Mizengo Pinda: Serikali ilivyotekeleza Maazimio ya Bunge Richmond

Mizengo Pinda: Serikali ilivyotekeleza Maazimio ya Bunge Richmond

Wakuu,
Mie kwa upeo wangu[/SIZE] nadhani Pinda ameongea kwa niaba ya serikali na tusimlaumu yeye.Kimsingi hoja ni nzuri na tatizo tulilo nalo sisi(siyo mimi)[/SIZE].tunataka lile tunalotaka ndilo liwe wakati haiwezekani.
Mwanakijiji alishawaomba sana muda mrefu,Mwadhirie nchi ila mkang'ang'ana nao.Hii nchi ndivyo ilivyo na mie napenda tu tuendelee kuwa jinsi tulivyo sababu tunapenda sana maisha ya haraka.




Kuna kadudumtu kameninong'oneza kuwa huyu bwana kala buku. Mmm ! kwa mtindo huu afadhali huo upeo wake abaki nao - ni monopoly yake.
 
ukutix2, wa mnazi wa mnazi! akiingia chenge je? wa mnazi x2, akiingia nimrod , wa mnazi wa mnazi, ukuti, ukuti ? wa mnazi wa mnazi, akiingia mwakyembe, uktu, ukuti, wa chungwa wa chungwa
 
Pinda ang'eamulu hawa watu wote wasimamishwe kazi na wajitetee na wapewe muda maalumu (time frame), ili iwe rahisi kufuatilia otherwise baadaye tutasahau maana kuna ofisi nyingine wata prolong sana hizi taratibu ila watu wasahau na hawa waovu baadaye waendelee na kazi.
Ila wananchi, vyombo vya habari, wabunge, NGOs, vyama vya siasa nk tunatakiwa kufuatilia na kuhakikisha watu hawa wote wamechukuliwa hatua za kinidhamu, tusiliache hili suala kwa serikali pekeyake
 
Ripoti ya utekelezaji kuhusu Richmond yaduwaza wabunge

*Naibu Spika awabembeleza waipokee, wengi watoka nje

Na Tausi Mbowe, Dodoma
Mwananchi

SAUTI za minong'ono zilikuwa zimetanda kwenye Ukumbi wa Bunge jana wakati Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, alipokamilisha kusoma hotuba yake ya utekelezaji wa mapendekezo ya Kamati ya Richmond, baada ya hatua kadhaa dhidi ya wahusika kumsubiri rais na watendaji wake.

Uwezekano wa wabunge kujiridhisha kwa kuchangia hotuba hiyo mara baada ya Waziri Mkuu kumaliza kutoa hoja, ulishindikana baada ya Naibu Spika, Anna Makinda, kuzima juhudi hizo akisema wataijadili taarifa hiyo katika kikao kijacho cha Novemba, mwaka huu.

Kati ya mapendekezo hayo ni machache tu ndiyo ambayo utekelezaji wake umekamilika huku mengine muhimu ambayo wabunge na wananchi walikuwa wanayasubiri kwa hamu yakiachwa kwa mamlaka zinazowajibika, likiwamo suala la Mwanasheria Mkuu wa Serikali, kusubiri hatua atakazochukuliwa na Rais Jakaya Kikwete, huku la Mkurugenzi wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) likiachwa mikononi mwa Katibu Mkuu Kiongozi.

Hali ya wabunge kutoridhishwa na ripoti hiyo ilionekana mara baada ya Waziri Mkuu Pinda, kumaliza kusoma ripoti yake wakati walipoanza kunong'ona na hawakusimama kuonyesha kwamba wameipokea hadi Naibu Spika alipowataka wampigie makofi kuonyesha kuridhishwa.

Baada ya Pinda kumaliza kusoma tamko hilo, Habibu Mnyaa Mbunge wa Mkanyageni (CUF) alisimama kwa kuomba wabunge waijadili ripoti hiyo ya utekelezaji, lakini akamzima.

"Waheshimiwa wabunge mtapata muda wa kuijadili ripoti hii, lakini kwanza mmepewa vitabu hivyo ili msome kwa makini na baadaye ndipo mje kuijadili katika kikao kingine ," alisema Makinda na kuongeza: "Naomba msipoteze vitabu hivyo kwa sababu hamtapewa vingine."

Wakati Makinda akiruhusu Bunge kuendelea na shughuli nyingine, baadhi ya wabunge walianza kutoka ukumbini, hali iliyozua kelele zaidi na Makinda akalazimika kutuliza hali hiyo. "Jamani mnaotoka, mtoke taratibu ili msisumbue wengine," alisema.

Nje ya Ukumbi wa Bunge, maoni yalikuwa tofauti, wakizungumza mara baada ya Waziri Mkuu Pinda, kusoma taarifa hiyo, baadhi ya wabunge walisema taarifa hiyo ni nzuri ingawa imeshindwa kuonyesha moja kwa moja hatua zilizochukuliwa kwa watuhumiwa wote waliohusika katika ubadhirifu huo.

Wabunge hao kwa nyakati tofauti walisema Waziri Mkuu amefanya haraka kutoa taarifa hiyo bungeni kutokana na ukweli kwamba, Watanzania wengi wanataka kuona serikali imewachukulia hatua watuhumiwa hao na si maneno matupu ya kuziachia mamlaka zifanye kazi hiyo.

Mjumbe wa kamati iliyoundwa kuchunguza mchakato wa zabuni iliyoipa ushindi kampuni ya kufua umeme wa dharura ya Richmond, Lucas Selelii, alisema ripoti hiyo imeweza kuonyesha ukweli na suala hilo na kuwatoa katika malalamiko kamati hiyo tofauti na madai ya baadhi ya wabunge kuwa kamati hiyo ilikuwa imewaonea.

“Leo sisi kama kamati tuna furaha sana, taarifa hii inaonyesha wazi kuwa kamati yetu haikumuonea mtu, tulichosema kilikuwa na ukweli ingawa utekelezaji wake umechukua muda mrefu sana tangu mwezi Februari mpaka leo ndio ripoti inatolewa,” alisema Selelii.

"Inashangaza kwamba kamati yetu ilifanya kazi kubwa katika muda wa miezi mitatu tu, lakini serikali ambayo ina kila kitu imefanya kazi hii kwa miezi sita na kutoa ripoti ambayo imeacha mambo mengi."

Kauli hiyo iliungwa mkono na aliyekuwa mwenyekiti wa Kamati hiyo, Dk Harrison Mwakyembe, na kusema ripoti hiyo ni mwanzo mzuri wa utekelezaji wa mapendekezo hayo na kwamba imegusa maeneo yote.

Dk. Mwakyembe ambaye pia ni Mbunge wa Kyela (CCM), alisema kinachotakiwa sasa ni kuziachia mamlaka zilizopewa jukumu la kuwawajibisha watuhumiwa wa ufisadi huo wafanye kazi yao na hatimaye kutoa matokeo yake.

Mbunge wa Kigoma Kaskazini (Chadema), Kambwe Zitto, alisema ameridhika na taarifa hiyo ya serikali na kwamba kambi ya upinzani inachosubiri ni kuona mamlaka zilizopewa jukumu la kuwachukulia hatua wahusika hao zinafanya hivyo haraka.

“Kikubwa ni kuwawajibisha wote waliohusika katika mchakato huo, kambi ya upinzani, inasubiri kwa hamu kubwa kuona mamlaka hizo zinawachukulia hatua za kinidhamu wote waliotuhumiwa,” alisisitiza Zitto.

