Mkasa wa kusisimua wa Rojaz katika kipindi cha Sitasahau cha Radio Free Africa

Hapa nimemkubali kwakweli akitimiza ahadi Mungu atambariki[emoji23]

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nitarudi

Sent from my SM-A115F using JamiiForums mobile app
 

Mkasa wa kusisimua wa Rojaz katika kipindi cha sitasahau cha radio free africa​



Sehemu ya 10



Michakato ikawa inaendelea huku duka likizidi kupanuka nami kwa upande wangu nikawa bize sana kiasi cha kunifanya kutoweza dukani kwa muda mwingi kwahiyo nikamchukua mmoja wa wanafamilia na kumuweka kusimamia shughuli za pale dukani akiwa kama muuzaji nami nitakuwa nikipita kutazama mahesabu lakini kaka alimzuia na akasema "kwanini tunauliza maswali yasiyo na majibu,kama wewe ni ndugu yetu kweli na unataka tuwe washirika na vitu vyako kweli kwanini unashindwa kutuambia ukweli?" Ilinipa shida sana hiyo na naamini hata wewe leo hauna pesa na watu wanakuna katika maisha ya kawaida siku ukapata pesa katika mazingira yoyote kwa sababu pesa inaweza kumjia yoyote yule,tizama mimi zimenijia katika mazingira haya sikuwahi kuwaza,sikuota ndoto na zimekuja nyingi katika maisha yangu hata wewe utakapopata pesa watu wakaona mabadiliko yako lazima kuna vitu watazungumza,kama hawatazungumza umejiingiza kwenye mambo mabaya,umejiingiza kwenye ushirikina utawatoa sadaka kuna shuhuda shuhuda za uongo watakwambia kuhusu wewe kumbe sio,mimi hizi pesa sijapata kwa njia zozote watu wanaweza wakanijudge nazo,nimepata katika mazingira ambayo nakueleza lakini siwezi kuzungumza,ni vitu ambavyo havizungumziki,nikamwambia kaka "mtakapokataa sitapoteza hata dakika moja,nina uwezo wa kuajiri mtu na nitamlipa tena nafikiri ntafanya nae kazi kwa mazingira mazuri kwa sababu atafanya vizuri na nitamlipa vizuri pia" lakini huyo ndugu yangu yeye alikuwa na utayari "mi nafanya bwana,kaka yeye ndio anazuia mi nafanya bwana" nikamwambia "tulia hapa fanya kazi,hufanyi kazi kama ndugu tu,unafanya kazi nakupa mshahara,wapi unaweza ukapata laki mbili mwisho wa mwezi na nakupa mahitaji yote laki mbili yaani umebaki nayo,chakula nakupa nauli nakupa utapata wapi kazi kama hiyo na natakaka kuona mwendo wako mwanzo na kama utaenda vizuri biashara inalipa ntakuongeza mshahara,tulia ufanye kazi achana na maneno ya kaka".

Nilizidi kugawa majukumu kwa sababu kuna jukumu kubwa liko mbele yangu,kuna biashara kubwa iko mbele yangu sasa ambayo naenda kuitazama,sikuishia hapo kwani nikaenda tena kwa yule mama ambaye ana watoto wa yule mshkaji kule gerezani,nilienda kama nilivyosema mapokeo ya yule mama yalikuwa yamebadilika sana ,pesa imefanya mapokeo ya mama yabadilike,mama sasa hivi anatabasamu na anaongea na mimi kwa sauti tofauti kabisa na ile ya mwanzo,yaani sasa hivi naipata sauti flani nzuri nzuri kwa huyu mama na nakumbuka sana nilipofika kwa mara ya pili kwani mara ya kwanza nilimwambia ntafika kuchukua majibu na nikawa busy nilipopata nafasi nikaenda tena hadi aliniandalia chakulaπŸ˜‚! Unaona? Pesa inakupa heshima,inakupa kibali,pesa inakupa vitu ambavyo hauwezi kuvipata kama huna pesa,ni kweli kabisa,nikapata chakula nikafurahi nikiwa na hawa watoto na nikamwambia "vipi kuhusu mawazo ambayo nilishea na wewe" akanambia "lolote utakalosema mimi nimeona iwe sawa,iwe sawa kwani siwezi kujua uliishi vipi na mzazi mwenzangu,siwezi kujua lakini ninachojua umekuja kwetu kwa mema tu" nikamwambia "ni kweli nimekuja kwa wema tu" nakumbuka tulizungumza mengi na akanipa michakato ambayo anataka kuifanya akasema yeye anapenda mambo ya vinywaji,anapenda mambo ya vinywaji yaani akifungua kama glocery inaweza ikamfaa,mimi nikamwambia "usiwaze kufungua glocery waza kufungua bar kubwa kabisa" akasema "kweli mi nifungue bar? Nimiliki bar ntaweza wapi?"

