Mkasa wa kusisimua wa Rojaz katika kipindi cha Sitasahau cha Radio Free Africa

Mkasa wa kusisimua wa Rojaz katika kipindi cha Sitasahau cha Radio Free Africa

MKASA WA KUSISIMUA WA ROJAZ:
katika kipindi cha sitasahau cha radio free Africa



Part 3



Maisha ya pale kituo cha polisi yalikuwa ni ya muda mfupi kwani utaratibu wa kimahakama ukafika na nikatakiwa kupelekwa gerezani wakati suala langu likiendelea kupatiwa ufumbuzi,wakati nikiwa gerezani kuna kaka mmoja tulitokea kujenga ukaribu wa kiurafiki nae na akawa msaada mkubwa kwangu katika mambo mengi yaliyokuwa yakinikabili,siku moja katika maisha yetu ya gerezani nikiwa na huyu kaka alinambia "kila nikikutizama macho yako nakuona ni mtu mwema sana" nikamuuliza "mimi?akaendelea "yaani hata wale watu wabobevu wa kufanya uchunguzi,watu ambao ukijitetea wanaona auhusiki ndio wanakubana lakini nakuona ni mtu mwema kabisa"

Nikamjibu "sijui,lakini mimi sipendi ubaya na mtu na napenda amani katika harakati zangu za kila siku" akaendelea "unajua uwa nawatizama watu wengi sana hapa lakini katika wengi sijaona mtu mwema kama wewe" nikamuuliza "mimi?" Akasema "ndio sijaona mtu kama wewe humu,wewe ni mtu mwema na kama haujajua basi siku moja utakapopata neema ya kutoka hapa utajua kama wewe ni mtu mwema itambue hiyo na iishi hiyo kwa sababu una upekee wako" nikahisi ni maneno ya faraja tu ananambia yakunitia moyo,kunisahaulisha tabu zangu na kunifanya nifurahi na kujiona ni wa pekee hata kama niko katika mazingira magumu na vitu kama lakini aliendelea kuniambia anamaanisha kwa kile anachokiongea,nakumbuka nilimuuliza "kwanini wewe uko hapa? Kwani wewe si mtu mwema?" Akanambia "hata nikikuambia hautaweza kuniamini lakini mimi natofautiana na wewe,angalia macho yangu yalivyo je una uwezo wa kumtambua mtu tabia zake,hisia zake na kile kilichopo ndani yake? Nikamwambia "hapana sina huo uwezo" akanambia "basi mimi ninao huo uwezo ila sikuutumia vizuri nikiwa uraiani,mimi sifanani na wewe,wewe umekuja kwa njia ambazo si za haki yaani umekuja kwa sababu kuna watu wamefanya mambo mabaya wamekuingiza na wewe lakini mimi ni tofauti na wewe" nikamwambia "utofauti wa mimi na wewe ni upi? Akasema "ni stori ndefu sana huwa sipendi kuzungumza lakini kiufupi niko hapa natumikia kile ambacho nilistahili,siku nyingine ntakueleza lakini siko hapa kwa makosa hakuna mtu amenisingizia,maisha yangu ya uraiani mwenendo wangu ndi ulionipeleka mimi kuwa"

Nilitamani kujua alifanya kitu gani kilichopelekea hadi yeye kuwa anastahili kutumikia kifungo anachokitumikia,alinambia "niko hapa gerezani natumikia miaka yangu 30 na mpaka kesi yangu inasomwa nimeshakaa miaka mingi" nikamuuliza "umekaa miaka mingapi?" Akanambia "sikuvunji moyo wakati mwingine kuna kesi uendeshaji wake uwa unachelewa kwani kabla ya kufikia hukumu unaweza kujikuta umekaa hata miaka 5" nikamuuliza "hivi mimi naweza kukaa hapa muda mrefu?" Akanambia "inategemea na jinsi kesi inavyoendeshwa,kadri kesi inavyoendeshwa uenda uchunguzi zaidi ukaitajika hivyo kupelekea kuchukua muda lakini nakuombea sana mdogo wangu kesi yako isichukue muda mrefu na uachiwe huru" huyu kaka tulikuwa tunazungumza sana na kiukweli alinijenga sana katika mazingira yale nakunipa matumaini.
Siku zikiwa zimepita siku moja huyu kaka aliniita na tukawa tunazungumza na alinambia"unajua kama ninao ndugu zangu lakini toka nimepata haya matatizo wamenitelekeza na kunisusa huku,huwezi amini kati yao wakati nikiwa uraiani nilijitolea sana katika kuwasaidia hata katika vitu ambavyo havikuwa na faida kwangu niliwapiga tafu lakini kwakuwa mimi nimekamatwa hakuna hata anayetaka kunisogelea wakihisi pengine nao wanaweza kuhusishwa na mimi lakini licha ya hivyo hata ilipotoka hukumu hakuna aliyesogea,wameniacha" nikamwambia "ni sehemu ya maisha,je hakuna hata mmoja aliyekuja kukuona? Akanambia "ninaye mtu ambaye yeye hajawahi kuniacha,uwa namimi katika mazingira yoyote yale hata niwe ndani na hauwezi amini yeye uniletea mahitaji toka siku siku ile ya kwanza nimekamatwa" nikamuuliza "ni wazazi wako? Ni mtu gani huyo?" Akanambia ni girl friend wake (mchumba wake) ndio ambaye hajawahi kumuacha toka siku ile amekamatwa,nikamwambia kuwa alibahatika kumpata mtu sahihi sana,akanambia anahisi anaweza kuchoka nami nikamjibu kama ana upendo wa kweli hatoweza kuchoka na akanijibu "sijui,nina watoto pia yupo mwanamke ambaye nilipata nae watoto,watoto wangu wana uhitaji sana lakini mimi baba ambaye nilikuwa nikipambana katika njia mbalimbali leo nipo hapa,watoto wangu hawako katika mazingira salama na huyu mwanamke kila anapokuja kuniona aachi kunipa lawama na sasa amekuwa ni mwanamke wakuhangaika hovyo na wanaume,sielewi hatima ya watoto wangu,nilizungumza na ndugu yangu lakini ndio hivyo wameniacha peke yangu" kiukweli maelezo yake yalinisikitisha sana na hasa aliponielezea juu ya wanae maumivu yaliutanda moyo wangu,alinambia kuwa uraiani alikuwa anapambana sana,anapambana kwelikweli kwa ajili ya watoto wake lakini kwakuwa yupo jela hatoweza tena kuwapambania,kiukweli nikazidi kuumia kwa maneno yake nikamwambia "pole sana ndugu yangu,umenigusa sana,najua ukiwa hapa kule nje kila kitu chako kinakuwa kimesimama na kama ulivyonitia moyo kwenye maswaibu yangu nami nakutia moyo,tutatoka siku moja tutatoka" akasema "ni kweli natambua ni kweli"

Siku zikawa zinaenda na tukawa tunashea mengi katika mazungumzo yetu ya kila siku na kuna siku mfungwa mmoja aliniambia naona uko na urafiki na mtu flani (akimtaja yule mfungwa ambaye uwa napigana nae stori)nami nikamjibu ndio kwani amekuwa kama kaka,kama mshkaji na mfariji ndio tunabadilishana mawazo akanambia jamaa ana miaka mingi huyo kwani sote tutatoka na tutamuacha humo humo na akakazia huyo anafia humo humo gerezani,kiukweli sikumtilia maanani kwani kama ni miaka ambayo tayari imeshatamkwa mfano atatumikia miaka 30 si atatumikia miaka husika kwanini aonekane kama atafia huku? Sentensi gani hizi?
Siku zilikwenda na kwenda,safari za kwenda na kurudi mahakamani hazikuisha na mara zote nilizokuwa nikisimamishwa kizimbani nilikuwa naeleza ukweli na lile nililokuwa nalijua tu,sikuwa napindapinda katika maelezo yangu,sikuwa na mengi yakuyaeleza kwakuwa yangu ni machache kwani nilielezea stori toka nimekutana na huyu kaka hadi kufikia kunifundisha udereva,umiliki wake wa gari na hata kuhusu yule abiria ukutanaji nae ulivyokuwa na kama ujuavyo jela nilipata vijiupeo kutoka kwa wabobevu wa sheria ambao walininoa namna ya kuongea kuwa lipi lakuepuka kuliongea,lipi lakulisema na kadhalika maana mahakamani kuna maswali yamitego ni muhimu kusimamia kile unachokiongea na kiwe cha kweli kwani niliamini ukweli ndio utakaoniweka huru!