Naye Mbunge wa Bumbuli, William Shelukindo (CCM), alishangazwa na utekelezaji wa mapendekezo hayo ulivyochukua muda mrefu, jambo ambalo alilosema kiutendaji linaweza kukwamisha maendeleo.

Mbunge wa Bariadi Magharibi, Andrew Chenge (CCM) alisema Waziri Mkuu ameeleza vizuri mapendekezo hayo kwani alijibu kila hoja.

Hata hivyo, Chenge alitofautiana na wabunge wengine waliotaka ripoti hiyo ijadiliwe bungeni na kusema kuwa haina haja ya kufanya hivyo kwani kujadili ripoti hiyo ni kupoteza muda hivyo ziachiwe mamlaka zichukue hatua kama ilivyopendekezwa.

“Haya yameshapita, tugange yajayo, kuijadili ripoti hiyo ni sawa na kupoteza muda, kila kitu kimeelezwa sawa kabisa, tuache sheria ifuate mkondo wake,”alisisitiza Chenge.

Naye Msemaji Mkuu wa Kambi ya upinzani Bungeni, Hamad Rashid Mohamed (CUF) alisema kambi ya upinzani imeridhishwa na ripoti hiyo kwa kuwa serikali imejitahidi kutoa majibu yaliyokidhi matarajio ya wabunge.

Mbunge wa Simanjiro, Christopher Ole-Sendeka (CCM), alisema ameridhika na hatua ya serikali kukiri kuwa kulikuwa na mapungufu katika mchakato huo ingawa alishangazwa na kasi ndogo iliyochukuliwa na serikali katika kupitia mapendekezo

Waliotakiwa kuwajibishwa katika sakata hilo ni pamoja na Mwanasheria Mkuu wa Serikali , Johnson Mwanyika, Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), Edward Hosea na Katibu Mkuu Wizara ya Nishati na Madini, Arthur Mwakapugi.

Wakati aliyekuwa Waziri Mkuu, Edward Lowassa, na mawaziri Nazir Karamagi na Dk Ibrahim Msabaha waliwajibika kwa kujiuzulu kwa maslahi ya taifa mara baada ya kutajwa kwenye kashfa hiyo, Mwanyika, Hosea na Katibu Mwakapugi hawajachukua hatua hiyo, huku baadhi yao wakisema wanasubiri Rais Jakaya Kikwete ambaye aliwapa wajibu huo awawajibishe akiona wanastahili.

Hosea ameingia katika kashfa hiyo baada ya Takukuru kuisafisha Richmond katika uchunguzi wake wa awali kufuatia taarifa ya uchunguzi wa taasisi yake kubainisha kwamba mkataba huo haukuwa na harufu ya kifisadi.

Baadhi ya mapendekezo ya Bunge kuhusu kashfa hiyo ni Msajili wa Makampuni (BRELA) kuifuta Kampuni ya Richmond na wamiliki wake kufunguliwa kesi ya jinai na kisha serikali kuangalia uwezekano wa kusitisha malipo kwa Kampuni ya Dowans. Serikali ilitekeleza pendekezo la kusitisha malipo kwa Dowans Agosti Mosi mwaka huu.

Michango mbalimbali ya wabunge iliifanya Kamati waliyoiunda kuchunguza suala hilo kuongeza mapendekezo mengine saba ambayo ni pamoja na kuitaka Serikali kuendesha uchunguzi wa kina kwa lengo la kubaini taarifa tete kuwa taarifa ya Takukuru kuhusu Richmond ilichezewa na kuitafuta taarifa halisi ya taasisi hiyo.

Mapendekezo mengine, ya kamati hiyo ni Serikali kujiepusha na matumizi ya mawakala katika manunuzi ya umma na kwamba, sheria ya manunuzi (PPRA) ipewe meno zaidi na ifanye kazi kwa kujitegemea bila kusimamiwa na Wizara ya Fedha. Suala hilo tayari limeshafanyiwa kazi.

Mengine ni serikali kupitia upya mikataba yote na kuanzisha maktaba kwa ajili ya utunzaji wa kumbukumbu katika ofisi za Bunge na kwamba, Timu ya Serikali
inayoshauri Mikataba (GNT) iwajibishwe na aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini, Nazir Karamagi na Mwanasheria Mkuu wa Serikali pia wawajibishwe.

Baada ya mapendekezo hayo Waziri Mkuu Pinda alisema serikali imeunda timu ndogo ya wataalam kutoka idara zake mbalimbali ili kupitia upya mapendekezo ya kamati hiyo ikiwa ni hatua ya mwanzo katika kutekeleza.

Akizungumza wakati wa kuahirishwa mkutano huo wa 10, Waziri Mkuu Pinda alisema serikali imepokea mapendekezo hayo na itayafanyia kazi ili iweze kuyatekeleza ndani ya miezi mitatu kama ilivyoagizwa na Bunge.

"Napenda kuwajulisha waheshimiwa wabunge kuwa nimeunda timu ndogo kupitia kwa makini mapendekezo ya Kamati ya Richmond, ila ni vema nikaeleza kuwa baadhi ya mapendekezo ni mazito na yanahitaji muda mwingi zaidi na mengine tutajitahidi kuyatekeleza ndani ya miezi mitatu kama ilivyopendekezwa na Kamati," alisema Pinda.

Timu aliyounda inahusisha wawakilishi kutoka Ikulu, Sekretarieti ya Mawaziri, Tume ya Maadili, Tamisemi, PPRA, Makandarasi, Utumishi wa Umma na Wizara ya Mipango, ilipaswa kupitia mapendekezo hayo na kutoa dira ya kuyatekeleza.

Waziri Pinda alikiri kuwepo kwa uzembe katika uwajibikaji kwenye serikali na kusema ripoti ya Richmond iliipa serikali changamoto mpya katika utendaji wake wa kazi.
 
Date::8/28/2008
Serikali, Tanesco waidai IPL mabilioni ya fedha kwa udanganyifu
Na Tausi Mbowe, Dodoma
Mwananchi

SERIKALI na Shirika la Umeme nchini (Tanesco) wanaidai Kampuni ya IPTL fedha zote ilizolipwa kimakosa kama gharama za uzalishaji (Capacity Charge) ambazo haikustahili kulipwa.

Hayo yalisemwa na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, wakati akitoa taarifa ya utekelezaji wa mazimio ya Bunge kuhusu kashfa ya umeme wa Richmond bungeni jana.

Pinda alisema mgogoro uliopo sasa baina ya Tanesco na IPTL unatokana na kutokubaliana kwa pande zote mbili kuhusu kiwango cha gharama za uzalishaji kinachotozwa na IPTL. Hata hivyo hakusema ni kiasi gani cha fedha kinachodaiwa.

"Kwa mujibu wa mkataba wa kuuziana umeme kati ya IPTL na Tanesco, inapaswa kukokotolewa kwa kuzingatia mtaji kwa asilimia 30 na faida ya asilimia 22.31 uliopaswa kuwekezwa ambao ni dola za Kimarekani 36.54 milioni wakati IPTL ilipoanza kuzalisha umeme na kuanza kuiuzia Tanesco Januari 2002.

Waziri Mkuu Pinda alisema katika uchunguzi uliofanywa na Tanesco, imegundulika kwamba mtaji halisi wakati IPTL inaanza kuzalisha umeme ulikuwa Sh 50,000 tu, hivyo mtaji huo ndio unaostahili kutumika kukokotoa gharama za uzalishaji inayolipwa na IPTL na si vinginevyo.

