Masokotz
JF-Expert Member
- Nov 26, 2018
- 3,713
- 6,121
Habari za wakati huu;
Kwanza nieleze kwa uwazi kabisa kwamba huu mjadala ni wa wazi hauna lengo la kubomoa bali unalengo la kujenga.
Kati ya mwaka 2016-2019 nilishirika katika utafiti mkubwa ambao ulikuwa na husu swali zima la Nguvu kazi(Labour Force).Katika utafit nilijifunza mengi sana ikiwapo historia, maendeleo na dhana ya Nguvu Kazi.Tulitazama Nguvu kazi ya dunia, Maeneo ya kiuchumi, kanda, mabara, mataifa na nchi moja moja. Tulitazama pia sekta mbalimbali za kiuchumi katika maeneo mbalimbali ya ulimmwengu ikiwa nchi zilizoendelea na zinazoendelea ikiwamo China, Uingereza na Tanzania.
Nilibahatika kujifunza mengi kwani pamoja na kwamba sikuwa mtaalam katika utafiti huu lakini nilipewa nafasi ya kipekee ambayo iliniwezesha kusoma maandiko mengi,kushiriki katika mijadala mingi na hata kupitia takwimu na taarifa nyingi. Utafiti ulikuwa unalenga sana kuelewa Changamoto za ulimwengu katika swala la Nguvu Kazi. Baadhi ya mambo tuliyotafiti yamejadiliwa katika tafiti na ripoti mbalimbali ikiwamo World Development Report 2020.
Moja kati ya swali ambalo tulijiuliza ni juu ya Mchango wa elimu kama ilivo katika mfumo wa sasa katika kuhakikisha kwamba tunakuwa na Nguvu kazi yenye TIJA.Hoja ilikuwa ni iwapo elimu ya sasa inamuaandaa msomi kwa ajili ya kufanya kazi za huko mbeleni kwani kwa mkasi ya maendeleo ya dunia tunaona kabisa kutaibuka aina nyingi mpya za kazi na pia aina nyingi sana za kazi kama tunavozifahamu sasa zitatoweka teknolojia kama AI,ML,IT,Space Technology,Robotics,etc zitabadilisha sana fani nyingi ulimwenguni swali ni Je tunawaandaaje watoto wetu kufanya kazi katika mazingira haya?
Miaka ya nyuma mafaili na nyaraka zote zilihifadhiwa ofisini,zilichapwa ofisini na hakuna namna mtu angeweza kufanya kazi bila kwenda ofisini lakini hali imebdailika kwa sasa.Ninapoandika andiko hili niko nyumbani kwangu,kwenye ofisi yangu ambayo iko nyumbani ambapo katika ofisi hii yangu ndgu ninahudumia wateja zaidi ya 50 ambao ni individuals,na kampuni 14 na kwa siku na pokea simu za kazi zisizopungua 20 na kuandika email zisizopungua 20 na kupokea email zisizopungua 20.
Kazi hii naifanya na wasidizi wawili tu ambao kila mmoja yuko nyumbani kwake na tunaunganishwa na mfumo wa kompyuta tu kufanya kazi zetu. Haya ni mabadiliko makubwa sana katika teknolojia. Ukiitazama workload yangu na project ambazo tunafanya utaona kwamba zinahitaji watu wengi zaidi na eneo kubwa zaidi lakini mimi natumia less space, less time, less resources huku nikitengeneza value kubwa kwa ajili yangu na wateja wangu.
Swali la kujiuliza ni Je kama katika udogo wa mtaji wangu na uwezo,uchache wa fursa,changamoto za kibiashara na kiuchumi nimeweza kufanya shughuli zangu nyumbani kwa kipindi chote hiki Je, huko mbele tunakoenda hali itakuwaje? Je, kama kila kampuni ikichagua kutumia mfumo wa teknolojia katika kufanya shughuki zake ni watu wangapi watakosa fursa kwa sababu ya kuwa wazito kujifunza teknolojia mpya? Je, tunawaandaaje watoto hawa na wafanyakazi hawa kwa ajili ya fursa zijazo?Tunawapa elimu itakayowafaa?Tunawapa skills zitakazowafaa?Tunawapa ujuzi utakaowafaa?
Mwaka Jana nilianza kufanya maandalizi ya Program mpya ya MVP (Managed venture Program) Ilikuwa ni Program nzuri sana na ya kipekee na ambayo na amini ingekuwa moja kati ya Program za mwanzo kabisa kama hizo hapa nchini.Itakapokamilika Program hii itaongeza Productivity ya wasomi wetu kwa asilimia 200 yaani kama mtu anafanya kazi yenye thamani ya TZS 1,000,000 basi atakuwa anafanya kazi ya 2,000,000 katika program hii.
