Mjue Konstantino Mkuu Kaisari wa kiroma ya kale

Mjue Konstantino Mkuu Kaisari wa kiroma ya kale

eden kimario

JF-Expert Member
Joined
Jun 13, 2015
Posts
10,356
Reaction score
16,379
Konstantino Mkuu
200px-Byzantinischer_Mosaizist_um_1000_002.jpg

Konstantino Mkuu (jina kamili: Flavius Valerius Constantinus; Niš, 27 Februari 272 – İzmit, 22 Mei 337) alikuwa Kaisari wa Dola la Roma tangu mwaka 306 akitawala peke yake tangu 324.

Anakumbukwa kama mtawala aliyefaulu kumaliza kipindi cha vita vya wenyewe kwa wenyewe na kukubali Ukristo kama dini huru katika dola.

Alihamisha mji mkuu kutoka Roma kwenda Bizanti iliyoitwa baadaye Konstantinopoli.

Alivyoingia ndani ya utawala

Baba yake Constantius alikuwa mmojawapo wa makaisari wanne walioshirikiana pamoja katika utawala wa dola. Baada ya kifo cha baba jeshi lake likamtangaza Konstantino kuwa Kaisari pia, lakini bila mawasiliano na wengine. Hata hivyo alikubaliwa kama Kaisari mdogo akihusika na majimbo ya Gallia na Britania.

Mwaka 311/312 fitina kati ya makaisari ilikuwa vita na Konstantino alilenga kupanua himaya yake. Mpinzani wake alikuwa hasa Maxentius aliyekaa Italia. Konstantino aliweza kumshinda kwenye mapigano kwenye daraja la Milvio mjini Roma.

Inasemekana kabla ya mapigano hayo alipatwa na ndoto alipoona msalaba wa Yesu Kristo katika jua akasikia sauti, "Utashinda chini ya alama hii!". Baadaye vikosi vya Konstatino vilikuwa na bendera iliyoonyesha herufi za chi-rho ambazo zilimaanisha jina la "Kristo".

Ushindi huu ulimfanya Konstantino awe mkuu wa nusu ya magharibi ya Dola la Roma.

Uhuru kwa Wakristo baada ya kuuawa sana



Hadi mwaka 311 Wakristo waliteswa vikali kwa amri ya Kaisari Diokletiano. Konstatino alibadilisha siasa hii baada ya ushindi na kukubali Ukristo kwa mara ya kwanza kama dini iliyoruhusiwa rasmi, akafaulu pia kupata kibali cha Kaisari mwenzake.

Mwaka 313 alikutana na Licinius, Kaisari wa mashariki ya dola. Pamoja makaisari hao wawili walipatana kutoa tamko la Milano lililotangaza mwisho wa dhuluma dhidi ya Wakristo: "Baada ya kukutana hapa Milano sisi Kaisari Konstantino na Kaisari Licinius tumeamua kuwapa Wakristo pamoja na watu wote uhuru wa kuchagua dini yao ili Mungu wa mbinguni atupe fadhili zake."

Konstantino hakufanya Ukristo kuwa dini rasmi na yeye mwenyewe hakupokea ubatizo hadi muda mfupi kabla ya kifo chake.

Hakuna hakika kuhusu sababu zake: inajulikana ya kwamba mama yake Helena alikuwa Mkristo lakini hakuna hakika alikuwa na athira gani katika malezi ya mwanawe.

Mtawala wa pekee

Tangu mwaka 316 Konstatino alianza kugongana na kaisari mwenzake wa mashariki Liceinius baada ya huyu kuonekana anasaidia mipango ya uasi dhidi ya Konstantino. Mwaka 324 alimshinda na kumkamata akawa mtawala wa pekee.

Hapa aliamua mara moja kuhamisha mji mkuu kutoka Roma kwenda Bizanti. Alitumia pesa nyingi kwa ujenzi wake na kuitangaza rasmi mwaka 330.

Aliratibu upya utawala wa dola akaweka misingi iliyoweza kudumu kwa miaka mingi baada yake.

