Mjane wa Augustino Mrema ajumuishwa kwenye mirathi

Mjane wa Augustino Mrema ajumuishwa kwenye mirathi

Mama yao si ndio kafariki, halafu sasa waende kwa mume na watoto halali wa marehemu mama yao kudai mali, mali ambazo mume halali kachuma kwa msaada wa mke wake na watoto wake. hiyo inakaaje kaaje. Ukizingatia baba yao ambae ndiye mchepuko tu kwa marehemu mama yao nae ndio anasubiri wapewe mgao ili achukue mali ambazo hajachuma kupitia watoto wake haramu?

Sheria inaruhusu hilo, sheria hiyo ilitungwa na wendawazimu au watu wenye akili timamu?
Yaani hawa watoto wa nje wa kujulikana wakati wa mirathi tu jamani.Kuna maswali hapa,hayana majibu.
 
Yaani watoto wa nje ya ndoa? Huyu jaji kachanganyikiwa.
Tanzania wanapata tu fresh kwa conditions hizi👇
1.kama uliwataja kweny urithi wao kama wanao.

2.Kama wanajulikana na ndugu na watu wako wa karibu kama wanao ,hapa pia uliwatambulisha kwa sababu wazee wengi suala la kuandika urithi ni mtihani wanaona kama kujiombea kifo.

Kuna watoto wa nje ila wanatambulika na ndugu na halina shaka kama ni wanao..
 
Kimsingi hakustahili kupata mgao wa mali kwani hizo mali alizikuta na hakushiriki kuzipata wakati mume wake anazipata yeye hakuwa mke wa mrema. Ila tafsiri ya mahakama imeamua apate. Kama kupata angepata sehemu ndogo sana kutokana na muda mfupi alioishi kwenye ndoa hiyo. Kwa wanandugu inauma sana mtu kupewa urithi wa mali wakati amedumu muda mfupi na hakuna mali iliyopatikana akiwa kwenye ndoa hiyo
Huo muda mfupi ndiyo alikuwa anamsafisha akijinyea, wakati watoto wake wa kuwazaa wanakula bata na kumyanyapaa. Anastahili kwa kweli
 
Sheria inasemaje kwenye hilo mkuu? Wa nje ya ndoa huwa hawastahili kwani?

Unawezakuta watoto wa ndani ya ndoa wameona wawape ndugu zao japo kidogo maana maisha haya kila kitu tutakufa tutakiacha
umeongea pwent kubwa sana mkubwa. watoto wa nje wananyanyasika sana na kutengwa wakati hawana hatia. na huu upuuzi upo kwenye jamii karibu zote hapa kwetu. ni ufala sana. big up sana mkuu.
 
Huo muda mfupi ndiyo alikuwa anamsafisha akijinyea, wakati watoto wake wa kuwazaa wanakula bata na kumyanyapaa. Anastahili kwa kweli
kwani alizidiwa sana kiasi cha kushindwa kwenda msalani peke yake mpaka asaidiwe kama mtoto mchanga, ile pisi kali aliyoia ni ya kumfuta akijinyea? Zile pesa za alizopata wakati anatongozwa aolewe zilimtosha
 
Goodlove ana miaka 18, mzee alimzaa akiwa na miaka 60? Usijekuta mamake ana miaka 28
 
kwani alizidiwa sana kiasi cha kushindwa kwenda msalani peke yake mpaka asaidiwe kama mtoto mchanga, ile pisi kali aliyoia ni ya kumfuta akijinyea? Zile pesa za alizopata wakati anatongozwa aolewe zilimtosha
Nenda kamuambie Jaji wa Rufaa hayo maneno, sisi tumefunga mjadala Temeke
 
Kimsingi hakustahili kupata mgao wa mali kwani hizo mali alizikuta na hakushiriki kuzipata wakati mume wake anazipata yeye hakuwa mke wa mrema. Ila tafsiri ya mahakama imeamua apate. Kama kupata angepata sehemu ndogo sana kutokana na muda mfupi alioishi kwenye ndoa hiyo. Kwa wanandugu inauma sana mtu kupewa urithi wa mali wakati amedumu muda mfupi na hakuna mali iliyopatikana akiwa kwenye ndoa hiyo
Sasa nyie ndugu muumie kwani huyo ndugu yenu mlimsaidia kutafuta nae?

Mtu akishakuwa mke halali basi ana uhalali na zile mali ingawa inaweza ikawa isiwe kwa kiasi chote lkn anapata kidogo.

Kama mumewe hakumbagua kwanini ndugu wambague?

Mahakama hapo ipo sahihi, watoto wote pamoja na wa nje, na mke wa marehemu hizo ndo mali zao. Na si baba wadogo au wakubwa.
 
Back
Top Bottom