Katika hatua za mwanzo nilipata watu wengi sana ambao walitaka kushiriki mpaka nikapata wasiwasi wa kwamba naweza nikashindwa ku scale up. Niliwaambia wale ambao walisign up mapema kwamba tutaenda taratibu kwa sababu ni program mpya na lazima nitafute enough skills kwa ajili ya kuhakikisha kwamba wateja wanapata huduma bora yenye thamani ya pesa zao.Kwa ajili ya Program Hii nilibahatika kukagua CV(Wasifu zaidi ya 1000) nilifanya Interview kwa njia ya simu zaidi ya 200 na za ana kwa ana zaidi 200.
Nilichojifunza ni kwamba kulikuwa na skills GAP kubwa sana katika wote niliozungumza nao hasa katika maswala ya teknolojia.Wengi bado wanaitazama teknolojia kama mazingaombwe na mchezo wa burudani.NIlikutana na wahitimua wa IT ambao walikuwa BUSY kutaka kutengeneza OS zao huku wakiiga fetaures kutoka kwa MS na nikawauliza kitu kitawafanya watu waache Windows OS watumie ya kwako? Nilikutana na watu wanatengeneza Program mbalimba nzuri na za kipekee ila wanakwama kwenye kuzifanya ziiingize Pesa.
Kuna watu wana Passion sana ila hawana mitaji au skills za kutosha na kuna watu wana mitaji na skills ila hawana Passion.Pia kuna ambao wanakuwa na Pasion na skills ili wakipata mitaji huu upande mwingine unapoa.Yaani ni kama vile wamelogwa.Nikakumbuka kauli ya Prof Shivji katika maandiko yake aliposema kwamba Taasisi za elimu zisiwe assembly line za wahitimu bali ziwe kisima cha maarifa, kitovu cha mijadala na kuzalisha maarifa mapya"Prof Shivji alikuwa sahihi kwani vyuo vilikuwa vianshindana kwa vigezo vya udahili na wahitimu huku kukiwa hakuna Publication za aina yoyote ile na hata zile chache zilizopo zikiwa hazina viwango. Ukitembelea vyuo vingi vikuu Tanzania utakuta hawana mfumo mzuri wa kuchapisha maandiko. Wasomi wachache ambao wanakiu ya kuchapa inabidi wahangaike kupeleka machapisho yao sehemu tofauti.Wachache ambao wanachapa kwa bidii ni wale ambao wanakimbiza kutafuta namna ya kula fedha za ufadhili(Grants) huku wakitoa maandiko ambayo hata ukitaka kuwa recite unashtuka kidogo.
Ukija huku mtaani utakuta idadi kubwa ya vijana wakitembeza CV huku wale ambao wako katika maofisi wakiwa wanapiga umbea kwa sababu ama ya uvivu,uzembe. Unakuta Mtumisihi wa serikali au sekta binafsi analala na kazi kwa muda mrefu huku akitumia muda mwingi kuzurura mitaani na mitandaoni na kupiga umbea na kusubiri mshahara utoke. Kwa ufupi unakuta katika masaa 8 ya kazi kwa siku tunatumia masaa 6 katika umbea soga na saga. Tunajikuta kama taifa tuna high unemployment and underemployment.
Jacob Mincer ambaye ni mmoja wa wasomi mahiri kuhusu masuala ya Labour Economics ametafit sana kuhusu changamoto za kufahamu nafasi ya Nguvu kazi katika uchumi. Ni mtu ambaye ukimsoma katika maandiko yako utapata uelewa zaidi juu ya changamoto ya miaka ijayo. Wapo wasome wengine katika eneo hilo ambao wamewahi kutoa michango ya kipekee kama Alvin Toffler aliyesema kwamba "Washamba/Wajinga wa miaka ijayo sio wale wasiojua kusoma na kuandika bali ni wale ambao watashindwa kujifunza,kubadilika na kujifunza upya"Hii sio tafsiri rasmi ila kiingereza chake ni hiki
Nimeleta mjadala huu hapa baada ya kumsikia Mbunge Kishimba ambaya naamni kabisa anastahili kuwa Education Theorist wa Zama Zetu hapa Tanzania kwa sababu ya namna mtazamo wake kuhusu elimu unavohoji maswala ya msingi katika mfumo wetu wa elimu.Nimeleta mjada huu ili nichokoze mjadala wa kitaifa kuhusu mfumo wetu wa elimu na changamoto zake kwani naamini kabisa ni suala ambalo linahitaji mtazamo wa kila mmoja wetu kwa kadiri ya uelewa wake kwa kuzingatia uelekeo wa elimu yetu.