Nakumbuka siku moja kaka alikuja kunitembelea gerezani na akanambia "mdogo wangu uko katika mazingira mazuri kabisa katika kesi hii na upelelezi unavyoendelea unaonesha hauhusiki kabisa kwahiyo wakati wowote waweza kuachiwa huru,huenda mara ijayo utakapoenda mahakamani yawezekana usirudi tena huku gerezani" nikamuuliza "ni kweli usemayo kaka?" Akasema "ndio" nikajawa na matumaini na furaha sana kwa maelezo haya ya kaka,kuna siku yule kaka mule jela alinambia "naona mwenendo wa kesi yako si mbaya na matumaini ya kutoka yanazidi kuchanua sana hongera sana" nikamwambia "kaka kuna siku ntaenda mahakamani na sitarudi tena huku" akanijibu "ni kweli na mimi nimefatilia huo ni ukweli kabisa,naomba nikuulize najua utatoka na utakapotoka na kwenda uraiani unaweza kunisaidia kitu?" Nikamjibu "ndio" akasema "ntashukuru sana utakaponisaidia katika hili jambo,naomba unisaidie ntakupa maelekezo naomba ukawasalimie watoto wangu" nikamwambia "kaka hakuna shida" akaongezea "na pia ntafurahi sana kama utapata fulsa yakuweza kwenda kumsalimia na mchumba wangu" nikamjibu "nitafanya hivyo pia kaka" akanambia "naomba tuwe ndugu,unajua ndugu sio lazima muwe mmezaliwa tumbo moja,unajua wako ndugu sasa hivi hata wakija nimekuwa siwaamini tena lakini moyo wangu nimejikuta nakuamini sana wewe,sijawahi kukuona enzi nikiwa uraiani tumekuja kukutana gerezani lakini mimi naamini kukutana kwetu Mungu amepanga tena amepanga tukutane katika mazingira kama haya,hivi unajua waweza kukutana na mtu sahihi hata ukiwa gerezani?" Mi nikacheka kwa hayo maneno yake nikamuuliza "mtu sahihi gerezani? Mtu gani awe sahihi mazingira kama haya?" Akanambia "mimi naweza kuwa mtu sahihi sanj kwako na nikawa mtu mwema kwako,jua nimekuona kuwa wewe ni mtu mwema tafadhali nakuomba nawe unirejeshee huo wema ntakaokupa" yale maneno aliyokuwa akinambia sikuwa nayaelewa alikuwa anamaanisha kitu gani,msisitizo wa maneno haya kwangu uliendelea mara kwa mara mpaka siku naenda mahakamani,nakumbuka siku hiyo sasa ndio naenda mahakamani kabla hatujatolewa nje kupandishwa karandinga alinambia "unakumbuka maneno niliyokuwa nikikwambia mara kwa mara ? Unaweza haya maneno ukayafanyia kazi?

Nikamwambia "kaka wala usiwaze kwani undugu si lazima kuzaliwa tumbo moja,tunakutana katika mazingira yoyote alafu tunatokea kuelewana,nakuahidi kaka kama nilivyokwambia nitaenda kuwasalimia watoto na nitaenda kumsalimia mchumba wako,na nikuahidi mimi ni kijana na kama Mungu atanipa neema ya kutoka nitaenda kupambana,nitaenda kupambana na napenda nikuahidi kitu kimoja nitaenda kuwatembelea watoto wako na chochote nitakachobarikiwa sitawasahau kwani najua wewe baba yao uliyekuwa ukipambana kwa ajili yao umekwama humu" akaniuliza "kweli? Kweli unasema? kweli Rojaz unaniahidi kitu kama hiki? Ndio maana niliona,macho yangu yaliona na moyo wangu ukavutika kuzungumza na wewe,wewe ni mtu mwema" kiukweli ninaikumbuka sana siku hiyo kwani alikuja akanikumbatia huku machozi yakindondoka na kunipigapiga mgongoni akanambia "aisante sana mdogo wangu,asante nakutegemea kwani hakuna mtu yoyote ambaye ameweza kuniahidi hivi kama wewe,sijawahi kupata rafiki mwema hivi kwani kuna mshkaji nilikuwa nae hapa karibu kweli lakini toka ametoka hajawahi kurudi tena kunitembelea,hakuwahi hata kwenda kuwatembelea wanangu,Rojaz kumbuka ahadi unayonipa mdogo wangu" nikamwambia "kaka amini ninachokwambia,sitasahau" mimi niliondoka na nikaweka hiyo ahadi kwenye kichwa changu,muda wa kwenda mahakamani ulipofika tukapandishwa kuelekea uko na kesi ilisomwa na mheshimiwa akangurumisha kesi na mwishowe hakimu akatamka kuwa kuanzia muda huo niko huru,kiukweli kutokana na kuwa sikuhusika sikustuka sana kwa uamuzi ule uliotolewa kwani nilijua ni suala la muda tu ili kuweza kuujua ukweli halisi,jela nilikaa kama mwaka mzima hadi kufikia hii siku ya kuachiwa huru na katika kesi iliyokuwa ikinikabili tulikuwa wengi na wengine waliendelea na kesi mbele,ndugu zangu walifusahi sana kwa ndwtgu yao kuwa huru na kujumuika nao tena uraiani,kaka akanambia "sheria zipo kwa ajili ya kutenda haki walimdhuru huyo kijana watabainika tu, sheria itawakamata na kuwahukumu" kwahiyo mimi nilitoka gerezani na kurudi uraiani hakika ilikuwa ni furaha sana kwetu sisi na nilpata somo kubwa kuwa ni vyema kuwa na tahadhari katika shughuli tunazofanya



Itaendelea!
Asante
 
MKASA WA KUSISIMUA WA ROJAZ:
katika kipindi cha sitasahau cha radio free Africa



Sehemu ya 4



Kitendo cha kuwa huru kiukweli nilimshukuru Mungu sana na kujisemea peke yangu moyoni kuwa ukimuona mtu anamfanyia hila mwingine na kupelekea huyo mtu kupelekwa jela ujue huyo sio mtu mzuri katika maisha yako,nilishukuru kwa kuwa haki imetendeka na imebainika kuwa kuwa mimi sio mhusika wa lile tukio ingawa haikuwa ndani ya siku moja au mbili lakini ukweli umejulikana,nimerejea sasa uraiani na maisha yanaendelea na nashukuru kwa uhuru nilionao kuweza kujiamulia mambo yangu,ndugu jamaa na marafiki walijitokeza wenye kunipongeza,wenye kunipa pole yote hayo niliyapokea lakini nina ahadi mimi nilimuahidi mtu nikiwa kule gerezani,huyu mtu nimekutana nae gerezani,huyu mtu aliniomba sana niende kuitembelea familia yake alinipa maelekezo tena alizungumza nami mengi kuhusiana na familia yake hasa kuhusu watoto wake kuwa kuna mwanamke ambaye alizaa nae hao watoto lakini kwa wakati huu hawako kwenye mahusiano na pia ana mchumba wake kwahiyo haya maelekezo yote nilikuwa nayakumbuka nyakati hizi wakati nipo uraiani,zilipita kama wiki tatu hivi nikawa nasikia kama mzigo ndani ya moyo wangu kwanini niahidi kitu alafu nishindwe kukitekeleza ni kweli kwamba nimeshindwa kwenda kuwaona hawa watoto?

Nikasema hapana na kwakuwa nilikuwa na vijisenti kidogo kwa sababu nimetoka gerezani familia yangu ipo nashukuru walinishika mkono na nikawa hapa nyumbani,nilitumia kapesa changu kidogo kwa kununua nyama kilo moja nakumbukb na nilinunua sukari nusu kilo nilivibeba nikiwa na dhumuni la kwenda kuitizama familia ya mtu ambaye nimekutana nae gerezani na wala sikuwa namjua kabla ya hapo yaani tumekutana gerezani,nikafata maelekezo hadi nikafika lile eneo ambalo nililoelekezwa,kweli nilifika na kweli ndicho nilichokutana nacho,nilikutana na mwanamke mmoja,mwanamke huyo alikuwa mnene na mweupe sana,alinikaribisha na nikamueleza ujumbe ambao nilikuwa nimepewa na rafiki wa kule gerezani,nakumbuka sentensi ambayo alinambia huyu mama "eeh kwahyo amekuambiaje?" Hii ndio sentensi ya kwanza huyu mama alinambia nami nikamwambia "amenituma nije kuwasalimia watoto" akanambia "eeh ukishawasalimia?" Nikamjibu ndio alivyoniagiza kuja kuwasalimia angalau nizungumze nao na kuwaeleza jinsi baba yao anawapenda sana na siku zote anawaombea baraka,akasema "hayo maneno nimeshayasikia sana je yanasaidia nini kwa watoto wangu,yanasaidia nini?

