MJADALA: Kwanini Padri Luther aliondoa baadhi ya vitabu kwenye Biblia, na kwanini alijiondoa kanisa Katoliki?

Hongera unayejua.Na sanamu ya maria inachukua nafasi gani kwenye utatu wenu unaoujua?

Sanamu ya Maria inatuonyesha na kutukumbusha mama wa Mkombozi wetu

Kwenye utatu mtakatifu, Mama Maria ndio Binadamu pekee aliye ishi na kuenjoy utatu mtakatifu wa Mungu, 1: Mimba yake ilikuwa ni kwa uwezo wa Roho mtakatifu, na aliambiwa mimba itatungwa baada ya kumpokea roho mtakatifu, na pia yeye ndie Binadamu wa Kwanza kumpokea Bwana Yesu, so kwenye utatu Mama maria ni kiungo kikubwa kati Mungu na Mwanadamu.

Mama Maria ni Sanduku la Agano, Sanduku la Agano ndilo liliokuwa linakaa Sheria alizopewa Musa, Na Yesu ndio Baba wa hizo Sheria na ndio Sheria yenyewe na alikaa ndani ya Mama Maria Mkingiwa wa Dhambi ya Asili,
kwenye Sanduku la Agano kulikuwa na Sanamu za Malaika wawili (makerubi) waliokuwa wanaangaliana Nyuso zao, na Mbawa zao ziklikuwa zinagusana na kila sanduku lilipokuwa linapita watu walikuwa wanasujudu, Je walikuwa wanazisujudia hizo Sanamu za Makerubi?

Wakatoliki tunapoona Sanamu ya Bikira Maria , tunalikumbuka Sanduku la Agano lililokuwa na Bwana wa Sheria (Yesu)
Napenda kusemaga hivi
KWA WAKATOLIKI BIKIRA MARIA SIO MUNGU, HASAMEI DHAMBI ILA NI BINADAMU WAKIPEKEE KABISA

jiwe la majiwe , Otorong'ong'o , MTAZAMO ,
 

Jibu maswali hayo....Kwanini unachomekea mambo ya Maria..??
 
Nilishasema na narudia Yesu ni Mungu

Kama ulishasema...hii kauli ilikuwa ina maanisha nini..?
Yesu ni Mwana wa Mungu, ni Mungu Mwana katika Utatu Mtakatifu "Trinity"

Hapo kwenye rangi...
Mwana katika Utatu Mtakatifu ni kitu gani...? Kwamba Kuna Wana wengi ila Yesu ni mmoja wapo...?

Kwanini unajichanganya...?
 
Kama ulishasema...hii kauli ilikuwa ina maanisha nini..?


Hapo kwenye rangi...
Mwana katika Utatu Mtakatifu ni kitu gani...? Kwamba Kuna Wana wengi ila Yesu ni mmoja wapo...?

Kwanini unajichanganya...?
Huna hoja bora ukae kimya tu utaonekana una busara.
 
Huna hoja bora ukae kimya tu utaonekana una busara.
Hahahahahaha.....

Hujui maana ya Utatu Mtakatifu....Simpy Wasabato(SDA) hamjawai kuamini Utatu Mtakatifu, hamuamini Utatu Mtakatifu na kamwe hamtokaa kuamini Utatu Mtakatifu...

Period
 
Ningependa kujua umesoma vitabu gani na vingapi mpaka ukaja na the 'reasons' zilizomtoa Martin Luther of Germany kutoka ukatoliki...umegusa the subject kwa juu,umewaponda wakristo wengine kwamba hatuijui historia ya kanisa..(shaking my head) the days of Luther were the dark ages and ur short review has talked nothing about the courageous and remarkable man(God bless Him)..I quote you,eti 'hata hivyo madai yake mengi hayakuwa na msingi wowote'..says who? Says you!..well this is sadly hilarious.We unadhani mtu aliyesimama na kutoa madai ambayo yalitikisa kanisa katoliki siyo ya msingi?? Well,nadhani umekuja na hoja shallow Sana na pia the article is soo 'catholic biased'...please write another article about Luther at least watu watakuwa interested hata kukuchallenge.This is so cheap.
 
Well,nadhani umekuja na hoja shallow Sana na pia the article is soo 'catholic biased'...please write another article about Luther at least watu
Hebu wewe unayejua tuambie sababu ya Luther kupunguza vitabu 7 vya Biblia..

