Mjadala kuhusu chanzo cha ulimwengu na maisha

Hoja dhaifu kwenye Quran?? We muislam wa wapi wewe? Nimekwambia nipe aya inayosema hivyo acha porojo mkuu, leta aya katika Quran mkuu na sio porojo zako hazina mantiki hapa.
Quran ilisha andikwa tokea huko mbinguni kisha ndio ikaanza kushuka kwa Muhammad kidogo kidogo

Quran 85
21 Bali hii ni Qur'ani tukufu

22.
Katika Ubao Ulio Hifadhiwa
 
Quran ilisha andikwa tokea huko mbinguni kisha ndio ikaanza kushuka kwa Muhammad kidogo kidogo

Quran 85
21 Bali hii ni Qur'ani tukufu

22.
Katika Ubao Ulio Hifadhiwa
Kutoka katika Arish ya mwenyezi mungu ilitoka kwa Mara moja hadi katika kituo chake kutoka hapo katika kituo ndio Roho mtakatifu huyu ni malaika mkuu Gibril au pia unaweza kumuita Gabriel akawa anaiteremsha kidogo kidogo kwa Muhammad

Hakika Sisi tumeiteremsha Qur'ani katika Laylatul Qadri, Usiku wa Cheo Kitukufu.

2.
Na nini kitacho kujuulisha nini Laylatul Qadri?

3.
Laylatul Qadri ni bora kuliko miezi elfu.

4.
Huteremka Malaika na Roho katika usiku huo kwa idhini ya Mola wao Mlezi kwa kila jambo.
 
Huyo Roho kwa mara ya kwanza kuja kwa Muhammad alimshika na akawa anamlazimisha asome mtume akajibu siwezi kusoma akaongeza nguvu kwa kum bana ndio akaanza kusoma
Point ya msingi kama Roho alikuwa anamlazimisha Muhammad asome ina maana Roho alikuja na maandishi ambayo ndio Quran

Quran 97
1 Soma kwa jina la Mola wako Mlezi aliye umba,

2.
Amemuumba binaadamu kwa tone la damu,

3.
Soma! Na Mola wako Mlezi ni Karimu kushinda wote!
 
Kwa hiyo broo hi Quran unayoiona mtume Muhammad alikuwa anaiandika kwa ajili ya waumini lakini yeye alikuwa amehifadhi moyoni mwake kwa uwezo wa mwenyezi mungu kwa hiyo pia unaweza kusema iliandikwa moyoni mwake

Quran 85--21
Tutakusomesha wala hutasahau,

Hapo mtume Muhammad anambiwa asiwe na wasiwasi kwa maana hayo anayosomeshwa na Roho hatayasahau

Na kwa kumalizia bro hata sasa 70% ya waislam wamehifadhi Quran hata Leo hii zikikusanywa hard copies zote zikichomwa moto waislam wachache tu wana kutana na kuiandika Quran kama ilivyo

Lakini pia Quran ina password iliyowekwa na Mungu mwenyewe ili watu wasitie maneno yao kama walivyo tia maneno katika Tourat, Zaburi na Injili na ndio maana wazungu wamehangaika wamechemka
Password yake ni 19 kuna yani vitu vya msingi katika Quran vinagawanyika kwa 19 bila ya baki

Nadhani hadi apo broo utakuwa umeelewa kuhusu Quran
 
Tone la damu ... fafanua.
 
[Quran 17:36] You shall not accept any information, unless you verify it for yourself. I have given you the hearing, the eyesight, and the brain, and you are responsible for using them.

Unakubaliana na hayo maelezo hapo juu???
 
[Quran 17:36] You shall not accept any information, unless you verify it for yourself. I have given you the hearing, the eyesight, and the brain, and you are responsible for using them.

Unakubaliana na hayo maelezo hapo juu???
Ndiyo.
 