Kiukweli huyu mama hakunipokea vizuri lakini nilishapewa tahadhari toka kule gerezani kuwa huyu mama ni mkorofi sana,sasa kwa sababu nilishaelezwa hayo ilibidi tu niwe mpole,akaendelea kunichamba "kwahiyo uko gerezani hakuna kitu anachona sisi kinatufaa zaidi ya hiyo nyama na sukari,kwahiyo tunaishi kwa ajili ya nyama na sukari? Hao ndugu zake washenzi wasio na maana kila siku napata ujumbe ntasaidiwa ntasaidiwa je nasaidiwa kitu gani? Ameharibu maisha yangu mbwa yule" akaanza kutamka maneno ya kashfa kumuhusu kaka yule na kiukweli ukiniuliza mimi nafahamu mengi kiasi gani kumuhusu yule kaka kule gerezani kiukweli sijui na hauwezi amini ni machache ambayo yeye amenieleza na upande wa pili wa ubaya wake mimi siuelewi lakini ni mtu aliyenifanyia wema nyakati tukiwa gerezani na alikuwa mtetezi wangu katika mambo mengi sababu gerezani kuna maisha yake uko,kuna watu wababe,wakorofi lakini kama kuna mtu anakukingia kifua unamuona huyu ni kaka,kaka mzuri kwahiyo hajawai kunitendea ubaya wowote na inawezekana kweli ni mtu mbaya kwa sababu alishanieleza kuwa yupo hapo kwa sababu alitakiwa kulipia yale yote aliyoyatenda uraiani,anatumikia kifungo anachoamini alistahili,huyu mama alizungumza mengi nami nikawa nimetulia tu namsikiliza na nikamwambia "tuzungumze tu kwani mimi ni mjumbe tu na mjumbe hauwawi,mimi ni mtu mwema tu ambaye nilifungwa na nikakutana na huyu ndugu baba watoto wako,ni mtu ambaye aliniomba sana nitakapotoka nisiache kuja kuwana watoto wake,sasa ahadi nilimpa na toka nimetoka gerezani ilitakiwa nifanye mapema na nimekuwa nikijisikia hatia kwa sababu nimeshindwa kulitekeleza hilo kwa haraka kwahiyo nimekuja ili kuweza kusikia amani ndani ya moyo wangu" nilimueleza hayo na nikapata nafasi ya kuzungumza na watoto,ana watoto wazuri sana,baba yuko gerezani na kwa mtu mwelevu ukitizama mazingira ulikuwa unapata picha kuwa hawakuwa na maisha mazuri kwahiyo mama anajipigania kwa vile anavyoweza na mama mbabe sana huyu maana hata akiongea tu unajua kama huyu mama ni mbabe,niliwambia watoto bac yao anawasalimia sana na anawapenda na siku moja anaamini atajumuika na nyinyi na nakumbuka mtoto wake mmoja mkubwa alinambia kuwa mama yao aliwaambia hawataweza tena kujumuika na baba yao katika maisha wanayoishi nami nikawaeleza kuwa sio kweli kwani baba siku moja atajumuika nao na wataungana nae na kula nae chakula pamoja na furaha itakuwa katika maisha yao ya kila siku.

Nikawaambia mimi ni anko wao na nitakuja mara kwa mara kuwatembelea na kama kuna uhitaji wa vifaa vyovyote vya shule wataniagiza na ntakaporejea tena ntawaletea hivyo vitu,wakaniandikia vitu vyao ingawa nilikuwa siko poa kivile na ukizingatia nina muda mfupi toka nitoke gerezani lakini mazingira yao yalinisukuma tu kuweza kufanya hilo jambo,mimi ni mwanaume tena mpambanaji nimeguswa sana na hii familia hasa hawa watoto,niliondoka nikiwa najisikia deni ndani yangu tena nakumbuka yule mtoto mdogo aliniuliza "utarudi kweli? Utakuja tena kuja kutuona? Nikamjibu "ntarudi na ntaleta hivi vitu mlivyoniagiza kwa ajili ya shule" nikaondoka zangu kurejea nyumbani na nakumbuka pia nilishea hili jambo na kaka nilipofika nyumbani,nilimueleza kaka jinsi nilivyoikuta familia ya yule ndugu wa kule gerezani,kaka alisikitika sana na kusema "maskini hakuwaza kama siku moja atakuwa mbali na watoto wake tazama sasa future ya watoto inaweza kuharibika kama mama atakosa misingi mizuri ya malezi kwa ajili ya watoto,akijichanganya tu anaharibu watoto lakini kama atasimama anaweza kuwalea watoto wake vyema" nikamueleza jinsi nilivyomuona ni kama mama ambaye ameshajichanganya sana na tukasikitika pamoja na nikamueleza jinsi watoto walivyonipa mahitaji yao ya vifaa vya shule lakini bro mimi navitoa wapi? Kaka akacheka na kunambia "ndio ukapambane sasa mwenzetu umeshapata familia eeh msamaria mwema umejikuta umekuwa na familia ya watoto wawili,mimi sina la kukusaidia nadhani unajua kuhusu hali yangu ya kipesa,wewe pambana bwana ahadi umetoa ipambanie" maisha yakaendelea na kaka kule gerezani nilimuahidi ntakapoenda kwa watoto wake ningekwenda kumjulisha maendeleo yao,kwakuwa mi niko kitaa nikaona sio vyema kukaa tu na ni vyema kusaka dili za kufanya kwakuwa maisha lazima yaendelee,katika kutafuta japo videiwaka na ukitilia maanani nimetoka gerezani kuaminika nako kukawa ni mtihani kwa walio wengi maana wengine akijua ulienda ndani anajua kama ulitenda kumbe uhusiki chochote,kuaminika kulipunguwa maana wanahisi unaweza kumpa gari yako ana mikosi gari ikapata matatizo yaani nikawa nakataliwa kihivyo,maisha yaliendelea kuwa magumu japo kaka alikuwa ananiambia "hivi ndivyo ilivyo kwa wewe kujenga kuaminika inahitaji muda kidogo,wako watakaoona una nuksi,wapo watakaona ulihusika kwa namna moja au nyingine ukweli unaujua wewe na Mungu wako lakini ni muda mfupi tu lakini uvumilivu unahitajika ili mambo haya yapite na tuyaruhusu yale mazuri yaje kwetu"

Familia yangu ilinitia sana moyo,ilinifariji sana,kila ninachojaribu kufanya kwangu kilikuwa hakifanikiwi pamoja na kuwa ni dereva mzuri tu hata deiwaka sipati,kuna siku nikaona ngoja nikamcheki mshkaji kule gerezani nikikumbuka pia nina ujumbe kutoka kwa watoto wake nimpelekee zile salamu watoto wake walinipa ,sijafanikiwa katika ahadi ambazo niliwaahidi,nikaenda na nikapata nafasi ya kuzungumza na mshkaji,mshkaji alinambia "umekuja?umekuja kuniona mimi?"

Alifurahi sana, Nikamwambia "ndio kaka si nilikuahidi" akanambia "nilihisi hautakuja maana siku niliona zinasogea na nikaona ahadi zako zitakuwa kama ahadi za watu wengine walizokuwa wakiniahidi" nikamwambia "hapana lazima ningekuja kwani sijawahi kumuahidi mtu kitu cha uongo sipendi kufanya hayo ya kuahidi alafu nisitekeleze,lakini nimerudi uraiani mambo yamekuwa si rahisi" akasema "najua hayawezi kuwa rahisi lazima ujipe muda" nikamwambia "ni kweli,kweli kabisa nimerelax najipa muda" akanambia "mambo yatakaa vizuri,amini Rojaz mambo yatakaa vizuri,niambie kuhusu watoto wangu" ndipo nilipomueleza mazingira niliyowakuta watoto wake ila wako na afya njema tu asiwe na wasiwasi akasema "wamesemaje? Wamenikumbuka?" Nikamjibu "ndio wanaonesha kukukumbuka sana na wanaonesha kukupenda sana" akasema "mama yao anawafanyia ukatili watoto hataki kabisa hata watoto wanitembelee,naumia sana" niliona jinsi anavyosononeka akizungumza hayo nikamwambia "mambo yatakaa tu sawa,nimewaahidi watoto wako kuwa wewe utatoka siku moja utajumuika nao" akacheka,akasema "mmh eeh wakasemaje" nikamwambia "inaonekana kama walikuwa hawana matumaini lakini nilipowaambia nyuso zao zimeonekana kuwa zenye furaha" akanambia "umewaambia vyema,asante nakushukuru sana,umerejesha furaha yangu na umenifanyia jambo ambalo sikuwahi kulitegemea,kwa hii sentensi naomba uamini ninachokisema,umetenda kwangu jambo kubwa sana,nimekuwa nikitamani nikutane na mtu mwenye utu kama wewe lakini hauwezi amini sijawahi kukutana nae" mimi nikatabasamu na kujiuliza hivi kitu gani cha thamani nimefanya hapa,haya ni maisha yangu ya kila siku kwani nimekuwa nikiguswa na watu wenye changamoto za hapa na pale na mimi ni huyu,mimi ndio Rojaz ninapomuahidi mtu kitu ninachoweza kwa hakika kukitenda lazima nikitekeleze kwahiyo nimefanya haya ndio maisha yangu ya kila siku hakuna wema ambao natakiwa nionekane nimetenda wema,haya ni maisha yangu ya kila siku,akanambia "aisee Rojaz nakushukuru sana umepanda kwangu kitu kikubwa sana,Rojaz unaweza kunisaidia kitu?"

