KERO Mkandarasi anayechimba mchanga Mto Tegeta anaharibu eneo kubwa la barabara, TARURA wapo kimya tu

KERO Mkandarasi anayechimba mchanga Mto Tegeta anaharibu eneo kubwa la barabara, TARURA wapo kimya tu

Hii ni kero ambayo mwananchi ameiwasilisha JF akitaka wahusika kuchukua hatua
A

Anonymous

Guest
IMG-20240515-WA0446.jpg

WhatsApp Image 2024-05-15 at 20.59.06_dba132c8.jpg
Asante sana JF kwa kutupa Wananchi platform kama hii za kueleza kero, dukuduku na mengine yote ambayo inaweza kuwa ngumu kuyafikisha kwenye mamlaka mbalimbali za binafsi na Serikali hasa kwa sisi Wananchi wa kawaida.

Kero yangu ambayo pia naweza kusema ni kero yetu inahusu mamlaka ya Wakala wa Barabara Mijini na Vijijini (TARURA).

TARURA wameshindwa kusimamia Sheria ya Uzito wa Barabara na kumruhusu mkandarasi anayechimba mchanga katika Mto Tegeta kuharibu eneo kubwa la Barabara ya Mkupita katika Kata ya Goba pamoja na pacha wa barabara hiyo kupitia Uwanja wa Nyala kuelekea Mto tegeta wanakochimba mchanga huo.

Hali hiyo imesababisha kero kubwa kwa Watumiaji wa barabara hiyo na kukwamisha ufanisi.

Mara kadhaa sisi Watumiaji wa njia hizo tumekuwa tukupata wakati mgumu kupita ikiwemo kuchelewa kati mishe zetu kutokana na changamoto hiyo.

Picha zaidi:

6cb87a38-32a3-459f-b26a-8c4567f62921.jpeg

76f8d895-126d-417c-94b1-c3bf6640d94d.jpeg

53b46260-267d-4e12-8e62-2ad691a91054.jpeg
 
Mm naona shida hapo sio huyo mkandarasi Bali shida ni hao TARURA kwa kutokarabati barabara hiyo maana kama amepewa kibali Cha kuchimba mchanga maeneo hayo mnataka apite wapi angani ama?
 
Sio kosa lake, anailipa serikali kodi kama sheria zetu zinavyohiyaji, ila serikali yetu imeshindwa kujenga miundombinu rafiki kwenye eneo lake la biashara. Huo ni uzeeeembe wa serikali yako. Sio kosa la mwekezaji
 
Hayo madude kwa barabara za mtaani ni noma. Hata kwenye lami kuna barabara nyingi tu hayaruhusiwi.
 
Hii nchi ni kichwa cha mwendawazimu. Kuna ile barabara ya Slipway/Yatch club Masaki,imeharibiwa na malori yanayohudumia site moja ya ujenzi wa mall kule. Zipo barabara nyingi za mitaa zinaharibiwa na malori yanayoleta mchanga/kokoto/saruji/nondo site.
 
Hii nchi ni kichwa cha mwendawazimu. Kuna ile barabara ya Slipway/Yatch club Masaki,imeharibiwa na malori yanayohudumia site moja ya ujenzi wa mall kule. Zipo barabara nyingi za mitaa zinaharibiwa na malori yanayoleta mchanga/kokoto/saruji/nondo site.
Mkuu huyo lake oil mwanzo alikuwa anapitisha malori ya mchanga maandazi road wakampiga pin wangezubaa kidogo tu ile barabara ingeoza kbc
 
Mkuu huyo lake oil mwanzo alikuwa anapitisha malori ya mchanga maandazi road wakampiga pin wangezubaa kidogo tu ile barabara ingeoza kbc
Huwa najiuliza sana, kama mimi nilieishia la 7B naona chanzo cha barabara kuharibika tangu mwanzo mpaka inaisha kabisa, hawa wasomi wetu wenye dhamana hawaoni?!! Sometimes unawaelewa watu wanaodharau wasomi wa Tz.
 
Back
Top Bottom