Waziri Mkuu alisema, serikali imesitisha malipo yote ya fedha zinazohusiana na mkataba baina ya Tanesco na Richmond uliorithiwa na Kampuni ya Dowans S.A.

Pinda alisema hatua zilizochukuliwa katika azimio la kwanza ni pamoja na Wizara ya Fedha na Uchumi na Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa serikali pamoja na Mamlaka ya udhibiti wa manunuzi ya umma (PPRA), wamekwisha kamilisha maeneo yote yenye upungufu na yanayohitaji marekebisho kwenye Sheria ya manunuzi ya umma ya mwaka 2004, hivyo serikali itawasilisha katika Mkutano wa 13 wa Bunge mapendekezo ya kufanya marekebisho katika sheria hiyo.

Kuhusu utata uliojitokeza katika mkataba baina ya Tanesco na Richmond uliorithiwa na Dowans, alisema serikali ilisitisha mkataba huo kuanzia Agosti mosi 2008 pamoja na kusitisha malipo yote ya fedha zilizoainishwa katika
mkataba huo.

Pinda alisema serikali imetafakari na kuzingatia kwa makini pendekezo hilo na kwamba kuanzia sasa balozi zote za nje zitakuwa zinashirikishwa kikamilifu katika kufanya uchunguzi wa kina kwa makampuni ya nje ambayo serikali inatarajia kuingia nayo mikataba.

Alisema serikali pia ilifanya uchunguzi juu ya usajili wa Kampuni ya Richmond Development Company LLC pamoja na Richmond Development Company (T) Limited kubaini uhalali wake na ili kujiridhisha kama usajili wake ulifanywa na BRELA ulikuwa klinyume cha sheria za nchi.

Alisema uchunguzi huo ulibaini kwamba kuna utata hivyo mwanasheria mkuu wa serikali alishauri juu ya Mamlaka ya BRELA kuifuta Kampuni ya Richmond Development Company (T)Limted kwa kuzingatia sheria ya makampuni na kwamba tayuari BRELA imekwisha toa notisi ya siku 30 kutaka kampuni hiyo kuwasilisha utetezi wake lakini mpaka sasa haijajibiwa.

Kuhusu ofisi ya Bunge kuanzisha maktaba maalumu itakayohusika na utunzaji wa mikataba yote inayoingizwa na serikali, taarifa hiyo inakubali utaratibu huo na itatoa ushirikiano ili kufanikisha utekelezaji wa azimio hilo.
 
Duh! Watu wanajieleza siku 14 tu baada ya timu kuwaandikia miezi mitatu inapita timu bado haijajua hatua gani za kinidhamu za kuchukuliwa. Ndio Ari mpya, Nguvu Mpya na Kasi Mpya? Ile mitambo pale Ubungo itaondoka lini na hela zilizolipwa tayari zitarudi lini? Linahitajika shinikizo na nguvu ya umma!

JJ
 
Date::8/28/2008
Mambo ya Richmond: Karamagi, Msabaha wachunguzwa
Na Ramadhan Semtawa
Mwananchi

SERIKALI imesema imeanza kuwachunguza mawaziri wa zamani wa wizara ya Nishati na Madini, Dk Ibrahim Msabaha na Nazir Karamagi, kama walihusika na rushwa wakati wa mchakato wa zabuni ya umeme wa dharura uliyoipa ushindi Kampuni ya Richmond Development Limted.

Mbali ya uchunguzi huo, serikali imetangaza pia kwamba Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Johnson Mwanyika, Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), Edward Hosea na Katibu Mkuu Wizara ya Nishati na Madini Athur Mwakapugi, wametakiwa kujieleza kutokana na kushindwa kuwajibika katika mchakato huo hadi kulitia taifa hasara.

Akitoa tamko hilo la utekelezaji wa maagizo ya Bunge kwa watuhumiwa wa mkataba wa Richmond bungeni jana, Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, alisema uchunguzi dhidi ya mawaziri hao wa zamani ambao kwa nyakati tofauti waliongoza Wizara ya Nishati na Madini, unalenga kuona kama walihusika na rushwa wakati wa utoaji zabuni.

Azimio namba nane la Bunge lilitaka Waziri wa Nishati na Madini (wakati wa mkataba, Karamagi) awajibishwe, azimio namba tano lilitaka AG awajibishwe namba tisa lilitaka Hosea awajibishwe, wote wawajibishwe na mamlaka ya juu (Rais) huku maafisa wengine nane wa Takukuru wawajibishwe na mamlaka husika kutokana na kuisafisha Richmond.

Katika azimio lake namba 14, lilimtaja Dk Msabaha (aliyekuwa Waziri wa Nishati, kabla ya Karamagi), Katibu Mkuu Mwakapugi na Kamishna wa Nishati Bashir Mrindoko, ambao nao walipaswa kuwajibishwa hata hivyo, tayari mawaziri hao wawili (Dk Msabaha na Karamagi), walishajiuzulu kabla ya kuwajibishwa katika Mkutano wa 10 wa Bunge uliofanyika Februari, mwaka huu.

Azimio la saba la Bunge lilitaka wajumbe wote wa Timu ya Wataalamu wa Kuishauri Serikali katika mazungumzo kuhusu Mikataba (GNT), ambao walitoka Benki Kuu (BoT), Shirika la Umeme (Tanesco), Wizara ya Nishati na Madini na Ofisi ya Mwanasheria Mkuu, wawajibishwe kutokana na kushindwa kuishauri serikali hadi taifa likaingia hasara kwa kuingia mkataba mbovu na Kampuni ya Richmond.

Akizungumzia utekelezaji wa azimio moja hadi jingine, Waziri Mkuu alifafanua kwamba, katika azimio namba 8 na 14, licha ya mawaziri hao kujiuzulu, serikali imeamua kujiridhisha ndiyo maana imeagiza vyombo vya dola vifanye uchunguzi wa kina kuona kama walihusika na jinai ya rushwa kabla ya hatua zaidi kuchukuliwa dhidi yao.

Pinda alifafanua kwamba, tayari pia serikali imeanza utekelezaji wa azimio namba 14 ambalo pia linamtaja Katibu Mkuu Mwakapugi, Mrindoko na namba tano linalomtaja Mwanasheria Mkuu na kuongeza kwamba wameandikiwa barua za kutakiwa kujieleza kwa Rais Jakaya Kikwete, kwa ajili ya kumchukulia hatua kwa kuwa ndiye mamlaka ya kikatiba kufanya hivyo.

Alifafanua kwamba, Hosea na Mwakapugi wametakiwa kujieleza kwa Katibu Mkuu Kiongozi (Philemon Luhanjo) ambaye atatoa maelekezo kwa serikali namna ya kutekeleza zaidi maazimio hayo.

Aliongeza kwamba, Takukuru inatakiwa kueleza kwanini ilishindwa kubainisha kasoro kama ilivyofanya Kamati ya Bunge katika mkataba wa Richmond na pia vipi haikubaini kupuuzwa ushauri wa Mamlaka ya Zabuni (PPRA).

Kuhusu utetezi wa Mwakapugi, Pinda alisema Katibu Mkuu huyo alitakiwa kujieleza kwanini alikiuka maelekezo ya Baraza la Mawaziri, PPRA na kushindwa kuishauri serikali kufanya uchunguzi zaidi kwa RDC kabla ya mkataba.

