCM kuwa ndo mshindi.
Na kamwe haitotokea hiyo NEC ije imtangaze mgombea asiye wa CCM kuwa ndo mshindi.
Tanzania kiuhalisia hatuna demokrasia ya vyama vingi.
Tuna maigizo tu ya demokrasia ya vyama vingi [ambayo mimi naiita ni demokrasia ya chama kimoja].
Hivi kuna ulazima wa kupiga kura kila baada ya miaka 5??
upinzani ukigomea kupiga kura, tatizo litakuwa ni nini?
kwa nini upinzani hauchukui hatua ya kukataa uchaguzi wowote mpaka TUME IWE HURU?? hivi akili zenu/zetu za kufikiri kuna jambo jipya inatokea wapi?
Hivi elimu zetu zinasaidia nini hapa? KAMA MIAKA 5 IKIFIKA UCHAGUZI UKAGOMEWA ACHA DUNIA IJUE KUWA NI UCHAGUZI WA CCM WENYEWE KWA WENYEWE...kama tume siyo huru, mnataka nini?
Ndio maana vita yangu, mawazo yangu,nguvu zangu,akili zangu, na hasira zanguhuwa ninazipeleka kwa wapinzani.....! HAWAKO strong enough, hawana logic? KWA NINI umpe mwananchi FALSE HOPE kuwa eti kuna uwezekano wa kuingia ikulu?? kwa hii tume huru?
Hao akina mbowe kweli wako serious kuingia ikulu? kwa TUME hii hii?
KUBADILI tume haihitaji katiba yote ibadilishwe, ni marekebisho ya katiba, MUUNDO NA MFUMO WA TUME SIYO MSAAFU UNABADILISHIKA!
atoke mwanasias mmoja jasiri, aweke proposal ya katiba apeleke mjadala bungeni!!!
wengine huwa tunashawishika kusema kuwa wapinzani ni WAPIGAJI HELA TU,huwezi kuwa mbumbumbu au mjinga kiasi gani kujua kuwa urais hautakuja kuwa wa upinzani kwa TUME HII
2010 slaa alilalamika, 2015 EL analalamika
fun enough akina EL, Sumaye na kingunge wanajua kila kitu na siri zote za ushindi wa CCM
CCM wamejisafisha sana na kupumbaza ulimwengu
ATOKE MTU ANAYEJIITA ANA AKILI TIMAMU ASEME NAMNA YA KUINGIA IKULU UPINZANI
huwa ninasemaga muwe genuine!!! utumbo wa upinzani mnaufumbia macho,kama na sawa kabisa na wale wa CCM
huku mnataka kujadili tathmini ya uchaguzi
hii aibu ya kuwa na logic mfu kama hizi tutaiweka au tunaiweka wapi?? where is our logic of great thinking??
kweli mtu na akili zako unaweka hope ye EL kushinda?? that was totally unafair kuwadanganya watanzania kiasi kile
Nguruvi ebu amkeni wakuu, taifa tunalipeleka pabaya kwa kutokuwa wakweli katika vitu ambavyo vinahitaji ukweli??
kwa nini mahaba, mapenzi, hisia na wishful thinking vinatuongoza??
ukisoma comment ya Nyanu Ngabu haina chenga; kama kuna mtu aliwaza kinyume na hapo hana uhalisia na HANA AKILI TIMAMU
comment kama hizi tumezitoa 2011, tunazitoa 2015...NA 2020 UPINZANI huu mnaouona una maana na unataka mabadiliko utaingia tena kwenye uchaguzi na tume ile ile; AKILI AU MATOPE??
samahani
Ile siku Rais mteule alipomtemblea Rais Ikulu niliangua kicheko sana. Nilicheka sanaI mean, it's a joke. Mwenyekiti wa CCM ambaye ndo rais anaunda tume ya taifa ya uchaguzi ambayo kazi yake kuu ni kuratibu, kuendesha, na kusimamia shughuli za uchaguzi ambazo CCM nayo inashiriki.
Mbona mgongano wa kimaslahi ni dhahiri kabisa hapo?
So why even bother taking part in such elections?
Foolishness.
Kwa mazingira ya sasa mimi binafsi sioni kabisa ulazima uliopo. Ni bora mara mia hizo hela zinazotumika kwenye hayo maigizo yanayoitwa 'uchaguzi' zikatumika kununulia mashine za CT-Scan na MRI kwenye hospitali zote za serikali.
Ni kama ulikuwepo kichwani mwangu. Kwa muda mrefu sana nimekuwa nikiwaza kwamba, ingekuwa ni juu yangu mimi basi hakuna chama cha upinzani ambacho kingeshiriki hayo maigizo.
Mahesabu yangu ni kwamba, kutokushiriki kwao kungeondoa au kupunguza uhalali wa 'ushindi' wa CCM na kuwa moja ya shinikizo la kuleta katiba mpya ambayo itaweka mazingira sawa kwa washindani wote katika chaguzi zijazo.
