Mjadala: Tanzania mabosi wengi ni mabosi-suti, uwezo hakuna

Mjadala: Tanzania mabosi wengi ni mabosi-suti, uwezo hakuna

OKW BOBAN SUNZU

Platinum Member
Joined
Aug 24, 2011
Posts
53,868
Reaction score
121,001
Kumekucha!

Lengo la mjadala huu ni kuwafahamisha wanajamii kuwa wakati mwingine wasiwe na mategemeo makubwa saana juu ya utendaji wa viongozi wao. Wachukulie kawaida tu kwamba tunaenda kimungu-mungu. Lakini wajue moja ya sababu zinazotufanya tukwame kwa miaka mingi ni kuwa na watu wa namna hii.

Wakati nikiwa mdogo niliamini kuwa boss au kiongozi mkubwa kama Mbunge, Waziri, Mkurugenzi nk unakuwa dude lenye akili kubwa sana. Somi moja matata lenye uwezo wa kufikiria mambo kwa kasi ya kompyuta. Aisee kumbe nilikuwa najidanganya sana. Hali ni tofauti kabisa.

Fikra hizi wengi wetu bado wanazo sana, wana imani kubwa sana na mabosi na viongozi wao. Lakini ukweli ni huo mabosi wengi wana vyeo vyeti, wamevaa masuti mazuri, gari nzuri lakini ni weupe katika kiwango cha juu sana. Yaaani hamna kitu-ni mradi tu.

Prof. Assad aliwahi kusema hili akashtumiwa sana. Lakini alisema anachokijua.

Achana na siasa halafu fikiria jinsi kina Halima Mdee walivyobakia kuwa wabunge. Au fikiria jinsi Dkt. Gwajima alivyoanza kuzungumzia mkono wa baunsa wakati anajibu hoja za Askofu kuhusu Corona. Au fikiria DED wa Gairo anatuhumiwa kuiba mabati ya Halmashauri. Unaweza kufikiria pia wabunge walivyoweza kupitisha tozo za miamala ya simu bila kujua kiwango, halafu wanataka tena wapelekewe wajadili upya huku wakilipwa posho. Hawa ni watu takribani 300.

Sitaki kuingiza siasa lakini nakupa mifano hai uelewe kwamba bosi wa kitanzania ukimtoa suti anabaki mtupu.

Tanatokaje hapo, hata mimi sijui kwa sababu idadi yao ni kubwa sana.
 
Umesema sahihi kabisa. Embu angalia JPM, majaliwa piko, job yustino, lusinde, nk nikituko
 
Tanzania mnaangalia sana vyeti na ufaulu. Hakuna uhusiano kati ya vyeti ama ufaulu na ufanyaji kazi ama ubunifu kazini.

Angalia serikalini, watu wana vyeti mbwa haruki ila utendaji kazi wao ni sifuri.

Utashangaa serikalini hata mtu kupandishwa cheo kigezo kikubwa ni elimu ama vyeti na sio uchapa kazi, mfumo wa hovyo kabisa.

Ndio maana wafanyakazi wa serikalini wanapigana kuu chini kupata vyeti, sio kusoma na kuelewa bali kupata vyeti.

Siku tukiachana na huu mfumo wa vyeti tutafika mbali.
 
Ulichosema ni sahihi kabisa maana taasisi au jumuiya yeyote ikiwemo nchi haiwezi kuendelea kupita uwezo wa kufikiri wa viongozi wake.

Takwimu zinaonesha mpaka miaka ya mwishoni mwa 70 Tanzania ilikua na GDP kubwa kuliko nchi zote za ukanda wa Africa mashariki kwa kuwa tulikua na kiongozi mwenye maono na akili kubwa. Nisingependa kuchambua viongozi waliofuatia lakini nyakati tulizopo sasa ni hatari zaidi maana tumepata kiongozi mbumbumbu kuliko wote.

Hali hiyo imesababishwa na mengi lakini kubwa ni kukosa elimu maarifa lakini pia ni hulka ya kutokuzingatia weledi kuanzia ngazi ya familia hivyo kuwa na aina ya watu wasiotambua lengo la kuumbwa na kuzoea hali mbaya na dhalili ya umaskini
 
Asante sana kwa bandiko hili murua, mjadala wa hoja hii unapaswa uwe mpana na wa kitaifa kwani hali ni mbaya sana kwa watendaji wetu. Shida ni kwamba wahusika hawatambui na wala hawana habari kwamba kuna tatizo kwao, wao wanaona kila kitu kiko sawa.