Nikamwambia "kwani wanaoweza wanawezaje,hata wewe utaweza" akasema "sijui,ntawezaje kupata huo mtaji wakuweza kufungua bar kubwa" nikwamwambia "wala usiwaze kuhusu hilo,kwenye bar uwa kuna namna yake unaweza usichukue bar nzima,unaweza kuwa na wenzako wewe ukachukua eneo la vinzaji wengine wakachukua eneo la chakula inategemea vile nyie wenyewe mnajipanga" akanambia "una mawazo kweli mazuri,umeniwa wazo zuri na umenipa akili nimekuwa sasa hivi nawazawaza vitu vingi lakini nimeona eneo la vinywaji mimi linanitosha kabisa lakini mtaji wake ni mkubwa sijui yani,sijui kama itawezekana" nikamwambia "wewe sema unachotaka,hicho unachotaka mimi kwangu itawezekana" aisee mama alifurahi sana,mama alifurahi sana kwa sababu sasa nimeshamaliza nataka kuondoka mama anatamani nibakiπŸ˜‚! Nabaki nafanya nini? Nabaki nafanya nini kwa huyu mama,nikamuaga na nikamuahidi ntakapokuja awe na majibu na ikiwezekana atafute hilo eneo liwe zuri,asitafute eneo ambalo hakuna biashara,atafute location nzuri nami nikamuahidi "nami nazidi kukutafutia uko kama nitapata eneo zuri nitakujuza mapema" tulizungumza na huyu mama haya manen kwa uzuri kabisa lakini najua huyu mama ana maswali mengi sana lakini alipokea ombi langu nililopeleka kwake.

Nakumbuka nimeondoka na kuendelea na mishe nyingine huyu mama akaanza kunitumia meseji "vipi Rojas uko poa? Wadogo zako huku ni wazima kabisa wanakusalimia sana" hakuishia hapo akawa ananipigia simu niongee nao,"ongea nao basi" nikamwambia "sawa" naongea nao nikawa mwenye furaha napiga nao story lakini akawa ananipigia simu majira hata ya usiku,majira hata ya usiku wa saa 4 ananipigia simu unaona,na hii ni nilipotoka round ya pili hii ambayo nilienda kuzungumza nae kuhusu kutafuta eneo la bar na nini,simu za usiku ananipigia ananiambia nini? Ananisalimia,ananitakia usiku mwema,basi tutaongea asubuhi,uko na nani,ananitumia meseji au tunazungumza kwenye simu na mazungumzo kama hayoπŸ˜‚

Mimi najua huyu mama anapotaka kwenda na kama nilivyosema awali kuwa pesa inaweza kumbadilisha kabisa mtu mawazo na kwa mtu unampa kwa lengo wewe wewe unalolijua na silo analowaza yeye,yeye anawaza vitu vingine kwa sababu huyu mama kwa jinsi nilivyoongea nae anavyowaza labda mimi nimefall in love na yeye,ndivyo akili yake ndivyo inavyomwambia na labda anaona ninavyoonesha nia yakutaka kumpa mtaji basi kabisa kwanini asiwe na mimi,ndivyo nilivyoendelea kuisoma akili ya huyu mama lakini mimi wala siko uko,yaani sijawahi kumtazama kwa huyu mama kwa umakini,sijawahi,yaani namuona ni mama ninayemheshimu,sijawahi ku pay atention kutazama chochote kuona kitanivutia kwenye upeo wa macho yangu kwake hata siku moja,nazungumza hiyo kwa ukweli kabisa,sijaona chochote kwa sababu nimebeba ile heshima ambayo mshkaji alinambia na mimi niko karibu na huyu mama kwa ajili ya hawa watoto ili nitimize ahadi ambayo rafiki yangu alinambia,nikasema ni akili zake tu ataelewa,atanielewa baadae wala sina haraka na hili.