Pinda alifafanua kwamba Mrindoko, alitakiwa kujieleza kutokana na kushindwa kumshauri Katibu Mkuu wake ambaye alikuwa ni mgeni wizarani hapo wakati alijua kampuni hiyo ya Richmond haikuwa na uwezo, kwani Juni 30, 2004 alisitisha mradi wa bomba la mafuta kutoka Dar es Salaam hadi Mwanza, baada ya kubaini udhaifu huo.

Kuhusu azimio namba 10 ambalo linahusu malipo ya dola za Marekani 4.8 milioni kwa Dowans, alisema uchunguzi wa kina BoT ulibaini kiasi hicho cha fedha kilikuwa ni halali kwani kililipwa kwa ajili ya kuingiza mitambo kwa ndege.

Waziri Mkuu aliongeza kwamba, baada ya serikali kufanyia kazi mapendekezo hayo ya Bunge imebaini kulikuwa na mapungufu ya usimamizi na uwajibikaji wakati wa mchakato wa mkataba huo hadi ulipotiwa saini Juni 23 mwaka 2006.

Alisema kutokana na uthibitisho huo serikali, licha ya kuchukua hatua kwa mawaziri na watendaji hao wa ngazi za juu, pia imetaka maafisa nane wa Takukuru na wajumbe wengine wote wa GNT, wajieleze kwanini walishindwa kutumia utaalamu wao kuliepusha taifa na hasara.

Waziri Mkuu aliongeza kwamba, uamuzi huo wa kuwapa nafasi ya kujieleza, unalenga kutoa haki ya msingi ya kumsikiliza mtu kabla ya hatua nyingine zaidi za kinidhamu kwa mujibu wa sheria hazijachukuliwa.

Huku akionekana kupitia njia ile aliyopita Rais Kikwete wakati akizungumzia watuhumiwa wa ufisadi katika Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA) ndani ya BoT, Pinda alisema utekelezaji huo umechukua miezi sita badala ya mitatu kutokana na kuwa jambo hilo linahitaji umakini na utekelezaji kwa mujibu wa sheria.

Akizungumzia azimio namba 17 ambalo lilitaka RDC ifutwe katika orodha ya Ofisi ya Msajili wa Makampuni na Majina ya Biashara (Brela), alisema uchunguzi umebaini kwamba katika ofisi hiyo kuna Kampuni ya Richmond Tanzania (LTD).

Pinda alifafanua kwamba, RDC haikusajiliwa Brela na kuongeza kwamba, hadi sasa haijathibitika uhusiano kama Richmond hiyo ya nje ilikabidhi majukumu yake kwa Richmond ya nchini.

Hata hivyo, alisema maelekezo ya serikali ni kwamba Brela ifute Richmond Tanzania (LTD), na kufafanua kwamba tayari kampuni hiyo ilipewa barua ili ijitetee lakini hadi sasa haijafanya hivyo.

Kuhusu kama RDC ilighushi nyaraka na kupata zabuni hiyo, alisema jinai huchunguzwa na polisi na kwamba tayari jeshi hilo linachunguza kuona kama wamiliki walifanya kosa hilo la jinai kupata zabuni.

Sakata la Richmond lilitikisa nchi kuanzia Juni mwaka 2006, miezi michache baada ya serikali ya awamu ya nne kuingia madarakani na nchi kukabiliwa na ukame na uhaba wa nishati, hivyo kulazimu serikali kutafuta mitambo ya dharura ya kukodi kwa ajili ya kufua umeme.

Hata hivyo, mpango huo uliingiza serikali ya awamu hiyo ya nne katika kashfa nzito ambayo ilifanya Bunge kuunda Tume yake chini ya Mbunge wa Kyela Dk Harrison Mwakyembe, ambayo katika mkutano wa 10 wa Bunge la Februari ilitoa matokeo yake ambayo yalisababisha aliyekuwa Waziri Mkuu Edward Lowassa, Dk Msabaha na Karamagi, kujiuzulu.
 
Date::8/28/2008
Mambo ya Richmond: Karamagi, Msabaha wachunguzwa
Na Ramadhan Semtawa
Mwananchi

SERIKALI imesema imeanza kuwachunguza mawaziri wa zamani wa wizara ya Nishati na Madini, Dk Ibrahim Msabaha na Nazir Karamagi, kama walihusika na rushwa wakati wa mchakato wa zabuni ya umeme wa dharura uliyoipa ushindi Kampuni ya Richmond Development Limted.

Mbali ya uchunguzi huo, serikali imetangaza pia kwamba Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Johnson Mwanyika, Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), Edward Hosea na Katibu Mkuu Wizara ya Nishati na Madini Athur Mwakapugi, wametakiwa kujieleza kutokana na kushindwa kuwajibika katika mchakato huo hadi kulitia taifa hasara.

Akitoa tamko hilo la utekelezaji wa maagizo ya Bunge kwa watuhumiwa wa mkataba wa Richmond bungeni jana, Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, alisema uchunguzi dhidi ya mawaziri hao wa zamani ambao kwa nyakati tofauti waliongoza Wizara ya Nishati na Madini, unalenga kuona kama walihusika na rushwa wakati wa utoaji zabuni.

Azimio namba nane la Bunge lilitaka Waziri wa Nishati na Madini (wakati wa mkataba, Karamagi) awajibishwe, azimio namba tano lilitaka AG awajibishwe namba tisa lilitaka Hosea awajibishwe, wote wawajibishwe na mamlaka ya juu (Rais) huku maafisa wengine nane wa Takukuru wawajibishwe na mamlaka husika kutokana na kuisafisha Richmond.

Katika azimio lake namba 14, lilimtaja Dk Msabaha (aliyekuwa Waziri wa Nishati, kabla ya Karamagi), Katibu Mkuu Mwakapugi na Kamishna wa Nishati Bashir Mrindoko, ambao nao walipaswa kuwajibishwa hata hivyo, tayari mawaziri hao wawili (Dk Msabaha na Karamagi), walishajiuzulu kabla ya kuwajibishwa katika Mkutano wa 10 wa Bunge uliofanyika Februari, mwaka huu.

Azimio la saba la Bunge lilitaka wajumbe wote wa Timu ya Wataalamu wa Kuishauri Serikali katika mazungumzo kuhusu Mikataba (GNT), ambao walitoka Benki Kuu (BoT), Shirika la Umeme (Tanesco), Wizara ya Nishati na Madini na Ofisi ya Mwanasheria Mkuu, wawajibishwe kutokana na kushindwa kuishauri serikali hadi taifa likaingia hasara kwa kuingia mkataba mbovu na Kampuni ya Richmond.

Akizungumzia utekelezaji wa azimio moja hadi jingine, Waziri Mkuu alifafanua kwamba, katika azimio namba 8 na 14, licha ya mawaziri hao kujiuzulu, serikali imeamua kujiridhisha ndiyo maana imeagiza vyombo vya dola vifanye uchunguzi wa kina kuona kama walihusika na jinai ya rushwa kabla ya hatua zaidi kuchukuliwa dhidi yao.

Pinda alifafanua kwamba, tayari pia serikali imeanza utekelezaji wa azimio namba 14 ambalo pia linamtaja Katibu Mkuu Mwakapugi, Mrindoko na namba tano linalomtaja Mwanasheria Mkuu na kuongeza kwamba wameandikiwa barua za kutakiwa kujieleza kwa Rais Jakaya Kikwete, kwa ajili ya kumchukulia hatua kwa kuwa ndiye mamlaka ya kikatiba kufanya hivyo.

Alifafanua kwamba, Hosea na Mwakapugi wametakiwa kujieleza kwa Katibu Mkuu Kiongozi (Philemon Luhanjo) ambaye atatoa maelekezo kwa serikali namna ya kutekeleza zaidi maazimio hayo.

