Mjinga mmoja wa IT ameniulia gari langu

Mjinga mmoja wa IT ameniulia gari langu

Okay sawa

Yule dereva wa break down naomba kujua siku ya ajali analipwa na nani, polisi?
Halipwi chochote pale .. Kumbuka ile ni ajali ni jambo la dharura ... Labda kama tu mwenye gari hatataka gari yake iende polisi au ilale polisi hapo ndio anaweza kumalizana na mwenye gari
Wao hesabu yao sio ya siku
 
Wakuu, salamu zenu!

Juzi natoka zangu Dodoma, Mdogo mdogo narudi zangu Dar! Basi nafika zangu pale Msolwa, mshenzi mmoja asiye na staha barabarani, anajifanya ana haraka ana overtake kijinga jinga! Tumekutana uso kwa pua, Ashukuriwe Mungu baba kwa kunitoa salama! Ila huyu mjinga nitadili naye sana tu naahidi hili


View attachment 1740392
Kumbe ni wewe mkuu.....hii ajali ilitokea mida ya saa 2 au 3 hivi ucku...nilikuwa natoka Dar naenda Mbeya...tulikaa hapo almost 2 hrs.
Pole mkuu
 
Wakuu, salamu zenu!

Juzi natoka zangu Dodoma, Mdogo mdogo narudi zangu Dar! Basi nafika zangu pale Msolwa, mshenzi mmoja asiye na staha barabarani, anajifanya ana haraka ana overtake kijinga jinga! Tumekutana uso kwa pua, Ashukuriwe Mungu baba kwa kunitoa salama! Ila huyu mjinga nitadili naye sana tu naahidi hili


View attachment 1740392
Pole sana mkuu. Barabarani unaweza kuwa na tahadhari zote lakini bado mzembe mwingine akakutoa roho au kukutia hasara kama hiyo.
 
Hii ni Total Loss


Kama una bima kubwa chukua mpunga wote kanunue gari mpya , usichukue Salvage.


IT hakuna madereva , hawana uzoefu na wengi ni deiwaka wanakimbiza ili warudi dar wadandie kazi nyingine
 
Hii ni Total Loss


Kama una bima kubwa chukua mpunga wote kanunue gari mpya , usichukue Salvage.


IT hakuna madereva , hawana uzoefu na wengi ni deiwaka wanakimbiza ili warudi dar wadandie kazi nyingine
Ana third party hivyo atalipwa na bima ya aliyemgonga
 
Pole mkuu kwa majanga....Vipi huyo dereva wa IT gari lake liliweza kuendelea na safaei au nalo liliishia hapo hapo..?
 
Wewe

kuna kesi haziendi mahakamani ? Wewe ndio umesema tuhakikishe kesi inaenda mahakamani. Sasa imekua tuyamalize polisi ?

Halafu PF maana yake ni Police Form. Mahakama inatoaje Police Form?

Na kwa nini niko mahakamani halafu hukumu ya kesi yangu apewe polisi ????

Halafu kwa Tanzania hapa hayo ma fomu 10 kidogo huwezi kuyapata na ku fixiwa gari lako au kulipwa ndani ya mwezi mmoja!

Na gharama za tow truck huwezi kuiita halafu umwambie vuta gari kisha utalipwa kesi ikiisha! Hesabu ya siku anaipelekaje? Na wewe uliyemuita ukishindwa kesi inakuaje ?

Ongea uhalisia brother.
1.Kesi tayari iko mahakamani, ndio kwanza imeandikishwa hata kutajwa haijatajwa na sijui itachukua muda gani.

2.Gari ilikaa siku 2 tu kituo cha polisi Chalinze, nilipoenda kupeleka claim form na cover note ya bima yangu, mkuu wa kituo akanikomalia, kuwa pale sio gereji so nitoe mkweche wangu, nililazimika kuingia mfukoni(300k) kuchukua breakdown toka Chalinze mpaka Kibamba ninakoishi.

3.Vehicle inspector naye akataka mpunga ili aniandikie kile yeye anadai "Ripoti nzuri".

Kifupi, niko mwanzoni tu,lakini nishaanza kuona ugumu wa mchakato wenyewe! Kama kuna mtu ana uzoefu na hizi habari naomba tuwasiliane kwa msaada zaidi!
 