Hata hivyo alipaswa kutetea mipaka ya dola dhidi ya Wagermanik na dhidi ya Waajemi

Haya ni machache tu kama unajua zaidi unakaribishwa
 
Salute Mkuu..
Kwakua umemgusia Constantine na Ukatoriki, Basi nami ngoja nimgusie Mfalme NERO na ukatoriki. Twende pamoja...
Wakuu Mfalme Nero alikuwa mtawala wa dola ya kirumi, kwani alikuwa mtawala wa dola hiyo kuanzia mwaka 54 baada ya Kristo hadi mwaka 68 baada ya Kristo akiwa mtawala wa mwisho wa ukoo wa Julius. Watawala wa dola hiyo waliomtangulia Nero walikuwa Augustus aliyetawala kuanzia mwaka 27 kabla ya Kristo hadi mwaka 14 baada ya Kristo na huyu ndiye mwanzilishi wa dola hiyo na ndiye anayetajwa na mwenjili Luka sura ile ya pili aya ya kwanza kuwa ndiye aliyeitisha sensa ya watu. Baada yake alifuatia Tiberius ambaye anatajwa na mwenjili Luka katika sura ile ya tatu aya ya kwanza, yeye alitawala kuanzia mwaka 14 baada ya Kristo hadi mwaka 37 baada ya kristo na ndiye aliyeshuhudia kazi za Yesu hadi kufa kwake. Baada ya Tiberius alifuata Kaligula aliyetawala kuanzia mwaka 37 baada ya kristo hadi mwaka 41 baada ya Kristo. Kisha akafuata Kladius aliyetawala kuanzia mwaka 41 baada ya Kristo hadi mwaka 54 baada ya Kristo. Huyu Klaudius ndiye anayetajwa katika kitabu cha Matendo ya Mitume sura ile ya kumi na nane aya ya pili, kuwa aliamuru wayahudi wote waondoke Roma. Baada ya Klaudius ndipo akafuata huyo Nero ambapo kwa kufuata mlolongo huo yeye alikuwa mtawala wa tano baada ya hao niliokutajia.
Ni kweli pia kwamba huyu Nero ni mmoja kati ya watu ambao historia inawatambua kuwa ni watu wabaya-kama anavyojulikana. Na hiyo ndiyo sababu ambayo wewe umetoa kuwa unataka kufahamu historia yake. Labda kabla ya kukupa historia ya huyu mtawala yaani Nero ni bora kama nikikueleza kwanza sababu zilizomfanya mtawala huyu abebe sifa hiyo ya ubaya.

Pengine umewahi kusikia juu ya madhulumu ya Kanisa! Kama umewahi kusikia basi kifupi madhulumu hayo yaliasisiwa na mtawala huyu Nero hapo mwaka 64 baada ya Kristo. Pamoja na kuongoza madhulumu ya wakristo, kama mtawala, inasemekana alikuwa katili sana na ushahidi wa ukatili huo ni kwamba alipanga na ufanikiwa mauaji ya mama yake mzazi hapo mwaka 59 baada ya Kristo yaani miaka mitano tu baada ya kuanza kutawala dola hiyo ya kirumi.

Zaidi ya hayo, Nero hakuona haya kumnyang’anya mke rafiki yake na kumuoa yeye mwenyewe kwa kutumia tiketi ya mamlaka aliyokuwa nayo. Kama haitoshi, Nero anafahamika zaidi kwa ubaya wake kwa sababu ndiye anayetajwa katika kitabu cha Ufunuo wa Yohane kwa namba 666 kama mnyama hatari sana. Hilo rejea kitabu cha Ufunuo 13:11-18.
Katika kipindi cha utawala wake ndipo mitume Petro na Paulo walipouawa katika mfululizo wa madhulumu.

