Mjadala: Kero za michango ya Sherehe katika jamii ya Watanzania

Mjadala: Kero za michango ya Sherehe katika jamii ya Watanzania

acha roho mbaya braza wangu, Kuna jamaa hapo ka komenti kuwa ye kwenye haruc yake hakutaka kuchangiwa kwakuwa naye hakuchangia. Sasa kama mtu unahwezo wa kujifanyia haruc yako bila kuchangisha mtu, hivo vi 50k ambavyo kwa mwezi vnaweza tokea mara 1 au 2 ndo ushindwe kweli??? Labda kama hela zako za majini. Binadamu tunasaidiana hizo mia mia zako kwa mwenzio mwenye shida zna umuhimu. ACHA ROHO MBAYA CHANGIA JAMII YAKO.
 
Wazo langu ni serikali kuingilia kati na kupiga maraufuku michango isiyo ya maendeleo. Mfano harusi, na mifano yake. Watanzania huu utamaduni ni wa nchi za kipato cha chini. Mungu ametujalia kuingia kipato cha kati, kwa hiyo michango ya harusi inaondoka yenyewe. Naomba wabunge waokoe hili janga ni tishio kwa wananchi maskini na matajiri pia.
Kwani unashikia bunduki ili uchange.. Mambo mengine mnajipa shida bure.
 
Aiseeee ila kuna watu mnaroho ngumu, kuanzia kipakmara ubatiizo graduu mtu ndugu wamejichanga we leo umefanikiwa hutaki kusikia habari za michango.

Hivi kuna ugumu gani kumchangia mtu unapoweza fanya hivyo, may be your hands are God's hands in their life na hilo suala , ila wewe unakujaa unalalama huku. So sad
 
Bro..kwa.mtu mzima life ni kusapotiana..sio lazima utoe Kama fulani alichotoa..toa/changia kutokana na mfuko wako...hata buku itakuwa Kama mark alart kwa watu / mtu uliyemchangia..japo now days ukichanga 100 tarajia kupata 100 nawe..hata kama uliyemchangia anauwezo wa kutoa zaidi ya hio..hata jali Hali yAko..

Michango ni uwekezaji.
yaaah certainly
 
Kama una ndoto ya kuoa/kuolewa, changa....kama una watoto wanakaribia kuoa/kuolewa, changa. Lakini kama unasomesha na bado bado sana kuozesha, au kama wewe umeamua hutaki kuoa/kuolewa...utaamua mwenyewe[emoji23][emoji23]
 
Wew unaelekea huwa unafanywa mwenyekit kabisa..acha hyo tabia mbaya..kama huna uwezo usifanye harus.sio kusumbua watu..misiba changia..mgonjwa changia..ada changia.ila sherehe..ni aibu
Bro..kanuni za kijamii..ni kwenye shida na raha..ukimiss Moja usije kuona watu hawakupendi ama wanakubagua..then jua si lazima likukute wewe binafsi Ila hata jamaa,watoto na wazazi wako ukataka mchango wa watu wakakususa..
 
Eti harusi ya fulani tulikula na kunywa mpaka vingine vilibaki. Kwa mwafrika ni sifa ila kwa mzungu ni matusi. Tujirekebishe!!
 
Back
Top Bottom