MJADALA: Kwanini Padri Luther aliondoa baadhi ya vitabu kwenye Biblia, na kwanini alijiondoa kanisa Katoliki?

MJADALA: Kwanini Padri Luther aliondoa baadhi ya vitabu kwenye Biblia, na kwanini alijiondoa kanisa Katoliki?

Umevurugwa
KWANINI PADRE Luther ALIFUKUZWA KANISA KATOLIKI? NA KWANINI ALIONDOA BAADHI YA VITABU KWENYE BIBLIA AGANO LA KALE?

Padre Luther alikuwa miongoni mwa Mapdre wenye karama nyingi ndani ya Kanisa katoliki wakati wake, Yeye alikuwa na Madai mengi sana juu ya mapungufu kwa kanisa. Hata hivyo madai yake mengi hayakuwa na msingi wowote.

Moja ya madai yake ilikuwa ni kuondoa kibali cha kwamba baada ya kuungama muumini asipewe stakabadhi ya kuonesha ameungama kwa kuwa kitubio ni siri ya MTU. Hili lilifanyiwa kazi. Mengine ikiwemo kurekebisha mfumo WA sala ya Kanuni ya Imani. Na mambo mengine mengi ambayo alipojibiwa, yeye hakuridhika pamoja na kueleweshwa vya kutosha. Alikuwa ni Great Thinker sana.


Mbaya zaidi alipokuja kusababisha mpaka akajitenga na kanisa ni kitendo cha kuondoa baadhi ya vitabu kwenye Biblia ikiwemo pia kupunguza baadhi ya mistari kwenye vitabu kama cha Esta na Cha Danieli.
Aliondoa vitabu vya Deutrokanoni na vingine baadhi na kuwa jumla ya vitabu 7 vilivyotolewa kwenye Biblia. Na kila kitabu alikuwa na sababu yake aliyoibainisha. Kimsingi alipata wafuasi wengi WA kumuunga mkono hoja yake hasa wale ambao walikuwa wanatafta njia ya kuchuma pesa kiulaini. Na hapo Biblia mpya ilianza yenye Vitabu pungufu.

Na ndio maana Leo watu hawaujui Ukristo vizuri na wanakinzana bila kujua historia ya kanisa. Watumishi wengi WA Mungu hasa HAWA WA kileo wasiojua nhistoria vizuri wao kila kitu wanapinga. Sio kosa lao Bali ni kosa la kutokujua historia ya kanisa.
Matumizi ya Ubani yalipingwa sana, na hapa ilikuwa ni kuondoa idadi ya waelewa. Kutokana na watu wengi walikuwa wamegeuka kama waganga kila mapepo ya kiwakabili walitumia ubani kuyafukuza na yalikimbia, lakini watu walijisahau kusali na kuomba na hata kufika ibadani ikawa nadra maana wanajua kujiponya kuondokana na majini na wachawi. Hapa Padre Luther na wenzake wakapiga marufuku matumizi ya ubani na kuwa sihi wakazanie Neno zaidi.

Hapa walichotakiwa kufanya ni kuliishi Neno la Mungu na wakati WA ibada basi ubani uchomwe kama Mungu alivyo agiza.
Luther na wenzake lengo lao lilikuwa ni biashara hapo baadae na kimsingi mpango huo ulifanikiwa. Na ndio maana mpaka Leo watu wametawaliwa na mfumo WA majini katika maisha yao kwa kuwa wamefungwa akili ya kujitambua na wanaamini maneno ya mdomoni na sio Maandiko ya Biblia kama yanavyosema.
Nimengi ya kujifunza sana Leo hii lakini kwa Leo naishia hapa.

deogratius Nalimi Kisandu.
1. 1. 2017.

Umevurugwa kama hujui jambo ni vyema ukanyamaza kimya.
 
mathayo 13.
54 akaenda kijijini kwake. Huko akawa anawafundisha watu katika sunagogi hata wakashangaa, wakasema, "Huyu amepata wapi hekima hii na maajabu? 55 Je, huyu si yule mwana wa seremala? Je, mama yake si anaitwa Maria, na ndugu zake si kina Yakobo, Yosefu, Simoni na Yuda? 56 Na dada zake je, si wote wako hapa pamoja nasi? Basi amepata wapi haya yote?" .
Ukienda kwenye lugha ya Kiingereza inaeleza kwa uwazi zaidi:

54. And when he was come into his own Country,he taught them in their synagogue.....
55. Is not this the Carpenter's son?is not his mother called Mary?and his brethren James, and Josef, and Simon, and Judas?
56. And his sisters, are they not all with us?....