Wakati michakato ikiwa inaendelea nikapata bahati kwa sababu niliwaambia watu wanitafutie eneo ambalo naweza kufungua bar,kuna mtu akanipa hiyo taarifa na nikamwambia huyo mama kuna eneo nimepata naye akanambia kuna eneo amepata akanambia "njoo Rojas ungekuja kwanza kuliona hili" nikamwambia sawa nikafunga safari nikaenda kuliangalia nikamwambia "sawa lakini lile mimi nililoambiwa naliona ni bora zaidi na ukilipenda wewe mwenyewe utakuwa na choice" akanambia "sawa" kweli tulienda pale na uzuri huyu mama ana uelewa sana yaani ameishi kwenye ulevi mpaka akawa na experience kubwa sana kwa sababu huyu mama ni mlevi mlevi sanaπŸ˜‚. Tulizungumza mengi hapa na makubaliano tulizungumza nao hapa katika hii bar,walizungumza mambo ya biashara,mwanzo wa kufanya biashara kilibainika nami ikabaki ni kutoa tu pesa sawasawa na uhitaji wa huyu mama aliokuwa nao na nakumbuka tumezungumza sasa tumerudi nimdrop mahali ili mimi niendelee na mishe zangu nakumbuka huyu mama akanambia "sijawahi katika maisha yangu kukutana na mtu akanisuprise kama ulivyonisuprise wewe,yaani mpaka natafuta eneo hadi wenzangu wananiuliza ni nini umekutana nacho,ni muujiza gani nimekutana nao,wananiambia mimi ni muongo,nawaambia ni rafiki wa mzazi mwenzangu wananikatalia wanasema wewe ni mtu wako" nikamwambia "huna hata sababu ya kujieleza kwao kwa sababu hata ukijieleza,hata ukijitetea watakuwa na majibu yao ila wewe baki na unachokijua kuwa ni rafiki wa mzazi mwenzio,mimi ninachokuombea ni ufanikiwe,unajua biashara haitaki uweke mbele urafiki na usipageuze pale marafiki wanakuja wanakunywa wanakopa" akasema "siwezi kufanya hayo makosa,nimeangaika sana kutafuta mtaji,siwezi kufanya hayo makosa yaani siku unanipa pesa na kusema nifanye biashara na ndio mwanzo wa mimi kutoka katika umaskini,sitaishi tena kuwa mwanamke wakuombaomba,sitaishi tena kuwa mwanamke wa kukutana na mtu aniambie kwamba atanipa pesa niende nikampe furaha,sitaishi tena hayo maisha kwani nimekuwa nikiangaika kwa ajili ya watoto wangu ili wale,ili wavae na ndio maana nimekuwa hata na tabia ambazo najua unajua" nikamwambia "hata wala mimi sijakuhukumu kwa chochote kile naamini hata iki unaenda kusimama nacho kitawafaa pia na watoto" akasema "kabisa,nakushukuru sana" nikamwambia "sawa,kesho ntapita benki na nitakuletea pesa zote unazozihitaji" akesema "kweli" nikamwambia "kweli namaanisha" nilizidi kumchanganya akili ya huyu mama kiukweli nikachanga akili yake isivyo kawaida.

Hapo mimi sikuwa na ukaribu na wanawake kwa kiwango hiki nilicho karibu na huyu mama,nikizungumza hivi najua unaelewa yaani ule uclose wa kuzungumza hivi,mishemishe kama hizi tunatafuta,tunawasiliana,tunaongea,kwa maeneo kama haya yaani ulezi wa mtoto,malezi kwa ujumla sijui nini kwa mara yangu ya kwanza yaani nayaishi hayo,akinambia "watoto wananini,wanahitaji sijui nini yaani moja,mbili,tatu" siunajua hayo ni mambo ya watu wa familia nami bado ni kijana sikuwahi kuishi hivyo,niliachana na huyu mama nami nikaendeleatna michakato yangu kama kawaida.

Nazidi kukimbizana na nikamkamilishia ahadi yake ya pesa yule mama,nilienda kumpa taarifa mshkaji wangu kule gerezani nikimjuza hatua jinsi nimepiga,jinsi ambavyo nimefanikiwa nilimweleza yote "vipi na suala la kuwahamisha kutoka pale wanapoishi kwenda kwenye nyumba nyingine?" Nikamwambia "yote yatakamilika" akafurahi sana na akanambia "kuwa mwangalifu sana na yule mwanamke anapenda sana hela na kwenye hela yule mwanamke anaweza fanya chochote,usije ingia tamaa nae kwani ni mwanake ambaye hajawahi kuwa na utulivu,asije kukushawishi kwa sababu ameona umeanza kuwa na pesa ukajikuta siku umedondoka nae,nakutahadhalisha kwa sababu nakupenda kwani mwanamke mwenye kubadilisha wanaume kama nguo hafai,si ni kweli?" Nikasema "ni kweli,hawezi kufanikiwa kwangu na nimeshamjengea mazingira mazuri sana kwenye akili yake naamini mpaka sasa ameelewa siko upande huo" akasema "ameshakutegatega eeh?" Nikamwambia "sio sana" akasema "lazima ulishinde hilo jaribu mtu mzima yule" nikamwambia "ni kweli " mengi nilimueleza na nikamwambia harakati zote zinazoendelea na alizidi kufurahi sana,alinambia lakini nisimsahau yule mwanamke niwe naenda hata kumjulia hali na nimsikilize nini anawaza ambacho tunaweza kumfanyia,nikamwambia "sawa,hivi ni hawa tu katika maisha yako unaowathamini uliwaza ukifanikiwa katika maisha utawafanya wawe bora zaidi na vipi kuhusu shangazi yake kule kijijini?" Akasema "sasa hayo nakuachia wewe" nikasema "unaniachia mimi vipi wakati hao ni ndugu zako?" Akasema "kama uliguswa na shangazi kwa sababu ya mapokezi yake sawa lakini mbona mimi hawaji kunitembelea? Si kwa sababu wanajua sina kitu,si wanajua nitaozea gerezani? Si hata kama mmoja angetokeza ungechukua hata milioni kumi ukampa imfae kwa biashara lakini wameniacha huku wanajua mimi nimeisha sasa mimi naweza ninkfanyaje,eti Rojas nifanye nini sasa,kama kuna siku kuna mtu ataamka kuja kunitembelea nitakwambia umpe pesa" tukacheka sana na akaniuliza "na wewe vipi kuhusu ndugu zako" nikamwambia "nina changamoto kubwa sana lakini sio kubwa kiasi nishindwe,nitasonga tu" akasema "ahadi yangu itunze,usimwambie mtu siri hii" nikamwambia "nakumbuka sana na nitaitunza siku zote za maisha yangu mpaka siku utakapotoka,utakapokuwa huru tena na tukaungana pamoja" akasema "naingoja kwa furaha sana siku hiyo" nikamwambia "lakini vipi kwa hizi pesa tulizopata haziwezi kubadilisha chochote katika hukumu yako?" Akacheka na akasema "natamani iwe hivyo Rojas lakini nimepoteza matumaini sijui kuna muujiza gani mbele yangu,sijui,sitaki hata kuyazungumzia hayo" nikamwambia "sawa,basi tutangea wakati mwingine" akasema "basi usichelewe sana hata kuja kunisalimia tena najua kuna kipindi utakuwa busy hutakuwa huji kabisa" nikamwambia "haiwezekani lazima nitakuja na nikikumbuka mafanikio yangu kuna mtu hiyo sauti tu yatosha kunikumbusha mi kuja" akanambia "Rojas wajua wewe ni mtu mwema sana,moyo wako ni wenye utu ndani yako lakini endapo ukishea na watu mambo yako ya sirini sana watu watageuza moyo wako utakuwa mbaya kuliko kawaida,basi endelea kutunza wema wako na siri zako ili watu ili wasiweze kukuharibu" kiukweli sikuweza kuelewa kwanini mtu huyu amekuwa akinisisitiza sentensi hii mara nyingi,hii sentensi amekuwa akiniambia toka nikiwa ndani gerezani kwamba watu ni wazuri wengine wana mioyo yenye utu ndani yao lakini watu wanawabadilisha kwa maneno,kwa kuchochea vitu vyenye hila ndani yao,watu wale wanabadilika na kuwa wabaya.