Daah Wabe utadhani uliwahi kuwepo sehemu ambayo nilikuwa nimekaa na washikaji nikiwapa hilo darasa la wapinzani kususia kushiriki hizi chaguzi chini ya mazingira sasa.
Ulichoandika ndicho mimi nimekuwa nikijaribu kuwaelimisha watu hususan nje ya hapa JF. Lakini nikiri pia kuwa ni wachache mno ambao hunielewa. Hapo ndo unapata taswira ya jinsi watu wengi walivyo kifikra.
Exactly! Uchaguzi ukisusiwa hata uhalali wa CCM utakuwa wa mashaka. Sijui kwa nini tu watu hawalioni hilo.
Kwa sababu, mara tu unapokubali kushiriki kwenye uchaguzi ambao unajua kabisa 'the odds are stacked against you' kwa sababu ya mazingira mabovu, maana yake ni kwamba umekubali kushiriki mchezo chini ya sheria 'mbovu' zilizopo.
Sasa kwa nini ufanye hivyo? Huo nao ni uwendawazimu tu. Ingekuwa juu yangu ningegomea mpaka pale tutakapokuwa na mazingira mazuri na yasiyompa 'undue advantage' mshiriki yeyote yule.
Nakubaliana nawe mia kwa mia. Vyama vya upinzani navyo vinastahili kabisa lawama kwa kubariki na kukubali katika chaguzi za kilaghai.
Wanacheza hao. Hivi hujagundua tu kwa nini CCM haina sana shauku ya kutaka katiba mpya na kupata tume huru ya uchaguzi?
Naam, hilo ni kweli. Lakini pia haitokuwa vyema kuwa na tume huru halafu itokee chama kingine kishinde uchaguzi halafu nacho kiendelee kutawala kwa kutumia katiba hii hii ya hovyo tuliyo nayo.
Katiba mpya na tume huru ya uchaguzi are way long overdue. Hivi vilitakiwa viwe ndo vitu vya kwanza kabisa kufanywa pindi tulipoamua kuingia kwenye siasa za vyama vingi.
Na kusema ukweli hata tume ya Nyalali ilipendekeza hivyo lakini CCM kwa kutumia ujinga wa walio wengi kwa manufaa yao, wakaliepuka kabisa hilo suala na sasa tunaona jinsi wanavyonufaika kwa kutokuwa na katiba mpya wala tume huru ya uchaguzi.
Nikupe tu mfano wa Afrika Kusini. Baada ya kuamua kuondokana na utawala kibaguzi, waliandika katiba ya wakaa [interim constitution] ambayo ilitumika katika kipindi cha mpito na baada ya uchaguzi wa 1994 wakaandika katiba mpya kwa kuwashirikisha wananchi wote.
Hiyo katiba iliidhinishwa na mahakama ya katiba mnamo tarehe 4 Disemba 1996 na ikasainiwa na rais Mandela tarehe 10 Disemba mwaka huo huo na ikaanza kutumika tarehe 4 Februari 1997.
Katiba ya Afrika Kusini inakubalika kuwa ndo moja ya katiba bora kabisa duniani.
Sasa hebu fikiria kwa mfano ANC wangeendelea kutawala kwa kutumia ile katiba ya zamani ya Makaburu na labda kwa kufanyiwa marekebisho ya hapa na pale.
Hivi unadhani kungekalika huko?
Ndo maana huwa nasema kwamba na sisi tulitakiwa kuanza huu mfumo wa vyama vingi na katiba mpya kabisa ambayo ingepunguza madaraka ya rais na ambayo ingeunda taasisi huru kama vile tume huru ya uchaguzi na kadhalika.
Tungekuwa tumefanya hivyo pengine labda kusingehitajika rais kuvamia vamia maofisi kukagua utendaji wa kazi.
Na afanye hivyo kwa dhati kabisa na si kwa sababu ya kutafuta kiki tu.
Mimi nimeshasema kamwe wapinzani hawataiona ikulu kwa kadri tume ya uchaguzi itakavyoendelea kuundwa na CCM.
I mean, it's a joke. Mwenyekiti wa CCM ambaye ndo rais anaunda tume ya taifa ya uchaguzi ambayo kazi yake kuu ni kuratibu, kuendesha, na kusimamia shughuli za uchaguzi ambazo CCM nayo inashiriki.
Mbona mgongano wa kimaslahi ni dhahiri kabisa hapo?
So why even bother taking part in such elections?
Foolishness.
Waberoya
Nadhani upo hapa siku nyingi. Hakika hakuna kipya wala hakuna aliyetarajia jipya kwa sisi wengine
Kama utakumbuka, tuliwapigia sana kelele walipokwenda Ikulu na nyuzi zipo zaidi ya 100.