Tuambie sababu iliyompelekea kutaka kuondoa vitabu vya Ufunuo, Yakobo na Waebrania...

Tupe sababu...
 
Hebu wewe unayejua tuambie sababu ya Luther kupunguza vitabu 7 vya Biblia..

Tuambie sababu iliyompelekea kutaka kuondoa vitabu vya Ufunuo, Yakobo na Waebrania...

Tupe sababu...
Unahangaika sana ndugu.Hii nguvu unayotumia kufuatilia hadithi za kutunga, ungeitumia kujiuliza kwa nini mnaabudu sanamu wakati Mungu amekataza, hilo lingekuwa la manufaa kwako na wenzako
 

Martin alitaka kuoa, alitaka awe na watoto
 
Unahangaika sana ndugu.Hii nguvu unayotumia kufuatilia hadithi za kutunga,
Hadithi za kutunga kivipi...? Nani katunga..? Historia inatungwa...???

ungeitumia kujiuliza kwa nini mnaabudu sanamu wakati Mungu amekataza,
Nani anaabudu sanamu...? Unajua maana ya kuabudu...?
hilo lingekuwa la manufaa kwako na wenzako
Lingekuwa na manufaa kama umgejibu au kunipa ufafunuzi wa yale niliyokuuliza..

Umebaki unarukaruka kama kuku mwenye kideri...Utatu Mtakatifu hujanipa jibu, picha hujanipa jibu...
Nikikuuliza hiki unarukia hiki...hopeless
 

Well said[emoji122] , unapoandika article kama hiyo ya luther, we need Quotes with reference.
 
Sitatochoka kukupa Theology halisi iliyojikita katika Biblia Takatifu, sio ile uliyokaririshwa tangu utoto kutoka kanisa lilioasi. Umekuwa na uelewa finyu wa Waadvesntista wasabato, na umekaririshwa uongo mwingi kiasi cha kuamini propaganda kuwa wasabato hawaamini kuwa Yesu ni Mungu na pia umedai hawaamini kuwa Roho Mtakatifu ni Mungu.Hizo ni propaganda chafy dhidi ya kanisa la Mungu, jiepushe nazo hiyo ni kazi ya mwovu ibilisi kwani yeye ni muongo tangu mwanzo.
Baada ya utangulizi huo nakuletea baadhi ya misisngi ya waadventista wasabato ili kuthibityisha kuwa kanisa hili linaegemea mafundisho yake kwa muujibu wa Biblia wala sio nje ya Hapo.

1.Maandiliko Matakatifu
Maandiko Matakatifu, yaani Agano la kale na Jipya ndiyo Neno la Mungu lililoandikwa,
likatolewa kwa uvuvio wa Mungu, kupitia kwa watu watakatifu walionena na kuandika kama
walivyoagizwa na Roho Mtakatifu. Ndani ya neno hili, Mungu amemkabidhi mwanadamu
maarifa yaliyo lazima kwa ajili ya wokovu. Maandiko matakatifu ni ufunuo usioweza kukosa
wa mapenzi yake. Ndiyo upeo wa tabia, kipimo cha uzoefu, ufunuo thabiti wenye mamlaka
wa mafundisho ya imani, na kumbukumbu aminifu ya matendo ya Mungu katika historia.
(2Petro 1:20,21. 2Timotheo 3:16,17. Zaburi 119: 105. Mithal 30: 5,6. Isaya 8:20. Yoh
17:17. 1Wathe 2:13. Waeb4:12.)

2.Utatu Mtakatifu
Kuna Mungu mmoja: Baba, Mwana, na Roho Mtakatifu, umoja wa nafsi tatu za milele.
Mungu hapatikani na mauti, mwenye nguvu zote, ajuaye yote, zaidi ya yote, na aliyeko
daima. Yeye hana mwisho na ni zaidi ya ufahamu wa kibinadamu, hata hivyo anafahamika
kupitia kujifunua kwake binafsi. Milele zote yu astahili kuabudiwa, kusujudiwa, kutumikiwa
na viumbe vyote. (kumb 6:4. Mith 28:19. 2kor 13:14. Waef 4:4-6. 1Petr 1:2 1Tim 1:17
Ufunuo 14:7)

3.Baba
Mungu Baba wa milele ndiye muumbaji, Chimbuko, Mtengenezaji, na Mfalme wa viumbe
wote. Ni mwenye haki na Mtakatifu, Mwingi wa rehema,, mwenye fadhili, si mwepesi wa
hasira, na mwingi wa uthabiti wa upendo na uaminifu. Tabia na uwezo vilivyodhihirishwa
ndani ya Mwana na Roho Mtakatifu pia ni ufunuo wa Baba. (Mwanzo 1:1 Ufu 4:11.
1wakor 15:28. Yoh 3:16. 1Yoh 4:8. 1Tim 1:17. Kut 34:6,7. Yoh 14:9).