Ingawa NERO hakuwa kiongozi pekee wa dola ya kirumi aliyeongoza madhulumu, kwani kuna wenzake tisa waliomfuata tena walikuwa wauaji hata kuliko Nero. Huyu tumemfahamu pia kwa sababu ametajwa pia katika kitabu cha Matendo ya Mitume 25:10. Yeye ndiye aliyepokea rufaa ya Paulo aliposhtakiwa na wayahudi baada ya kesi kuanza kusikilizwa na Festus.

Baada ya kupata maelezo juu ya mazingira yaliyomfanya Nero asikike au kufahamika na hasa kwa ubaya wake, basi sasa nikupe historia yake kama ulivyoniomba.

Nero alizaliwa mwaka 38 baada ya kristo katika sehemu iliyoitwa Antium kwa wakati ule siku hizi sehemu hiyo inaitwa Anzio, karibu na mji wa Roma huko Italia. Baba yake aliitwa Domitius na mama yake aliitwa Agrippina ambaye alikuwa dada wa mtawala wa dola hiyo hiyo aliyeitwa Kaligula-kama nilivyokuambia pale awali kuwa Kaligula alikuwa mtawala wa tatu. Huyu mama aliolewa kwa mara ya pili na kaisali Kladius- naye nilimtaja pale awali kuwa alimtangulia Nero. Aliolewa kwake mnamo mwaka 49 baada ya kristo. Hivyo Nero alilelewa na huyo baba yake wa kambo yaani mume wa mama yake.

Akiwa na miaka 17 tu ya kuzaliwa, NERO alikabidhiwa dola ya kirumi kama mtawala. Hii ilikuwa mwaka 54 baada ya Kristo-kama nilivyokuambia hapo awali. Miaka mitano ya mwanzo ya utawala wake ilielezewa kuwa na mafanikio makubwa. Wakati wake mradi mkubwa kabisa wa maji na uzalishaji nafaka ulimalizika baada ya kuanzwa na Klaudius mtawala aliyemtangulia. Kwa kweli katika kipindi hiki Nero alionekana kama mtawala bora kabisa na mwenye hekima, ndiyo maana Mtume Paulo aliposhtakiwa na wayahudi alikata rufaa ili kesi yake ikasikilizwe na mtawala huyu akijua kuwa alikuwa mtu mwenye busara na hivyo angetenda haki. Rejea. Matendo ya Mitume 24-25. Pamoja na kuwa na busara, huyu bwana alikuwa anapenda sana michezo. Bila shaka kwa wakati wetu huu angekuwa kipenzi cha vijana na wanapenda michezo.

Nilisema hapo awali kuwa Nero alimnyang’anya rafiki yake mke na kumuoa yeye mwenyewe. Huyu mke wa rafiki yake ndiye aliyeanza kuififisha nyota ya mafanikio ya Nero. Huyo alikuwa mshauri wake mkuu kiasi kwamba Nero alikuwa hamsikilizi yeyote isipokuwa huyo mke wa rafiki yake aliyekuwa anaitwa Salvius Otho na huyo mke wake aliitwa Poppaea.

Mwaka 59 baada ya Kristo, Nero kama nilivyokuambia hapo awali kuwa alipanga mauaji ya mama yake na mwaka huo huo alimtaliki mke wake aliyeitwa Octavia (huyu ndiye binti ya Claudius) na kumuoa Poppea –yaani mke wa rafiki yake. Baada ya kumuoa akampa jina Augusta.

Kutokana na kutotulia kwake, Nero alianza kuonja mporomoko mkubwa wa kiuchumi katika dola yake hata washirika wake walichukizwa naye. Katika harakati za kurekebisha uchumi katika dola yake, mwaka 62 baada ya Kristo Nero alifanya marejereo ya sheria iitwayo Maiestas, sheria ambayo ilisababisha marajiri wengi kuuawa kwa tuhuma tu jambo ambalo lilizidi kuchochea chuki na uhasama dhidi yake.