Nimekuwa nikikimbizana sana,michakato imekuwa mingi sana na ukiwa na pesa kuna connection ya watu wenye pesa wanakuja kwako,iki ni kitu cha ajabu sana kwani wakati nikiwa sina kitu watu niliokuwa nazungumza nao,watu waliokuwa wananisogelea katika maisha yangu ni watu wa hali ya chini sana yaani ni mtu ambaye hauwezi hata kumuomba hata kiasi flani cha pesa kwa mfano nikiwa hata na simu naweza kumkosa mtu wa kumpigia kumuomba hata elfu kumi,hao ndio watu waliokuwa wamenizunguka lakini wingu la pesa limekuja katika maisha yangu yaani kuna watu wanakuja kwangu wenye pesa,wenye kuzungumza habari ya pesa,wenye kuzungumza fulsa ya biashara flani,nami maombi yangu kila mtu apate pesa,kila mtu apate pesa kwa mazingira yoyote yale pesa ije kwenye maisha yako,vitu vinabadilika sana kwani hauwi kama mwanzo,ongea yako inabadilika,tembea yako inabadilika,akili zako pia zinabadilika,kuwaza kwako kuna badilika,yaani vitu vyako vinabadilika haviwi kama kawaida.

Nikapata mtu alinambia "kama una hela na uzidi kuwa na hela zaidi kuna eneo la kuwekeza pesa" akanishauri niwekeze pesa kwenye eneo la madini,sasa huo ni mwanga mpana sana,ni mambo makubwa sana mengine sitaweza kuyazungumza yote kwa upana lakini alinambia "chungulia huku uone jinsi michakato inavyofanyika na jinsi watu wanapata pesa,ukiwa na pesa unaweka pesa unapata pesa" mengi nilielezwa nami nilivutiwa sana na uko "nikasema basi ntachungulia uko" mimi ni kijana nimekuwa nikiendesha taxi na sina elimu kubwa ni elimu yangu hii yakujipambania katika maisha lakini nina neema ya kujua jua vibiashara biashara hivi,naona kuendesha taxi kulifanya akili yangu kukua kwa haraka kwahiyo akili yangu sasa inatizama wapi nitupe pesa wapi wapi nitupe pesa,tulifanikiwa kupata magari matano kwa pamoja na yote tukayafanya taxi ambayo yote yalikuja kwa pamoja,yalipofika tu jambo la kwanza kulifanya ni kwenda kule gerezani na kwenda kumwambia habari hizi,nikamwambia "hizi gari ni za kwako" akasema "hapana hizi gari ni za kwako Rojas,kwa sababu hauwezi kuandika jina langu,utaandika majina ya watoto wangu" nakumbuka sana hii sentensi, alinambia "Rojas katika vitu ambavyo unafanya sitakwambia vyote uandike kwa majina ya watoto wangu,tutakuwa tunagawana au unasemaje?" Sikupinga katika maneno haya, basi akanambia "basi katika magari haya mawili tu andika majina ya watoto wangu" nikamwambia "unajua bado uko gerezani na michakato ya nje bado haujajua,kuna process za hapa na pale,kuna vitu vya kuandika nitafanya hivyo lakini kama umekuwa ukiniamini mimi mtu mwema sawasawa neno lako ntalibeba na ntalifanyia kazi" tuliongea mengi na akanipa ushauri kuhusiana na biashara na akanambia "wewe ni mimi,wewe ni mimi niko uraiani sasa,ninafurahia kila hatua yako" nikamwambia "ahsante,nashukuru sana" mimi nimekuwa nikija huku gerezani mara kwa mara kuja kumpa feedback ya nini kimekuwa kikiendelea.