Pole mkuu kwa majanga....Vipi huyo dereva wa IT gari lake liliweza kuendelea na safaei au nalo liliishia hapo hapo..?
Hata yeye pia gari yake iliumia! Zote mbili zilivutwa kupelekekwa kituo cha polisi Chalinze
IMG_20210327_223633.jpg
 
Mahakamani kesi inakaa muda gani, na kipindi hicho unatumia usafiri gani na wakili wako analipwa na nani? Na nani anai tow gari kutoka njia panda Dodoma kuipeleka garage karibu na unakoishi ili uweze kuifuatilia kama BIMA wataamua kui fix?

Ajali sio suala rahisi kama unavyomwambia eti arilaksi!

Police report yenyewe unaweza kuifuatulia mwezi mzima wanajidai polisi mhusika yuko msibani, wanataka rushwa.

Na gereji za Wachina nazo (supposed to be the best of all) usidhani wako profesheno kiviiiile, wanahitaji kuwafuatilia kama garage zetu za Kiswahili.
Kwani ni gari ya aina gani hio mkuu?
 
nilishawaii kutana na kirikuu nacho kinanianzishia ligi barabarani usiku kuchek naona ni IT... kinakimbia hatari
 
Wakuu, salamu zenu!

Juzi natoka zangu Dodoma, Mdogo mdogo narudi zangu Dar! Basi nafika zangu pale Msolwa, mshenzi mmoja asiye na staha barabarani, anajifanya ana haraka ana overtake kijinga jinga! Tumekutana uso kwa pua, Ashukuriwe Mungu baba kwa kunitoa salama! Ila huyu mjinga nitadili naye sana tu naahidi hili


View attachment 1740392
Niuzie hiyo gari niirudishe kwenye mstari
 
1.Kesi tayari iko mahakamani, ndio kwanza imeandikishwa hata kutajwa haijatajwa na sijui itachukua muda gani.

2.Gari ilikaa siku 2 tu kituo cha polisi Chalinze, nilipoenda kupeleka claim form na cover note ya bima yangu, mkuu wa kituo akanikomalia, kuwa pale sio gereji so nitoe mkweche wangu, nililazimika kuingia mfukoni(300k) kuchukua breakdown toka Chalinze mpaka Kibamba ninakoishi.

3.Vehicle inspector naye akataka mpunga ili aniandikie kile yeye anadai "Ripoti nzuri".

Kifupi, niko mwanzoni tu,lakini nishaanza kuona ugumu wa mchakato wenyewe! Kama kuna mtu ana uzoefu na hizi habari naomba tuwasiliane kwa msaada zaidi!
Exactly..... Exaaaaactly!

Mchakato wa bima na ajali ni mrefu, costly, corrupt, exploitative and stressfull!

Mshana Jr. anachukulia mambo kirahisi rahisi anatuambia hatujui mambo ya BIMA eti jamaa a-relax kwa sababu kagongwa yeye, atalipwa na bima ya yule mwingine, vipi kama yule mwingine hana bima ?

Eti beak down tow truck ni bure siku ya ajali kwa vile ajali ni dharura hakuna aliyepanga. Basi wagonjwa wangetibiwa bure na maiti zisingeshikiliwa maana hakuna aliyepanga kuumwa wala kufa.
 
1.Kesi tayari iko mahakamani, ndio kwanza imeandikishwa hata kutajwa haijatajwa na sijui itachukua muda gani.

2.Gari ilikaa siku 2 tu kituo cha polisi Chalinze, nilipoenda kupeleka claim form na cover note ya bima yangu, mkuu wa kituo akanikomalia, kuwa pale sio gereji so nitoe mkweche wangu, nililazimika kuingia mfukoni(300k) kuchukua breakdown toka Chalinze mpaka Kibamba ninakoishi.

3.Vehicle inspector naye akataka mpunga ili aniandikie kile yeye anadai "Ripoti nzuri".

Kifupi, niko mwanzoni tu,lakini nishaanza kuona ugumu wa mchakato wenyewe! Kama kuna mtu ana uzoefu na hizi habari naomba tuwasiliane kwa msaada zaidi!
Kuna mkasa kama huo ulitokea kibaha.

Gari iligongwa na canter. Wakapelekwa kituo cha polisi palepale kibaha.

Gharama za kuvuta gari zilikuja kulipwa na bima ya aliemgonga.

Kesi ikaenda mahakamani, ndani ya miezi miwili hukumu ikatoka na gari ikachukuliwa kupelekwa garage kutengenezwa.

Kiuhalisia gari haitakiwi kutolewa polisi bila hukumu ya mahakama. Maana bado kuna kesi mahakamani na huo ni ushahidi.

Unaweza kulichukua ukaliharibu zaidi na kampuni ya bima ikagoma kulipa.

Huyo polisi amekufanyia unyama.
 
Back
Top Bottom