Aliongeza kwamba, Takukuru inatakiwa kueleza kwanini ilishindwa kubainisha kasoro kama ilivyofanya Kamati ya Bunge katika mkataba wa Richmond na pia vipi haikubaini kupuuzwa ushauri wa Mamlaka ya Zabuni (PPRA).

Kuhusu utetezi wa Mwakapugi, Pinda alisema Katibu Mkuu huyo alitakiwa kujieleza kwanini alikiuka maelekezo ya Baraza la Mawaziri, PPRA na kushindwa kuishauri serikali kufanya uchunguzi zaidi kwa RDC kabla ya mkataba.

Pinda alifafanua kwamba Mrindoko, alitakiwa kujieleza kutokana na kushindwa kumshauri Katibu Mkuu wake ambaye alikuwa ni mgeni wizarani hapo wakati alijua kampuni hiyo ya Richmond haikuwa na uwezo, kwani Juni 30, 2004 alisitisha mradi wa bomba la mafuta kutoka Dar es Salaam hadi Mwanza, baada ya kubaini udhaifu huo.

Kuhusu azimio namba 10 ambalo linahusu malipo ya dola za Marekani 4.8 milioni kwa Dowans, alisema uchunguzi wa kina BoT ulibaini kiasi hicho cha fedha kilikuwa ni halali kwani kililipwa kwa ajili ya kuingiza mitambo kwa ndege.

Waziri Mkuu aliongeza kwamba, baada ya serikali kufanyia kazi mapendekezo hayo ya Bunge imebaini kulikuwa na mapungufu ya usimamizi na uwajibikaji wakati wa mchakato wa mkataba huo hadi ulipotiwa saini Juni 23 mwaka 2006.

Alisema kutokana na uthibitisho huo serikali, licha ya kuchukua hatua kwa mawaziri na watendaji hao wa ngazi za juu, pia imetaka maafisa nane wa Takukuru na wajumbe wengine wote wa GNT, wajieleze kwanini walishindwa kutumia utaalamu wao kuliepusha taifa na hasara.

Waziri Mkuu aliongeza kwamba, uamuzi huo wa kuwapa nafasi ya kujieleza, unalenga kutoa haki ya msingi ya kumsikiliza mtu kabla ya hatua nyingine zaidi za kinidhamu kwa mujibu wa sheria hazijachukuliwa.

Huku akionekana kupitia njia ile aliyopita Rais Kikwete wakati akizungumzia watuhumiwa wa ufisadi katika Akaunti ya Madeni ya Nje (EPA) ndani ya BoT, Pinda alisema utekelezaji huo umechukua miezi sita badala ya mitatu kutokana na kuwa jambo hilo linahitaji umakini na utekelezaji kwa mujibu wa sheria.

Akizungumzia azimio namba 17 ambalo lilitaka RDC ifutwe katika orodha ya Ofisi ya Msajili wa Makampuni na Majina ya Biashara (Brela), alisema uchunguzi umebaini kwamba katika ofisi hiyo kuna Kampuni ya Richmond Tanzania (LTD).

Pinda alifafanua kwamba, RDC haikusajiliwa Brela na kuongeza kwamba, hadi sasa haijathibitika uhusiano kama Richmond hiyo ya nje ilikabidhi majukumu yake kwa Richmond ya nchini.

Hata hivyo, alisema maelekezo ya serikali ni kwamba Brela ifute Richmond Tanzania (LTD), na kufafanua kwamba tayari kampuni hiyo ilipewa barua ili ijitetee lakini hadi sasa haijafanya hivyo.

Kuhusu kama RDC ilighushi nyaraka na kupata zabuni hiyo, alisema jinai huchunguzwa na polisi na kwamba tayari jeshi hilo linachunguza kuona kama wamiliki walifanya kosa hilo la jinai kupata zabuni.

Sakata la Richmond lilitikisa nchi kuanzia Juni mwaka 2006, miezi michache baada ya serikali ya awamu ya nne kuingia madarakani na nchi kukabiliwa na ukame na uhaba wa nishati, hivyo kulazimu serikali kutafuta mitambo ya dharura ya kukodi kwa ajili ya kufua umeme.

Hata hivyo, mpango huo uliingiza serikali ya awamu hiyo ya nne katika kashfa nzito ambayo ilifanya Bunge kuunda Tume yake chini ya Mbunge wa Kyela Dk Harrison Mwakyembe, ambayo katika mkutano wa 10 wa Bunge la Februari ilitoa matokeo yake ambayo yalisababisha aliyekuwa Waziri Mkuu Edward Lowassa, Dk Msabaha na Karamagi, kujiuzulu.

Lowassa hachunguzwi?
 
Kwa kawaida uchunguzi wa jinai huwa hauna pingamizi na kikwazo, sasa kama Karamagi na Msabaha wanachunguzwa katika uchunguzi ambao aliyewaongoza na ambaye wachunguzi hawana ushahidi wa kama alishiriki jinai yoyote ama la!!

Sasaa ni bora akatokea mtu akasema haya yafuatayo (na pengine ndiye).

"WAKIENDELEA KUTUZUGA TUTAANIKA HATA USHAHIDI WA YULE MWANASHERIA ALIYEKWENDA KUBEBA MZIGO WA MZEE NJE YA NCHI NA KUUKABIDHI KWA WAHUSIKA NA JINSI WALIVYOKABIDHIWA".

Mtu huyo atakuwa ameisaidia sana Tanzania Yetu njema. Mungu atamzidishia. Kwa anayewahusu kina Karamagi, Msabaha, Lowassa na ...... awapelekee ujumbe huu wajue kwamba wapo watu wanaojua kilichotokea na baadhi wako kule kule walikochukulia
 
Kazi kwelikweli....Labda kwa mwendo Haki ya watuhumiwa itapatikana...

Halisi Maneno yako Mazito Mkuu
 
Wakuu naomba tuingie hapa http://www.shipping-worldwide.com/ kwa details zaidi ya gharama ya air cargo. Hii serikali inatutania na inatuona ni mabwege bwege wa kutupwa.

Kuna haja ya kuwa na special snipers kueliminate kizazi cha viongozi wetu wabovu............ I smell a rat, blood, and hush!!!! the...of......

For airlift 200 ton cargoflight from US to Singapore is $400,000.00
For airlift 200 ton cargoflight from US to Nigeria is $300,000.00
For airlift 200 ton cargoflight from US to Kenya is $500,000.00

Why??
For airlift 200 ton cargoflight from US to Tanzania is more than $4,865,000.00

For passenger jet of 300 People onboard cost $2000.00 for each passenger for two ways from US to Dar-Es-Salaam which is equal to $600,000.00


By Ship, 200 ton cost $70,000.00 from US TO DAR-ES-SALAAM.

"AZIMIO NAMBA 10:
"Gavana wa Benki Kuu pamoja na Bodi ya Wakurugenzi wachunguze kwa makini uhalali wa malipo ya ziada (US$ 4,865,000) yaliyofanywa kwa Dowans Holdings A.S iliyorithi majukumu ya Richmond Development Company na kuwachukulia hatua waliohusika na uzembe huo."
HATUA ZILIZOCHUKULIWA:
Wizara ya Fedha na Uchumi na Benki Kuu ya Tanzania wamechunguza na kuona kuwa malipo ya US$ 4,865,000 yaliyolipwa kwa Kampuni ya Dowans Holdings S.A. iliyorithi majukumu ya Richmond Development Company LLC ni halali. Malipo hayo yalilipwa tarehe 2 Februari 2007 ikiwa ni gharama za ndege za usafirishaji wa mitambo ya kukodi ya umeme wa dharura, baada ya kupokea Invoice Na. EFD786675. Uchunguzi unaonyesha kuwa, taratibu zote za malipo zilifuatwa na malipo yalifanywa baada ya kuhakikiwa na TANESCO, Wizara ya Nishati na Madini na HAZINA baada ya kupata ushauri wa Kisheria kutoka kwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali kwamba yanawiana na Mkataba husika."
 
