Mjue Mtemi Mkwawa wa uhehe na Wahehe

lole Gwagisa, Yericko Nyerere,

..napenda kujua Mkwawa alikuwa akipata wapi silaha za kivita?

..je, kuna ukweli wowote kuhusu tuhuma kwamba alikuwa akijihusisha na biashara wa WATUMWA??

..ugomvi wa Mkwawa na Wajerumani ulikuwa kuhusu nini haswa?
 
Last edited by a moderator:
lole Gwagisa, Yericko Nyerere,

..napenda kujua Mkwawa alikuwa akipata wapi silaha za kivita?

..je, kuna ukweli wowote kuhusu tuhuma kwamba alikuwa akijihusisha na biashara wa WATUMWA??

..ugomvi wa Mkwawa na Wajerumani ulikuwa kuhusu nini haswa?

Swali la nyongeza. Je Mkwawa Mwinyigumba alikuwa mhehe 100%?
 
lole Gwagisa, Yericko Nyerere,

..napenda kujua Mkwawa alikuwa akipata wapi silaha za kivita?

..je, kuna ukweli wowote kuhusu tuhuma kwamba alikuwa akijihusisha na biashara wa WATUMWA??

..ugomvi wa Mkwawa na Wajerumani ulikuwa kuhusu nini haswa?
mkwawa silaha za kivita alikuwa akitengeneza yeye mwenyewe baada ya kuuziwa bunduki ya kwanza na waarabu ndipo akadokolezea teknolojia hiyo na akafanikiwa kutengeneza ya kwake, ikumbukwe pia huyu jamaa alikuwa mwizi wa technolojia mpya ya mapambano kila alipoiona, ndo maana alikuwa akiwashinda sana maadui zake kama wangoni ambao aliiba mbinu za mapambano kwao na akatumia kuwapigia wao. ukienda kalenga utaiona hiyo buduki inyosemekana aliitengeneza yeye mwenyewe na sehemu ambayo lilikuwa ghala la silaha lililosheni baluti, lakini pia ikumbukwe kuwa alikuwa akiteka na kuwanyang'anya silaha maadui, mfano kwa mjerumani aliteka bunduki mi tatu na kumi pamoja na mizinga mitatu.
ugomvi kati ya mkwawa na wajerumani ulianzia pale mkwawa aliopowatoza wajerumani kodi kwa kupita kwenye himaya yake, lakini wajerumani walikataa ndipo mkwawa akaamua kufunga ile trade root ya kwenda kilwa ndipo uhasama ulipoaanza na kuzaa vita ya kwanza iliyopiganiwa lugalo ambayo alishinda kisha wajerumani wakajipanga tena kwa kushirikiana na makabila hasimu ya wahehe ndipo walipomshinda japo kwa tabu.
hakuna ushahidi wa wazi ambao unaonyesha mkwawa kuwa alijihusisha na biashara ya utumwa maana yeye mwenyewe alikuwa na tabia ya kuwakamata mateka na kuwatumikisha mwenyewe bila kuwauza na hili linathibitishwa na koo mbalimbali zinazopatikana kalenga kwenye ngome yake ambazo nyingi sio za kihehe bali ni za makabila mbalimbali na pia kuna maeneo kama ikonongo huko walikuwa wakiwekwa wageni wale wasio wahehe na mkwawa kwa ajiri ya kulima.

pa kuna swali kauliza zakimi kama mkwawa alikuwa mhehe 100% ukweli ni kwamba mkwawa ni mjuu wa aliyekuwa mfalme wa wahehe. baba ake mkwawa inasemekana alitokea huko ethiopia na ni mhabeshi ambaye alikuwa muwindaji sasa alipofika lilinga ndipo akakaribishwa na mfalme akaa kwake kwa siku kazaa na akampa binti wa huyo mfalme mimba kisiri baada ya kuona hivyo akakimbia na huyo binti ndipo alipomzaa mkwavinyika yaani mtwaa nchi ambaye anafahamika kama mkwawa.
 
mkuu hapo naona fuatilia vizuri, mwambambe mwalunyungu hakuwa askari wa mnyigumba bali ndiye aliyekuwa jemedari mkuu wa mkwawa, baadaye akaja kumpindua mkwawa na mkwawa kufanikiwa kukimbilia dodoma na wala hayawahi kukimbilia morogoro na alifika dodoma huku akiwa amejipaka masizi na majivu kama mtumwa. morogoro ni sehemu ambayo dawa za kumrudisha mkwawa nyumbani zilipoenda kuchukuliwa sababu mizimu ya wahehe ilipatikana huko sehemu za lulanga. ikumbukwe kuwa huyu mwambambe ni shujaa ambaye alivunja rekodi ya kukimbia katika wanajeshi wa enzi hizi na alikuwa na nguvu za ajabu wao wanasema haijawahi tokea, hata mkwawa aliporudi walimfukuzia umbali mrefu mno mbaka alipoenda kujificha pale kichakani ambapo inasemekana walikuwa wakimpiga mikuki ila yeye aliidaka na kuirudisha ambapo aliwauwa askari wengi wa mkwawa mbaka alipochoka ndipo askari mmoja alipofanikiwa kumlenga kifuani na kumwua.
 
