MJADALA: Kwanini Padri Luther aliondoa baadhi ya vitabu kwenye Biblia, na kwanini alijiondoa kanisa Katoliki?

MJADALA: Kwanini Padri Luther aliondoa baadhi ya vitabu kwenye Biblia, na kwanini alijiondoa kanisa Katoliki?

Maria alipalizwa mbinguni pakikucha nitakuletea mstari labda ninukulu Ishara mkubwa ilionekana mbinguni Mwanamke aliyejipamba vzuri na taji la nyota kichwani mwake,ipo kkwenye Ufunuo asubuhi nitakupa vzuri zaidi
Mwanamke wa Ufunuo 12 ni Kanisa la Kristo,kitabu cha Ufunuo kinatumi lugha ya mfano. Mwanamke safi ni kanisa la Mungu linalotii amri zake, Kahab mkuu wa Ufunuo 17:5 ni kanisa lililoasi Amri za Mungu, ushahidi wa kibiblia unaonyesha kanisa hili ni Roman Catholic.Mnyama wa ufunuo 13 na 14 ni mamlaka ya kipapa.Utaona kuna mfanano mkubwa baina ya kahaba wa ufunuo 17 na mnyama w ufunuo 13 na 14.Hapa utaona kanisa la rumi likitumia nguvu za kisiasa kushinikiza ibada ya uongo."Wafalme wa nchi wamezini naye" . uzinzi hapa husimamia uasi wa Amri za Mungu. Kanisa la roma limeasi amri za Mungu na kuanzisha ibada iliyo kinyume na Mungu.Yaani wamebadili Sabato ya siku ya saba na kuifanya jumapili ambayo ni siku ya kwanza ya juma.wamebadili ubatizo kwa kunyunyiza maji badala ya kuzamishwa,Yesu hakunyunyiziwa maji alipokuwa mchanga bali alibatizwa akiwa mtu mzima ili nasi tufuate mfano wake. Kanisa la roma limeondoa amri ya pili inayokataza ibada ya sanamu na kanisa limejaa sanamu eti kwa majina ya watakatifu! Amri za Mungu katika kutoka 20 zimebadilishwa kama zinavyoonekana kwenye misale ya waumini.Wametimiza unabii wa Daniel 7:25." Naye ataazimu kubadili majira na sheria".
 
Mwanamke wa Ufunuo 12 ni Kanisa la Kristo,kitabu cha Ufunuo kinatumi lugha ya mfano. Mwanamke safi ni kanisa la Mungu linalotii amri zake
Toa ujinga wa kutuletea ngonjera za Ellen G White hapa.....Hivi unajua hata dhima ya Kitabu cha Apokalse ya Yohana...? Unajua kiliandikwa lini na kiliwahusu kina nani hasa...???

Tutolee ngonjera za makambi na lesson
 
Yaani wamebadili Sabato ya siku ya saba na kuifanya jumapili ambayo ni siku ya kwanza ya juma.
Hivi unaijua historia mpaka kufikia SDA kuanzs kutumia Jumamosi kama siku yao ya kukutana...??

Labda huwafahamu hawa watu....

Unahitaji kumjua vizuri William Miller, Joseph Bates, Hiram Edson na Ellen G White...

Ukiwajua vizuri hao wanaharakati na jinsi walivyofukuzwa kwenye makanisa yao ndio utajua kwanini huwa mnakutana kila Jumamosi...
 
Toa ujinga wa kutuletea ngonjera za Ellen G White hapa.....Hivi unajua hata dhima ya Kitabu cha Apokalse ya Yohana...? Unajua kiliandikwa lini na kiliwahusu kina nani hasa...???
Unaonyesha una juhudi sana lakini si katika kutafuta wokovu bali katika kutetea uovu wa kahaba mkuu, yaani kanisa lililoasi Amri za Mungu na kutunga ibada ya uongo.Eti kanisa lanafundisha mwanadamu aiyehai akamuombe mfu! Huo ndo unaitwa umizimu.
Tutolee nginjera za makambi na lesson
 
Toa ujinga wa kutuletea ngonjera za Ellen G White hapa.....Hivi unajua hata dhima ya Kitabu cha Apokalse ya Yohana...? Unajua kiliandikwa lini na kiliwahusu kina nani hasa...???