Walishangaa kwa sababu kwa macho ya kibinadamu hakukuwa na tofauti kati ya familia zao na familia ya Yusufu waliyemtambua kama ndiye Baba yake Yesu.

Kama walivyokuwa wao na watoto wengi wenye tabia tofauti ndivyo familia ya Yusufu ilivyokuwa.Ila walimshangaa mtoto Yesu kapata wapi ufahamu mkubwa hivyo?

Yohana 7:2-5 inatuambia pia juu ya kaka zake Yesu na inaenda mbali zaidi kwa kutuambia pia kuwa sio watu wa Galilaya peke yao bali ata kaka zake Yesu pia hawakumuamini Yesu kuwa ni Kristo.
 
Toka mwanzo hata mwisho wa dunia biblia itabaki kuwa na vitabu 72/73..,

Ndugu ninapoandika 72/73 na maana hii..

Kitabu cha Maombolezo kiuhalisia ni kitabu cha Yeremia...Huwa kinaitwa Maombolezo ya Yeremia...

Sasa Biblia zingine huwa zinaweka kama kitabu Kimoja yani ' Yeremia na maombolezo ya Yeremia"

Biblia zingine (nyingi) hutengenisha na kufanya kuwa vitabu viwili yani Maombolezo na Yeremia...(Ila kimsingi ni kitabu kimoja)
Ndio maana huwa naandika 72/73..., usiogope..Najua ulikuwa hujui nasasa nimekujuza
Ahahahahaha hiyo source unayoitumia umelishwa matango pori
 
Ukienda kwenye lugha ya Kiingereza inaeleza kwa uwazi zaidi:

54. And when he was come into his own Country,he taught them in their synagogue.....
55. Is not this the Carpenter's son?is not his mother called Mary?and his brethren James, and Josef, and Simon, and Judas?
56. And his sisters, are they not all with us?....

Walishangaa kwa sababu kwa macho ya kibinadamu hakukuwa na tofauti kati ya familia zao na familia ya Yusufu waliyemtambua kama ndiye Baba yake Yesu.

Kama walivyokuwa wao na watoto wengi wenye tabia tofauti ndivyo familia ya Yusufu ilivyokuwa.Ila walimshangaa mtoto Yesu kapata wapi ufahamu mkubwa hivyo?

Yohana 7:2-5 inatuambia pia juu ya kaka zake Yesu na inaenda mbali zaidi kwa kutuambia pia kuwa sio watu wa Galilaya peke yao bali ata kaka zake Yesu pia hawakumuamini Yesu kuwa ni Kristo.
Mathayo 1:25 inamalizia kwa kusema kuwa Yusufu alilala na Maria baada ya Yesu kuzaliwa.

upload_2017-1-2_14-47-39.png
 
Kwenye kitabu cha ufunuo unayajua yale makanisa saba? Kama Yesu alianzisha kanisa katoliki, Mbona kanisa katoliki halikutajwa kwenye yale makanisa saba? Jibu Hilo swali kwanza?
Wewe hayo makanisa saba umeshawahi kuyaona...??
 
Ahahahahaha hiyo source unayoitumia umelishwa matango pori
Source gani....?

Unachokataa nini hasa..??

Kuwa kitabu cha Mombolezo sio Maombolezo ya Yeremia...??

Soma theology angalau unaweza jibizana na mimi..
 
Yusufu hakufanya ngono na Maria hadi yesu alipozaliwa. baaday ya hapo wakafanya ngono na kuzaa hao ndugu wa yesu niliokutajia.
Jinga kabisa...??

Sasa fuatana na mimi
Maneno kaka na dada ktk utamaduni wa Wayahudi yalimaanisha ndugu yoyote wa karibu..(Rejea Mwa 13:8; 29:11-15), Mtu wa kabila moja (Hes 16:10) Hata Myahudi mwenzie (Kumb 15:12)

Hivyo Kaka na dada wa Yesu wanaotajwa ktk Injili ni wale ambao sisi tungewaita watoto wa Baba mdogo, mkubwa nk nk...

Na pia, kama Maria alikuwa na watoto wengine, kwanini Yesu hakumkabidhi Maria kwa hao na badala yake alimkabidhi kwa mwanafunzi wake(Yn 19:25-27)
 
Source gani....?

Unachokataa nini hasa..??