Ninataka kuchokoza mjadala kuhusu thamani ya elimu yetu(Cost vs Output) Je elimu yetu inatupa Return On Investment tunayostahili au kutarajia?je kuna haja ya kila mtu kuwa na Degree, Masters au PHD?Je kuna haja hata ya kila mtu kuwa na Cheti cha ngazi ya elimu fulani. Je, kati ya Cheti na maarifa yanayomjenga mtu kipi ni Cha muhimu?Je tuendelee kuwa taifa la vyeti, passmark na elimination?Je mfumo wetu wa elimu una mantiki yoyote katika muundo wake wa sasa iwpo shule zetu hazina maktaba, hazitumii teknolojia ya kisasa katika kutoa elimu,hazizingatii uwezo na kipaji cha mwananfunzi, na wala hakizingatii mahitaji ya kijamii na mazingira ya mwanafunzi?
Kuna maswali mengi ya kujiuliza mintarafu elimu yetu na mustakabali wa nchi yetu.Ni maswali ambayo hayahitaji siasa, uchama, udini, ukabila aua hata tofauti za kielimu ziletwazo na vyeti. Ni majadala ambao unahitaji kutazama changamoto zetu katika uhalisia wake na kuzitafutia suluhu kwa pamoja kama askari walioko vitani ambao wajibu wao ni mmoja tu kushinda vita.
Mwandishi wa makala hii anaweza kufikiwa kwa email:masokotz@yahoo.com ili kuendeleza mjada huu nje ya jukwaa hili.
Hata hivyo maoni yote yatakayowekwa hapa yatakusanywa na mwandishi kwa kuzingati uzito wake na kuwasililishwa wizara ya elimu kwa ajili ya mjadala zaidi. Tujitahidi kujadili kwa staha, maarifa, hekima, heshima, utulivu na kama mods itawapendeza basi niwe nimechokoza mjadala wa elimu yetu kwa kuufanya uzi huu uwe sticky thready.
Kuhusu kichwa cha mada hii ningeonmba kibaki kama kilivyo kwani tunatafuta Jibu la hilo swali
Kwanza nieleze kwa uwazi kabisa kwamba huu mjadala ni wa wazi hauna lengo la kubomoa bali unalengo la kujenga.
Kati ya mwaka 2016-2019 nilishirika katika utafiti mkubwa ambao ulikuwa na husu swali zima la Nguvu kazi(Labour Force).Katika utafit nilijifunza mengi sana ikiwapo historia, maendeleo na dhana ya Nguvu Kazi.Tulitazama Nguvu kazi ya dunia, Maeneo ya kiuchumi, kanda, mabara, mataifa na nchi moja moja. Tulitazama pia sekta mbalimbali za kiuchumi katika maeneo mbalimbali ya ulimmwengu ikiwa nchi zilizoendelea na zinazoendelea ikiwamo China, Uingereza na Tanzania.
Nilibahatika kujifunza mengi kwani pamoja na kwamba sikuwa mtaalam katika utafiti huu lakini nilipewa nafasi ya kipekee ambayo iliniwezesha kusoma maandiko mengi,kushiriki katika mijadala mingi na hata kupitia takwimu na taarifa nyingi. Utafiti ulikuwa unalenga sana kuelewa Changamoto za ulimwengu katika swala la Nguvu Kazi. Baadhi ya mambo tuliyotafiti yamejadiliwa katika tafiti na ripoti mbalimbali ikiwamo World Development Report 2020.
Moja kati ya swali ambalo tulijiuliza ni juu ya Mchango wa elimu kama ilivo katika mfumo wa sasa katika kuhakikisha kwamba tunakuwa na Nguvu kazi yenye TIJA.Hoja ilikuwa ni iwapo elimu ya sasa inamuaandaa msomi kwa ajili ya kufanya kazi za huko mbeleni kwani kwa mkasi ya maendeleo ya dunia tunaona kabisa kutaibuka aina nyingi mpya za kazi na pia aina nyingi sana za kazi kama tunavozifahamu sasa zitatoweka teknolojia kama AI,ML,IT,Space Technology,Robotics,etc zitabadilisha sana fani nyingi ulimwenguni swali ni Je tunawaandaaje watoto wetu kufanya kazi katika mazingira haya?