Mwanzo:2.1
Basi mbingu na nchi zikamalizika, na jeshi lake lote.
Mwanzo:2.2
Na siku ya saba Mungu alimaliza kazi yake yote aliyoifanya; akastarehe siku ya saba, akaacha kufanya kazi yake yote aliyoifanya.
Mwanzo:2.3
Mungu akaibarikia siku ya saba, akaitakasa kwa sababu katika siku hiyo Mungu alistarehe, akaacha kufanya kazi yake yote aliyoiumba na kuifanya.
Mwanzo:2.4
Hivyo ndivyo vizazi vya mbingu na nchi zilipoumbwa. Siku ile Bwana Mungu alipoziumba mbingu na nchi
Mwanzo:2.5
hapakuwa na mche wa kondeni bado, wala mboga ya kondeni haijachipuka bado, kwa maana Bwana Mungu hajainyeshea nchi mvua, wala hapana mtu wa kuilima ardhi;
Mwanzo:2.6
ukungu ukapanda katika nchi, ukatia maji juu ya uso wote wa ardhi.
Mwanzo:2.7
Bwana Mungu akamfanya mtu kwa mavumbi ya ardhi, akampulizia puani pumzi ya uhai; mtu akawa nafsi hai.
Mwanzo:2.8
Bwana Mungu akapanda bustani upande wa mashariki wa Edeni, akamweka ndani yake huyo mtu aliyemfanya.
Mwanzo:2.9
Bwana Mungu akachipusha katika ardhi kila mti unaotamanika kwa macho na kufaa kwa kuliwa; na mti wa uzima katikati ya bustani, na mti wa ujuzi wa mema na mabaya.
Mwanzo:2.10
Ukatoka mto katika Edeni wa kuitilia bustani maji, na kutokea hapo ukagawanyika kuwa vichwa vinne.
Mwanzo:2.11
Jina la wa kwanza ni Pishoni; ndio unaozunguka nchi yote ya Havila, ambako kuna dhahabu;
Mwanzo:2.12
na dhahabu ya nchi ile ni njema; huko kuna bedola, na vito shoham.
Mwanzo:2.13
Na jina la mto wa pili ni Gihoni; ndio unaozunguka nchi yote ya Kushi.
Mwanzo:2.14
Na jina la mto wa tatu ni Hidekeli; ndio unaopita mbele ya Ashuru. Na mto wa nne ni Frati.
Mwanzo:2.15
Bwana Mungu akamtwaa huyo mtu, akamweka katika bustani ya Edeni, ailime na kuitunza.
Mwanzo:2.16
Bwana Mungu akamwagiza huyo mtu, akisema, Matunda ya kila mti wa bustani waweza kula,
Mwanzo:2.17
walakini matunda ya mti wa ujuzi wa mema na mabaya usile, kwa maana siku utakapokula matunda ya mti huo utakufa hakika.
Mwanzo:2.18
Bwana Mungu akasema, Si vema huyo mtu awe peke yake, nitamfanyia msaidizi wa kufanana naye.
Mwanzo:2.19
Bwana Mungu akafanyiza kutoka katika ardhi kila mnyama wa msituni, na kila ndege wa angani, akamletea Adamu ili aone atawaitaje; kila kiumbe hai, jina alilokiita Adamu likawa ndilo jina lake.
Mwanzo:2.20
Adamu akawapa majina yao kila mnyama wa kufugwa, na ndege wa angani, na kila mnyama wa mwituni; lakini hakuonekana wa kumsaidia Adamu aliyefanana naye.
Mwanzo:2.21
Bwana Mungu akamletea Adamu usingizi mzito, naye akalala; kisha akatwaa ubavu wake mmoja, akafunika nyama mahali pake,
Mwanzo:2.22
na ule ubavu alioutwaa katika Adamu Bwana Mungu akaufanya mwanamke, akamleta kwa Adamu.
Mwanzo:2.23
Adamu akasema, Sasa huyu ni mfupa katika mifupa yangu, na nyama katika nyama yangu, basi ataitwa mwanamke, kwa maana ametwaliwa katika mwanamume.
Mwanzo:2.24
Kwa hiyo mwanamume atamwacha baba yake na mama yake naye ataambatana na mkewe, nao watakuwa mwili mmoja.
Mwanzo:2.25
Nao walikuwa uchi wote wawili, Adamu na mkewe, wala hawakuona haya.
 
Ufafanuzi... Mungu alimsimulia hii story nani?...
Maana ya Mungu kustarehe ni nin.... Je, ina maana Mungu huwa anafikiria pia??

Akampulizia puani pumzi... (hivi kulikuwa na haja ya kumpulizia?)
 
Safi sana.
 
BIG BANG THEORY


ABIOGENESIS

GOD CREATION
 
In short, Mungu ana fast forward less important details ili mwanadamu usije ukajifanya una akili nyingi.

We humans are always unpredictable, deviant, variants ,(according to loki)
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…