Kanisa halitausahau mwaka 64 baada ya Kristo mwaka huo ndipo yalipoanza madhulumu ya wakristo. Ilikuwaje. Nero katika harakati za kurekebisha uchumi na kujaribu kurudisha uhusiano wake na watu, alipanga kuurekebisha na kuujenga upya mji wa Roma ambao wakati huo ndiyo ulikuwa makao makuu ya dola ya kirumi. Alichokifanya yeye ni kusababisha moto mkubwa kuunguza mji huo kusudi baada ya kuuungua aujenge upya. Jambo hilo alilifanya kwa siri, kumbe siri hiyo ilifichuka watu walianza kumsakama tena ndipo Nero alipozihamishia tuhuma hizo kwa wakristo ambao wakati huo walionekana kuwa watu wa pekee. Wakristo wengi waliuawa kikatili hasa mjini Roma.
Kabla ya kuanza mauaji hayo ya wakristo, matukio niliyoyataja hapo awali, yaani ya kushuka kwa uchumi, kuchoma moto mji wa Roma na mauaji ya matajiri, yalimpunguzia Nero umaarufu na kukaanza vulugu sehemu nyingi za dola yake. Kulikuwa na migomo na maandamano mengi hasa Afrika, Hispania-sehemu ambazo wakati huo zilikuwa chini ya dola ya kirumi. Hata baada ya kuanza madhulumu hayo, NERO hakuweza kurudisha heshima yake na machafuko yalizidi na misukosuko iliongezeka. Mnamo tarehe 9/6/68 baada ya Kristo Nero aliamua kujiua na huo ndiyo ukawa mwisho wa historia ya maisha yake hapa duniani. Alikufa akiwa kijana tu wa miaka 31 ya kuzaliwa. Baada ya kifo chake dola hiyo iliongozwa na mtawala aliyeitwa Galba aliyefanya kazi kwa mwaka mmoja tu akafuatiwa na wengine hadi mwaka 476 ikiwa chini ya Romulus Agustus kama mtawala wa mwisho kabla ya kuangushwa kwa dola hiyo ya kirumi na wabaribaria.

Kwa hii ndiyo historia ya Nero aliyekuwa mtawala wa Dola ya kirumi. Anakumbukwa sana katika historia ya kanisa letu kwa sababu hasa ya uovu alioufanya kama nilivyokueleza hapo awali kuwa aliwaua mitume Petro na Paulo, aliwaua matajiri wengi wa nchi yake, aliuchoma moto mji wa Roma na kisha kuwatesa na kuwaua kikatili wakristo wengi sana. Kwa kweli sehemu kubwa ya kipindi cha utawala wake kiligubikwa na madhulumu.
Lakini nilikuambia pia kwambwa, huyu Nero hakuwa mbaya tangu kuzaliwa. Mwanzoni alikuwa mtu mwema tu na kipenzi cha watu. Alikuwa mwanamichezo na mpenda maendeleo lakini mke aliyemtwaa kutoka kwa rafiki yake ndiye aliyempotosha hata akapewa rekodi mbaya ya maisha yake hapa duniani. Kwetu sisi hilo liwe fundisho. Watu tunaweza kuwa wema lakini wema huo unageuka na kuwa ubaya kwa kupotoshwa na watu. Mwishoni mema yote husahauliwa na mabaya ndiyo hurekodiwa. Kama illivyompata bwana Nero.
Cc.
Palantir
 
Kabla na baada ya hapo hao watawala wa roma walikuwa wauwaji wakubwa wa wakristo lakini leo wanaheshimiwa nakuitwa watakatifu wa kanisa katoli
Utawaweza waliomezeshwa wakameza
 
Wakina nani?
Wanaosema Petro ndio Papa wa kwanza wakati Petro kafa hata hiko cheo hakipo. Hata catholic church halijazaliwa. Infact nadhani aliuwawa huko huko Rome na watawala wa Roma.
 
Wanaosema Petro ndio Papa wa kwanza wakati Petro kafa hata hiko cheo hakipo. Hata catholic church halijazaliwa. Infact nadhani aliuwawa huko huko Rome na watawala wa Roma.
Ndio petro kafia Rome.
Mbona hiko cheo aliachiwa na yesu mwenyewe..? Soma hapa..
Nami nakuambia, Wewe ndiwe Petro, na juu ya mwamba huu nitalijenga kanisa langu; wala milango ya kuzimu haitalishinda.
Mathayo 16:18


Unajua historia ya petro..
?
Unajua papa ni nani?
 
