Miungu yetu ilishindwa, Mizimu yetu ikapigwa, Sasa tumekuwa Jamii iliyoanguka na hatuna Tumaini la kusimama

Miungu yetu ilishindwa, Mizimu yetu ikapigwa, Sasa tumekuwa Jamii iliyoanguka na hatuna Tumaini la kusimama

Mungu huyo wa Israel ni mdhaifu sana.

Alishindwa kuwaokoa waisraeli kwenye concentration camps za Adolph Hitler wakauwawa maelfu kwa maelfu.

Halafu kuna waafrika wajinga kazi kukesha makanisani wakipayuka kama mbayuwayu kumuomba huyo Mungu wa Israel..
Unafaa uelewe ile ilikuwa ni adhabu kutoka na wao kuulizwa kuwa yesu hana kosa lolote la kumhukumu wakamwambia pilato damu ya yesu isiyo na atia iwe juu yao na watoto wao lakin siyo mara ya Kwanza kutiwa mikononi mwa adui zao, kuna vipind vya babeli, miaka 70, jangwan walifungwa Mika 40, lakin akishakaa upande wao usijichamganye
 
Mungu huyo wa Israel ni mdhaifu sana.

Alishindwa kuwaokoa waisraeli kwenye concentration camps za Adolph Hitler wakauwawa maelfu kwa maelfu.

Halafu kuna waafrika wajinga kazi kukesha makanisani wakipayuka kama mbayuwayu kumuomba huyo Mungu wa Israel..
Hapa umesema waafrika ni wajinga kazi kukesha makanisani
Swali langu wewe mwenye akili umevumbua nini mpaka sasa
 
Unafaa uelewe ile ilikuwa ni adhabu kutoka na wao kuulizwa kuwa yesu hana kosa lolote la kumhukumu
Unaweza kuthibitisha ilikuwa ni adhabu na ulete sehemu ya andiko inayo thibitisha hili?
wakamwambia pilato damu ya yesu isiyo na atia iwe juu yao na watoto wao lakin siyo mara ya Kwanza kutiwa mikononi mwa adui zao, kuna vipind vya babeli, miaka 70, jangwan walifungwa Mika 40, lakin akishakaa upande wao usijichamganye
 
Tulikubali bila kuhoji kuandika Mungu wetu kwa silabi ndogo "mungu " na wa kwao kwa herufi kubwa "Mungu ". Ni hapo tulimdharau Mungu wetu wa Kiafrika na kutukuza Mungu wao wa Israel.
 
MIUNGU YETU ILISHINDWA, MIZIMU YETU IKAPIGWA, SASA TUMEKUWA JAMII ILIYOANGUKA NA HATUNA TUMAINI TENA LA KUSIMAMA.

Anàandika, Robert Heriel
Mtibeli.

Mila zetu, Desturi zetu, tamaduni zetu, utambulisho wetu na kila kilichokuwa chetu kiliitwa Potofu baada ya kushindwa.
Upotofu upo kwa walioshindwa. Kama tungeshinda katika vita Ile wala istilahi "POTOFU” Isingesikika.
Ni potofu kwa sababu tulishindwa.

Miungu ya Mababu zetu ilishindwa vibaya katika vita ya miungu "god's War" sijajua nini kilipelekea kushindwa kwao. Bado najiuliza.
Je Haikuwa na nguvu ya kutosha kukabiliana na Miungu ya kigeni?
Je Haikuwa na akili na mbinu kabambe za kuwashinda maadui?
Nini kilitokea mpaka Anguko kuu la kutisha lilipotokea ambalo limedumu mpaka leo na hatujui litaendelea mpaka Lini.

Miungu ikishapigwa waumini hawana ujanja tena.
Wakati Ukristo na uislamu unaingia Afrika Wazee na Babu zetu walipambana vilivyo kuukataa kwa nguvu zote lakini ninawasiwasi Miungu yao haikuwapa sapoti ya kutosha kukabiliana na ugeni Ule mbaya.
Au miungu ile ilitoa sapoti lakini haikuwa na nguvu kushinda Maadui waliokuja.

Hatuwezi kusema Waafrika walisaliti miungu yao. Ila ninachokiona ni kuwa miungu ya kiafrika ilizidiwa na haikuwa na nguvu ya kutosha kukabiliana na miungu ya kigeni.

Nakumbuka mpaka nazaliwa zilikuwepo jitihada mbalimbali za wazee wetu wakijitahidi kufurukuta kujaribu kupambana na ujio wa wageni na miungu yao lakini walikuwa wanapambana wakiwa wameshashindwa kwani miungu yao ilikuwa aidha imekimbia au imetekwa au pengine hata kuuawa na miungu ya kigeni.

Miungu ndio imebeba mila, desturi, tamaduni na utambulisho wa jamii husika. Sasa kitendo cha miungu hiyo kupigwa Katiak vita na kufukuzwa au kuangamizwa kabisa kunaiathiri na kuua kabisa desturi , mila na tamaduni ya jamii zao.

Ni mila potofu kwa sababu miungu hiyo imeshindwa.
Ni mila potofu kwa sababu miungu hiyo haina nguvu na haina vigezo na uhalali wa kuitwa miungu.
Ni mila potofu kwa sababu miungu hiyo imeshindwa kutetea Watu wake.
Ni mila potofu kwa sababu miungu hiyo imeshindwa kulinda rasilimali za himaya zao mpaka zinaibiwa na wageni.

Ni mila potofu kwa sababu, miungu hiyo imeshindwa kuwapa Watu wake Akili na kutatua kero na changamoto za jamii yao ikiwemo Umaskini na ujinga.

Miungu na mizimu yako inaposhindwa hauna chochote utakachofanya zaidi ya kujisalimisha kwa miungu ya kigeni.
Ni pigo takatifu ambalo kunyanyuka haiwezekaniki.

Vita ya Miungu, waafrika walipoteza na hatujui miungu yetu ilikimbia, au ipo mateka au iliuawa.
Nyota ya matumaini ya Ukombozi haipo kwa sababu huwezi kukomboa jamii au taifa pasipo Miungu ya kwenu.

Acha Nipumzike sasa.
Nawatakia maandalizi mema ya Sabato.

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam

Ina maana ilikuwa Miungu bandia. Ilikuwa fake. Ilikuwa haina misimamo wala nguvu za kuleta matuaini. Ila sasa, hatuja kombolewa kifrika
 
Ni wapi nimesema wamevumbua kitu
We ndo umewaita wajinga namimi nikakuuliza we mwenye akili umefanya nini
Kuna uhusiano gani wa kuvumbua kitu au kutokuvumbua kitu na uwepo wa Mungu?

Nawaita wajinga kwa sababu hawawezi kuthibitisha uwepo wa huyo Mungu na huyo Mungu mwenyewe hawezi kujitetea mwenyewe na kujidhihirisha yupo mpaka atetewe.
 
Kuna uhusiano gani wa kuvumbua kitu au kutokuvumbua kitu na uwepo wa Mungu?

Nawaita wajinga kwa sababu hawawezi kuthibitisha uwepo wa huyo Mungu na huyo Mungu mwenyewe hawezi kujitetea mwenyewe na kujidhihirisha yupo mpaka atetewe.
Wewe mwenye akili ambaye huamini kwenye Mungu umevumbua nini au umefanya nini cha maana
 
Back
Top Bottom