Kuna tetesi kuwa Balali ameonekana akikatiza mitaa ndani ya gari la kifahari na alionekana akiingia kwenye gari na kuelekea kusikojulikana ,japo haikuweza kufahamika kama alikuwa ndie mwenyewe au ni mtu wamefanana.
 
Nyambala umesema kweli. Leo niliongea na Selelii, Manyanya, Kilango na Mwakyembe kuhusu utekelezaji wa maazimio ya Bunge. Wao wanasema faraja kubwa waliyonayo ni kwamba taarifa hiyo ya Waziri Mkuu itajadiliwa mwezi Novemba, kipindi ambacho maamuzi yote kiporo yatakuwa yamepatiwa majibu. Kama utekelezaji utaendelea kuyumba, kwa lugha ya mama Kilango, "patakuwa padogo" au "patachimbika".
 
Kuna tetesi kuwa Balali ameonekana akikatiza mitaa ndani ya gari la kifahari na alionekana akiingia kwenye gari na kuelekea kusikojulikana ,japo haikuweza kufahamika kama alikuwa ndie mwenyewe au ni mtu wamefanana.
Wee Mwiba, usitupe kiwewe wenzio. Tetesi hizo zimetokea wapi?
 
Ripoti ya utekelezaji kuhusu Richmond yaduwaza wabunge


Waziri Mkuu,Mizengo Pinda, wakati akitoa taarifa ya utekelezaji wa maazimio ya Bunge kuhusu kashfa ya ufisadi wa kampuni hewa inayojulikana kwa kifupi kama Richmond Bungeni Dodoma Alhamisi.
*Naibu Spika awabembeleza waipokee, wengi watoka nje

Na Tausi Mbowe, Dodoma


SAUTI za minong'ono zilikuwa zimetanda kwenye Ukumbi wa Bunge jana wakati Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, alipokamilisha kusoma hotuba yake ya utekelezaji wa mapendekezo ya Kamati ya Richmond, baada ya hatua kadhaa dhidi ya wahusika kumsubiri rais na watendaji wake.


Uwezekano wa wabunge kujiridhisha kwa kuchangia hotuba hiyo mara baada ya Waziri Mkuu kumaliza kutoa hoja, ulishindikana baada ya Naibu Spika, Anna Makinda, kuzima juhudi hizo akisema wataijadili taarifa hiyo katika kikao kijacho cha Novemba, mwaka huu.


Kati ya mapendekezo hayo ni machache tu ndiyo ambayo utekelezaji wake umekamilika huku mengine muhimu ambayo wabunge na wananchi walikuwa wanayasubiri kwa hamu yakiachwa kwa mamlaka zinazowajibika, likiwamo suala la Mwanasheria Mkuu wa Serikali, kusubiri hatua atakazochukuliwa na Rais Jakaya Kikwete, huku la Mkurugenzi wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru) likiachwa mikononi mwa Katibu Mkuu Kiongozi.


Hali ya wabunge kutoridhishwa na ripoti hiyo ilionekana mara baada ya Waziri Mkuu Pinda, kumaliza kusoma ripoti yake wakati walipoanza kunong'ona na hawakusimama kuonyesha kwamba wameipokea hadi Naibu Spika alipowataka wampigie makofi kuonyesha kuridhishwa.


Baada ya Pinda kumaliza kusoma tamko hilo, Habibu Mnyaa Mbunge wa Mkanyageni (CUF) alisimama kwa kuomba wabunge waijadili ripoti hiyo ya utekelezaji, lakini akamzima.


"Waheshimiwa wabunge mtapata muda wa kuijadili ripoti hii, lakini kwanza mmepewa vitabu hivyo ili msome kwa makini na baadaye ndipo mje kuijadili katika kikao kingine ," alisema Makinda na kuongeza: "Naomba msipoteze vitabu hivyo kwa sababu hamtapewa vingine."


Wakati Makinda akiruhusu Bunge kuendelea na shughuli nyingine, baadhi ya wabunge walianza kutoka ukumbini, hali iliyozua kelele zaidi na Makinda akalazimika kutuliza hali hiyo.


"Jamani mnaotoka, mtoke taratibu ili msisumbue wengine," alisema.


Nje ya Ukumbi wa Bunge, maoni yalikuwa tofauti, wakizungumza mara baada ya Waziri Mkuu Pinda, kusoma taarifa hiyo, baadhi ya wabunge walisema taarifa hiyo ni nzuri ingawa imeshindwa kuonyesha moja kwa moja hatua zilizochukuliwa kwa watuhumiwa wote waliohusika katika ubadhirifu huo.


Wabunge hao kwa nyakati tofauti walisema Waziri Mkuu amefanya haraka kutoa taarifa hiyo bungeni kutokana na ukweli kwamba, Watanzania wengi wanataka kuona serikali imewachukulia hatua watuhumiwa hao na si maneno matupu ya kuziachia mamlaka zifanye kazi hiyo.


Mjumbe wa kamati iliyoundwa kuchunguza mchakato wa zabuni iliyoipa ushindi kampuni ya kufua umeme wa dharura ya Richmond, Lucas Selelii, alisema ripoti hiyo imeweza kuonyesha ukweli na suala hilo na kuwatoa katika malalamiko kamati hiyo tofauti na madai ya baadhi ya wabunge kuwa kamati hiyo ilikuwa imewaonea.


"Leo sisi kama kamati tuna furaha sana, taarifa hii inaonyesha wazi kuwa kamati

yetu haikumuonea mtu, tulichosema kilikuwa na ukweli ingawa utekelezaji wake umechukua muda mrefu sana tangu mwezi Februari mpaka leo ndio ripoti inatolewa," alisema Selelii.


"Inashangaza kwamba kamati yetu ilifanya kazi kubwa katika muda wa miezi mitatu tu, lakini serikali ambayo ina kila kitu imefanya kazi hii kwa miezi sita na kutoa ripoti ambayo

imeacha mambo mengi."


Kauli hiyo iliungwa mkono na aliyekuwa mwenyekiti wa Kamati hiyo, Dk Harrison Mwakyembe, na kusema ripoti hiyo ni mwanzo mzuri wa utekelezaji wa mapendekezo

hayo na kwamba imegusa maeneo yote.


Dk. Mwakyembe ambaye pia ni Mbunge wa Kyela (CCM), alisema kinachotakiwa sasa ni

kuziachia mamlaka zilizopewa jukumu la kuwawajibisha watuhumiwa wa ufisadi huo

wafanye kazi yao na hatimaye kutoa matokeo yake.


Mbunge wa Kigoma Kaskazini (Chadema), Kambwe Zitto, alisema ameridhika na taarifa

hiyo ya serikali na kwamba kambi ya upinzani inachosubiri ni kuona mamlaka

zilizopewa jukumu la kuwachukulia hatua wahusika hao zinafanya hivyo haraka.