Familia yangu ilizidi kushtushwa mpaka nikaitwa na vikao lakini nakumbuka siku moja kaka yangu alinambia "mdogo wangu njoo tuongee" awamu hii kaka alizungumza mpaka alitokwa na machozi "kama ni mafanikio mdogo wangu mimi sikatai,mimi ni kaka yako sdna neno moja nipate amani moyoni mwangu,tunaangaika,tunateseka,unatusaidia ni kweli lakini sitaki mdogo wangu jambo baya likutokee,sitaki shida ikotekee kwani unajua jinsi ambavyo tunavyokupenda na jinsi ambavyo nakupenda,nimejitoa kwa mangapi kwa ajili yako,kuna siri unanificha mimi?" Unajua huyu kaka yangu na mpenda sana,alilia kwa machozi sana na nikaona SIWEZI KUMFICHA KWELI KAKA YANGU,naweza kuwaficha wote lakini kadri siku zinavyoenda naona hapa panazidi kuwa pagumu kwa kaka ndipo niliposukumwa kutamani kusema ili kaka awe na amani katika hili.



ITAENDELEA!
 

Mkasa wa kusisimua wa Rojaz katika kipindi cha sitasahau cha radio free africa​



Sehemu ya 11



Moyo wangu unatunza siri na moja kati ya vitu nilimuahidi huyu kaka kule gerezani ni kuhusiana na kutunza siri,niliifanya siri hii kuwa ya sisi wawili peke yetu na yeye akiniambia "nimekupa siri ya maisha yangu sijawahi kumpa mtu yoyote hii siri mahali nimetunza pesa sikuwahi kumwambia mtu na ndio maana kile kijumba watu hupita na pengine wengine uenda kufanya shughuli zao uko na hawajawahi kujua chini ya ardhi ziko pesa nyingi,mimi nikamuahidi ya kwamba nitaitunza siri hii lakini kaka amezungumza nami katika lugha ya urafikiya undugu kabisa,nasikia moyoni mwangu angalau niweze kusema nae jambo,nikamwambia kaka "kuna vitu ni vigumu sana hata kusema,naogopa hata kusema" kaka akanambia "ni kitu gani mdogo wangu kama ni cha hatari niko tayari hata mimi kuingia kukusaidia sitamani kukuona unapata matatizo,unajua" nikamwambia "kaka najua" nikaketi na kaka na nikamwambia "hii ni siri,ni siri ambayo sijawahi kutaka kumwambia mtu yoyote yule" kaka akanambia "hata mimi ntaifanya kuwa siri kwa sababu wewe mdogo wangu umetaka iwe siri,niambie" ndipo nilipoanza kumwambia kaka ila nilimwambia kwa uchache sikumueleza kwa upana kama safari ya huyo mtu na mimi ilipoanzia,nilimwambia "kaka ni kweli nina pesa,unaona nafanya maendeleo haya unaona ninavyoagiza magari,unaona jinsi nimefungua biashara yaani kufungua duka la jumla na nimeweka pale kiasi cha milioni ishirini,ni kweli nina pesa lakini kaka hizo pesa si zangu,ni pesa za mtu na huyo mtu amekuwa anatamani kufanya makubwa sana lakini yeye amekosa hiyo bahati ya kuishi maisha ambayo mimi naishi ya uhuru" kaka anakanambia "una maanisha nini,ni nini ambacho unamaanisha? Ni mtu gani ambaye kakosa uhuru,ni vitu gani unazungumza,nikamwambia "kuna mtu amenipa majukumu ya kumfanyia vitu vyake kwakuwa yeye hawezi kufanya hivyo" akanambia "ni nani huyo na kiasi gani cha pesa akupe hata uweze kuagiza magari mengi kiasi hiki na hizo pesa unaweka wapi mwisho wa siku uweze utahatarisha maisha yako na hizo pesa unazijua amezitoa wapi? Kaka alinihoji kwa kuonesha kunijali sana na ni kweli kaka ananijali sana,nikamwambia "mtu huyu yuko gerezani kaka" kaka akashangaa sana "yupo gerezani? Sasa mtu yupo gerezani anawezaje kukupa wewe pesa? Nikamwambia "kaka ni stori ndefu sana ila elewa niko na pesa ila si za kwangu,mtu huyo yuko gerezani anatumikia kifungo na ameniomba nimsaidie kufanya hivi vitu nikiwa uraiani,kwahiyo nimechukua majukumu yake nafanya vitu ambavyo yeye alitamani kuvifanya ili siku moja akitoka gerezani aone hatua ameshaipiga kuliko pesa kuendelea kukaa sehemu bila kuzalishwa" nakumbuka kaka alinambia "kwahiyo umekaa chini na kunitungia kastori,umenitungia kasimulizi kakusadikika flani hivi,iko kitu kinawezekanaje? Hakuna kitu kama iko unanidanganya" nikamwambia "kaka nilihisi hata nikikwambia hautaweza kuniamini" akanambia "ni nani uko gerezani,ni nani ambaye awe na pesa hizi akupe wewe,hana ndugu? Hana watu wa karibu akupe wewe?