Kabla na baada ya hapo hao watawala wa roma walikuwa wauwaji wakubwa wa wakristo lakini leo wanaheshimiwa nakuitwa watakatifu wa kanisa katoli
Kama mtawala gani anayeitwa "Mtakatifu"!?..
Kabla ya hapo hapakua hapakuwa na mtu anayeitwa papa upapa ulikuja baadaye cha ajabu wanasema petro alikuwa papa wa kwanza
Wewe dini gani!?..Lakini haya mambo mbona mnapenda yashabikia?.. Hebu nipe msimamo wa dini yako kwanza!.
Wanaosema Petro ndio Papa wa kwanza wakati Petro kafa hata hiko cheo hakipo. Hata catholic church halijazaliwa. Infact nadhani aliuwawa huko huko Rome na watawala wa Roma.
Hujui historia lakini umebwabwaja hivyo!.. Kuna kitu kinaitwa 'uvumilivu katika dini' hebu jifunze!..
 
Wanaosema Petro ndio Papa wa kwanza wakati Petro kafa hata hiko cheo hakipo. Hata catholic church halijazaliwa. Infact nadhani aliuwawa huko huko Rome na watawala wa Roma.

Ndio petro kafia Rome.
Mbona hiko cheo aliachiwa na yesu mwenyewe..? Soma hapa..
Nami nakuambia, Wewe ndiwe Petro, na juu ya mwamba huu nitalijenga kanisa langu; wala milango ya kuzimu haitalishinda.
Mathayo 16:18


Unajua historia ya petro..
?
Unajua papa ni nani?
Sasa wapi hapo Yesu kamwambia kuwa utakuwa papa? NA nisehemu gani palipo andikwa kuwa kanisa hilo litakuwa ni Roman catholic?
 
Sasa wapi hapo Yesu kamwambia kuwa utakuwa papa? NA nisehemu gani palipo andikwa kuwa kanisa hilo litakuwa ni Roman catholic?
Unajua maana ya Papa na papa ni nani?

Kwani ninyi kila mnachofanya kimeandikwa kwenye biblia?
 
Linganisheni na hii

UNAYOJIFUNZA KUTOKANA NA HISTORIA

Konstantino

Konstantino alikuwa maliki wa kwanza wa Roma kudai kuwa Mkristo. Kwa kufanya hivyo, alikuwa na uvutano mkubwa kwenye historia ya ulimwengu. Aliikubali dini hiyo ambayo hapo awali waumini wake waliteswa na alisaidia kuanzisha dini zinazodai kuwa za Kikristo. Hivyo, Ukristo huo ukawa “chombo chenye nguvu zaidi kisiasa na kijamii” kilichobadili historia, kulingana na ensaiklopidia moja (The Encyclopædia Britannica).

KWA nini utake kujua kuhusu maliki wa zamani wa Roma? Ikiwa unapendezwa na Ukristo, basi unapaswa kujua kwamba harakati za kisiasa na za kidini za Konstantino zimeathiri imani na desturi za makanisa mengi leo. Hebu tuone jambo hilo.

MAKANISA—YATAMBULIWA KISHERIA KISHA YATUMIWA VIBAYA

Katika mwaka wa 313 W.K., Konstantino alitawala majimbo ya Magharibi ya Milki ya Roma, na Licinius na Maximinus wakatawala Majimbo ya Mashariki. Konstantino na Licinius waliwapa watu wote uhuru wa kuabudu kutia ndani Wakristo. Konstantino aliulinda Ukristo, kwa kuwa aliamini dini hiyo ingewaunganisha watu katika milki yake.*

