Mjumbe wa Congress ataka Trump afanyiwe impeachment kwa matamshi yake kuhusu Gaza

Mjumbe wa Congress ataka Trump afanyiwe impeachment kwa matamshi yake kuhusu Gaza

Webabu

JF-Expert Member
Joined
Apr 29, 2010
Posts
8,870
Reaction score
14,258
Tamko alilolitoa Donald Trump akiwa na Benjamin Netanyahu akisema ataichukua Gaza na kuijenga upya kwa kuwaondosha wapalestina imepelekea mshtuko mkubwa kwa viongozi wa mataifa mengi pamoja na wanasiasa wa Marekani.


Wanasiasa waliokuwepo ukumbini wakati Trump akisema hayo kama hitimisho la mazungumzo yake na Netanyahu hapo majuzi baadhi yao walificha nyuso zao kwenye mikono kutokana na haya waliyoipata kwa tamko hilo la raisi wao.


Kuna wanasiasa nchini Ireland na mataifa mengine ambao wametoa matamko makali ya kumdharau Trump kwa matamshi yake hayo.Mmoja wao amesema ikulu ya Marekani kwa sasa ni kama haina mtu.

Kwa upande wake Al Green ambaye ni mjumbe wa Congress kutoka chama cha Democrat amesema atapeleka kwenye baraza vipengele vya kumshtaki Trump ili aachie madaraka (impeach)Akaongeza kwa kusema kuwa tamko kama hilo halingetajwa kama utani hasa kutamkwa na raisi wa taifa kubwa kama Marekani.

Mbali na hivyo hilo ni jambo kubwa kwa sera za nchi ambalo lingepaswa lipitie kwenye vikao rasmi vya kiserikali kabla ya kutamkwa hadharani kitu ambacho hakikufanyika.

Wanasias wengine wa Marekani wako waliosema matakwa ya Trump kuhusu Gaza hayatafanyika na hayatekelezeki.Wapalestina wenyewe wamemwita raisi huyo kuwa ni mwendawazimu.

 
Safari ni ndefu ila tutafika tu 🙂🙂
FB_IMG_17385820059708186.jpg
 
Kwahiyo unategemea Democrats wamsifie Trump? Huyo ndio keshakuwa Rais wa US wamvimilie tu wasubir muda wake uishe wamchague mwingine
 
Kwahiyo unategemea Democrats wamsifie Trump? Huyo ndio keshakuwa Rais wa US wamvimilie tu wasubir muda wake uishe wamchague mwingine
Kosa hilo sio la chama cha kidemocratic pekee.Wajumbe wa chama chake wanaweza wakaona kosa la raisi wao kama ilivyotokea Korea Kusini.
 
Hii kauli ya Trump,itakua ilimshtua mpaka Netanyau mwenyewe.
Inatokezea mtu unamsimulia mtu shida yako ili akusaidie kupata ufumbuzi.Mwishowe ukamkuta ili kukusaidia anavuta mipaka na kujifanya yeye ndiye mwenye ugomvi akawaingiza hata majirani zako ambao ulikuwa na uhusiano nao au hawakuwa wabaya kwako.
Hapo unajuta kwanini ulimfuata huyu jamaa,Limekuwa zomwe.Naamini Netanyahu amekuwa kama hivyo kwa Trump.Sio msaada aliutaka kwa muda huo japo alikuwa na mipango kama hiyo kwa siri.Trump amemtilia Netanyahu kitumbua chake.
 
Inatokezea mtu unamsimulia mtu shida yako ili akusaidie kupata ufumbuzi.Mwishowe ukamkuta ili kukusaidia anavuta mipaka na kujifanya yeye ndiye mwenye ugomvi akawaingiza hata majirani zako ambao ulikuwa na uhusiano nao au hawakuwa wabaya kwako.
Hapo unajuta kwanini ulimfuata huyu jamaa,Limekuwa zomwe.Naamini Netanyahu amekuwa kama hivyo kwa Trump.Sio msaada aliutaka kwa muda huo japo alikuwa na mipango kama hiyo kwa siri.Trump amemtilia Netanyahu kitumbua chake.
Ninyi INAONEKANA hamfuatilii mambo.

Hilo suala la kuichukua Gaza, Israel ilikuwa nalo Toka utawala wa Biden, sema utawala wa Biden uliwagomea...
 
Ninyi INAONEKANA hamfuatilii mambo.

