Mjane wa Mrema atoswa, familia yapinga wosia uliachwa na Mrema. Mjane apokonywa nyumba ya Salasala

Huyo Mwanamke Mjane ameonewa, amenyanyaswa.

Alikuwa Mke wa Ndoa sio hawara, kwanini asirithishwe Mali za Mumewe?

Uonevu wa wazi.
 
Sasa hao nao wanadhani hizo mali zitawafikisha wapi? Maana mali za marehemu huwa hazikai labd kama aliwashirikisha kuzitunza na kuziendeleza toka mwanzo.
Marehemu wa kwenu ndio mali zao hazikai, Wachaga zinakaa
 
Nyie ni makatili, yaani huyo bibi mliamua kumfanya mtunzaji wa mji kwa maish yake yote bila malipo
 
Kwa taarifa yako watoto tangu wanapoanza kujitambua hadi wanapokuwa watu wazima wanashiriki kwenye uchumi wa familia kwa asilimia zote. Hata kufagia nyumba baba anapokuwapo kazini, kutumwa mahali, na kazi nyinginezo ni sehemu ya uchumi wa familia. Ni ushiriki huu unawafanya wawe warithi halali kabisa wa mali za wazazi wao.
 
Sasa hao nao wanadhani hizo mali zitawafikisha wapi? Maana mali za marehemu huwa hazikai labd kama aliwashirikisha kuzitunza na kuziendeleza toka mwanzo.
Mali ni ya baba yao na mama yao mzazi hata isipowafikisha popote hiyo ni habari nyingine kikubwa ni ni haki yao kurithi.
 
na ukidum miezi miwili upewe sahani na kijiko[emoji23]
 
Kupoa keshapoa labda useme kuanza kuoza
Kisheria mama ana haki lakini kiubinadamu ...
 
Kupoa keshapoa labda useme kuanza kuoza
Kisheria mama ana haki lakini kiubinadamu ...
Sheria ipi inampatia haki mshana?? Sheria inaangalia mazingira ya hiyo haki pia. Yani mali achume mke na mume na huyo mke ana watoto ameacha halafu mke aliyeolewa miez 5 iliyopita mahakama impe haki 100% kama watoto watapinga yeye kurithi??
Labda watoto waridhie wenyewe. Ila wakipinga asee mama dorini atapewa kitanda na mashuka
 
Hapo sio kushiriki katika kujenga uchumi wa familia, ni kutimiza majukumu kama Watoto, ndio mana wanalishwa, wananunuliwa nguo na kusomeshwa...ni Watoto.

Kisheria Mke bila kujali ana kazi au hana ndio anachangia ukuaji wa uchumi wa familia, hata kama hajanunua hata kitasa cha mlango...na anapaswa kurithi mali za Mumewe kama walifunga ndoa.
 
Alisema hakufuata pesa; kwani anadai sehemu ya mali za marehemu?
 
Raia Mwema limekuwa Gazeti la Udaku? Mbona Kuna Mambo Mengi Muhimu sana ya Kuandika, na Sio Udaku wa Mke wa Mrema???
Siyo udaku. Ulimwengu wa sasa ni wa Tehama. Ni juu yako kuchuja vya kumeza na kutema.
 
Ha ha ha! Eti mbususu, ... Utelezi !
 
Kwani wewe baba unapokuwa kazini mtoto analeta maji, analeta kitunguu ili upikiwe ukirudi kazini unakula unavimbiwa unalala hapo anafanyaje?? Kwani kinachofanya hata mwanamke jobless apewe mgao ni nini? Ni hayo hayo kwamba nae kuna majukum anatimiza.
Watoto wana sehemu kwenye ujenzi wa uchumi wa nyumbani hata kama utapinga hadi kesho
 
Kwa sasa ni kama tunafanya ramli tuu maana wosia wenyewe hakuna ajuaye mpaka sasa.. Labda tutakapouona ndio tunaweza kuwa na mjadala mzuri
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…