Mje hapa wale wazee wa watoto wachache

Mje hapa wale wazee wa watoto wachache

maganjwa

JF-Expert Member
Joined
Sep 11, 2012
Posts
2,800
Reaction score
2,339
Screenshot_20220827-075509.png
 
Amekupa hizo data za kulinganisha hivyo vitu viwili?

Mwambie bilionea mwenzake Sahil (Oman) anamshinda, yeye Musk ana watoto 9 mwenzake anaongoza kwa watoto 15.

Aendelee kuzaa, kwani ameishiwa mbegu?
Yeye na utajiri wote anao 9, wewe pangu pakavu je uwe na wangapi? Wajiunge kakikundi ka mabilionea wazae kwa kutuonyesha mfano kama akiweza apate watoto 100, nasi tutafuata kulingana na uchumi wetu tutawaunga mkono kwa angalau watoto 5-10.

Kuwa na hela si kuwa na ufahamu mzuri: yeye anatafuta watu wa kufanyia biashara kwa kutumia watu wengine. Azae wake.

Anajua ni watoto wangapi hawafiki miaka mitano na kufa kwa utapiamlo huku Afrika?
Alete hizo hela za kutunza watoto ili watu wamfyatulie.
 
Swala la watu kupungua Wala halihusiani na sera nk bali kinachoamua ni Hali ya maisha na kiwango cha elimu..

Ukitaka watu waendelee kuzaa tuu lazima uwafanye wajinga na maskini lakini wakielimika na kuwa na kipato au kufukuzia kipato automatically wanpunguza wenyewe mambo ya kuzaa na kutiana hovyo..
 
Mie kwa mke wangu nazaa watatu tu, lakini nitagawa mbegu kwa wanawake wanaotaka sharti awe na kazi ya kudumu au biashara iliyochangamka hasa.
 
Kwa hela alizo nazo hata akiwa na watoto 700 hawezi ona tatizo.ila wale wa <$1 tunapambana😁😁
 
Lengo la kupromote ushoga ni kupunguza idadi ya watu duniani
 
Back
Top Bottom