ni kweli himaya ya mkwawa ilikuwa ni kubwa sana maana tiyari alikuwa amefika mbeya, songea dodoma, tabora na morogoro kiasi kwamba utawala wake ungedumu mda mrefu zaidi basi nusu ya tanganyika ingekuwa ya uhehe maana wakati huo hakuna kabila lililokuwa na uwezo wa kuwadhibiti wahehe, na mkwawa inasemekana yeye alikuwa anajihami zaidi na wamasai ambao alisikia wana nguvu hivyo alianza kujiandaa kufanya vita nao.
 
mkwawa alikuwa ni zao kati ya muwindaji wa kihabeshi na binti wa mfalme wa wahehe wakati huo


Kwa hiyo unakubaliana kuwa hakuwa mhehe 100%. Na vilevile kutokana uhabeshi wake alifanana na tipu tipu na sio wahehe wengine.
 

Hiyo sehemu niliyo highlight nyekundu na kupigia mstari sahihi ni Mwamyinga
 
Kwa hiyo unakubaliana kuwa hakuwa mhehe 100%. Na vilevile kutokana uhabeshi wake alifanana na tipu tipu na sio wahehe wengine.
unachosema ni ukweli kabisa, lakini la kufanana na tipu tipu sina uhakika, ukimfuatilia sana umbo lake na tabia zake zilikuwa ni za kihehe kabisa, vyovyote itavyokuwa alikuwa na damu ya kihehe na uhehe kumbuka aliikuta ikiwa imara na yenye nguvu ye aliendeleza pale alipoishia mnyigumba ambaye alifanya kazi kubwa ya kuwaunganisha wahehe na kuliimarisha jeshi na kutanua hikaya ya mhehe
 
Pia naomba tuliweke wazi kuwa mkwawa hakuwa chief bali alikuwa king(mfalme), naona hili limepotoshwa kwa muda mrefu na watoto mashuleni wanafundishwa hivyo kitu ambacho ni uongo
 

Katika posti yako moja umesema kuwa Mkwawa alipata bunduki kutoka kwa waarabu na kuanza kutengeneza zake mwenyewe. Na unakanusha kuwa hakuusika na biashara ya watumwa.

Hili uweze kutengeneza bunduki ni lazima uwe na chuma. Kwa historia ninayojua mimi, wahehe hawakuwa na technologia ya chuma. Makabila yalikuwa na technologia ya kufua chuma ni wafipa, walogo, wahaya .....

Pili katika vita ya kwanza na wajerumani, jeshi la mkwawa ziliteka bunduki kama 300 kutoka kwa majeshi wa ujerumani. Bunduki hizi zilikuwa nzuri kuliko zile za waarabu. Kama wahehe walikuwa na utaalamu wa kutengeneza bunduki kwanini hawakukopi zile za mjerumani?

Tatu huwezi kutumia bunduki bila kuwa na risasi au baruti. Wakati wajerumani wanateka ngome ya Mkwawa walikuta hazina kubwa baruti na meno ya tembo. Kwa sababu uheheni hakuna baruti, je ni biashara gani alikuwa anafanya?

Nne Mwamubambe ambaye alikuwa ni shemeji ya Mkwawa ni mnyamwezi. Alichukuliwa utumwa na wahehe na kulelewa na baba yake Mkwawa. Kama Mkwawa au Baba yake hakujishughulisha na biashara ya utumwa huyu Mwamubambe alifikaje uheheni?
 
lole Gwagisa, Yericko Nyerere,

..napenda kujua Mkwawa alikuwa akipata wapi silaha za kivita?

..je, kuna ukweli wowote kuhusu tuhuma kwamba alikuwa akijihusisha na biashara wa WATUMWA??

..ugomvi wa Mkwawa na Wajerumani ulikuwa kuhusu nini haswa?


Swali la nyongeza. Je Mkwawa Mwinyigumba alikuwa mhehe 100%?