"Kikubwa ni kuwawajibisha wote waliohusika katika mchakato huo, kambi ya upinzani,

inasubiri kwa hamu kubwa kuona mamlaka hizo zinawachukulia hatua za kinidhamu wote

waliotuhumiwa," alisisitiza Zitto.


Naye Mbunge wa Bumbuli, William Shelukindo (CCM), alishangazwa na utekelezaji wa mapendekezo hayo ulivyochukua muda mrefu, jambo ambalo alilosema kiutendaji linaweza kukwamisha maendeleo.


Mbunge wa Bariadi Magharibi, Andrew Chenge (CCM) alisema Waziri Mkuu ameeleza vizuri mapendekezo hayo kwani alijibu kila hoja.


Hata hivyo, Chenge alitofautiana na wabunge wengine waliotaka ripoti hiyo ijadiliwe bungeni na kusema kuwa haina haja ya kufanya hivyo kwani kujadili ripoti hiyo ni kupoteza muda hivyo ziachiwe mamlaka zichukue hatua kama ilivyopendekezwa.


"Haya yameshapita, tugange yajayo, kuijadili ripoti hiyo ni sawa na kupoteza muda, kila kitu kimeelezwa sawa kabisa, tuache sheria ifuate mkondo wake,"alisisitiza Chenge.


Naye Msemaji Mkuu wa Kambi ya upinzani Bungeni, Hamad Rashid Mohamed (CUF) alisema kambi ya upinzani imeridhishwa na ripoti hiyo kwa kuwa serikali imejitahidi kutoa majibu yaliyokidhi matarajio ya wabunge.


Mbunge wa Simanjiro, Christopher Ole-Sendeka (CCM), alisema ameridhika na hatua ya serikali kukiri kuwa kulikuwa na mapungufu katika mchakato huo ingawa alishangazwa na kasi ndogo iliyochukuliwa na serikali katika kupitia mapendekezo



Waliotakiwa kuwajibishwa katika sakata hilo ni pamoja na Mwanasheria Mkuu wa Serikali , Johnson Mwanyika, Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (Takukuru), Edward Hosea na Katibu Mkuu Wizara ya Nishati na Madini, Arthur Mwakapugi.


Wakati aliyekuwa Waziri Mkuu, Edward Lowassa, na mawaziri Nazir Karamagi na Dk Ibrahim Msabaha waliwajibika kwa kujiuzulu kwa maslahi ya taifa mara baada ya kutajwa kwenye kashfa hiyo, Mwanyika, Hosea na Katibu Mwakapugi hawajachukua hatua hiyo, huku baadhi yao wakisema wanasubiri Rais Jakaya Kikwete ambaye aliwapa wajibu huo awawajibishe akiona wanastahili.


Hosea ameingia katika kashfa hiyo baada ya Takukuru kuisafisha Richmond katika uchunguzi wake wa awali kufuatia taarifa ya uchunguzi wa taasisi yake kubainisha kwamba mkataba huo haukuwa na harufu ya kifisadi.


Baadhi ya mapendekezo ya Bunge kuhusu kashfa hiyo ni Msajili wa Makampuni (BRELA)

kuifuta Kampuni ya Richmond na wamiliki wake kufunguliwa kesi ya jinai na kisha serikali kuangalia uwezekano wa kusitisha malipo kwa Kampuni ya Dowans. Serikali ilitekeleza pendekezo la kusitisha malipo kwa Dowans Agosti Mosi mwaka huu.


Michango mbalimbali ya wabunge iliifanya Kamati waliyoiunda kuchunguza suala hilo kuongeza mapendekezo mengine saba ambayo ni pamoja na kuitaka Serikali kuendesha uchunguzi wa kina kwa lengo la kubaini taarifa tete kuwa taarifa ya Takukuru kuhusu Richmond ilichezewa na kuitafuta taarifa halisi ya taasisi hiyo.


Mapendekezo mengine, ya kamati hiyo ni Serikali kujiepusha na matumizi ya mawakala katika manunuzi ya umma na kwamba, sheria ya manunuzi (PPRA) ipewe meno zaidi na

ifanye kazi kwa kujitegemea bila kusimamiwa na Wizara ya Fedha. Suala hilo tayari limeshafanyiwa kazi.


Mengine ni serikali kupitia upya mikataba yote na kuanzisha maktaba kwa ajili ya utunzaji wa kumbukumbu katika ofisi za Bunge na kwamba, Timu ya Serikali

inayoshauri Mikataba (GNT) iwajibishwe na aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini,

Nazir Karamagi na Mwanasheria Mkuu wa Serikali pia wawajibishwe.


Baada ya mapendekezo hayo Waziri Mkuu Pinda alisema serikali imeunda timu ndogo ya wataalam kutoka idara zake mbalimbali ili kupitia upya mapendekezo ya kamati hiyo ikiwa ni hatua ya mwanzo katika kutekeleza.


Akizungumza wakati wa kuahirishwa mkutano huo wa 10, Waziri Mkuu Pinda alisema serikali imepokea mapendekezo hayo na itayafanyia kazi ili iweze kuyatekeleza ndani ya miezi mitatu kama ilivyoagizwa na Bunge.


"Napenda kuwajulisha waheshimiwa wabunge kuwa nimeunda timu ndogo kupitia kwa

makini mapendekezo ya Kamati ya Richmond, ila ni vema nikaeleza kuwa baadhi ya mapendekezo ni mazito na yanahitaji muda mwingi zaidi na mengine tutajitahidi

kuyatekeleza ndani ya miezi mitatu kama ilivyopendekezwa na Kamati," alisema Pinda.


Timu aliyounda inahusisha wawakilishi kutoka Ikulu, Sekretarieti ya Mawaziri, Tume ya Maadili, Tamisemi, PPRA, Makandarasi, Utumishi wa Umma na Wizara ya Mipango,

ilipaswa kupitia mapendekezo hayo na kutoa dira ya kuyatekeleza.


Waziri Pinda alikiri kuwepo kwa uzembe katika uwajibikaji kwenye serikali na kusema ripoti ya Richmond iliipa serikali changamoto mpya katika utendaji wake wa

kazi.

source :Mwananchi.
 
...What's the fate of ZE BIG "SAMAKIS"?

AZIMIO NAMBA 5:

HATUA ZILIZOCHUKULIWA:
(i) Kikatiba, Mwanasheria Mkuu wa Serikali ndiye Mshauri Mkuu wa Serikali katika masuala yote ya Sheria za Nchi. Hivyo, ana wajibu mkubwa wa kuishauri Serikali katika maeneo ambayo anaona yanakiuka Sheria, Taratibu na Kanuni za Nchi.

Kutokana na nafasi yake Kikatiba, Mamlaka yake ya Nidhamu ni Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Kwa hiyo, Mwanasheria Mkuu wa Serikali ambaye alikuwa miongoni mwa Watendaji Wakuu watatu waliokuwa wanaishauri Serikali, suala lake la kuhusishwa kwake katika Mchakato mzima wa Mkataba huo linashughulikiwa na Ofisi ya Rais, IKULU.

...dah, huyu 'mzigo' ushamuelemea huyu, basi tena aka 'amekwenda na maji!'!...