Tukawaambia juisi za maembe na mengine siyo muhimu kama wao kutaka mfumo ubadilike
Bandiko 42 hapo kuna mahali tumesema hivi '' Haya yote yanafungwa katika mwamvuli mmoja wa uzembe wa wapinzani''
Kabla ya uchaguzi, tuliwaambi wazi uchaguzi wetu haupo katika kura , tulisema ''Uchaguzi ni zaidi ya sanduku la kura''
Nakubaliana nawe kabisa na wengi watakubaliana nasi kuwa upinzani una uzembe. Hili halikuhitaji diploma kulitambua
Tena umeongezea jambo moja muhimu. Hawa waliokuwa CCM wanajua mbinu.
Wanajua kuwa haitatoke ikatangazwa tofauti na inavyotakiwa iwe.
Nape aliwaambia ukweli, hata goli la mkono lazima. Bulembe akasema Ikulu 'Ngo'
Na yote hayo yalisikika na tume, haikufanya lolote kwasababu inajua ukweli
Sasa kuna pande kadhaa kuhusu hili suala
1. Wapinzani watamke wazi kuwa hawataenda katika uchaguzi mkuu mwingine na katiba au tume iliyopo
2. Kuna umuhimu wa wapinzani kubadili uongozi. Watu wale wale waliofanya yale yale kwa miaka 20 hawawezi kuja na jambo jipya isipokuwa marudio. Na kwa hili wapinzani wabadili uongozi mzima wa Upinzani bungeni
3. Hoja ya kwanza wanaotakiwa kusimama nayo ni kubadili mfumo. Wasikubali kuburuzwa kwa namna yoyote
Umma unaona na kuwaunga mkono. Hii ni fursa isiyotakiwa kupotezwa kama ilivyokuwa nyuma
4. Sisi wananchi tuna shea yetu. Tunadhani hili ni suala la wapinzani tu.
Tumesahau kuwa ni suala letu.Leo tunaona ubabaishaji, kwamba watu wale wale waliokuwa katika mfumo ulele na wakishirika kufanya yale yale wanaonekana wanakuja na mapya. Kwamba, wamekuwa malaika usiku mmoja tu!
Hakuna anayeomba radhi kwa madhila ya nyuma kwasababu wote ni sehemu ya mfumo ule ule.
Haiwezeakani wakaukana mfumo uliowafikisha hapo. Kama hatusimama na kutaka mabadiliko ya mifumo yetu tutabaki kuhuzunika na kulalamika.
Nguvu ya umma ndiyo iliyopelekea kuanzishwa kwa mchakato. Kwa bahati mbaya sana, wapinzani hawakuwa na maono licha ya tahadhari zote tulizowapa.
Na sisi wananchi tukaridhika kudanganywa na mchakato tukijua haukuwa na udhibiti wetu.
Leo wamekaa wanataka kurudisha katiba ile ile iliyoandikwa na CCM
Watafanikiwa kwasababu hatukuwauliza wakati wanapita katika mikutano yao.
Walikaa kimya wakisubiri wapewe 'rungu' waaanze kufanya yao.
Tukiendelea kukaa kimya wataendelea kutupumbaza. Tuwaambie wazi hatuhitaji mabadiliko ya sura za wakurugenzi.
Tunahitaji mabadiliko ya mfumo mzima wa kujitawala.
Mfumo utakaotupa sisi sauti zaidi ya kujiendesha kama taifa na si kikundi cha watu au mtu
Hatuhitaji 'one man show' tunahitaji mass participation. Tumeishi na one man show na kubaki taifa la omba omba.
Sasa si wakati wake, ni wakati wa sisi kutaka mabadiliko ya mifumo yetu mibovu
Tunaona mifumo mibovu inavyotuletea matatizo.
Wiki ijato bunge la JMT linaanza kukiwa hakuna wajumbe wa BLW znz.
Hawapo ndani ya bunge lakini tunaambiwa ni la JMT. Tunaambiwa mfumo ni kamili
Leo tunaona NEC na ZEC zikiwa vyombo viwili tiofauti kabisa. Katiba inatuelekeza ni vyombo vinavyofanya kazi kwa ushirikiano. Uhalisia umetimia tunaona yale ya katiba ni maandishi tu kumbe nchi inaongozwa tofauti
Tumeambiwa Rais wa JMT ndiye mkuuwa taifa la Tanzania.
Tunaona Rais akiwa kama mtazamaji wakati sehemu ya nchi ikiwa na tatizo.
Tumeona nguvu moja ikifanya kazi kama taifa kwamba, nguvu za nchi zipo kwa mtu na si timu au watu
Haya yote tunapaswa kuyaona kama matatizo. Hayo ya MRI ni matokeo ya kuwa na mfumo mbovu
Sasa wapo wenye platform, na wapo wenye sauti, wakasimama na kusema hapana au ndiyo sauti yao itafika nyikani.
Itasikika kwa mfalme aliye juu akiangalia nyika kwa chini. Mfalme atatupa haki za kufikiri, kupanga na kuchagua, si kwasababu anataka bali mfumo utamlazimisha. Huko ndiko tunakotaka kwenda si sura za Wakurugenzi