Mjadala: Ni ipi dawa ya kutibu maumivu ya jino bila kung'oa?

Sasa nasukutua kwa mda gani. Na pia nikimalizd kusukutua je, naacha ivyoivyo mdomo au naweza piga mswaki?
 
Sasa nasukutua kwa mda gani. Na pia nikimalizd kusukutua je, naacha ivyoivyo mdomo au naweza piga mswaki?

sukutua mara mbili au tatu kisha tema kaa kama dakika 30 piga mswaki endelea na ratiba zako na hakikisha unafanya hivyo mara tatu au tano utarudi humu JF kunishukuru mkuu.
 
Na mkojo unang'arisha pia? Ila dogo uwe makini usimeze ikawa "urine cycle"
 
nina allergy na matabularaza samahani sana.
Kama unajua unang'arisha c unatujuza tu au hadi tukulazimishe? Hujui watu wana meno ya njano? Kuna umuhimu wa kuanzisha thread mpya ndo unielekeze? Af haiitwi tabularaza utatia aibu...
 
Nashukuru mkuu, nikifanikiwa nitakufahamisha
 
Nenda hispital utapata ushauri murua kabisa. Na watajua ni njia gan ya kukusaidia. Kama meno yame oza kabisa wata ng'oa ila kama yameathirika kidogo. Watakusafisha na kuziba yaliyo toboka. Pesa yako tu
Brother, hujawahi kwenda hospitali kwa tiba ya meno ukayaona yale mapatasi ya kungolea? au unaongea tuu kiurahisi kama ule usemi " uwe unapenda kwenda kucheki afya yako hospitalini hata kama huumwi , ukifika kule unakuta wagojwa wamejaaa, sasa docta atakuhudumia wewe mzima au wale wagojwa ambao hawajapata hata nafasi kwa wingi wao?''

Madaktari wa meno wanasoma muda mwingi tena nasikia wakishamaliza kozi ya udactari wa kawaida wanaoneza miaka mingine ya kulisomea jino, sasa inakuwaje hawajapata suluisho la kudumu?mbona ni kungoa tuu, na madaktari wa macho, pua, wangekuwa hivyo tungekuwaje? kama ni kungoa tuu kwa nini kozi isitolewe tuu VETA?

Uzibaji wa meno, uwe wanaoita wa muda au wa kudumu bado haujaleta suluhu.

Meno ya badia baada ya kungoa meno bado hakuna yaliyopatikana kumsaidia huyu kibohgoyo, haya ya kuweka na kutoa kula huwezi, kuongea ni kuchezesha ulimi tuu.

Haya wanayosema wanayagandisha kwenye fizi ni hatari tupu, ukiyatafunia yanaenda kukgusa mishipa ya fahamu....maumivu utakayoyapata.......omera utatamani uyapige ngumi yasambaratike.

Nashauri, madactari wa sekta hii waongeze juhudi kufanya utafiti kuliondoa hili tataizo sugu ambalo linaweza kushababisha idadi ya vibogoyo kuongezeka kwa kasi.
 
Habarini wana jamvi,

Kama kichwa kinavoeleza ni kwamba niling'oa jino siku ya Ijumaa lakini napata maumivu makali sana. Japokuwa kuna dawa ya kukausha na kusafishia mdomo nilipewa lakini haitulizi maumivu.

Naomba wataalam wanisaidie dawa bora ya kusaidia kutuliza maumivu.
 
Rudi kwa dentist au muone daktari, kama tangu Ijumaa inflammation haijakwisha inaelekea kuna infection.
 
Habari Jf,

kuna hii dawa ya mti shamba kama sijakosea mti wake unaitwa Mlele/msele.
Jinsi ya kuianda.

Toa magome ya mti huo ya chemshe kwa maji safi kisha tumia maji hayo kusukutua mdomoni kwa dakika chache.



 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…