Tutolee ngonjera za makambi na lesson
Upuuzi mtupu ulioandika, ndio maana Martin Luther alianza kulipinga kanisa la roma baada ya kuona limeacha kufuata Biblia na kujitangia misale, ndicho ufanyacho eti tusiifuate Biblia ila tuamini hadithi za kutunga za kwenye misale.badilikeni, Yesu anakuja.
 
Upuuzi mtupu ulioandika, ndio maana Martin Luther alianza kulipinga kanisa la roma baada ya kuona limeacha kufuata Biblia na kujitangia misale, ndicho ufanyacho eti tusiifuate Biblia ila tuamini hadithi za kutunga za kwenye misale.badilikeni, Yesu anakuja.
Hiyo ndio sababu iliyomfanya aondoe vitabu 7 vya Agano la Kale....

Hiyo ndio sababu iliyomfanya atake kuondoa vitabu vya Ufunuo, Yakobo na Waebrania..

Hebu nipe sababu kama unaijua, uniambia aliviondoa kwa mamlaka ya nani...??
 
Wewe ulietoa somo la ufunuo nimefulahiya sana kuusu hili somo labda nikulekebishe kidogo bibilia inasema mara tu alipokwisha kutwaa hicho kitabu. Wale viumbe hai wanne pamoja na wale wazee irini na wanne walianguka kifudifudi mbele mbele ya mwanakondoo. Kila mmoja alikuwa na kinubi na bakuli na bakuli za dhahabu zilizojaa ubani. Ambao nimaombi ya watakatifu.. Nisawa kweli yalikuwa nimaombi yawatakatifu.. lakini. Bibilia haisemi kama yalikuwa ni maombi ya watakatifu waliokufa hapana..ila bibilia inatambua watakatifu walioko duniani inaamana walioko hai si wafu..



ZABURI 16:3, “Watakatifu waliopo duniani ndio walio bora, hao ndio ninaopendezwa nao ”

1Petro1: 15 - 17
bali kama yeye aliyewaita alivyo mtakatifu, ninyi nanyi iweni watakatifu katika mwenendo wenu wote;
16 kwa maana imeandikwa, Mtakuwa watakatifu kwa kuwa mimi ni mtakatifu.

17 Na ikiwa mnamwita Baba, yeye ahukumuye kila mtu pasipo upendeleo, kwa kadiri ya kazi yake, enendeni kwa hofu katika wakati wenu wa kukaa hapa kama wageni.
 
Evidence plz ebu tuaminishe kwamba RC wametumia kitabu cha Ufunuo kinatumika hvyo unavyosema.

ZABURI 16:3, “Watakatifu waliopo duniani ndio walio bora, hao ndio ninaopendezwa nao ”

1Petro1: 15 - 17
bali kama yeye aliyewaita alivyo mtakatifu, ninyi nanyi iweni watakatifu katika mwenendo wenu wote;
16 kwa maana imeandikwa, Mtakuwa watakatifu kwa kuwa mimi ni mtakatifu.

17 Na ikiwa mnamwita Baba, yeye ahukumuye kila mtu pasipo upendeleo, kwa kadiri ya kazi yake, enendeni kwa hofu katika wakati wenu wa kukaa hapa kama wageni.
 
ZABURI 16:3, “Watakatifu waliopo duniani ndio walio bora, hao ndio ninaopendezwa nao ”
Haya jikite kwenya mada..

Tupe sababu za Martin Luther kupunguza vitabu 7 vya Agano la kale...

Pia tupe sababu zilizompelekea kutaka kuondoa vitabu vya Ufunuo, Yakobo na Waebrania...
 
Na unaposema "kipaumbele" unataka kumaanisha kitu gani hasa...? Kipaumbele ni nini..?

Kwamba kaburi lipo ila halijapewa kipaumbele cha kuandikwa kwenye biblia...??? Ni kipaumbele gani unataka kuzungumzia hapa..?
Sakata lote la Yesu Wayahudi hawalitambui sembuse Maria? enzi hizo hakukuwa na mwanamke aliyepewa hadhi kwenye jamii, kwenye dini wala kwenye bibilia zsidi ya kuwataja tu walichofanya kuwatendea wanaume maarufu kama vile kueazaa, kuwapa chakula na kuwaimbia au kiwatukuza wanaume hao
 
Mamlaka haya aliyapata kutoka kwa nani angali Biblia ilikuwa imeshakamilika...
biblia hasa agano la kale tumeitoa kwa wayahudi. sasa wayahudi hawakuwa na hivyo vitabu saba vya kina Judith na Tobith. wakatoliki waliviongeza ndiyo sababu Luther aliviondoa.
 