Hilo suala la kuichukua Gaza, Israel ilikuwa nalo Toka utawala wa Biden, sema utawala wa Biden uliwagomea...
Na lingewezekana kama Misri ingekubali rushwa ya kufungua mpaka wake ili watu wa Gaza waingie jangwa la Sinai.Hapo peke yake ndipo Misri iliposaidia watu wa Gaza juu ya kwamba walikuwa na uwezo hata wa kuzuia vita visitokee au visiuwe watu wengi kiasi kile na kulifikisha jeshi la israel mpaka Rafah.
Kazi ya kuishawishi Misri ifungue mpaka wake ilikuwa ndio lengo kuu la Blinke muda wote akienda Misri
 
achaneni na mambo yasiowahusu

TRUMP piga kazi usicheke na kima
 
Tamko alilolitoa Donald Trump akiwa na Benjamin Netanyahu akisema ataichukua Gaza na kuijenga upya kwa kuwaondosha wapalestina imepelekea mshtuko mkubwa kwa viongozi wa mataifa mengi pamoja na wanasiasa wa Marekani.
Wanasiasa waliokuwepo ukumbini wakati Trump akisema hayo kama hitimisho la mazungumzo yake na Netanyahu hapo majuzi baadhi yao walificha nyuso zao kwenye mikono kutokana na haya waliyoipata kwa tamko hilo la raisi wao.
Kuna wanasiasa nchini Ireland na mataifa mengine ambao wametoa matamko makali ya kumdharau Trump kwa matamshi yake hayo.Mmoja wao amesema ikulu ya Marekani kwa sasa ni kama haina mtu.
Kwa upande wake Al Green ambaye ni mjumbe wa Congress kutoka chama cha Democrat amesema atapeleka kwenye baraza vipengele vya kumshtaki Trump ili aachie madaraka (impeach)Akaongeza kwa kusema kuwa tamko kama hilo halingetajwa kama utani hasa kutamkwa na raisi wa taifa kubwa kama Marekani.
Mbali na hivyo hilo ni jambo kubwa kwa sera za nchi ambalo lingepaswa lipitie kwenye vikao rasmi vya kiserikali kabla ya kutamkwa hadharani kitu ambacho hakikufanyika.
Wanasias wengine wa Marekani wako waliosema matakwa ya Trump kuhusu Gaza hayatafanyika na hayatekelezeki.Wapalestina wenyewe wamemwita raisi huyo kuwa ni mwendawazimu.

Trump anaweza asimalize muhula wake, ana maadui wengi san ndani na nje ya nchi
 
Kwahiyo unategemea Democrats wamsifie Trump? Huyo ndio keshakuwa Rais wa US wamvimilie tu wasubir muda wake uishe wamchague mwingine
Tatizo ile Kauli yake atamm naamin ni Utani na alitaka kuwafuraisha Walokole wenzie duniani lkn!!!! Lkn apo apo imewaudhi wapenda Haki Duniani akiwemo uyo AI Green

ndio mana kasema sijali chochote lkn nitasimama kwaajili ya Haki!!! Kaule ile kaitoa Tramp kipindi kibaya kwa mtazamo wangu kwamaana bado Duniani imechukizwa sana na picha Walizoona zikikanyaga Utu wa Binadam

kias ya kuokota unga barabarani lkn picha Za mauaji ya watu wengi zimewaudhi watu wengi wapenda Amani Duniani kwasasa Tramp akisafiri popote atakutana na Wapenda aman wenye chuki kali dhidi yke
 
Wanasiasa waliokuwepo ukumbini wakati Trump akisema hayo kama hitimisho la mazungumzo yake na Netanyahu hapo majuzi baadhi yao walificha nyuso zao kwenye mikono kutokana na haya waliyoipata kwa tamko hilo la raisi wao.
Kuna wanasiasa nchini Ireland na mataifa mengine ambao wametoa matamko makali ya kumdharau Trump kwa matamshi yake hayo.
Zama za maamuzi magumu😆😂🤣
 
Wanasiasa waliokuwepo ukumbini wakati Trump akisema hayo kama hitimisho la mazungumzo yake na Netanyahu hapo majuzi baadhi yao walificha nyuso zao kwenye mikono kutokana na haya waliyoipata kwa tamko hilo la raisi wao.
Kuna wanasiasa nchini Ireland na mataifa mengine ambao wametoa matamko makali ya kumdharau Trump kwa matamshi yake hayo.
Zama za maamuzi magumu😆😂🤣
 
Back
Top Bottom