Nimewahi kufanya kazi kwenye taasisi moja ya kigeni, inayotoa ajira nyingi kwa Watanzania na raia wengi wa kigeni, ilikuwa ni aibu kubwa pale watanzania wanapoitwa kwa ajili ya usaili, wanakuja na vyeti vingi vya kuvutia, lakini wanapopata kazi ni aibu kubwa, kwani mara nyingi uwezo wao haukuwa ukilingana na vyeti walivyoonesha, na kila uchunguzi ulipofanyika vyeti vyao havikuwa halisi bali vilikuwa vya kughishi. Wengine walikuwa watu wenye hadhi lakini utendaji na utu wao ni sifure.

Mungu tusaidie maana tuna safari kubwa huko tuendako.
 
Kumekucha!

Lengo la mjadala huu ni kuwafahamisha wanajamii kuwa wakati mwingine wasiwe na mategemeo makubwa saana juu ya utendaji wa viongozi wao. Wachukulie kawaida tu kwamba tunaenda kimungu-mungu. Lakini wajue moja ya sababu zinazotufanya tukwame kwa miaka mingi ni kuwa na watu wa namna hii.

Wakati nikiwa mdogo niliamini kuwa boss au kiongozi mkubwa kama Mbunge, Waziri, Mkurugenzi nk unakuwa dude lenye akili kubwa sana. Somi moja matata lenye uwezo wa kufikiria mambo kwa kasi ya kompyuta. Aisee kumbe nilikuwa najidanganya sana. Hali ni tofauti kabisa.

Fikra hizi wengi wetu bado wanazo sana, wana imani kubwa sana na mabosi na viongozi wao. Lakini ukweli ni huo mabosi wengi wana vyeo vyeti, wamevaa masuti mazuri, gari nzuri lakini ni weupe katika kiwango cha juu sana. Yaaani hamna kitu-ni mradi tu.

Prof. Assad aliwahi kusema hili akashtumiwa sana. Lakini alisema anachokijua.

Achana na siasa halafu fikiria jinsi kina Halima Mdee walivyobakia kuwa wabunge. Au fikiria jinsi Dkt. Gwajima alivyoanza kuzungumzia mkono wa baunsa wakati anajibu hoja za Askofu kuhusu Corona. Au fikiria DED wa Gairo anatuhumiwa kuiba mabati ya Halmashauri. Unaweza kufikiria pia wabunge walivyoweza kupitisha tozo za miamala ya simu bila kujua kiwango, halafu wanataka tena wapelekewe wajadili upya huku wakilipwa posho. Hawa ni watu takribani 300.

Sitaki kuingiza siasa lakini nakupa mifano hai uelewe kwamba bosi wa kitanzania ukimtoa suti anabaki mtupu.

Tanatokaje hapo, hata mimi sijui kwa sababu idadi yao ni kubwa sana.
Umemsahau pia wavaa magauni kama mama yetu
 
Tanzania mnaangalia sana vyeti na ufaulu. Hakuna uhusiano kati ya vyeti ama ufaulu na ufanyaji kazi ama ubunifu kazini.

Angalia serikalini, watu wana vyeti mbwa haruki ila utendaji kazi wao ni sifuri.

Utashangaa serikalini hata mtu kupandishwa cheo kigezo kikubwa ni elimu ama vyeti na sio uchapa kazi, mfumo wa hovyo kabisa.

Ndio maana wafanyakazi wa serikalini wanapigana kuu chini kupata vyeti, sio kusoma na kuelewa bali kupata vyeti.

Siku tukiachana na huu mfumo wa vyeti tutafika mbali.
Nadhani hata vyeti vingetolewa visiwepo kabisa Mana hakuna uhusiano wowote.
Mtu awe anasomea kitu basi akienda anapewa anajifanya hakuna haha ya cheti.

Yaaani tusome kupata maarifa naa sio vyeti
 
Wenye uwezo(akili) wanakuwa wapi mpaka wanatawaliwa(kuongozwa) na wasio na uwezo? Labda 'We are reflection of our leaders!
Nakumbuka kuanzia Ngazi ya Shule huwa wanaopata Uongozi ni wale wanaojua kujipendekeza Kwa Walimu na kuwapelekea Umbeya Umbeya..