Miaka ya nyuma mafaili na nyaraka zote zilihifadhiwa ofisini,zilichapwa ofisini na hakuna namna mtu angeweza kufanya kazi bila kwenda ofisini lakini hali imebdailika kwa sasa.Ninapoandika andiko hili niko nyumbani kwangu,kwenye ofisi yangu ambayo iko nyumbani ambapo katika ofisi hii yangu ndgu ninahudumia wateja zaidi ya 50 ambao ni individuals,na kampuni 14 na kwa siku na pokea simu za kazi zisizopungua 20 na kuandika email zisizopungua 20 na kupokea email zisizopungua 20.
Kazi hii naifanya na wasidizi wawili tu ambao kila mmoja yuko nyumbani kwake na tunaunganishwa na mfumo wa kompyuta tu kufanya kazi zetu. Haya ni mabadiliko makubwa sana katika teknolojia. Ukiitazama workload yangu na project ambazo tunafanya utaona kwamba zinahitaji watu wengi zaidi na eneo kubwa zaidi lakini mimi natumia less space, less time, less resources huku nikitengeneza value kubwa kwa ajili yangu na wateja wangu.
Swali la kujiuliza ni Je kama katika udogo wa mtaji wangu na uwezo,uchache wa fursa,changamoto za kibiashara na kiuchumi nimeweza kufanya shughuli zangu nyumbani kwa kipindi chote hiki Je, huko mbele tunakoenda hali itakuwaje? Je, kama kila kampuni ikichagua kutumia mfumo wa teknolojia katika kufanya shughuki zake ni watu wangapi watakosa fursa kwa sababu ya kuwa wazito kujifunza teknolojia mpya? Je, tunawaandaaje watoto hawa na wafanyakazi hawa kwa ajili ya fursa zijazo?Tunawapa elimu itakayowafaa?Tunawapa skills zitakazowafaa?Tunawapa ujuzi utakaowafaa?
Mwaka Jana nilianza kufanya maandalizi ya Program mpya ya MVP (Managed venture Program) Ilikuwa ni Program nzuri sana na ya kipekee na ambayo na amini ingekuwa moja kati ya Program za mwanzo kabisa kama hizo hapa nchini.Itakapokamilika Program hii itaongeza Productivity ya wasomi wetu kwa asilimia 200 yaani kama mtu anafanya kazi yenye thamani ya TZS 1,000,000 basi atakuwa anafanya kazi ya 2,000,000 katika program hii.
Katika hatua za mwanzo nilipata watu wengi sana ambao walitaka kushiriki mpaka nikapata wasiwasi wa kwamba naweza nikashindwa ku scale up. Niliwaambia wale ambao walisign up mapema kwamba tutaenda taratibu kwa sababu ni program mpya na lazima nitafute enough skills kwa ajili ya kuhakikisha kwamba wateja wanapata huduma bora yenye thamani ya pesa zao.Kwa ajili ya Program Hii nilibahatika kukagua CV(Wasifu zaidi ya 1000) nilifanya Interview kwa njia ya simu zaidi ya 200 na za ana kwa ana zaidi 200.
Nilichojifunza ni kwamba kulikuwa na skills GAP kubwa sana katika wote niliozungumza nao hasa katika maswala ya teknolojia.Wengi bado wanaitazama teknolojia kama mazingaombwe na mchezo wa burudani.NIlikutana na wahitimua wa IT ambao walikuwa BUSY kutaka kutengeneza OS zao huku wakiiga fetaures kutoka kwa MS na nikawauliza kitu kitawafanya watu waache Windows OS watumie ya kwako? Nilikutana na watu wanatengeneza Program mbalimba nzuri na za kipekee ila wanakwama kwenye kuzifanya ziiingize Pesa.
Kuna watu wana Passion sana ila hawana mitaji au skills za kutosha na kuna watu wana mitaji na skills ila hawana Passion.Pia kuna ambao wanakuwa na Pasion na skills ili wakipata mitaji huu upande mwingine unapoa.Yaani ni kama vile wamelogwa.Nikakumbuka kauli ya Prof Shivji katika maandiko yake aliposema kwamba Taasisi za elimu zisiwe assembly line za wahitimu bali ziwe kisima cha maarifa, kitovu cha mijadala na kuzalisha maarifa mapya"Prof Shivji alikuwa sahihi kwani vyuo vilikuwa vianshindana kwa vigezo vya udahili na wahitimu huku kukiwa hakuna Publication za aina yoyote ile na hata zile chache zilizopo zikiwa hazina viwango. Ukitembelea vyuo vingi vikuu Tanzania utakuta hawana mfumo mzuri wa kuchapisha maandiko. Wasomi wachache ambao wanakiu ya kuchapa inabidi wahangaike kupeleka machapisho yao sehemu tofauti.Wachache ambao wanachapa kwa bidii ni wale ambao wanakimbiza kutafuta namna ya kula fedha za ufadhili(Grants) huku wakitoa maandiko ambayo hata ukitaka kuwa recite unashtuka kidogo.
