MJADALA: Kwanini Padri Luther aliondoa baadhi ya vitabu kwenye Biblia, na kwanini alijiondoa kanisa Katoliki?

MJADALA: Kwanini Padri Luther aliondoa baadhi ya vitabu kwenye Biblia, na kwanini alijiondoa kanisa Katoliki?

Limesema Kanisa Katoliki na Ndo lenye mamlka hayo na Ndo maana Biblia Ilitoka Huko... Kwani Yesu aliagiza Mjenge Makanisa? Ni wapi pameandikwa Mjenge kanisa.. yeye si Alikuwa anaabudu Yerusalem
Ngoja nikuache maana umeamua kujitoa ufahamu
 
Unaongelea Biblia hii ambayo vitabu vyake vilikusanywa na kuchaguliwa na Kanisa Katoliki?.
Yaani Swala amfunishe samaki kuogelea?.Haya ni maajabu ya karne.
Hakuna Kanisa linalofuata Mafundisho ya Mungu yaliyoanishwa katika Biblia kama kanisa Katoliki Takatifu la Mitume.Hakuna.
Acha maneno lete maandiko
 
Embu niambie mstari ndani ya biblia ulioandikwa hivyo Hata meno katoliki tusiongeze neno wala kupunguza leta mstari.
Biblia Si kila Kitu Kwahy Si Biblia Pekee yenye Majibu... Mengine utayapata Kanisani na Ni kanisa Katoliki pekee nyie Wengine Hamna Hilo.. maana Roho Wenu ni Mfu.. Ameshaacha Kuwafunulia mmebakia na Biblia tu ,mambo mapya hamna.. mkaamua mkatoa na Vitabu vingine....

Fuata Historia ya Kanisa Lako halina Tofauti na Gwajima na Rwakatale yote yameanzishwa na Watu badala ya Kristo Mwenyewe..
 
Unajua maana ya neno Catholic?...
We unajua..?? Kwanini unahisi sijui....Haya ngoja nikuekeze
Catholic ni neno la Kigiriki (Katolikos)linalomaanisha -eny, -iliyo enea....Universal....Ukisoma Biblia ya kigiriki pale Yesu anawambia wafuasi wake enendeni ulimmwenguni "kote".... Hapo kwenye "Kote" utapata inaandikwa " Katolikos".... Na neno hilo ndio likatoolewa jina la Kanisa na kuanza kuitwa rasmi Catholic Church ......

Kama ulikua hujui
Aliyekuambia sijui ni nani...??

anglikana nao wanaitwa Anglican Catholic
Anglican hawaitwi Anglucan Catholic... Ila Watu hupenda kuwapachika au kujipachika Anglo-Catholic, na hii ni kutokana Liturujia ya Anglican haina tofauti na ya Catholic...mfanano huo ndio ukawafanya waanglikana wajione kama Wakatoliki....

, Orthodox Catholic
Hakuna kina kinaitwa Orthodox Catholic....
, na ndiyo maana hakuna dhehebu linaloitwa Catholic
Catholic siyo dhehebu ni Kanisa Kamili...
ila lipo Roman Catholic..
Hakuna kitu kinaitwa Roman Catholic ila kuna Catholic Church

nenda kasome maana ya Catholic
Nimeshakueleza hapo juu....

Nafikiri wewe ndio unapaswa kusoma...
 
Lakini Wa kristo ambao siyo wakatoliki kuna swala mnanitatiza sana ivi kwanini mnakua wazito kuutambua mchango Wa mama maria katika ukombozi Wa dunia hii, ivi unawezaje kuumwabudu mwana na ukaacha kumweshimu mama , kuusu mama maria nadhani niwakati Wa maadhehebu mengine ya kikristo kujitazama na kuumpa nafasi katika maisha yao, sikia nikwambie karne zilizo pita mwana mmke alidharauliwa sana na nadhani ndiyo sababu ya madhehebu mengi kutokumpa huyu mama nafasi katika makanisa yao
 
ichumu lya,
Wayahudi wa hawakivichukua kutokana na mapokeo yake yalikuwa kwa lugha ya Kigiriki...Wao walikuwa wanataka vitabu vilivyoandikwa kwa lugha ya kiebrania pekee...

Na hivi vitabu viliandika na Wayahudi walioishi Misri....

Pia hujatueleza ni kwanini Luther alipunguza vitabu vya Yakobo, Waebrania na Ufunuo wa Yohana ..
 
kumbe hata maana ya wa protestant hujui....

Hata Anglican nae ni m protestant halaf Biblia na idadi ya vitabu wanaliyo nayo wa anglikana na hiyo hiyo ya wa Pentecoste na Assembles
Kakudanganya nani.. ?? Anglican high Church/Episcopal Church hayanatofauti na Catholic Church hata mafundisho yao..Ndio maana sometimes huwa wanapenda jiita Anglo-catholic...Na biblia yao inavitabu 73/72
 
Ni kwl mkuu nina mjomba wangu ni padri nilienda kumtembelea pale ofcn kwao kurasini nkakuta friji yake imejaa mivinyo plus bia za kutosha akawa anapga bia kama kawaida kwhyo kwa mujibu wa biblia yao pombe kwao ni halali kbsa sikushangaa hata maparoko huwa wananyonya sana mivinyo

Sitakujibu hili, ili nisiharibu mada...
 