AZIMIO NAMBA 8:
"Waziri wa Nishati na Madini, Mhe. Nazir Karamagi (Mb.), aliyeshabikia sana uhaulishaji wa Mkataba kutoka kwa Richmond Develeopment Company LLC kwenda kwa Dowans Holdings S.A. awajibishwe"

HATUA ZILIZOCHUKULIWA:
Mheshimiwa Nazir Karamagi (Mb.), aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini alijiuzulu mwezi Februari 2008 kwa kuwajibika kutokana na suala hili. Hata hivyo, kwa lengo la Serikali kujiridhisha kuhusu ushiriki na ushauri wake katika suala hili, Vyombo vya Dola vinaendelea na uchunguzi wa kina kwa lengo la kutaka kujua kama kuna rushwa yoyote ambayo ilijitokeza katika mchakato huu inayomhusisha Mheshimiwa Nazir Karamagi (Mb.), katika suala hili. Taarifa ya uchunguzi huo itawezesha Serikali kuamua juu ya hatua zaidi zinazostahili kuchukuliwa dhidi yake.

...vyombo vya dola! ndio hao hao TAKUKURU?...kesi ya nyani kumpelekea ngedere?... haya, tutafika tu...

AZIMIO NAMBA 9:
"Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU awajibishwe kwa manufaa ya Umma na Maofisa wa TAKUKURU walioshiriki katika zoezi la uchunguzi na kuandaa Taarifa ya Richmond Development Company LLC iliyoficha ukweli nao pia wawajibishwe kwa manufaa ya Umma."

HATUA ZILIZOCHUKULIWA:
Zoezi la kufanya uchunguzi lililofanywa na TAKUKURU lilihusisha Watumishi wafuatao:

(i) Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU, Bw. Edward Hosea akiwa ndiye Msimamizi Mkuu wa Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU), iliyohusika na uchunguzi wa mchakato mzima wa Zabuni ya umeme wa dharura, ulioipa ushindi Kampuni ya Richmond Development Company LLC.

(ii) Mkurugenzi wa Upelelezi Bw. Alex Mfungo ambaye ndiye aliyesimamia zoezi zima la uchunguzi na kuandaa Ripoti ya Uchunguzi ya TAKUKURU kuhusu suala hili.

Ili kutekeleza Azimio hili, Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU amepelekewa barua ya kutakiwa kujieleza na Mamlaka yake ya Nidhamu ambaye ni Katibu Mkuu Kiongozi.


...inanifurahisha, Mkurugenzi huyo yupo madarakani, mkurugenzi huyo huyo anachunguzwa, halafu naye anatakiwa awahukumu walio chini yake kwa kosa hilo hilo kama lake...


...Vilevile, Wasaidizi walio chini yake walioshiriki katika zoezi la uchunguzi, nao wametakiwa kutoa maelezo yao kwa Mkurugenzi Mkuu wa TAKUKURU ambaye ndiye Mamlaka yao ya Nidhamu. Hii ni kwa kuzingatia Misingi ile ile ya Kanuni Asilia ya Haki ya Kusikilizwa Kwanza (Natural Justice).

,...yaani ni yale yale ya "nani atamfunga paka kengele" au nani atayesema 'mfalme yupo uchi'!...haaaya, kanyaga twende tu...

AZIMIO NAMBA 10:
"Gavana wa Benki Kuu pamoja na Bodi ya Wakurugenzi wachunguze kwa makini uhalali wa malipo ya ziada (US$ 4,865,000) yaliyofanywa kwa Dowans Holdings A.S iliyorithi majukumu ya Richmond Development Company na kuwachukulia hatua waliohusika na uzembe huo."

HATUA ZILIZOCHUKULIWA:
Wizara ya Fedha na Uchumi na Benki Kuu ya Tanzania wamechunguza na kuona kuwa malipo ya US$ 4,865,000 yaliyolipwa kwa Kampuni ya Dowans Holdings S.A. iliyorithi majukumu ya Richmond Development Company LLC ni halali. Malipo hayo yalilipwa tarehe 2 Februari 2007 ikiwa ni gharama za ndege za usafirishaji wa mitambo ya kukodi ya umeme wa dharura, baada ya kupokea Invoice Na. EFD786675. Uchunguzi unaonyesha kuwa, taratibu zote za malipo zilifuatwa na malipo yalifanywa baada ya kuhakikiwa na TANESCO, Wizara ya Nishati na Madini na HAZINA baada ya kupata ushauri wa Kisheria kutoka kwa Mwanasheria Mkuu wa Serikali kwamba yanawiana na Mkataba husika.

...Pheeeew! atleast now you can R.I.P Daudi Ballali.

AZIMIO NAMBA 14:

"Waziri wa Nishati na Madini, Dkt. Ibrahim Msabaha (Mb.), na Katibu Mkuu, Ndugu Arthur Mwakapugi wachukuliwe hatua kali za kinidhamu kwa kuliingiza Taifa kwa makusudi kwenye Mkataba wa Kampuni ya Mfukoni."

HATUA ZILIZOCHUKULIWA:
a) Mheshimiwa Dkt. Ibrahim Msabaha (Mb.), aliyekuwa Waziri wa Wizara ya Ushirikiano wa Afrika Mashariki alijiuzulu mwezi Februari 2008 kwa kuwajibika kutokana na suala hili. Hata hivyo, kwa lengo la Serikali kujiridhisha zaidi kuhusu ushiriki na ushauri wake katika suala hili, Vyombo vya Dola vinaendelea kuendesha uchunguzi wa kina. Lengo ni kutaka kujua kama kuna rushwa yoyote inayomhusisha Mheshimiwa Dkt. Ibrahim Msabaha (Mb.), ambayo ilijitokeza katika mchakato huu, ili hatimaye uamuzi stahiki dhidi yake uweze kuchukuliwa.

...funika kombe hilo mwanaharamu apite, ...justice delayed is justice denied!

b) Kuhusu Katibu Mkuu wa Wizara ya Nishati na Madini Bw. Arthur Mwakapugi ambaye alikuwa miongoni mwa Wajumbe watatu wa Kamati iliyoundwa na Makatibu Wakuu wa Fedha na Uchumi, Nishati na Madini pamoja na Mwanasheria Mkuu wa Serikali, naye amepelekewa barua ya kutakiwa ajieleze katika maeneo ambayo Kamati Teule ya Bunge ilibaini kuwa hakuyazingatia kwa maslahi ya Taifa. Hatua hii imechukuliwa kwa kuzingatia Sheria na Kanuni za Nidhamu katika Utumishi wa Umma na Misingi ya Kanuni Asilia ya Haki ya Kusikilizwa Kwanza (Natural Justice), kabla ya hatua nyingine kuchukuliwa.

...no comment!

AZIMIO NAMBA 16:

"Kwa kuzingatia umuhimu wa nafasi aliyonayo Mheshimiwa Waziri Mkuu katika uendeshaji wa shughuli za Serikali na Uongozi wa Nchi kwa ujumla, ni wajibu wake yeye mwenyewe kupima uzito wa matokeo ya uchunguzi huu na wajibu wake Kikatiba ndani na nje ya Bunge. Vilevile, ni wajibu wa Bunge ambalo linathibitisha uteuzi wake kwa mujibu wa Ibara ya 51 ya Katiba kuangalia kama matokeo ya uchunguzi huu hayataathiri hadhi na uzito wake ndani ya Bunge".

HATUA ZILIZOCHUKULIWA:
Azimio hili lilitekelezwa mwezi Februari 2008 kwa kuwa aliyekuwa Waziri Mkuu aliamua kujiuzulu kwa kuwajibika kisiasa kwa maslahi ya Taifa.

...what? oh, ...ok!, this means his case is officially dismissed!
 
..AG Mwanyika alishang'aka kwamba yeye siyo mwizi, na waandishi wa habari wasimfuatefuate.

..tena aliwa-challenge waandishi kwamba kama kuna mtu ana taarifa zozote juu yake azitoe.
 
Back
Top Bottom