Basi baada ya Baba kuondoka nilimwambia mama leo ndo siku ya mwisho kukushuhudia unalia sitokubali tena, nikachukua simu nikampigia Babu yangu nikamwambia Baba kampiga sana mama naomba mje tumchukue tumpeleke hospitali, basi bibi na uncle na Babu wakafika ila walivyokuja tu na Baba akawa ameludi akaanza kuzuia mama asipelekwe popote Ukazuka ugomvi mkubwa pale ghafla tena Baba ndo akaharibu kabsa akamtukana bibi yetu (Kum*** la ma**k),
Aisee hapa ndo nikajua sasa kweli huyu mzee ni hakuna kitu kabisa kichwani yani badala ya kuketi chini aombe hata msamaha yeye anatukana wakwe tena?,... basi akataka hadi kumpiga bibi ila wakina uncle wakamzuia na wakamchukua mama tukaondoka tukapitia Polisi wakachukua PF3 (kama nimekosea mnirekebishe, nasikiaga watu wakiita hivyo),
Kuanzia hapo tukahamia nyumbani kwa Babu, na Baba akaanza kuja kuomba misamaha pale lakini safari hii walimkatalia kabisa maana sio mara ya kwanza kwenda kwa babu na bibi kuomba misamaha kwa makosa yale yale ya kumpiga mama na Kuwatukana,
INAENDELEA