Nikasema "ndio mimi niko hapa" akasema "sawa Rojaz naomba sasa ukamtembelee msichana wangu,najua amevunjika moyo,watu wamemvunja moyo lakini naomba ukanipelekee salamu" nikamwambia "nikamwambie nini? Akasema "najua wewe ni mtu mwema we nenda kazungumze nae tu,ukamwambie jinsi tulivyoishi vyema tukiwa huku gerezani na jinsi ambavyo nilikuwa nikimzungumzia vizuri na jinsi ambavyo nampenda,kitu ambacho kinaniuma ni kukosa uhuru na kuishi na mwanamke ambaye ninampenda" nakumbuka nilitabasamu tu aliponambia hayo,nikamwambia "brother siku utapata chance na utaishi na mwanamke unayempenda" akasema "haiwezekani,hawezi kuningoja mie majira yote hayo,najua na sitamlaumu,sitamlaumu hata siku moja" nikamwambia "sawa" ila alifurahi sana,yaani unafanya kitu kwa mtu yaani unamuona anafurahi mpaka unashangaa alifurahi nini kwa kiwango iki na alisema "umenipa furaha isiyo ya kawaida,baada ya hapo nakumbuka niliondoka nakurudi zangu nyumbani na harakati zangu za kudonoadonoa kama kawaida ziliendelea kama kawaida kwa sababu mambo yalikuwa bado hayajakaa vizuri,kweli siku nilipanga na kama alivyonielekeza nilienda,mimi niliombwa kwahiyo kama niliombwa na nilimuahidi kutenda ndio nilienda sasa,kweli nilikutana na huyo mwanamke na nikafanya nilivyoelekezwa kikubwa nilimpa salamu zake nyingi sana na nikamueleza jinsi huyu kaka anavyompenda na jinsi anavyojisikia vibaya kuishi gerezani na kukosa kuishi na mwanamke anayempenda,mwanamke wa ndoto yake,kiukweli yule dada nilimuona ni mtu aliyekwisha mkatia tamaa mshkaji lakini mimi nilimwambia mapenzi ya kweli uwa hayafi,mapenzi ni kuvumilia na kama kweli unampenda utamvumilia na siku moja atakuwa huru na mtaungana tena uraiani na kuishi yale maisha mliyokuwa mkiishi awali,lakini mtu akiwa gerezani na hasa ambao wana miaka mingi gerezani watu wao wa karibu wanakuwa na ukaribu siku zile za mwanzo lakini kadri siku zinavyosogea watu huchoka na huyu ndio binadamu alivyo,atakuwa na bidii sana mwaka wa kwanza,mwaka wa pili,ukianza mwaka wa tatu anaanza kuchechemea baadae aah anaanza kuchoka,anachoka kweli kweli anaona kwani nini na jamii nayo watu wako tofauti,mtu ameshaenda gerezani miaka thelathini unamngoja wa nini,huyo mtu amefungwa kifungo cha maisha unamngoja wa nini ushindwe kuendelea na maisha yako,watu wana mapokeo tofauti mwingine anaanza maisha mapya,mwingine anavumilia lakini unamuona hizi ni dalili za mwisho hizi kachoka kabisa lakini ujumbe mimi kama mjumbe nilifikisha na nilimwambia ntakuwa nakuja mara kwa mara kukusalimia na kukujulia hali kwa namna moja au nyingine lakini ni mwanamke ambaye maelezo yangu aliyapokea kikawaida tu "nashukuru,asante" yaani hivyo.

Nashukuru baada ya muda nikapata gari lakujishikiza kama deiwaka yaani gari lina dereva wake nami nakuwa kama namsaidia pale anapokuwa amechoka,kaka ndio aliniunganisha kwa huyo jamaa mwenye gari nikawa napigapiga mishe ujue ukitoka jela inakuwa sio rahisi kurudisha uaminifu katika jamii inayokuzunguka,ni watu wenye imani kubwa kwako tu ndio watakaothubutu kuweza kukupata tena nafasi ya kukukabidhi gari wao wanajua ni changamoto tu za kimaisha umekutana nazo tena haukuhusika kiukweli inabidi mtu akujue kwa ukaribu sana kama huyu mtu ananipa gari analerax na naenda na kurudi salama,kweli maisha yakawa yanaenda na Mungu akajaalia nikawa napata vijipesa kidogo nakumbuka nikaenda kununua vifaa kidogo nakumbuka ilikuwa ni peni,rula rula,madaftali na nikaenda kuwacheki wale watoto wa mshkaji,nikaenda kuwatizama wale watoto nakuwapatia yale mahitaji na pia nilibahatika kununua na chakula,nilinunua unga,mchele,mafuta,nilinunua nyama,mafuta kile kidumu kidogo yaani nikaenda safari hii angalau na kifurushi,vifaa vya watoto nilibeba hivyo vichache ingawa waliniandikia vingi,najua mazingira ya pale vyakula ilikuwa ni kitu bora zaidi kukipa kipaumbele katika nilivyochukua,nimefika Mungu mwema nikamkuta na yule mama na akanambia "umekuja tena?" Nikamwambia "ndio bwana nimekuja tena,nimekuja kuwaona hawa ndugu zangu" ilikuwa ni siku nzuri tena ukitilia maanani ilikuwa ni jumamosi wakanambia anko umekuja? Yaani walinikumbuka,nikawaambia "

Si mnakumbuka niliwaambia kuwa ntakuja? Mambo kati hapa hayakuwa rahisi sikupata pesa haraka yakununua vitu ndio maana nikachelewa lakini nimekuja" nikawapatia vitu vyao na chakula,awamu hii yule mama angalau alinipokea vizuri akasema "eeh una ujumbe gani mwenzetu" nikamjibu "sina ujumbe wowote nimekuja tu kwa ajili ya kuwaona hawa ndugu zangu" akasema "haya tunashukuru" nikazungumza na watoto nakuwakabidhi vitu vyao japo sikuwa nimewakamilishia nikawaambia kuwa nitakuja tena na waandike vingine wanavyovihitaji,kwahiyo vile ambavyo sikuvinunua wakaandika na vingine ndio maana kaka anasema mwenzetu umekuwa na familia siku hizi lakini ni mzigo ambao niliubeba ndani yangu kwa kuwaona hawa watoto ambao hawana hatia yoyote,niliondoka hapo nikiwa na furaha kwelikweli na nikiwa na amani sana kwamba leo mimi nimefanikiwa kuwapa chakula watu ambao pengine wangekula mlo mmoja au kesho labda wangekula mlo mmoja au wangeangaika kwenda kuombaomba lakini mimi kwa mchele kidogo,kwa mafuta nimewastili siku mbili tatu watapata chakula kizuri,nilirudi kwa furaha na nikalala usingizi mzuri sana.

Pilikapilika ziliendelea na huku nikiendelea kumuelezea kaka kile kinachoendelea kuhusiana na mimi kwenda kuwatembelea hawa watoto,nilienda tena kuwatembelea hawa watoto,na nikaenda tena,nakumbuka nilienda kama mara tano kwenda kuwatembelea hawa watoto na kila ninapoenda kile nilichobarikiwa naenda kuwapelekea,sasa wameshanizoea na huyu mama alishanizoea hata siku moja alishaniambia "wewe ni rafiki wa baba ...(akitaja jina la mtoto wake) ina maana mmejuliana gerezani,unamjua mtu huyu?" Nikamwambia "sitaki kujua chochote ninachojua ni mtu mwema,tulipokuwa gerezani tumeishi vizuri na hili ni ombi lake kwangu na kwa sababu mimi nipo uraiani hawa wamekuwa kama wadogo zangu"
Muda ukaenda baada ya kuwatembelea hawa watoto na nikaona sasa ni wakati wa kwenda gerezani kumsalimia ndugu yangu,ameshakuwa ndugu yangu angalaunimpashe jinsi mambo yanavyoenda uko uraiani na jinsi watoto wake wanavyoendelea vizuri na maisha yanaendelea,nilipofika gerezani awamu hii na kupata nafasi ya kuzungumza na huyu kaka ambaye mimi nilimkuta gerezani na kumuacha uko viko vitu aliniambia nilishangaa sana!




Itaendelea!
 
MKASA WA KUSISIMUA WA ROJAZ:
katika kipindi cha sitasahau cha radio free Africa



Sehemu ya 4



Kitendo cha kuwa huru kiukweli nilimshukuru Mungu sana na kujisemea peke yangu moyoni kuwa ukimuona mtu anamfanyia hila mwingine na kupelekea huyo mtu kupelekwa jela ujue huyo sio mtu mzuri katika maisha yako,nilishukuru kwa kuwa haki imetendeka na imebainika kuwa kuwa mimi sio mhusika wa lile tukio ingawa haikuwa ndani ya siku moja au mbili lakini ukweli umejulikana,nimerejea sasa uraiani na maisha yanaendelea na nashukuru kwa uhuru nilionao kuweza kujiamulia mambo yangu,ndugu jamaa na marafiki walijitokeza wenye kunipongeza,wenye kunipa pole yote hayo niliyapokea lakini nina ahadi mimi nilimuahidi mtu nikiwa kule gerezani,huyu mtu nimekutana nae gerezani,huyu mtu aliniomba sana niende kuitembelea familia yake alinipa maelekezo tena alizungumza nami mengi kuhusiana na familia yake hasa kuhusu watoto wake kuwa kuna mwanamke ambaye alizaa nae hao watoto lakini kwa wakati huu hawako kwenye mahusiano na pia ana mchumba wake kwahiyo haya maelekezo yote nilikuwa nayakumbuka nyakati hizi wakati nipo uraiani,zilipita kama wiki tatu hivi nikawa nasikia kama mzigo ndani ya moyo wangu kwanini niahidi kitu alafu nishindwe kukitekeleza ni kweli kwamba nimeshindwa kwenda kuwaona hawa watoto?

Nikasema hapana na kwakuwa nilikuwa na vijisenti kidogo kwa sababu nimetoka gerezani familia yangu ipo nashukuru walinishika mkono na nikawa hapa nyumbani,nilitumia kapesa changu kidogo kwa kununua nyama kilo moja nakumbukb na nilinunua sukari nusu kilo nilivibeba nikiwa na dhumuni la kwenda kuitizama familia ya mtu ambaye nimekutana nae gerezani na wala sikuwa namjua kabla ya hapo yaani tumekutana gerezani,nikafata maelekezo hadi nikafika lile eneo ambalo nililoelekezwa,kweli nilifika na kweli ndicho nilichokutana nacho,nilikutana na mwanamke mmoja,mwanamke huyo alikuwa mnene na mweupe sana,alinikaribisha na nikamueleza ujumbe ambao nilikuwa nimepewa na rafiki wa kule gerezani,nakumbuka sentensi ambayo alinambia huyu mama "eeh kwahyo amekuambiaje?" Hii ndio sentensi ya kwanza huyu mama alinambia nami nikamwambia "amenituma nije kuwasalimia watoto" akanambia "eeh ukishawasalimia?" Nikamjibu ndio alivyoniagiza kuja kuwasalimia angalau nizungumze nao na kuwaeleza jinsi baba yao anawapenda sana na siku zote anawaombea baraka,akasema "hayo maneno nimeshayasikia sana je yanasaidia nini kwa watoto wangu,yanasaidia nini?