Ukija huku mtaani utakuta idadi kubwa ya vijana wakitembeza CV huku wale ambao wako katika maofisi wakiwa wanapiga umbea kwa sababu ama ya uvivu,uzembe. Unakuta Mtumisihi wa serikali au sekta binafsi analala na kazi kwa muda mrefu huku akitumia muda mwingi kuzurura mitaani na mitandaoni na kupiga umbea na kusubiri mshahara utoke. Kwa ufupi unakuta katika masaa 8 ya kazi kwa siku tunatumia masaa 6 katika umbea soga na saga. Tunajikuta kama taifa tuna high unemployment and underemployment.
Jacob Mincer ambaye ni mmoja wa wasomi mahiri kuhusu masuala ya Labour Economics ametafit sana kuhusu changamoto za kufahamu nafasi ya Nguvu kazi katika uchumi. Ni mtu ambaye ukimsoma katika maandiko yako utapata uelewa zaidi juu ya changamoto ya miaka ijayo. Wapo wasome wengine katika eneo hilo ambao wamewahi kutoa michango ya kipekee kama Alvin Toffler aliyesema kwamba "Washamba/Wajinga wa miaka ijayo sio wale wasiojua kusoma na kuandika bali ni wale ambao watashindwa kujifunza,kubadilika na kujifunza upya"Hii sio tafsiri rasmi ila kiingereza chake ni hiki
The illiterate of the 21st century will not be those who cannot read and write, but those who cannot learn, unlearn, and relearn. ”
Nimeleta mjadala huu hapa baada ya kumsikia Mbunge Kishimba ambaya naamni kabisa anastahili kuwa Education Theorist wa Zama Zetu hapa Tanzania kwa sababu ya namna mtazamo wake kuhusu elimu unavohoji maswala ya msingi katika mfumo wetu wa elimu.Nimeleta mjada huu ili nichokoze mjadala wa kitaifa kuhusu mfumo wetu wa elimu na changamoto zake kwani naamini kabisa ni suala ambalo linahitaji mtazamo wa kila mmoja wetu kwa kadiri ya uelewa wake kwa kuzingatia uelekeo wa elimu yetu.
Ninataka kuchokoza mjadala kuhusu thamani ya elimu yetu(Cost vs Output) Je elimu yetu inatupa Return On Investment tunayostahili au kutarajia?je kuna haja ya kila mtu kuwa na Degree, Masters au PHD?Je kuna haja hata ya kila mtu kuwa na Cheti cha ngazi ya elimu fulani. Je, kati ya Cheti na maarifa yanayomjenga mtu kipi ni Cha muhimu?Je tuendelee kuwa taifa la vyeti, passmark na elimination?Je mfumo wetu wa elimu una mantiki yoyote katika muundo wake wa sasa iwpo shule zetu hazina maktaba, hazitumii teknolojia ya kisasa katika kutoa elimu,hazizingatii uwezo na kipaji cha mwananfunzi, na wala hakizingatii mahitaji ya kijamii na mazingira ya mwanafunzi?
Kuna maswali mengi ya kujiuliza mintarafu elimu yetu na mustakabali wa nchi yetu.Ni maswali ambayo hayahitaji siasa, uchama, udini, ukabila aua hata tofauti za kielimu ziletwazo na vyeti. Ni majadala ambao unahitaji kutazama changamoto zetu katika uhalisia wake na kuzitafutia suluhu kwa pamoja kama askari walioko vitani ambao wajibu wao ni mmoja tu kushinda vita.
Mwandishi wa makala hii anaweza kufikiwa kwa email:masokotz@yahoo.com ili kuendeleza mjada huu nje ya jukwaa hili.
Hata hivyo maoni yote yatakayowekwa hapa yatakusanywa na mwandishi kwa kuzingati uzito wake na kuwasililishwa wizara ya elimu kwa ajili ya mjadala zaidi. Tujitahidi kujadili kwa staha, maarifa, hekima, heshima, utulivu na kama mods itawapendeza basi niwe nimechokoza mjadala wa elimu yetu kwa kuufanya uzi huu uwe sticky thready.
Kuhusu kichwa cha mada hii ningeonmba kibaki kama kilivyo kwani tunatafuta Jibu la hilo swali