Kuwa kitabu cha Mombolezo sio Maombolezo ya Yeremia...??

Soma theology angalau unaweza jibizana na mimi..
siyo theology tu nimepiga na eschatology, kitu ambacho wewe ulivyo shallow katika theology ni ngumu sana wewe kuitolea maelezo,vinginevyo unabaki ktk mafundisho mepesimepesi tu
 
Chimbuko la imani ya Katoliki ni Petro, pale alipoambiwa juu ya mwamba huu nitalijenga kanisa, fuatilia. Kanisa katoliki lilianzishwa na Yesu
Nafikiri alitaka kumaanisha chimbuko la Dogma hiyo ya kupalizwa mbinguni
 
Huyu Bwana Degratius Nalimi Kisandu ni kichaa....certified lunatic...
 
siyo theology tu nimepiga na eschatology, kitu ambacho wewe ulivyo shallow katika theology ni ngumu sana wewe kuitolea maelezo,vinginevyo unabaki ktk mafundisho mepesimepesi tu
Sasa kweli wewe mbumbumbu wa kiwango cha mwisho...

Mtu aliyesoma Theology nikimwambia kitabu cha Maombolezo na Yeremia ni kitabu kimoja hawezi kukataa..

Ngoja nikuulize unazijua Apocripha books..?
 
Biblia inasema Bikra Maria ataitwa mbarikiwa, na dunia itamsifu kuwa yeye ni mbarikiwa. Bikra Maria kwa mujibu wa kumbukumbu za kanisha hakufa, alipaazwa. Ujui historia, huyu mama ni the special, hata waprotestant wakimtupa sisi Wakatoliki tutaendelea kutimiza unabii kwa kumuita mbarikiwa
Hakuna kitabu kwenye bibilia kimeandikwa maria alipaizwa.na mafundisho ya katoliki yanasema alikufa lakini mwili wake ulipotea kwabla ya maazishi.kwenyebibilia watu wawil tu ndio walio paizwa wakiwa hai ni enoko na eliya tu.
 
Kanisa Katoliki limekuwa likifundisha kwa miaka na miaka kwamba tunaweza kuwaomba watakatifu walioko mbinguni watuombee kwa Mungu. Je, jambo hili lina ukweli kibiblia? Je, hili ni fundisho la Mungu au ni la wanadamu? Je, mtu anayefanya hivyo anampendeza Mungu au anamuudhi?

Hakuna mahali popote katika Biblia ambapo tumeagizwa kuwaomba watakatifu ili watuombee kwa Mungu. Sasa haya mafundisho yanatoka wapi? Unawezaje kuwafundisha watu kitu kisicho kwenye Biblia halafu usiwe na hatia ya kuongeza au kupunguza ujumbe wa Mungu; maana Bwana anasema kuwa atakayeongeza au kupunguza katika neno lake ana hatia. (Ufunuo 22:19).

Iweje basi leo watu wengine wafundishe kuwa Maria mtakatifu mama wa Yesu anaweza kutuombea msamaha kwa mwanawe? Yesu ndiyempatanishi pekee kati yetu na Mungu. Unataka hadi mtu aseme nini ndipo ujue kuwa fundisho hili ni la uongo na hili ni la kweli?

Maandiko pia yanasema: ... basi kwa kadiri hii Yesu amekuwa mdhamini wa agano lililo bora zaidi. ... yeye, kwa kuwa anakaa milele, anao ukuhani wake usioondoka. Naye, kwa sababu hii, aweza kuwaokoa kabisa wao wamjiao Mungu kwa yeye; maana yu hai siku zote ili awaombee. (Ebr. 7:22-25).

Vipi sasa kuhusu watakatifu walio mbinguni?

Maandiko yanasema wazi: Asionekane kwako ... mtu awaombaye wafu. Kwa maana mtu atendaye hayo ni chukizo kwa BWANA. (Kumb. 18:10-12).

Je, wafu maana yake nini? Watakatifu walio mbinguni ni sehemu ya wafu au ni sehemu ya walio hai?

Labda utaniambia, “Ah, wafu maana yake ni watu wenye dhambi waliotengwa na Mungu.” Sikatai. Maana hiyo ni sawa. Ni mojawapo ya maana ya kuwa mfu. Lakini, Biblia inasema kuhusu maskini Lazaro: Ikawa yule maskini alikufa... (Lk 16:22).

