Mjadala: Kero za michango ya Sherehe katika jamii ya Watanzania

View attachment 235905

Kwa kweli michango ya harusi, sijui kitchen Party, Bag party, Send off party na kadhalika imekuwa too much. Unakuta mtu unakuwa na kadi za kudai michango hadi zaidi ya kumi kwa wakati moja. Tabu ya nyongeza ni kwamba viwango vinavyotegemewa ni vya juu. Tutafika?

Je, haijafika mahali wanajamii ya Tanzania tukapunguza madoido na gharama za shughuli hizi?

==============

Katika kumbukumbu zangu mimi, Harusi mtu ulikuwa unafanya kwa uwezo wako, unaita marafiki zako na ndugu mnasherekea hicho kilichopo.

Sasa mtu anakuletea Kadi tena ina kiwango na Watu hawakuchangii sababu wanakupenda ni kama wanakukopesha kwamba na wao siku yao ikifika na wewe utachanga.

Michango Inafika mpaka mamilioni ya pesa watu wanakuja wanakunywa na kula wewe na mwenza wako mnaenda kuanza maisha (wengine hata nyumba hamna) na deni la watu kama mia moja waliokuchangia ambao na wewe inabidi uwachangie.

HIVI NI MIMI TU NINAYEONA KUWA HUU NI UPUUZI NA UJINGA AU KUNA YEYOTE ANAYENIUNGA MKONO?





 
Uswahilini kuna mpaka michano ya birthday.....

Na siku hizi kuna michango ya kufunga kikao pia...
 
Nafikiri ingekuwa bomba tukachanga tukamwachia bwana na bibi harusi kama tume pata 4m tuwape waanzie maisha kama mtaji na harusi iishie pale tu wanapotoka kanisani au baada ya kufunga ndoa kwa waislam
 
Last month nimechangia harusi kama tatu ivi na mwezi huu kama 2 ivi natarajia kuchangia.
 
Nafikiri ingekuwa bomba tukachanga tukamwachia bwana na bibi harusi kama tume pata 4m tuwape waanzie maisha kama mtaji na harusi iishie pale tu wanapotoka kanisani au baada ya kufunga ndoa kwa waislam

hapo ndipo napenda wakenya, sherehe ni minor? better save for the maharusi to start new life!!
 
yote hii si hiyari mwisho wa siku? kuna anayelazimishwa?

sichangii kwa unafiki huku moyo ukiniuma, kama siwezi namwambi muhusika dhahiri kuwa sitaweza kukuchangia. na moyo wangu unakuwa na amani. kazi kwake kunielewa.
 
yote hii si hiyari mwisho wa siku? kuna anayelazimishwa?

sichangii kwa unafiki huku moyo ukiniuma, kama siwezi namwambi muhusika dhahiri kuwa sitaweza kukuchangia. na moyo wangu unakuwa na amani. kazi kwake kunielewa.


hata mimi nashangaa....kwani mmelazimishwa???kama hamuwezi/hampendi msichangie hizo harusi......
 
hata mimi nashangaa....kwani mmelazimishwa???kama hamuwezi/hampendi msichangie hizo harusi......

ndo unafiki huo PRONDO, mtu anakuchangia huku anakung'ong'a kwa nyuma. Ya nini ujitese mwenyewe kiasi hicho badala tu ya kuwa wazi na kuiweka huru nafsi yako!!!
 
sijawahi kuchangia harusi ya mtu ...............na kwa muelekeo niuonao, i never will.

kawaida hununua zawadi na kuipeleka na kwa wale walokuwa kama hujaleta mchango hatukupi kadi ya harusi .............huwa siendi harusi zao. I am not desperate kwenda shughulini kiasi cha kuwa nilazimishwe kiingilio
 
Michango hii tunaindekeza wenyewe. Ni jukumu la maharusi kujuwa pamoja na familia zao kujuwa how they will finance their wedding. Sioni ulazima wa kuchangia kila kitu. It's high time we killed this culture ambayo sjiui tumeitoa wapi.
 

same here!!!
na ninamwambia mtu openly with a pure heart.

'kiingilio'' lol...........umenifurahisha hapo.
 

Gaijin...umenimaliza kabisa, lol...mie hapa nilipo nina kadi za mpka ubatizo, yaani ndugu anabatiza mtoto anakutumia sms kuna kadi yako ya mchango n unaanzia 50 elfu,(hapo kwa ndugu ukisema huna unajua lawama zake tena) ubarikio m 3, wacha mbali haruc...huku nairobi cjawahi kuombwa mchango, ni zawadi yangu tu najiendea kwenye sherehe.
 
sasa sharti la kuwa toa 50000 ndio nikupe kadi si ni sawa na kiingilio tu!

mtu na afanye harusi kwa mujibu wa kipato chake .............kulazimisha wenziwe kumchangia ni tabia za ajabu tu. Hapo unamlazimisha na mtu kuvaa wenyewe wanaita theme color!

akanunue nguo ya rangi hiyo unayotaka na vikorombweza vyake na kisha alipe na kiingilio! .......mimi harusi za sare kwanza huwa siendi pia.....nimemaliza primary zamani, uniform basi kwa kweli
 
ndo unafiki huo PRONDO, mtu anakuchangia huku anakung'ong'a kwa nyuma. Ya nini ujitese mwenyewe kiasi hicho badala tu ya kuwa wazi na kuiweka huru nafsi yako!!!



mie sasa mpaka nimeamua kadi napokea kuchanga sichangi, hiyo ya kumwambia mtu live mwenzio imenishinda...hebu nipe maarifa coz kweli nikikaa vibaya na hii michango nitarudi njoro kulima kahawa.
 
mie sasa mpaka nimeamua kadi napokea kuchanga sichangi, hiyo ya kumwambia mtu live mwenzio imenishinda...hebu nipe maarifa coz kweli nikikaa vibaya na hii michango nitarudi njoro kulima kahawa.
dearest, sio rahisi na inataka moyo mgumu kama wangu. kiukweli mimi ni mtu wa misimamo, na I stand by my principles. So ukija na kadi yako nakwambia tu ukweli sasa how you take that ndo mi sijui (I can imagine though). ntakwambia vizuri kuwa mimi ningependa kuja kwenye harusi lakini huwa sichangi nanunua zawadi tu, so its at your discretion that unipe invitation card au lah!!!
 
heheh unachangia harusi halaf wiki 5 baada ya harusi bwanaharusi anafumaniwa gesti na kadada kachaf chafu ,ukifuatilia hela ya kuhonga kapata wapi? unagundua ni ile hela ya mchango ! kweli Bongo tambarare.
 
aki kuuliza zawadi gani mwambie UPANDE wa KANGA
 

hahaaa G unanichekesha sana aisee lol!!

suala la kufanya harusi kulingana na kipato watu naona halijawaingia akilini bado. tena mi naona hii inakufanya uwe 'stress free' kabisa. Plan it they way you can afford it, usiwe mzigo kwako mwenyewe na kwa wengine pia!!!
 
Kwanza nachukia sherehe za kujitakia zisizokuwa na ubunifu wala mvuto. Matarumbeta yale yale, Ma MC wale wale, lugha zile zile, chakula kile kile, mapambo yale yale, ratiba ile ile, vinywaji vile vile, watu wale wale (sic), onesho lile lile kwa nini niende? Kwa msingi huo ukiongeza na mchango ndo umemalizia.Kiingilio wakati onesho ni lile lile?Inakuwa ngumu. Huwa natunza nguvu zangu kwa shughuli zisizo za kujitakia kama kuzika, kuangalia wagonjwa nk. Huko nitapeleka mchango hata kama sijaulizwa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…