KWANINI PADRE Luther ALIFUKUZWA KANISA KATOLIKI? NA KWANINI ALIONDOA BAADHI YA VITABU KWENYE BIBLIA AGANO LA KALE?

Padre Luther alikuwa miongoni mwa Mapdre wenye karama nyingi ndani ya Kanisa katoliki wakati wake, Yeye alikuwa na Madai mengi sana juu ya mapungufu kwa kanisa. Hata hivyo madai yake mengi hayakuwa na msingi wowote.

Moja ya madai yake ilikuwa ni kuondoa kibali cha kwamba baada ya kuungama muumini asipewe stakabadhi ya kuonesha ameungama kwa kuwa kitubio ni siri ya MTU. Hili lilifanyiwa kazi. Mengine ikiwemo kurekebisha mfumo WA sala ya Kanuni ya Imani. Na mambo mengine mengi ambayo alipojibiwa, yeye hakuridhika pamoja na kueleweshwa vya kutosha. Alikuwa ni Great Thinker sana.


Mbaya zaidi alipokuja kusababisha mpaka akajitenga na kanisa ni kitendo cha kuondoa baadhi ya vitabu kwenye Biblia ikiwemo pia kupunguza baadhi ya mistari kwenye vitabu kama cha Esta na Cha Danieli.
Aliondoa vitabu vya Deutrokanoni na vingine baadhi na kuwa jumla ya vitabu 7 vilivyotolewa kwenye Biblia. Na kila kitabu alikuwa na sababu yake aliyoibainisha. Kimsingi alipata wafuasi wengi WA kumuunga mkono hoja yake hasa wale ambao walikuwa wanatafta njia ya kuchuma pesa kiulaini. Na hapo Biblia mpya ilianza yenye Vitabu pungufu.

Na ndio maana Leo watu hawaujui Ukristo vizuri na wanakinzana bila kujua historia ya kanisa. Watumishi wengi WA Mungu hasa HAWA WA kileo wasiojua historia vizuri wao kila kitu wanapinga. Sio kosa lao Bali ni kosa la kutokujua historia ya kanisa.
Matumizi ya Ubani yalipingwa sana, na hapa ilikuwa ni kuondoa idadi ya waelewa. Kutokana na watu wengi walikuwa wamegeuka kama waganga kila mapepo ya kiwakabili walitumia ubani kuyafukuza na yalikimbia, lakini watu walijisahau kusali na kuomba na hata kufika ibadani ikawa nadra maana wanajua kujiponya kuondokana na majini na wachawi. Hapa Padre Luther na wenzake wakapiga marufuku matumizi ya ubani na kuwa sihi wakazanie Neno zaidi.

Hapa walichotakiwa kufanya ni kuliishi Neno la Mungu na wakati WA ibada basi ubani uchomwe kama Mungu alivyo agiza.
Luther na wenzake lengo lao lilikuwa ni biashara hapo baadae na kimsingi mpango huo ulifanikiwa. Na ndio maana mpaka Leo watu wametawaliwa na mfumo WA majini katika maisha yao kwa kuwa wamefungwa akili ya kujitambua na wanaamini maneno ya mdomoni na sio Maandiko ya Biblia kama yanavyosema.
Nimengi ya kujifunza sana Leo hii lakini kwa Leo naishia hapa.

deogratius Nalimi Kisandu.
1. 1. 2017.
Dhambi inawatafuna,
 
Kwa kifupi Martin luther naweza kusema alikuwa ni Opportunistic...Alipata loop hole ya kuondoa vitabu vya Agano la kale, baada ya kurejea mitaguso ya Kanisa(hasa mtaguso wa trent) masahihisho yanahitajika hapa....


Wakati Kanisa Katoliki lina-compile Bible, Kuna vitabu 7 vya Agano la Kale ambavyo vilipokelewa kwa lugha ya Kigiriki...Hivyo Wayahudi(Waisrael) hawakuvitambua vitabu hivyo simply bze of language....Hivyo Luther akatumia mwanya huo kuviondoa....

Ila alishindwa kuondoa vya Agano jipya maana hivyo vilikuwa nje ya uwezo wake.....Ila ni bahati tuu, maana alisha viondoa vitabu 3... Calvin alimsihi sana kuvirudisha...

Kituko

Asante kaka, ntachangia na mimi nikikaa vizuri, lakini cha muhimu hapo ni kuwa wakati hilo la Martin Luther la kukengeuka na kuangaika na vitabu vya Biblia, kulikua hakuna Dini ya Bi Helen, wala hawa "wapakwa" mafuta, Biblia ilikuwa chini ya himaya ya Wakatoliki na walikuwa wanailinda, na hata Luther alipotoa vitabu alivyovitoa, Biblia halisi bado iko Mikononi mwa Wakatoliki
 
Any way acha nendelee ku stick kwenye swali langu la msingi,,,, katika biblia ni wapi tumeambiwa maombi yetu yapitie kwa Bikra Maria?
B/Maria ni Mtakatifu hivyo....
Sio Bikira Maria Pekee, Watakatifu wote jukumu lao ni kutuombea....Soma Ufunuo 5:8 uone Wazee 24 , wakizunguka kiti cha Mwana Kondo(Yesu) wanafanya nini..?