Nikamwambia "kaka huyu ni mtu ambaye yuko gerezani ana muda kidogo lakini ndugu zake walimtelekeza uko gerezani,hakuna watu wamekuwa wakienda kumwangalia hata kumtia moyo,hakumuona mv wa kumpa hilo jukumu,kipindi mimi naenda gerezani na nikaanza kuwa na urafiki naye ndio kipindi aliniamini nakuniona ni mtu mwema na akaniomba kama naweza kuwa mwaminifu kwake,ndicho kaka kilichotokea" kaka akaniuliza "ndio mwenye wale watoto uliokuwa ukijipa stress? Nikamwambia "ndio kaka" kaka akaanza kuamini katika nnachokisema baada ya kuendelea kumwambia lakini kaka aliyashangaa sana haya maelezo ambayo mimi namwambia nakumbuka sikutaka kumuweka kaka kiundani zaidi niliongea hayo tu kwa uchache,aliniuliza "pesa ziko wapi? Nikamwambia "kaka siwezi kukwambia" akasema "mimi ni kaka yako" nikamwambia "kaka naweza kukwambia vyote lakini nilimwambia mtu huyo sitasema kwa sababu ni maelekezo yake aliyonipa,kama nilivyokwambia kaka hizi pesa si za kwangu ila yeye aliniruhusu nifungue duka,lile duka la nafaka ni la kwangu lakini kuhusu magari sio ya kwangu,hivi vitu vingi sio vya kwangu"

Nilimueleza kaka yangu kwa upendo kabisa kwa sababu huyu ni kaka yangu na niko nae karibu sana katika mahangaiko yangu,katika mateso yangu kwa mfano kipindi kile nimekwenda gerezani ni kaka ndio alinipigania mpaka hatua ya mwisho akunyamaza,hakutulia mpaka alipoona mimi mdogo wake nimeachiwa huru kwahiyo yupo na mimi siku zote kwahiyo naamini nimemwambia kaka yangu naamini nimemwambia mtu sahihi,nilishea na kaka hayo na kaka alizidi kuniuliza maswali lakini sikujibu yote kwa sababu sikutaka kuzungumza kila kitu,aliniuliza "sasa ulipataje hizo pesa,alizihifadhi wapi?" Hayo yote aliniuliza lakini sikusema.
Baada ya kumwambia kaka hayo maneno nakumbuka niliporejea nyumbani nilisikia moyo wangu unauma sana,nilisikia moyo wangu unapatwa na uchungu kwanini nimesema,nilijilaumu kwanini kinywa changu kimezungumza siri ambayo nimeitunza kwa ahadi kuwa nitaitunza na sitaisema,mbona naumia hivi nami naona nimemwambia mtu sahihi,mbona nimemueleza kaka yangu kwanini nasikia hivi vibaya? Sikulala mpaka asubuhi,ushawahi kufanya jambo alafu ukawa unajilaumu kwanini unafanya? Mimi nilisikia hatia ndani yangu kwanini nimemwambia kaka,kama ningenyamaza kwani nini kingetokea,angenifanya nini? Niliona nimekosea,sikutakiwj kufanya hivyo.

Lakini unajua neno linapotamkwa linakuwa lishatamkwa unakuwa hauna namna yoyote yakuweza kulifuta tayari linakuwa lishatamkwa,nakumbuka kulipopambazuka na siku mpya kuingia kaka alinitumia meseji ikisema Rojas nataka tuongee,naomba nije nyumbani kwako tuzungumze,nilikuwa na ratiba za mishe zangu za hapa na pale lakini kaka yangu namheshimu sana na kama anasema ana jambo anataka kuja nyumbani litakuwa ni muhimu sana,nikamwambia kaka sawa na kaka alikuja nyumbani akanambia "mdogo wangu sijalala usiku kwa maneno uliyoniambia nimekosa usingizi,sijajua uko katika hatari kwa kiasi gani sijui lakini tu kwa experience yangu ya maisha,kwa maisha mimi nimeishi,mimi ni kaka yako najua vitu vingi,napata mashaka sana,nasikia kukosa amani sana kuhusiana na kile umenieleza jana lakini kuna kitu nimesikia amani nacho ndani ya moyo kwa sababu umesema huyo mtu yuko gerezani na hajawahi kumwambia mtu yoyote kuhusiana na hizo pesa,sasa mdogo wangu mimi najambo nataka kukwambia,mtu yupo gerezani na pesa unazo wewe uraiani unajua anatoka lini? Sikujua kaka kwanini ananiuliza maswali kama haya tena akiwa siriasi kweli amefunga safari tuje tuzungumze kuhusiana na hili na nikamwambia "kaka, sijui labda kuna neema itakuja ya yeye kutoka au pengine hiyo neema isipotokea uenda maisha yake yote akamaliza gerezani" "kwani amefungwa kifungo cha maisha? Nikamwambia "kaka kesi ya huyo mtu ilikuwa ngumu sana kwa maelezo ambayo nimepata,alinambia ni miaka 30 lakini nikaja nikagundua yule mtu amefungwa maisha" akasema "amewezaje kukudanganya wakati ni rahisi tu kujua miaka ya mtu" nikamwambia "unamaanisha nini? Akasema "mimi naweza kuifanya hiyo kazi nikajua miaka yake ambayo anatumikia uko gerezani,yaani tujue miaka yake ni mingapi,ni wa kutoka au siwakutoka kwa sababu hapo tupate uhakika" sasa nikawa najiuliza kwanini kaka azungumze hivyo,nikamwambia "yanini kuyajua hayo kwa sababu mimi nimemshauri kitu kwa sababu anazo pesa nyingi alizitafuta katika nafasi yake akiwa uraiani na pesa inanguvu nami nilimshauri ikiwezekana sehemu ya pesa yake ebu atumie uenda akaupata uhuru kwa nguvu akarudi huku uraiani kama ni rushwa au namna yoyote ile itakavyowezekana" nakumbuka kaka akanambia "wewe umshauri maneno kama hayo kwanini? Nikamwambia "kaka ni mtu mwema tu" akanambia "unajua hizi pesa amezitoa wapi? Nikamwambia "hajawahi kunieleza wapi alipozitoa" akanambia "hawa ndio watakuwa watu ambao ni wahujumu uchumi" nikamwambia "unamaanisha nini? Akanambia "kuna watu ambao walijilimbikizia pesa lakini kuna nyakati kuna msako uwa unapita na watu uhofia kuhusiana na hizo pesa kwa sababu hawaziweki benki wanaogopa,watu wengi kumekuwa na historia walikuwa wakichimbia pesa ardhini,vipi hizi pesa hakukwambia ukazichukue ardhini?