Kiukweli huyu mama hakunipokea vizuri lakini nilishapewa tahadhari toka kule gerezani kuwa huyu mama ni mkorofi sana,sasa kwa sababu nilishaelezwa hayo ilibidi tu niwe mpole,akaendelea kunichamba "kwahiyo uko gerezani hakuna kitu anachona sisi kinatufaa zaidi ya hiyo nyama na sukari,kwahiyo tunaishi kwa ajili ya nyama na sukari? Hao ndugu zake washenzi wasio na maana kila siku napata ujumbe ntasaidiwa ntasaidiwa je nasaidiwa kitu gani? Ameharibu maisha yangu mbwa yule" akaanza kutamka maneno ya kashfa kumuhusu kaka yule na kiukweli ukiniuliza mimi nafahamu mengi kiasi gani kumuhusu yule kaka kule gerezani kiukweli sijui na hauwezi amini ni machache ambayo yeye amenieleza na upande wa pili wa ubaya wake mimi siuelewi lakini ni mtu aliyenifanyia wema nyakati tukiwa gerezani na alikuwa mtetezi wangu katika mambo mengi sababu gerezani kuna maisha yake uko,kuna watu wababe,wakorofi lakini kama kuna mtu anakukingia kifua unamuona huyu ni kaka,kaka mzuri kwahiyo hajawai kunitendea ubaya wowote na inawezekana kweli ni mtu mbaya kwa sababu alishanieleza kuwa yupo hapo kwa sababu alitakiwa kulipia yale yote aliyoyatenda uraiani,anatumikia kifungo anachoamini alistahili,huyu mama alizungumza mengi nami nikawa nimetulia tu namsikiliza na nikamwambia "tuzungumze tu kwani mimi ni mjumbe tu na mjumbe hauwawi,mimi ni mtu mwema tu ambaye nilifungwa na nikakutana na huyu ndugu baba watoto wako,ni mtu ambaye aliniomba sana nitakapotoka nisiache kuja kuwana watoto wake,sasa ahadi nilimpa na toka nimetoka gerezani ilitakiwa nifanye mapema na nimekuwa nikijisikia hatia kwa sababu nimeshindwa kulitekeleza hilo kwa haraka kwahiyo nimekuja ili kuweza kusikia amani ndani ya moyo wangu" nilimueleza hayo na nikapata nafasi ya kuzungumza na watoto,ana watoto wazuri sana,baba yuko gerezani na kwa mtu mwelevu ukitizama mazingira ulikuwa unapata picha kuwa hawakuwa na maisha mazuri kwahiyo mama anajipigania kwa vile anavyoweza na mama mbabe sana huyu maana hata akiongea tu unajua kama huyu mama ni mbabe,niliwambia watoto bac yao anawasalimia sana na anawapenda na siku moja anaamini atajumuika na nyinyi na nakumbuka mtoto wake mmoja mkubwa alinambia kuwa mama yao aliwaambia hawataweza tena kujumuika na baba yao katika maisha wanayoishi nami nikawaeleza kuwa sio kweli kwani baba siku moja atajumuika nao na wataungana nae na kula nae chakula pamoja na furaha itakuwa katika maisha yao ya kila siku.

Nikawaambia mimi ni anko wao na nitakuja mara kwa mara kuwatembelea na kama kuna uhitaji wa vifaa vyovyote vya shule wataniagiza na ntakaporejea tena ntawaletea hivyo vitu,wakaniandikia vitu vyao ingawa nilikuwa siko poa kivile na ukizingatia nina muda mfupi toka nitoke gerezani lakini mazingira yao yalinisukuma tu kuweza kufanya hilo jambo,mimi ni mwanaume tena mpambanaji nimeguswa sana na hii familia hasa hawa watoto,niliondoka nikiwa najisikia deni ndani yangu tena nakumbuka yule mtoto mdogo aliniuliza "utarudi kweli? Utakuja tena kuja kutuona? Nikamjibu "ntarudi na ntaleta hivi vitu mlivyoniagiza kwa ajili ya shule" nikaondoka zangu kurejea nyumbani na nakumbuka pia nilishea hili jambo na kaka nilipofika nyumbani,nilimueleza kaka jinsi nilivyoikuta familia ya yule ndugu wa kule gerezani,kaka alisikitika sana na kusema "maskini hakuwaza kama siku moja atakuwa mbali na watoto wake tazama sasa future ya watoto inaweza kuharibika kama mama atakosa misingi mizuri ya malezi kwa ajili ya watoto,akijichanganya tu anaharibu watoto lakini kama atasimama anaweza kuwalea watoto wake vyema" nikamueleza jinsi nilivyomuona ni kama mama ambaye ameshajichanganya sana na tukasikitika pamoja na nikamueleza jinsi watoto walivyonipa mahitaji yao ya vifaa vya shule lakini bro mimi navitoa wapi? Kaka akacheka na kunambia "ndio ukapambane sasa mwenzetu umeshapata familia eeh msamaria mwema umejikuta umekuwa na familia ya watoto wawili,mimi sina la kukusaidia nadhani unajua kuhusu hali yangu ya kipesa,wewe pambana bwana ahadi umetoa ipambanie" maisha yakaendelea na kaka kule gerezani nilimuahidi ntakapoenda kwa watoto wake ningekwenda kumjulisha maendeleo yao,kwakuwa mi niko kitaa nikaona sio vyema kukaa tu na ni vyema kusaka dili za kufanya kwakuwa maisha lazima yaendelee,katika kutafuta japo videiwaka na ukitilia maanani nimetoka gerezani kuaminika nako kukawa ni mtihani kwa walio wengi maana wengine akijua ulienda ndani anajua kama ulitenda kumbe uhusiki chochote,kuaminika kulipunguwa maana wanahisi unaweza kumpa gari yako ana mikosi gari ikapata matatizo yaani nikawa nakataliwa kihivyo,maisha yaliendelea kuwa magumu japo kaka alikuwa ananiambia "hivi ndivyo ilivyo kwa wewe kujenga kuaminika inahitaji muda kidogo,wako watakaoona una nuksi,wapo watakaona ulihusika kwa namna moja au nyingine ukweli unaujua wewe na Mungu wako lakini ni muda mfupi tu lakini uvumilivu unahitajika ili mambo haya yapite na tuyaruhusu yale mazuri yaje kwetu"

Familia yangu ilinitia sana moyo,ilinifariji sana,kila ninachojaribu kufanya kwangu kilikuwa hakifanikiwi pamoja na kuwa ni dereva mzuri tu hata deiwaka sipati,kuna siku nikaona ngoja nikamcheki mshkaji kule gerezani nikikumbuka pia nina ujumbe kutoka kwa watoto wake nimpelekee zile salamu watoto wake walinipa ,sijafanikiwa katika ahadi ambazo niliwaahidi,nikaenda na nikapata nafasi ya kuzungumza na mshkaji,mshkaji alinambia "umekuja?umekuja kuniona mimi?"

Alifurahi sana, Nikamwambia "ndio kaka si nilikuahidi" akanambia "nilihisi hautakuja maana siku niliona zinasogea na nikaona ahadi zako zitakuwa kama ahadi za watu wengine walizokuwa wakiniahidi" nikamwambia "hapana lazima ningekuja kwani sijawahi kumuahidi mtu kitu cha uongo sipendi kufanya hayo ya kuahidi alafu nisitekeleze,lakini nimerudi uraiani mambo yamekuwa si rahisi" akasema "najua hayawezi kuwa rahisi lazima ujipe muda" nikamwambia "ni kweli,kweli kabisa nimerelax najipa muda" akanambia "mambo yatakaa vizuri,amini Rojaz mambo yatakaa vizuri,niambie kuhusu watoto wangu" ndipo nilipomueleza mazingira niliyowakuta watoto wake ila wako na afya njema tu asiwe na wasiwasi akasema "wamesemaje? Wamenikumbuka?" Nikamjibu "ndio wanaonesha kukukumbuka sana na wanaonesha kukupenda sana" akasema "mama yao anawafanyia ukatili watoto hataki kabisa hata watoto wanitembelee,naumia sana" niliona jinsi anavyosononeka akizungumza hayo nikamwambia "mambo yatakaa tu sawa,nimewaahidi watoto wako kuwa wewe utatoka siku moja utajumuika nao" akacheka,akasema "mmh eeh wakasemaje" nikamwambia "inaonekana kama walikuwa hawana matumaini lakini nilipowaambia nyuso zao zimeonekana kuwa zenye furaha" akanambia "umewaambia vyema,asante nakushukuru sana,umerejesha furaha yangu na umenifanyia jambo ambalo sikuwahi kulitegemea,kwa hii sentensi naomba uamini ninachokisema,umetenda kwangu jambo kubwa sana,nimekuwa nikitamani nikutane na mtu mwenye utu kama wewe lakini hauwezi amini sijawahi kukutana nae" mimi nikatabasamu na kujiuliza hivi kitu gani cha thamani nimefanya hapa,haya ni maisha yangu ya kila siku kwani nimekuwa nikiguswa na watu wenye changamoto za hapa na pale na mimi ni huyu,mimi ndio Rojaz ninapomuahidi mtu kitu ninachoweza kwa hakika kukitenda lazima nikitekeleze kwahiyo nimefanya haya ndio maisha yangu ya kila siku hakuna wema ambao natakiwa nionekane nimetenda wema,haya ni maisha yangu ya kila siku,akanambia "aisee Rojaz nakushukuru sana umepanda kwangu kitu kikubwa sana,Rojaz unaweza kunisaidia kitu?"