Serikalini likewise, ukiwa mzuri Wa majungu, fitna na kujipendekeza Kwa mabosi unapewa Privilege zaidi kuliko wale wasio na shobo, hii huenda mpaka Ngazi za Ubunge, Uwaziri na hatimaye Ngazi za juu kabisa.

Kwa mfano, Nape Nnauye alifukuzwa uwaziri pale alipotaka kuvalia njuga suala la Makonda kuvamia Clouds, Ndugulile baada ya kupingana na Mkuu wake kuhusu njia tunazotumia dhidi ya Corona.

View attachment 1907502View attachment 1907504
 
Wenye uwezo(akili) wanakuwa wapi mpaka wanatawaliwa(kuongozwa) na wasio na uwezo? Labda 'We are reflection of our leaders!
Umesema ukweli mkuu, sisi ndio tumewachagua tena kwa kura za mafuriko na wengine tukaamua kuwasaidia kuiba kura
 
Kuna msemo unasema "Wenye nguvu hawana uwezo; Wenye uwezo hawana nguvu".
Tafsiri yangu:
Wenye akili hawana mamlaka; Wenye mamlaka hawana akili.
 
Kumekucha!

Lengo la mjadala huu ni kuwafahamisha wanajamii kuwa wakati mwingine wasiwe na mategemeo makubwa saana juu ya utendaji wa viongozi wao. Wachukulie kawaida tu kwamba tunaenda kimungu-mungu. Lakini wajue moja ya sababu zinazotufanya tukwame kwa miaka mingi ni kuwa na watu wa namna hii.

Wakati nikiwa mdogo niliamini kuwa boss au kiongozi mkubwa kama Mbunge, Waziri, Mkurugenzi nk unakuwa dude lenye akili kubwa sana. Somi moja matata lenye uwezo wa kufikiria mambo kwa kasi ya kompyuta. Aisee kumbe nilikuwa najidanganya sana. Hali ni tofauti kabisa.

Fikra hizi wengi wetu bado wanazo sana, wana imani kubwa sana na mabosi na viongozi wao. Lakini ukweli ni huo mabosi wengi wana vyeo vyeti, wamevaa masuti mazuri, gari nzuri lakini ni weupe katika kiwango cha juu sana. Yaaani hamna kitu-ni mradi tu.

Prof. Assad aliwahi kusema hili akashtumiwa sana. Lakini alisema anachokijua.

Achana na siasa halafu fikiria jinsi kina Halima Mdee walivyobakia kuwa wabunge. Au fikiria jinsi Dkt. Gwajima alivyoanza kuzungumzia mkono wa baunsa wakati anajibu hoja za Askofu kuhusu Corona. Au fikiria DED wa Gairo anatuhumiwa kuiba mabati ya Halmashauri. Unaweza kufikiria pia wabunge walivyoweza kupitisha tozo za miamala ya simu bila kujua kiwango, halafu wanataka tena wapelekewe wajadili upya huku wakilipwa posho. Hawa ni watu takribani 300.

Sitaki kuingiza siasa lakini nakupa mifano hai uelewe kwamba bosi wa kitanzania ukimtoa suti anabaki mtupu.

Tanatokaje hapo, hata mimi sijui kwa sababu idadi yao ni kubwa sana.
Umesema vema sana.
 
Nakumbuka kuanzia Ngazi ya Shule huwa wanaopata Uongozi ni wale wanaojua kujipendekeza Kwa Walimu na kuwapelekea Umbeya Umbeya..

Serikalini likewise, ukiwa mzuri Wa majungu, fitna na kujipendekeza Kwa mabosi unapewa Privilege zaidi kuliko wale wasio na shobo, hii huenda mpaka Ngazi za Ubunge, Uwaziri na hatimaye Ngazi za juu kabisa.

Kwa mfano, Nape Nnauye alifukuzwa uwaziri pale alipotaka kuvalia njuga suala la Makonda kuvamia Clouds, Ndugulile baada ya kupingana na Mkuu wake kuhusu njia tunazotumia dhidi ya Corona.

View attachment 1907502View attachment 1907504
Huko shuleni kwenu, shuleni kwetu wenye akili ndio tulikuwa viongozi. Kuanzia class monitor hadi head girl wote vichwa
 
Back
Top Bottom