Konstantino alishangaa kuona migogoro mingi iliyogawanya Ukristo. Akiwa na nia ya kuleta makubaliano, alianzisha na baadaye kulazimisha watu wafuate mafundisho aliyodai kuwa ya kweli. Ili kumfurahisha, makasisi walilegeza msimamo wao na kwa kufanya hivyo, hawakutozwa kodi na pia walipewa misaada mingi ya kifedha. Mwanahistoria Charles Freeman aliandika: “Kufuata mafundisho ya Kikristo yaliyoonwa kuwa ya kweli kulifungua njia ya kuingia mbinguni na pia njia ya kupata mali nyingi duniani.” Makasisi wakawa watu mashuhuri katika mambo yaulimwengu. Mwanahistoria A.H.M. Jones alisema: “Kanisa lilikuwa limepata mlinzi na pia bwana mkubwa.”

“Kanisa lilikuwa limepata mlinzi na pia bwana mkubwa.”—Mwanahistoria A.H.M. Jones

JE, ULIKUWA UKRISTO WA KWELI?

Mapatano kati ya Konstantino na maaskofu yalitokeza dini yenye mafundisho ya Kikristo na ya kipagani. Isingeweza kuwa vingine, kwa kuwa lengo lake halikuwa kutafuta dini ya kweli bali alitaka kuunganisha imani mbalimbali. Kwa kweli, alikuwa mtawala wa milki ya kipagani. Mwanahistoria mmoja alisema kuwa, ili kufurahisha dini zote, Konstantino aliamua “kutounga mkono waziwazi upande wowote katika shughuli zake za kibinafsi na za serikali kwa ujumla.”

Ingawa alidai kuutetea Ukristo, Konstantino alishikilia imani za kipagani. Kwa mfano, alikuwa mnajimu na mwaguzi—mazoea ya kichawi ambayo Biblia hukataza. (Kumbukumbu la Torati 18:10-12) Tao la Konstantino huko Rome lina mchoro wake akitoa dhabihu kwa miungu ya kipagani. Aliendelea kumtukuza mungu huyo kwa kuweka picha yake kwenye sarafu na kuendeleza ibada ya mungu-jua. Na baadaye hata aliruhusu wakaaji wa mji mdogo wa Umbria, huko Italia wajenge hekalu kwa ajili yake na familia yake, na akaweka makuhani wahudumu katika hekalu hilo.

Konstantino alibatizwa na kuwa “Mkristo” siku chache kabla ya kifo chake mwaka wa 337 W.K. Wasomi wengi huamini kuwa aliahirisha kubatizwa ili aendelee kuungwa mkono kisiasa na Wakristo na wapagani katika milki yake. Kwa kweli, maisha yake na kuchelewa kwake kubatizwa kunafanya watu wengi watilie shaka imani yake ya Kikristo. Hata hivyo, jambo moja ni hakika: Kanisa ambalo Konstantino aliweka rasmi lilikuja kuwa shirika lenye nguvu kisiasa na kidini, ambalo lilimwacha Kristo na kufuata mambo ya ulimwengu. Lakini, Yesu alisema hivi kuhusu wafuasi wake: “Wao si sehemu ya ulimwengu, kama vile ambavyo mimi si sehemu ya ulimwengu.” (Yohana 17:14) Kanisa hilo—ambalo sasa lilikuwa linafuata mambo ya ulimwengu—lilitokeza madhehebu mengine mengi.

Tunajifunza nini kutokana na mambo hayo yote? Hatupaswi kukubali tu mafundisho ya kanisa lolote bali tunahitaji kuyachunguza kwa kutumia Biblia.—1 Yohana 4:1.

Watu wengi wanatilia shaka ikiwa kwa kweli Konstantino aligeuka na kuwa Mkristo, kwa sababu, kulingana na kitabu fulani, aliendelea “kukubali ibada za kipagani, hadi mwishoni mwa utawala wake.”

TAARIFA FUPI

Konstantino alikuwa maliki wa Majimbo ya Magharibi ya Milki ya Roma kuanzia mwaka wa 306 W.K. na akawa maliki pekee wa Majimbo ya Mashariki na Magharibi kutoka mwaka wa 324 W.K. hadi 337 W.K.