Nikasema "ndio mimi niko hapa" akasema "sawa Rojaz naomba sasa ukamtembelee msichana wangu,najua amevunjika moyo,watu wamemvunja moyo lakini naomba ukanipelekee salamu" nikamwambia "nikamwambie nini? Akasema "najua wewe ni mtu mwema we nenda kazungumze nae tu,ukamwambie jinsi tulivyoishi vyema tukiwa huku gerezani na jinsi ambavyo nilikuwa nikimzungumzia vizuri na jinsi ambavyo nampenda,kitu ambacho kinaniuma ni kukosa uhuru na kuishi na mwanamke ambaye ninampenda" nakumbuka nilitabasamu tu aliponambia hayo,nikamwambia "brother siku utapata chance na utaishi na mwanamke unayempenda" akasema "haiwezekani,hawezi kuningoja mie majira yote hayo,najua na sitamlaumu,sitamlaumu hata siku moja" nikamwambia "sawa" ila alifurahi sana,yaani unafanya kitu kwa mtu yaani unamuona anafurahi mpaka unashangaa alifurahi nini kwa kiwango iki na alisema "umenipa furaha isiyo ya kawaida,baada ya hapo nakumbuka niliondoka nakurudi zangu nyumbani na harakati zangu za kudonoadonoa kama kawaida ziliendelea kama kawaida kwa sababu mambo yalikuwa bado hayajakaa vizuri,kweli siku nilipanga na kama alivyonielekeza nilienda,mimi niliombwa kwahiyo kama niliombwa na nilimuahidi kutenda ndio nilienda sasa,kweli nilikutana na huyo mwanamke na nikafanya nilivyoelekezwa kikubwa nilimpa salamu zake nyingi sana na nikamueleza jinsi huyu kaka anavyompenda na jinsi anavyojisikia vibaya kuishi gerezani na kukosa kuishi na mwanamke anayempenda,mwanamke wa ndoto yake,kiukweli yule dada nilimuona ni mtu aliyekwisha mkatia tamaa mshkaji lakini mimi nilimwambia mapenzi ya kweli uwa hayafi,mapenzi ni kuvumilia na kama kweli unampenda utamvumilia na siku moja atakuwa huru na mtaungana tena uraiani na kuishi yale maisha mliyokuwa mkiishi awali,lakini mtu akiwa gerezani na hasa ambao wana miaka mingi gerezani watu wao wa karibu wanakuwa na ukaribu siku zile za mwanzo lakini kadri siku zinavyosogea watu huchoka na huyu ndio binadamu alivyo,atakuwa na bidii sana mwaka wa kwanza,mwaka wa pili,ukianza mwaka wa tatu anaanza kuchechemea baadae aah anaanza kuchoka,anachoka kweli kweli anaona kwani nini na jamii nayo watu wako tofauti,mtu ameshaenda gerezani miaka thelathini unamngoja wa nini,huyo mtu amefungwa kifungo cha maisha unamngoja wa nini ushindwe kuendelea na maisha yako,watu wana mapokeo tofauti mwingine anaanza maisha mapya,mwingine anavumilia lakini unamuona hizi ni dalili za mwisho hizi kachoka kabisa lakini ujumbe mimi kama mjumbe nilifikisha na nilimwambia ntakuwa nakuja mara kwa mara kukusalimia na kukujulia hali kwa namna moja au nyingine lakini ni mwanamke ambaye maelezo yangu aliyapokea kikawaida tu "nashukuru,asante" yaani hivyo.

Nashukuru baada ya muda nikapata gari lakujishikiza kama deiwaka yaani gari lina dereva wake nami nakuwa kama namsaidia pale anapokuwa amechoka,kaka ndio aliniunganisha kwa huyo jamaa mwenye gari nikawa napigapiga mishe ujue ukitoka jela inakuwa sio rahisi kurudisha uaminifu katika jamii inayokuzunguka,ni watu wenye imani kubwa kwako tu ndio watakaothubutu kuweza kukupata tena nafasi ya kukukabidhi gari wao wanajua ni changamoto tu za kimaisha umekutana nazo tena haukuhusika kiukweli inabidi mtu akujue kwa ukaribu sana kama huyu mtu ananipa gari analerax na naenda na kurudi salama,kweli maisha yakawa yanaenda na Mungu akajaalia nikawa napata vijipesa kidogo nakumbuka nikaenda kununua vifaa kidogo nakumbuka ilikuwa ni peni,rula rula,madaftali na nikaenda kuwacheki wale watoto wa mshkaji,nikaenda kuwatizama wale watoto nakuwapatia yale mahitaji na pia nilibahatika kununua na chakula,nilinunua unga,mchele,mafuta,nilinunua nyama,mafuta kile kidumu kidogo yaani nikaenda safari hii angalau na kifurushi,vifaa vya watoto nilibeba hivyo vichache ingawa waliniandikia vingi,najua mazingira ya pale vyakula ilikuwa ni kitu bora zaidi kukipa kipaumbele katika nilivyochukua,nimefika Mungu mwema nikamkuta na yule mama na akanambia "umekuja tena?" Nikamwambia "ndio bwana nimekuja tena,nimekuja kuwaona hawa ndugu zangu" ilikuwa ni siku nzuri tena ukitilia maanani ilikuwa ni jumamosi wakanambia anko umekuja? Yaani walinikumbuka,nikawaambia "

Si mnakumbuka niliwaambia kuwa ntakuja? Mambo kati hapa hayakuwa rahisi sikupata pesa haraka yakununua vitu ndio maana nikachelewa lakini nimekuja" nikawapatia vitu vyao na chakula,awamu hii yule mama angalau alinipokea vizuri akasema "eeh una ujumbe gani mwenzetu" nikamjibu "sina ujumbe wowote nimekuja tu kwa ajili ya kuwaona hawa ndugu zangu" akasema "haya tunashukuru" nikazungumza na watoto nakuwakabidhi vitu vyao japo sikuwa nimewakamilishia nikawaambia kuwa nitakuja tena na waandike vingine wanavyovihitaji,kwahiyo vile ambavyo sikuvinunua wakaandika na vingine ndio maana kaka anasema mwenzetu umekuwa na familia siku hizi lakini ni mzigo ambao niliubeba ndani yangu kwa kuwaona hawa watoto ambao hawana hatia yoyote,niliondoka hapo nikiwa na furaha kwelikweli na nikiwa na amani sana kwamba leo mimi nimefanikiwa kuwapa chakula watu ambao pengine wangekula mlo mmoja au kesho labda wangekula mlo mmoja au wangeangaika kwenda kuombaomba lakini mimi kwa mchele kidogo,kwa mafuta nimewastili siku mbili tatu watapata chakula kizuri,nilirudi kwa furaha na nikalala usingizi mzuri sana.

Pilikapilika ziliendelea na huku nikiendelea kumuelezea kaka kile kinachoendelea kuhusiana na mimi kwenda kuwatembelea hawa watoto,nilienda tena kuwatembelea hawa watoto,na nikaenda tena,nakumbuka nilienda kama mara tano kwenda kuwatembelea hawa watoto na kila ninapoenda kile nilichobarikiwa naenda kuwapelekea,sasa wameshanizoea na huyu mama alishanizoea hata siku moja alishaniambia "wewe ni rafiki wa baba ...(akitaja jina la mtoto wake) ina maana mmejuliana gerezani,unamjua mtu huyu?" Nikamwambia "sitaki kujua chochote ninachojua ni mtu mwema,tulipokuwa gerezani tumeishi vizuri na hili ni ombi lake kwangu na kwa sababu mimi nipo uraiani hawa wamekuwa kama wadogo zangu"
Muda ukaenda baada ya kuwatembelea hawa watoto na nikaona sasa ni wakati wa kwenda gerezani kumsalimia ndugu yangu,ameshakuwa ndugu yangu angalaunimpashe jinsi mambo yanavyoenda uko uraiani na jinsi watoto wake wanavyoendelea vizuri na maisha yanaendelea,nilipofika gerezani awamu hii na kupata nafasi ya kuzungumza na huyu kaka ambaye mimi nilimkuta gerezani na kumuacha uko viko vitu aliniambia nilishangaa sana!