Nikashtuka,nikamwambia "kaka kwanini tunazungumza haya na wakati tulishazungumza jana na tumeshamaliza kwa sababu niliona nikushirikishe kaka yangu" akasema "ah umenishirikisha ila wewe bado mdogo hujui vitu vingi mimi ni kaka yako,sasa mimi ni kaka yako mimi najua maisha na najua vitu vingi,unajua ni kwanini huyu mtu kakutafuta wewe? Kwanini uwe wewe ushawahi kujiuliza? Hana watu ambao ameshawahi kufanya nao dili? Hawapo? Kwanini iwe wewe? Unajua kwanini? Nikamwambia "ndio najua" akaniuliza "unajua nini? Nikamwambia "najua kwakuwa tulikuwa marafiki,tuliishi kwa furaha na akaona mimi ni mtu ambaye sina shida yoyote" akasema "sio kweli,iko sababu nyuma ya huyo mtu kukutafuta wewe" sasa mimi kweli uenda kaka yangu ana upeo mpana na akili nyingi kuliko mimi siwezi kataa,sasa mimi namuuliza kaka "kwa sababu zipi? Anasema "si unaona hujajua kwanini akutafute wewe,ngoja nikwambie mdogo wangu mitego ya pesa ni mikubwa sana,waweza pesa itumia leo pesa isiyo halali inaweza ikakuletea shida hata baada ya miaka 10 baadae inaweza ikakuhukumu,ikawa kitanzi kwako,ikatesa moyo wako na maisha yako na ndugu zako" nikamwambia "unamaanisha nini" akasema "pesa hiyo siyo halali,hiyo pesa ni pesa haramu na amefanya hivyo ili siku hukumu ikija ikukute wewe na yeye akiwa pembeni ametulia" nikamwambia "sasa litampata vipi mtu aliye gerezani" nakumbuka kaka akanambia "ndio maana nakwambia wewe bado mdogo,uelewa wako bado mdogo haujajua kuchanganua mambo,usalama wako Rojas ni kukata kila connection ya wewe na huyo mtu wa gerezani na kukata connection na majukumu yote aliyokupatia na hizi pesa zisiwe chini yake,ziwe ni pesa zako sijui kama unanielewa? Kaka alinambia maneno hayo tena ni siku ya pili tu yaani nimemwambia jana na leo ananiamkia asubuhi kumepambazuka kaka anakuja na ujumbe kama huu,nikamwambia "kaka mimi Rojas siwezi kufanya kitu kama hicho,siwezi kufanya kama hivyo,siwezi kutumia pesa isiyo ya kwangu kuifanya ya kwangu siwezi,siwezi kaka kufanya hivyo,ahadi niliyompa mtu huyu nitaitimiza siku zote siwezi kuikengeuka hata kiku kimoja maana nimetafuta pesa katika nyakati zote sikuwahi kupata kwanini nimsaliti mtu ambaye amekuwa mwaminifu kwangu ambaye ameamua kunitunuku na kunitoa katika umaskini nakunipa maisha mengine,kwanini kaka unazungumza maisha ya ushetani hivyo" nakumbuka kaka akacheka na akasema "ushetani? Mdogo wangu kweli hauyajui maisha? Nazungumza mambo ya maana wewe unasema ushetani mimi nazungumza ushetani?" Kiukweli sikupenda kabisa kauli za kaka kabisa na nikamwambia "ndio maana moyo wangu umekosa amani kabisa kukushirikisha,hukustahili kunambia maneno haya tena ikiwa mapema kama hivi" akanambia "nakwambia mapema kwakuwa wewe hujui,wewe bado mdogo hujui kadri unavyozidi kwenda gerezani,wewe si kila siku uwa unaenda gerezani mwisho wa siku utastukiwa,huyu mtu bado anafatiliwa kule gerezani usihisi watu wametulia kumfatilia nisikilize mimi ninachosema" kaka akanambia "huyu ni mhujumu uchumi hawezi kukwambia na mimi ndio nakwambia sasa kwa sababu najua haya mambo ziko nyakati hata wewe ulikuwa bado mdogo kuna watu walifanya hujuma,walihujumu uchumi hawa watu walifanya namna nyingi hawajaacha kufatilia siku mpaka anapokufa ndio huyo mtu ndio wanaacha hivi ninakwambia we si uwa unaenda si una route za kwenda? Unavyoenda watu wameshachora ramani,kuna mtu ana dot dot alikuwa gerezani ametoka lakini anaendeleza ukaribu na huyu mtu,mdogo wangu sasa hivi unakamatwa,unakamatwa na unaniingiza kwenye matatizo kata hiyo connection haraka sana usiende gerezani unakamatwa na ninavyozungumza hivi na pengine si siku nyingi kutoka leo na umezungumza kwangu kwa sababu Mungu hataki upate matatizo"