Konstantino alidai kuwa alihakikishiwa kupitia ndoto au maono, kwamba Mungu wa Wakristo angemsaidia katika vita.

Akimshukuru Mungu kwa kumpa ushindi fulani wa kivita, Konstantino “aliamuru mara moja” mkuki uliochongwa kamamsalaba uwekwe kwenye mkono wa sanamu yake iliyowekwa “katika eneo linalotembelewa sana huko Rome.”—Mwanahistoria Paul Keresztes.

Konstantino alikuwa na cheo cha kipagani cha pontifex maximus, au kuhani mkuu, na alijiona kuwa bwana wa dini zote katika milki yake..


“Maliki mzuri—na hata Mkristo mzuri—hana budi kuchagua kati ya kupoteza kibali cha Mungu au kupoteza umaarufu wake. Alipoanza kutawala, Konstantino alikuwa tayari kufanya chochote kile hata kufanya dhambi ili aendelee kushikilia mamlaka.”—Richard Rubenstein, Profesa wa kutatua mizozano na masuala ya umma.
 
Linganisheni na hii

UNAYOJIFUNZA KUTOKANA NA HISTORIA

Konstantino

Konstantino alikuwa maliki wa kwanza wa Roma kudai kuwa Mkristo. Kwa kufanya hivyo, alikuwa na uvutano mkubwa kwenye historia ya ulimwengu. Aliikubali dini hiyo ambayo hapo awali waumini wake waliteswa na alisaidia kuanzisha dini zinazodai kuwa za Kikristo. Hivyo, Ukristo huo ukawa “chombo chenye nguvu zaidi kisiasa na kijamii” kilichobadili historia, kulingana na ensaiklopidia moja (The Encyclopædia Britannica).

KWA nini utake kujua kuhusu maliki wa zamani wa Roma? Ikiwa unapendezwa na Ukristo, basi unapaswa kujua kwamba harakati za kisiasa na za kidini za Konstantino zimeathiri imani na desturi za makanisa mengi leo. Hebu tuone jambo hilo.

MAKANISA—YATAMBULIWA KISHERIA KISHA YATUMIWA VIBAYA

Katika mwaka wa 313 W.K., Konstantino alitawala majimbo ya Magharibi ya Milki ya Roma, na Licinius na Maximinus wakatawala Majimbo ya Mashariki. Konstantino na Licinius waliwapa watu wote uhuru wa kuabudu kutia ndani Wakristo. Konstantino aliulinda Ukristo, kwa kuwa aliamini dini hiyo ingewaunganisha watu katika milki yake.*

Konstantino alishangaa kuona migogoro mingi iliyogawanya Ukristo. Akiwa na nia ya kuleta makubaliano, alianzisha na baadaye kulazimisha watu wafuate mafundisho aliyodai kuwa ya kweli. Ili kumfurahisha, makasisi walilegeza msimamo wao na kwa kufanya hivyo, hawakutozwa kodi na pia walipewa misaada mingi ya kifedha. Mwanahistoria Charles Freeman aliandika: “Kufuata mafundisho ya Kikristo yaliyoonwa kuwa ya kweli kulifungua njia ya kuingia mbinguni na pia njia ya kupata mali nyingi duniani.” Makasisi wakawa watu mashuhuri katika mambo yaulimwengu. Mwanahistoria A.H.M. Jones alisema: “Kanisa lilikuwa limepata mlinzi na pia bwana mkubwa.”

“Kanisa lilikuwa limepata mlinzi na pia bwana mkubwa.”—Mwanahistoria A.H.M. Jones

JE, ULIKUWA UKRISTO WA KWELI?

Mapatano kati ya Konstantino na maaskofu yalitokeza dini yenye mafundisho ya Kikristo na ya kipagani. Isingeweza kuwa vingine, kwa kuwa lengo lake halikuwa kutafuta dini ya kweli bali alitaka kuunganisha imani mbalimbali. Kwa kweli, alikuwa mtawala wa milki ya kipagani. Mwanahistoria mmoja alisema kuwa, ili kufurahisha dini zote, Konstantino aliamua “kutounga mkono waziwazi upande wowote katika shughuli zake za kibinafsi na za serikali kwa ujumla.”