4.Mwana
Mungu Mwana wa milele alifanya mwili katika Yesu Kristo. Kupitia kwake vitu vyote
viliumbwa, tabia ya mungu imefunuliwa, wokovu wa wanadamu unakaribishwa na
ulimwengu unahukumiwa. Milele zote Mungu kweli, Alifanyika mwanadamu kweli, Yesu
aliye kristo. Alichukuliwa mimba kwa uwezo wa Roho Mtakatifu na kuzaliwa na bikira
Mariamu. Akaishi na kupitia uzoefu majaribu kama mwanadamu, lakini kwa ukamilifu
alioonyesha kwa mfano wa haki na upendo wa Mungu. Kwa miujiza yake alidhihirisha
uwezo wa Mungu na alithibitishwa kama Masihi aliyeahidiwa. Aliteseka na kufa kwa hiari
msalabani kwa ajili ya dhambi zetu, na kama mbadala wetu, Alifufuliwa kutoka kwa wafu,
na akapaa kuhudumu katika hekalu la mbinguni kwa niaba yetu. Atakuja tena katika
utukufukwa ajili ya ukombozi wa mwisho wa watu wake na urejeshwaji wa vitu vyote. (Yoh 1: 1-3,14. Wakol 1: 15-19,. Wafil 2:5-11. Yoh 10:30, 14:9 Warum 6:23. 2Wakor 5:17-19.
Yoh 5:22. 1Wakor 15:3,4. Luka 1:35. Yoh 14:1-3)

5.Roho Mtakatifu
Mungu Roho wa milele alikuwa mtendaji pamoja na Baba na Mwana katika uumbaji,
kufanyika mwili, na katika ukombozi. Aliwavuvia waandishi wa mabadiliko matakatifu.
Alijaza maisha ya kristo na uwezo. Huwavuta na kuwasadikisha wanadamu, na wale
wanaoitikia huwafanya upya na kuwabadilisha katika sura ya Mungu. Akipelekwa na Baba
na Mwana ili kuwa siku zote pamoja na watoto wake, hutoa karama za kiroho kwa kanisa,
huliwezesha kumshuhudia kristo, na kwa upatano wa maandiko huliongoza kwenye ukweli
wote. (Mwa 1,2. Luka 1:35, 4:18. Mdo 10:38. 2Petr 1:21. 2Wakor 3:18. Yoh 14:16-18,26,
15:26,27, 16:7-13)

Hii ni baadhi ya misingi mikuu ya imani ya Waadvenstista Wasabato, kama una swali zaidi kuhusu mismamo wa Waadvenstista Wasabato kuhusu Utatu Mtakatifu, niulize sitachoka kukuelimisha kwa kutumia Maadikiko Matakatifu "sola scriptura" wala sio hadithi za kutunga.
 
Mbona umeongea mambo ya kawaida Sana. Huo ni msingi wa ukristo Sio usabato. Kama huamini katika fumbo hilo huwezi kuwa mkristo
 
Mbona umeongea mambo ya kawaida Sana. Huo ni msingi wa ukristo Sio usabato. Kama huamini katika fumbo hilo huwezi kuwa mkristo
Kuna mtu anajiita Otorong'ong'o alikuwa anapotosha watu kuwa wasabato hawaamini Utatu Mtakatifu. hoja hii ni mahsusi kumpa ukweli ulivyo kuhusu wasabato.
 
Sitatochoka kukupa Theology halisi iliyojikita katika Biblia Takatifu, s
Unajua maana ya Theology...???

Aliyekuambia ulichokiandika ni theology ni nani..??

Hizo copy and paste baada ya kujichanganya ndo ukaenda kuzifukua wapi..??

Tangu lini Wasabato mkaamini Utatu Mtakatifu . ??
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…