Wakuu, mniwie radhi kwa kutoonekana jukwaa hili la historia, hasa historia ya watukua wetu kama Mtwa Mkwavinyika Mnikungu (Mkwawa).
Namshukuru sana mkuu mnyikungu kwa kuendeleza historia ya Mtwa Mkwawa.
Mimi nitarudi na stories nyingine za ziada.
 
kaka asante kwa changamoto zako, naomba nikujibu japo kidogo kama ifuatavyo, si kweli kama wahehe hawakua wafua chuma, wahehe ni wafua chuma wazuri tu, technolojia ya kufua chuma ilikuwepo toka enzi na enzi ndo maana vitu kama mikuki nyengo na vitu vingine vya chuma walitengenezea wao wenyewe, pia nikukumbushe kitu kimoja kulithibitisha hili. wahehe kila kitu hufanyika kulingana na koo husika, kuna koo za matabibu kama wakina nyenza na kina maliga na kulikuwepo na koo na wafua vyuma kama na watengenezaji wa bunduki kama kina nyakasonga, mbaka leo ukitafuta koo hizo bado zinatengeneza bunduki shotgun maarufu kama magobole.

pili umeuliza kwa nini wahehe hawakucopy bunduki za mjerumani, ndugu yangu bunduki za kipindi kile zote zilikuwa ni shotgun au magobole, liwe la mwarabu au mjerumani zote zilikuwa zinafana kabisa. kwahiyo asingeweza kuiga kitu ambacha tiyari alikuwa ameisha kiiga.

tatu umesema mwenyewe alikutwa ana hazina kubwa ya meno ya tembo na baruti. wingi wa meno ya tembo inadhihirisha kabisa kuwa huyu jamaa alikuwa akifanya biashara ya meno ya tembo hasa ukizingatia yeye alikuwa anapatikana kwenye mbuga ya wanyama inayofahamika kama ruaha sasa.kumbuka meno ya tembo ndo ilikuwa biashara kubwa sana wakati huo.

mwisho naomba kukanusha habari za kuwa mwambambe alichukuliwa mtumwa, mwambambe ni mhehe kabisa na anatokea ukoo wa kina mwalunyungu ambao ndo ulikuwa unatawala uhehe kabla ya mkwawa. labda wewe umesoma vitabu fulani vya wazungu vinavyosema mkwawa alipinduliwa na wangoni wakiongozwa na mwambambe kitu ambacho si cha kweli. hata sababu ya mwambambe kumpindua mkwawa ilikuwa hiyo kuwa aliona kama kapolwa ufalme na mkwawa. pia naomba utofautishe tofauti kati ya mateka na watumwa, mkwawa alikuwa na mateka wa vita alivyopigana na makabila mbalimbali kama wangoni, wasangu, wabena,wasafwa, wanyamwezi na mengine mengi ambao mwisho wa siku aliwafanya watumwa kwa kuwatumikisha yeye mwenyewe na sio kuwauza ndo maana irnga utakutana na koo nyingi za kingoni, kigogo na nyingine kutoka makabila mengine ambao ama watekwa na kubakishwa hapa kufanya kazi au waliletwa na wafalme wa makabila mengine kama hongo ili mkwawa asiende kuwashambulia.
 
Yale mafuvu 83 yaliyobakia ndo inakuwaje? Ngoja niende Bremen Museum kuwauliza.
Isike naye alijilipua. Ile yeye ni baruti nadhani hawakupata kitu. Kinjiketile ilikuwaje? Kaburi lake lipo?

ulivyoenda Bremen walisemaje mkuu zitto?
 
Wote tunatambua ushujaa wa Mtemi Mkwawa dhidi ya mkoloni Mjerumani. Mjerumani alipigwa round ya kwanza na mbabe Mkwawa akakimbia na kwenda kujipanga tena .

Aliporudi for second round, zikapigwa tena ila kidume Mkwawa aligoma kushikwa na Mjerumani na kwa ujasiri wa ajabu akaamua kujiua. Ukiachana na Wahehe, hakuna kabila lolote ambalo limeweza kuonesha ushujaa kama wa Wahehe.

Na ndio maana Mzungu alichukua fuvu la mbabe Mkwawa na kuondoka nalo ili kulichunguza zaidi kuhusiana na ushujaa wa huyu kidume. Wahehe ni mashujaa sana. Hata sasa hivi wapo hivyo hivyo tofauti na makabila mengine.
 
kwanza mkwawa hakua mhehe

ila ujasiri wa kujinyonga ndio ujasiri mkubwa zaidi duniani
 
kwanza mkwawa hakua mhehe

ila ujasiri wa kujinyonga ndio ujasiri mkubwa zaidi duniani

Pole sana mkuu nani aliye kudanganya kuwa mkwawa alijinyonga??

na kwa taarifa yako mkwawa hakujinyonga na lile fuvu la kichwa ni kanya boya tuu.soon nitakupa story kamili stay tuned.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…