Je, ‘alikufa’ maana yake si alikuwa mfu? Na tunafahamu kuwa Lazaro alienda mbinguni. Kwa hiyo, kwa sisi tulio duniani, Lazaro ni mfu aliye mbinguni. Ni vivyo hivyo kwa habari ya watakatifu wote ambao hawako duniani leo. Ni wafu! Je, haijaandikwa kwamba: Heri wafu wafao katika Bwana tangu sasa. (Ufu. 14:13). Je, ‘wafu wafao’ katika Bwana ni watakatifu au si watakatifu?

Biblia inasema: Watu wangu wanaangamizwa kwa kukosa maarifa. (Hosea 4:6). “Wanaangamizwa”, sio “wanaangamia!” Siku ya mwisho hutasema, “Bwana, mimi sikujua.” Ni kweli hukujua, lakini hicho hakitakuwa kigezo cha kusamehewa. Kujua ni sehemu ya wajibu wa kila anayetarajia wokovu wa Bwana. Ni jukumu lake kujua! Ukimtumainia mwanadamu badala ya Neno la Mungu uko kwenye hatari kubwa ya kupotea kutokana na kudanganywa!

Mungu tunayemwabudu anaona yote, anasikia yote, anajua yote, na yuko mahali pote kwa wakati uleule. Sasa, unaponiambia kwamba mtakatifu Petro au Yohana au Maria anaweza kusikia maombi ya watu milioni moja wanaoomba Tanzania; milioni moja Kenya, milioni tano Marekani, nk, na kuweza kuyafanyia kazi; una maana kuwa mtakatifu huyo ni lazima awe na tabia zote hizo hapo juu ambazo ni za Mungu Mwenyezi peke yake!! Je, hilo ni jambo linaloingia akilini?

Acha kudanganywa kwa mafundisho ya uongo! Acha kuangalia wanadamu usoni na kusema, “Huyu kwa elimu aliyo nayo hawezi kunidanganya.” Elimu na cheo si hoja ya msingi. Hoja ni kuwa je, anachosema kinatokana na Neno la Mungu?

Mwisho nakuomba utafakari maneno yafuatayo kutoka kwa Bwana:

Kwa kuwa liko tumaini kwa yule aliyeambatana na wote walio hai (maana ni afadhali mbwa aliye hai kuliko simba aliyekufa); kwa sababu walio hai wanajua ya kwamba watakufa; lakini wafu hawajui neno lolote, wala hawana ijara tena; maana kumbukumbu lao limesahauliwa. Mapenzi yao na machukio yao, na husuda yao, imepotea yote pamoja; wala hawana sehemu tena katika jambo lolote lililofanyika chini ya jua. (Mhubiri 9:4-6).

Kazi kwako! Usiuze haki ya mzaliwa wa kwanza kwa ujira wa kunde za mlo mmoja kama alivyofanya Esau!

Tumeitwa kupokea wokovu; si kushikilia dini. Okoka leo. Mkaribishe Yesu awe Bwana na Mwokozi wako. Yesu hakuleta dini bali alileta wokovu.

Biblia inasema: Ukimkiri Yesu kwa kinywa chako ya kuwa ni Bwana, na kuamini moyoni mwako ya kuwa Mungu alimfufua katika wafu, utaokoka. (Warumi 10:9).

Mafundisho mengine ya uongo ni ya watu kusema, “Hakuna kuokoka duniani.” Bwana Yesu alipoenda nyumbani kwa Zakayo, alitamka maneno haya: Leo wokovu umefika nyumbani humu, kwa sababu huyu naye ni mwana wa Ibrahimu. (Luka 19:9).

Maandiko pia yanasema: ... wakati uliokubalika nalikusikia, siku ya wokovu nalikusaidia; tazama, wakati uliokubalika ndio sasa; tazama,siku ya wokovu ndiyo sasa. (2 Wakorintho 6:2).

Sasa unaokokaje? Imeandikwa: Kwa maana, kwa moyo mtu huamini hata kupata haki, na kwa kinywa hukiri hata kupata wokovu. (Warumi 10:10).

Tafuta watu wanaokiri wokovu nao watakusaidia. Mungu akubariki na kukufungua macho ya rohoni ili uweze kufanya yale aliyoagiza Bwana wetu Yesu Kristo na si kutumainia maagizo ya wanadamu na wanadini. Ubarikiwe na Bwana.

COPY & PASTE
Source: Yesu Ni Njia: Je, Watakatifu Hutuombea Tulio Duniani?
 
Back
Top Bottom