Ingawa alidai kuutetea Ukristo, Konstantino alishikilia imani za kipagani. Kwa mfano, alikuwa mnajimu na mwaguzi—mazoea ya kichawi ambayo Biblia hukataza. (Kumbukumbu la Torati 18:10-12) Tao la Konstantino huko Rome lina mchoro wake akitoa dhabihu kwa miungu ya kipagani. Aliendelea kumtukuza mungu huyo kwa kuweka picha yake kwenye sarafu na kuendeleza ibada ya mungu-jua. Na baadaye hata aliruhusu wakaaji wa mji mdogo wa Umbria, huko Italia wajenge hekalu kwa ajili yake na familia yake, na akaweka makuhani wahudumu katika hekalu hilo.

Konstantino alibatizwa na kuwa “Mkristo” siku chache kabla ya kifo chake mwaka wa 337 W.K. Wasomi wengi huamini kuwa aliahirisha kubatizwa ili aendelee kuungwa mkono kisiasa na Wakristo na wapagani katika milki yake. Kwa kweli, maisha yake na kuchelewa kwake kubatizwa kunafanya watu wengi watilie shaka imani yake ya Kikristo. Hata hivyo, jambo moja ni hakika: Kanisa ambalo Konstantino aliweka rasmi lilikuja kuwa shirika lenye nguvu kisiasa na kidini, ambalo lilimwacha Kristo na kufuata mambo ya ulimwengu. Lakini, Yesu alisema hivi kuhusu wafuasi wake: “Wao si sehemu ya ulimwengu, kama vile ambavyo mimi si sehemu ya ulimwengu.” (Yohana 17:14) Kanisa hilo—ambalo sasa lilikuwa linafuata mambo ya ulimwengu—lilitokeza madhehebu mengine mengi.

Tunajifunza nini kutokana na mambo hayo yote? Hatupaswi kukubali tu mafundisho ya kanisa lolote bali tunahitaji kuyachunguza kwa kutumia Biblia.—1 Yohana 4:1.

Watu wengi wanatilia shaka ikiwa kwa kweli Konstantino aligeuka na kuwa Mkristo, kwa sababu, kulingana na kitabu fulani, aliendelea “kukubali ibada za kipagani, hadi mwishoni mwa utawala wake.”

TAARIFA FUPI

Konstantino alikuwa maliki wa Majimbo ya Magharibi ya Milki ya Roma kuanzia mwaka wa 306 W.K. na akawa maliki pekee wa Majimbo ya Mashariki na Magharibi kutoka mwaka wa 324 W.K. hadi 337 W.K.

Konstantino alidai kuwa alihakikishiwa kupitia ndoto au maono, kwamba Mungu wa Wakristo angemsaidia katika vita.

Akimshukuru Mungu kwa kumpa ushindi fulani wa kivita, Konstantino “aliamuru mara moja” mkuki uliochongwa kamamsalaba uwekwe kwenye mkono wa sanamu yake iliyowekwa “katika eneo linalotembelewa sana huko Rome.”—Mwanahistoria Paul Keresztes.

Konstantino alikuwa na cheo cha kipagani cha pontifex maximus, au kuhani mkuu, na alijiona kuwa bwana wa dini zote katika milki yake..


“Maliki mzuri—na hata Mkristo mzuri—hana budi kuchagua kati ya kupoteza kibali cha Mungu au kupoteza umaarufu wake. Alipoanza kutawala, Konstantino alikuwa tayari kufanya chochote kile hata kufanya dhambi ili aendelee kushikilia mamlaka.”—Richard Rubenstein, Profesa wa kutatua mizozano na masuala ya umma.
Tushawazoe mkuu hii Copy yako si mara ya kwanza kuisoma humu..
 
Back
Top Bottom