Itaendelea!
shikamkono01 tunasubiri mwendelezo boss
 
MKASA WA KUSISIMUA WA ROJAZ:
katika kipindi cha sitasahau cha radio free Africa



Sehemu ya 4



Kitendo cha kuwa huru kiukweli nilimshukuru Mungu sana na kujisemea peke yangu moyoni kuwa ukimuona mtu anamfanyia hila mwingine na kupelekea huyo mtu kupelekwa jela ujue huyo sio mtu mzuri katika maisha yako,nilishukuru kwa kuwa haki imetendeka na imebainika kuwa kuwa mimi sio mhusika wa lile tukio ingawa haikuwa ndani ya siku moja au mbili lakini ukweli umejulikana,nimerejea sasa uraiani na maisha yanaendelea na nashukuru kwa uhuru nilionao kuweza kujiamulia mambo yangu,ndugu jamaa na marafiki walijitokeza wenye kunipongeza,wenye kunipa pole yote hayo niliyapokea lakini nina ahadi mimi nilimuahidi mtu nikiwa kule gerezani,huyu mtu nimekutana nae gerezani,huyu mtu aliniomba sana niende kuitembelea familia yake alinipa maelekezo tena alizungumza nami mengi kuhusiana na familia yake hasa kuhusu watoto wake kuwa kuna mwanamke ambaye alizaa nae hao watoto lakini kwa wakati huu hawako kwenye mahusiano na pia ana mchumba wake kwahiyo haya maelekezo yote nilikuwa nayakumbuka nyakati hizi wakati nipo uraiani,zilipita kama wiki tatu hivi nikawa nasikia kama mzigo ndani ya moyo wangu kwanini niahidi kitu alafu nishindwe kukitekeleza ni kweli kwamba nimeshindwa kwenda kuwaona hawa watoto?

Nikasema hapana na kwakuwa nilikuwa na vijisenti kidogo kwa sababu nimetoka gerezani familia yangu ipo nashukuru walinishika mkono na nikawa hapa nyumbani,nilitumia kapesa changu kidogo kwa kununua nyama kilo moja nakumbukb na nilinunua sukari nusu kilo nilivibeba nikiwa na dhumuni la kwenda kuitizama familia ya mtu ambaye nimekutana nae gerezani na wala sikuwa namjua kabla ya hapo yaani tumekutana gerezani,nikafata maelekezo hadi nikafika lile eneo ambalo nililoelekezwa,kweli nilifika na kweli ndicho nilichokutana nacho,nilikutana na mwanamke mmoja,mwanamke huyo alikuwa mnene na mweupe sana,alinikaribisha na nikamueleza ujumbe ambao nilikuwa nimepewa na rafiki wa kule gerezani,nakumbuka sentensi ambayo alinambia huyu mama "eeh kwahyo amekuambiaje?" Hii ndio sentensi ya kwanza huyu mama alinambia nami nikamwambia "amenituma nije kuwasalimia watoto" akanambia "eeh ukishawasalimia?" Nikamjibu ndio alivyoniagiza kuja kuwasalimia angalau nizungumze nao na kuwaeleza jinsi baba yao anawapenda sana na siku zote anawaombea baraka,akasema "hayo maneno nimeshayasikia sana je yanasaidia nini kwa watoto wangu,yanasaidia nini?

Kiukweli huyu mama hakunipokea vizuri lakini nilishapewa tahadhari toka kule gerezani kuwa huyu mama ni mkorofi sana,sasa kwa sababu nilishaelezwa hayo ilibidi tu niwe mpole,akaendelea kunichamba "kwahiyo uko gerezani hakuna kitu anachona sisi kinatufaa zaidi ya hiyo nyama na sukari,kwahiyo tunaishi kwa ajili ya nyama na sukari? Hao ndugu zake washenzi wasio na maana kila siku napata ujumbe ntasaidiwa ntasaidiwa je nasaidiwa kitu gani? Ameharibu maisha yangu mbwa yule" akaanza kutamka maneno ya kashfa kumuhusu kaka yule na kiukweli ukiniuliza mimi nafahamu mengi kiasi gani kumuhusu yule kaka kule gerezani kiukweli sijui na hauwezi amini ni machache ambayo yeye amenieleza na upande wa pili wa ubaya wake mimi siuelewi lakini ni mtu aliyenifanyia wema nyakati tukiwa gerezani na alikuwa mtetezi wangu katika mambo mengi sababu gerezani kuna maisha yake uko,kuna watu wababe,wakorofi lakini kama kuna mtu anakukingia kifua unamuona huyu ni kaka,kaka mzuri kwahiyo hajawai kunitendea ubaya wowote na inawezekana kweli ni mtu mbaya kwa sababu alishanieleza kuwa yupo hapo kwa sababu alitakiwa kulipia yale yote aliyoyatenda uraiani,anatumikia kifungo anachoamini alistahili,huyu mama alizungumza mengi nami nikawa nimetulia tu namsikiliza na nikamwambia "tuzungumze tu kwani mimi ni mjumbe tu na mjumbe hauwawi,mimi ni mtu mwema tu ambaye nilifungwa na nikakutana na huyu ndugu baba watoto wako,ni mtu ambaye aliniomba sana nitakapotoka nisiache kuja kuwana watoto wake,sasa ahadi nilimpa na toka nimetoka gerezani ilitakiwa nifanye mapema na nimekuwa nikijisikia hatia kwa sababu nimeshindwa kulitekeleza hilo kwa haraka kwahiyo nimekuja ili kuweza kusikia amani ndani ya moyo wangu" nilimueleza hayo na nikapata nafasi ya kuzungumza na watoto,ana watoto wazuri sana,baba yuko gerezani na kwa mtu mwelevu ukitizama mazingira ulikuwa unapata picha kuwa hawakuwa na maisha mazuri kwahiyo mama anajipigania kwa vile anavyoweza na mama mbabe sana huyu maana hata akiongea tu unajua kama huyu mama ni mbabe,niliwambia watoto bac yao anawasalimia sana na anawapenda na siku moja anaamini atajumuika na nyinyi na nakumbuka mtoto wake mmoja mkubwa alinambia kuwa mama yao aliwaambia hawataweza tena kujumuika na baba yao katika maisha wanayoishi nami nikawaeleza kuwa sio kweli kwani baba siku moja atajumuika nao na wataungana nae na kula nae chakula pamoja na furaha itakuwa katika maisha yao ya kila siku.

Nikawaambia mimi ni anko wao na nitakuja mara kwa mara kuwatembelea na kama kuna uhitaji wa vifaa vyovyote vya shule wataniagiza na ntakaporejea tena ntawaletea hivyo vitu,wakaniandikia vitu vyao ingawa nilikuwa siko poa kivile na ukizingatia nina muda mfupi toka nitoke gerezani lakini mazingira yao yalinisukuma tu kuweza kufanya hilo jambo,mimi ni mwanaume tena mpambanaji nimeguswa sana na hii familia hasa hawa watoto,niliondoka nikiwa najisikia deni ndani yangu tena nakumbuka yule mtoto mdogo aliniuliza "utarudi kweli? Utakuja tena kuja kutuona? Nikamjibu "ntarudi na ntaleta hivi vitu mlivyoniagiza kwa ajili ya shule" nikaondoka zangu kurejea nyumbani na nakumbuka pia nilishea hili jambo na kaka nilipofika nyumbani,nilimueleza kaka jinsi nilivyoikuta familia ya yule ndugu wa kule gerezani,kaka alisikitika sana na kusema "maskini hakuwaza kama siku moja atakuwa mbali na watoto wake tazama sasa future ya watoto inaweza kuharibika kama mama atakosa misingi mizuri ya malezi kwa ajili ya watoto,akijichanganya tu anaharibu watoto lakini kama atasimama anaweza kuwalea watoto wake vyema" nikamueleza jinsi nilivyomuona ni kama mama ambaye ameshajichanganya sana na tukasikitika pamoja na nikamueleza jinsi watoto walivyonipa mahitaji yao ya vifaa vya shule lakini bro mimi navitoa wapi? Kaka akacheka na kunambia "ndio ukapambane sasa mwenzetu umeshapata familia eeh msamaria mwema umejikuta umekuwa na familia ya watoto wawili,mimi sina la kukusaidia nadhani unajua kuhusu hali yangu ya kipesa,wewe pambana bwana ahadi umetoa ipambanie" maisha yakaendelea na kaka kule gerezani nilimuahidi ntakapoenda kwa watoto wake ningekwenda kumjulisha maendeleo yao,kwakuwa mi niko kitaa nikaona sio vyema kukaa tu na ni vyema kusaka dili za kufanya kwakuwa maisha lazima yaendelee,katika kutafuta japo videiwaka na ukitilia maanani nimetoka gerezani kuaminika nako kukawa ni mtihani kwa walio wengi maana wengine akijua ulienda ndani anajua kama ulitenda kumbe uhusiki chochote,kuaminika kulipunguwa maana wanahisi unaweza kumpa gari yako ana mikosi gari ikapata matatizo yaani nikawa nakataliwa kihivyo,maisha yaliendelea kuwa magumu japo kaka alikuwa ananiambia "hivi ndivyo ilivyo kwa wewe kujenga kuaminika inahitaji muda kidogo,wako watakaoona una nuksi,wapo watakaona ulihusika kwa namna moja au nyingine ukweli unaujua wewe na Mungu wako lakini ni muda mfupi tu lakini uvumilivu unahitajika ili mambo haya yapite na tuyaruhusu yale mazuri yaje kwetu"

Familia yangu ilinitia sana moyo,ilinifariji sana,kila ninachojaribu kufanya kwangu kilikuwa hakifanikiwi pamoja na kuwa ni dereva mzuri tu hata deiwaka sipati,kuna siku nikaona ngoja nikamcheki mshkaji kule gerezani nikikumbuka pia nina ujumbe kutoka kwa watoto wake nimpelekee zile salamu watoto wake walinipa ,sijafanikiwa katika ahadi ambazo niliwaahidi,nikaenda na nikapata nafasi ya kuzungumza na mshkaji,mshkaji alinambia "umekuja?umekuja kuniona mimi?"