Luka anasema:

BIBLIA TAFSIRI YA ULIMWENGU MPYA
Luka 1:
1 Kwa kuwa wengi wamechukua daraka la kukusanya habari za mambo ya hakika+tunayosadiki kikamili kati yetu,2 sawa na vile wale ambao tangu mwanzo+walikuwa mashahidi wa kujionea+ na watumishi wa ujumbe+walivyotuletea haya,3 mimi pia niliazimia, kwa sababu nimefuata kwa uangalifu mambo yote tangu mwanzo kwa usahihi, kukuandikia hayo kwa utaratibu wenye kufuatana,+mtukufu+Theofilo

Ukisoma hayo tu, utaelewa kuwa hapo hakuna kitabu cha Mungu. Labda uwe punguani.

Maana Luka hapo anakiri ameandika ili amfurahishe kiongozi "Theofilo" tu.
 
Kila andiko kwenye Biblia ni neno la Mungu yaani ni Mungu mwenyewe ....angalia unapofikiri unapinga Ukatoliki kumbe unampinga Mungu ....tukianza kuchagua andiko hili ni muono wa kibinadamu na hili ni Mungu tunaenda kubaya sana.....Yesu ni Mungu hivyo hatuombei bali yeye ndio mpaji ...ila Mapadre, wachungaji, watakatifu n.k wanaweza kutuombea kwa Mungu ....kama wewe ni Mkristo na huamini kuna maisha baada ya kifo basi ule ufufuko wa Yesu ulikuwa kazi bure ......kama Yesu alitokewa na Musa, Eliya kumtia moyo ....enzi zenu si mngesema ni wafu/ mizimu ile?
Mungu hajaandika kitu tafadhali wacha hadithi, ya mungu ni mengi sana hayaandikiki na hakuna anayeweza kuyaandika maana hayajui. Vitab hivi viliandikwa na watu wema wenye nia njema na wenye maono waliotaka kutatua tatizo la kijamii la wanajamii hisika/maalum
 
biblia hasa agano la kale tumeitoa kwa wayahudi. sasa wayahudi hawakuwa na hivyo vitabu saba vya kina Judith na Tobith. wakatoliki waliviongeza ndiyo sababu Luther aliviondoa.
Unajua biblia imekaa ikiwa complete tena yenye pumzi ya Mungu kwa Miaka zaidi ya 1500... Sasa ni mamlaka gani huyo Luther na aliyapata wapi kupunguza vitabu vya Agano la Kale...?

Miaka yote hiyo biblia imtunzwa aje mtu mmoja kwa siku moja kuondoa vitabu 7..

Hiv hujui kama siyo Calvin leo ungashupaza shingo yako ukitetea uharamia ambao Martin Luther aliotaka kuufanya kwenye vitabu vya Agano jipya....? Hivi hujui kama siyo Calvin leo Waprotestant mngekuwa na vitabu 24 vya Agano jipya. ? Hivi ungekuja kufanya utetezi gani hapa...?
 
Mungu hajaandika kitu tafadhali wacha hadithi, ya mungu ni mengi sana hayaandikiki na hakuna anayeweza kuyaandika maana hayajui. Vitab hivi viliandikwa na watu wema wenye nia njema na wenye maono waliotaka kutatua tatizo la kijamii la wanajamii hisika/maalum
Wewe hebu jiondoe hapa maana huna unachojua..
 
Ka
Wewe hebu jiondoe hapa maana huna unachojua..
kama ndo hivyo hata komputers, simu na ndege zimetengenezwa na Mungu. Maana watu waliondika bibilia na quran wanasema "wenyewe" wametumwa na Mungu hivyo ni Mungu kaandika, kwanini watu waliobuni hii JF nao wasiwe wametumwa na mungu hivyo iwe ni Mungu aliyeibuni jf?
 
Back
Top Bottom