Ngoja nikuandikie
Ufunuo 5:8
Hata alipokitwa kile kitabu, hao wenye uhai 4 na wazee 24, walianguka mbele za mwana kondoo, kila mmoja na kinubi na vitasa vya dhabu vilivyojaa manukato, ambayo ni MAOMBI YA WATAKATIFU


Hivyo ni wazi, watakatifu kazi yao ni kutuombea...Sasa sijui utapingana na hapo pia...
 
Kakudanganya nani.. ?? Anglican high Church/Episcopal Church hayanatofauti na Catholic Church hata mafundisho yao..Ndio maana sometimes huwa wanapenda jiita Anglo-xatholic...Na biblia yao inavitabu 73/72
Acha uongo wew am Anglican na nimezaliwa na kubatizwa low church na sasa ninasali high church hiyo biblia unayoisema wew haipo
 
Mkuu kwa hili huna data.... Martine hakuwa Askofu, alikuwa Padre na miongoni mwa sababu zilizomuondoa kwenye kanisa Katoliki ni hili la Uaskofu, alipinga hairakia ya Kanisa na vyeo kama Uaskofu, Upapa na mengineyo. Sema tu mengi aliyoyapinga aliishia kuayatenda akiwa kwenye kanisa lake. Mengine ni suala la Useja, hakutaka kabisa kulisikia na alipoondoka aliondoka na Mtawa wa kike aliyeishia kuwa mkewe.

Mambo ni mengi sana na yanahitaji muda wa kutosha. Lakini niseme tu kwamba "siyo kila alilolipinga lilikuwa baya" mengine aliyapinga kihalali kabisa japo njia aliyoitumia haikuhalalisha kitendo chake!!!

Pili, Biblia za wapeotestanti na wapentekoste zina vitabu 66 wakati biblia ya Wakatoliki ina vitabu 72. Hili lilitokana na kuwa baadhi ya yaliyomo kwenye vitabu hivyo (deuterokanoni) vinapingana na mafundisho yao. Sababu nyingi ni za kibinadamu tu!!! Hili lilikuwa rahisi sana kwake kwani suala zima la "Utaifa" liliingizwq kwenye huu mchakato wa Luther kujiondoa kanisa, matokeo yake kwa vile alikuwa Mjerumani, dhehebu lake likawa "dini dora" ya Ujerumani, katika hali kama hii, ni rahisi kwa uwezo wa kifedha kuchapisha Biblia zenye vitabi 66 na kuviondoa vile vingine!!!!
kwa hiyo kumbe katoliki ni dini dola huko italia na spain pia anglikan ni dini dola kule uingereza
 
Acha uongo wew am Anglican na nimezaliwa na kubatizwa low church na sasa ninasali high church hiyo biblia unayoisema wew haipo
High Church ndugu halina tifauti na Catholic Church...Na Rozari kule tunasali vizuri....

Low Church walitaka kujifananisha na Lutherans hivyo waka-copy kila kitu kutoka Lutheran

Kama kweli wewe ni Anglican High Church nenda pale Cathedral ya St. Alban posta DSM, then angalia mandhari ya ndani ya Kanisa, kisha Nenda St. Joseph Cathedral posta ungalie uone kama utaona tofauti ....Hakuna tofauti
 
Yesu ni Mungu sawa na Baba na Roho Mtakatifu...Mungu anatuombeaje sasa....??

Kuwa makini, ndio maana Waislam wanawasumbua kuwa Yesu si Mungu....
Mtu hawez kwenda kwa baba ila kwa njia yangu.. Yesu anejiweka kuwa mtu wa kwanza kumuona kabla ya kufika kwa baba ni kama receptionist.. Sio koss kumuomba Mungu moja kwa moja,

habari za kumtaka mtu akuombee zilikua enzi hizo ambapo makuhani hiyo ndiyo ilikua kazi yao kwamba mtu wa kawaida alikua hana uwezo wa kupiga magoti na kumuomba Mungu isipokua alipaswa kupeleka sadaka yake kwa kuhani na mahitaji yake kuhani ndio anamuombea, lakiniujio wa Yesu ulivunja vifungo vyote na ndio maana anasema Ombeni nanyi mtapewa halaf anasema ni nani ambae anaweza kumpa nyoka mwanae amuombae samaki.

maana yake ni kuwa sisi ni watoto yeye ni baba haina haja ya kupita pita sijui kwa maria au kwa nani, pray direct yupo aliyepewa jukumu la kutusaidia kuomba ambae ni Roho mtakatifu huyu hutusaidia kuomba maana peke yetu hatuwez kuomba ipasavyo....
 
Back
Top Bottom