Kaka anaendelea kunambia vitu yaani mimi naenda gerezani kila siku sikuwahi kuwaza hata siku moja kuwa hizi route za kwenda gerezani ninazofanya labda zinaweza zikawa na ishara yoyote lakini kaka anasema huyu mtu bado yuko kwenye uangalizi kwani amehukumiwa lakini haimaanishi kwamba ameachiwa,huyu bado anafatiliwa yuko kwenye uangalizi.
Toka kaka amezungumza siku ile alinipa hofu,nilianza kuwa nahofu moyoni mwangu kwa maneno kaka aliyoniambia,nakumbuka kama baada ya siku mbili toka siku zile tumezungumza na nikamkatalia kaka akaja na akanambia kitu cha ajabu sana,mimi nilizungumza na kaka na sikuwa nimemtaja mtu kwa majina yake ambaye ndiye yuko gerezani,ambaye ndiye amenipa hili dili na mimi nafanya hivi katika mazingira na sikumuweka kaka kiuwazi sana,kaka alinijia na jina kamili,jina kamili la yule ndugu kule gerezaniπŸ˜‚ na akanambia alikuwa gereza flani na akapelekwa gereza flani,yaani amemjua sasa kuliko hata mimi,kuliko mimi ambaye nafanya nae kazi katika mfumo ambao nimekuambia na akanambia uwa naenda gerezani mara ngapi (akanipa idadi),niliogopa sana na nikamuuliza "kaka umeyajuaje yote haya" akasema "nimejua kwakuwa mimi ni mkubwa kwako,mimi ni kaka yako,najua mambo kuliko wewe,hivi unajua kuna watu pale gerezani kila unapoenda kumtembelea uwa wanarekodi? Unajua wewe mpaka sasa hivi inawezekana umeshaanza kufatiliwa mpaka unavyoondoka asubuhi mpaka jioni shughuli zako unavyofanya na watu unaoongea nao,unajua iko kitu?" Niliogopa sana na kaka akasema "uko unatazamwa mdogo wangu,watu wanakufatilia" nikamuuliza "kaka umejuaje,umeyajuaje haya?" Kwa sababu kaka yangu ni mtu wa kawaida tu,ni mtu wa kawaida kusema amjue hadi mfungwa hivyo mimi nilivyomueleza hadi apate connection na kujua mimi nilienda siku flani na siku flani huyo ni mtu wa namna gani,si unaona unaogopa,unajua hii sentensi ninayokwambia maana yake nini,maana yake yule mtu ni kweli siku zimepita ila bado anaendelea kufatiliwa na amemtafuta mtu mdhaifu mdogo ili isiwe rahisi mtu yoyote kujua lakini mambo yashajulikana,unajua uko katika hatari kwa kiasi gani? Unajua?

Niko hapa kaka yako nataka nikusaidie,nataka nikusaidie,utapata matatizo upigwe kifungo cha maisha,kwanini hajatumia ndugu zake,kwanini akutumie wewe? Maneno ya kaka yalizidi kuniogopesha na labda kutokana na umri wangu sielewi lakini niliogopa,naogopa kwenda gerezani,sitaki kwenda tena uko.



ITAENDELEA!
 
Ndugu zangu jana jioni nilidhani nimeipost sehemu ya 10 kumbe haikukubali na muda huu natizama ndio nagundua hilo,poleni kwa usumbufu na ndio nimetupia vipande viwili,tuenjoy story wandugu!
Ssante cuzo hapo mchanganyo umeanza. Je kaka mkweli au anampoteza maboya...
Naona hela zikienda kuyeyuka, kuna ndugu huwa na wivu mtu akipata pesa. Acha tuone yajayo... barikiwa kwa uandishi cuzo ake.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…