Tamko la serikali lililotolewa na Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, Alhamisi, Aprili 24, bungeni Dodoma, kuwa inafuatilia taarifa za tuhuma kuhusu matumizi mabaya ya madaraka dhidi ya viongozi wa Serikali ya Awamu ya Tatu, na iwapo ikithibitika kuwa walitenda makosa, watachukuliwa hatua zinazostahili, linaonyesha kuwa sasa Mkapa anaweza kufikishwa mahakamani.
Taarifa hiyo ambayo Kikwete anaeleza kuwa hatakuwepo katika maadhimisho ya Sikukuu ya Mei Mosi, ilieleza kuwa wafanyakazi wakiipiga vita rushwa, vigogo wanaodaiwa kupokea rushwa watapata wakati mgumu wa kufanikisha vitendo vyao viovu.
Rais amewaomba wafanyakazi wafanye mambo matatu, kwanza, wajiepushe wao wenyewe na vitendo vya rushwa
.wakatae kutumika katika vitendo vya rushwa
na wasaidie kutoa taarifa za rushwa ili zifanyiwe kazi na wahusika wabanwe, inasomeka sehemu ya taarifa hiyo ya Rais Kikwete.