Alifurahi sana, Nikamwambia "ndio kaka si nilikuahidi" akanambia "nilihisi hautakuja maana siku niliona zinasogea na nikaona ahadi zako zitakuwa kama ahadi za watu wengine walizokuwa wakiniahidi" nikamwambia "hapana lazima ningekuja kwani sijawahi kumuahidi mtu kitu cha uongo sipendi kufanya hayo ya kuahidi alafu nisitekeleze,lakini nimerudi uraiani mambo yamekuwa si rahisi" akasema "najua hayawezi kuwa rahisi lazima ujipe muda" nikamwambia "ni kweli,kweli kabisa nimerelax najipa muda" akanambia "mambo yatakaa vizuri,amini Rojaz mambo yatakaa vizuri,niambie kuhusu watoto wangu" ndipo nilipomueleza mazingira niliyowakuta watoto wake ila wako na afya njema tu asiwe na wasiwasi akasema "wamesemaje? Wamenikumbuka?" Nikamjibu "ndio wanaonesha kukukumbuka sana na wanaonesha kukupenda sana" akasema "mama yao anawafanyia ukatili watoto hataki kabisa hata watoto wanitembelee,naumia sana" niliona jinsi anavyosononeka akizungumza hayo nikamwambia "mambo yatakaa tu sawa,nimewaahidi watoto wako kuwa wewe utatoka siku moja utajumuika nao" akacheka,akasema "mmh eeh wakasemaje" nikamwambia "inaonekana kama walikuwa hawana matumaini lakini nilipowaambia nyuso zao zimeonekana kuwa zenye furaha" akanambia "umewaambia vyema,asante nakushukuru sana,umerejesha furaha yangu na umenifanyia jambo ambalo sikuwahi kulitegemea,kwa hii sentensi naomba uamini ninachokisema,umetenda kwangu jambo kubwa sana,nimekuwa nikitamani nikutane na mtu mwenye utu kama wewe lakini hauwezi amini sijawahi kukutana nae" mimi nikatabasamu na kujiuliza hivi kitu gani cha thamani nimefanya hapa,haya ni maisha yangu ya kila siku kwani nimekuwa nikiguswa na watu wenye changamoto za hapa na pale na mimi ni huyu,mimi ndio Rojaz ninapomuahidi mtu kitu ninachoweza kwa hakika kukitenda lazima nikitekeleze kwahiyo nimefanya haya ndio maisha yangu ya kila siku hakuna wema ambao natakiwa nionekane nimetenda wema,haya ni maisha yangu ya kila siku,akanambia "aisee Rojaz nakushukuru sana umepanda kwangu kitu kikubwa sana,Rojaz unaweza kunisaidia kitu?"

Nikasema "ndio mimi niko hapa" akasema "sawa Rojaz naomba sasa ukamtembelee msichana wangu,najua amevunjika moyo,watu wamemvunja moyo lakini naomba ukanipelekee salamu" nikamwambia "nikamwambie nini? Akasema "najua wewe ni mtu mwema we nenda kazungumze nae tu,ukamwambie jinsi tulivyoishi vyema tukiwa huku gerezani na jinsi ambavyo nilikuwa nikimzungumzia vizuri na jinsi ambavyo nampenda,kitu ambacho kinaniuma ni kukosa uhuru na kuishi na mwanamke ambaye ninampenda" nakumbuka nilitabasamu tu aliponambia hayo,nikamwambia "brother siku utapata chance na utaishi na mwanamke unayempenda" akasema "haiwezekani,hawezi kuningoja mie majira yote hayo,najua na sitamlaumu,sitamlaumu hata siku moja" nikamwambia "sawa" ila alifurahi sana,yaani unafanya kitu kwa mtu yaani unamuona anafurahi mpaka unashangaa alifurahi nini kwa kiwango iki na alisema "umenipa furaha isiyo ya kawaida,baada ya hapo nakumbuka niliondoka nakurudi zangu nyumbani na harakati zangu za kudonoadonoa kama kawaida ziliendelea kama kawaida kwa sababu mambo yalikuwa bado hayajakaa vizuri,kweli siku nilipanga na kama alivyonielekeza nilienda,mimi niliombwa kwahiyo kama niliombwa na nilimuahidi kutenda ndio nilienda sasa,kweli nilikutana na huyo mwanamke na nikafanya nilivyoelekezwa kikubwa nilimpa salamu zake nyingi sana na nikamueleza jinsi huyu kaka anavyompenda na jinsi anavyojisikia vibaya kuishi gerezani na kukosa kuishi na mwanamke anayempenda,mwanamke wa ndoto yake,kiukweli yule dada nilimuona ni mtu aliyekwisha mkatia tamaa mshkaji lakini mimi nilimwambia mapenzi ya kweli uwa hayafi,mapenzi ni kuvumilia na kama kweli unampenda utamvumilia na siku moja atakuwa huru na mtaungana tena uraiani na kuishi yale maisha mliyokuwa mkiishi awali,lakini mtu akiwa gerezani na hasa ambao wana miaka mingi gerezani watu wao wa karibu wanakuwa na ukaribu siku zile za mwanzo lakini kadri siku zinavyosogea watu huchoka na huyu ndio binadamu alivyo,atakuwa na bidii sana mwaka wa kwanza,mwaka wa pili,ukianza mwaka wa tatu anaanza kuchechemea baadae aah anaanza kuchoka,anachoka kweli kweli anaona kwani nini na jamii nayo watu wako tofauti,mtu ameshaenda gerezani miaka thelathini unamngoja wa nini,huyo mtu amefungwa kifungo cha maisha unamngoja wa nini ushindwe kuendelea na maisha yako,watu wana mapokeo tofauti mwingine anaanza maisha mapya,mwingine anavumilia lakini unamuona hizi ni dalili za mwisho hizi kachoka kabisa lakini ujumbe mimi kama mjumbe nilifikisha na nilimwambia ntakuwa nakuja mara kwa mara kukusalimia na kukujulia hali kwa namna moja au nyingine lakini ni mwanamke ambaye maelezo yangu aliyapokea kikawaida tu "nashukuru,asante" yaani hivyo.

Nashukuru baada ya muda nikapata gari lakujishikiza kama deiwaka yaani gari lina dereva wake nami nakuwa kama namsaidia pale anapokuwa amechoka,kaka ndio aliniunganisha kwa huyo jamaa mwenye gari nikawa napigapiga mishe ujue ukitoka jela inakuwa sio rahisi kurudisha uaminifu katika jamii inayokuzunguka,ni watu wenye imani kubwa kwako tu ndio watakaothubutu kuweza kukupata tena nafasi ya kukukabidhi gari wao wanajua ni changamoto tu za kimaisha umekutana nazo tena haukuhusika kiukweli inabidi mtu akujue kwa ukaribu sana kama huyu mtu ananipa gari analerax na naenda na kurudi salama,kweli maisha yakawa yanaenda na Mungu akajaalia nikawa napata vijipesa kidogo nakumbuka nikaenda kununua vifaa kidogo nakumbuka ilikuwa ni peni,rula rula,madaftali na nikaenda kuwacheki wale watoto wa mshkaji,nikaenda kuwatizama wale watoto nakuwapatia yale mahitaji na pia nilibahatika kununua na chakula,nilinunua unga,mchele,mafuta,nilinunua nyama,mafuta kile kidumu kidogo yaani nikaenda safari hii angalau na kifurushi,vifaa vya watoto nilibeba hivyo vichache ingawa waliniandikia vingi,najua mazingira ya pale vyakula ilikuwa ni kitu bora zaidi kukipa kipaumbele katika nilivyochukua,nimefika Mungu mwema nikamkuta na yule mama na akanambia "umekuja tena?" Nikamwambia "ndio bwana nimekuja tena,nimekuja kuwaona hawa ndugu zangu" ilikuwa ni siku nzuri tena ukitilia maanani ilikuwa ni jumamosi wakanambia anko umekuja? Yaani walinikumbuka,nikawaambia "

Si mnakumbuka niliwaambia kuwa ntakuja? Mambo kati hapa hayakuwa rahisi sikupata pesa haraka yakununua vitu ndio maana nikachelewa lakini nimekuja" nikawapatia vitu vyao na chakula,awamu hii yule mama angalau alinipokea vizuri akasema "eeh una ujumbe gani mwenzetu" nikamjibu "sina ujumbe wowote nimekuja tu kwa ajili ya kuwaona hawa ndugu zangu" akasema "haya tunashukuru" nikazungumza na watoto nakuwakabidhi vitu vyao japo sikuwa nimewakamilishia nikawaambia kuwa nitakuja tena na waandike vingine wanavyovihitaji,kwahiyo vile ambavyo sikuvinunua wakaandika na vingine ndio maana kaka anasema mwenzetu umekuwa na familia siku hizi lakini ni mzigo ambao niliubeba ndani yangu kwa kuwaona hawa watoto ambao hawana hatia yoyote,niliondoka hapo nikiwa na furaha kwelikweli na nikiwa na amani sana kwamba leo mimi nimefanikiwa kuwapa chakula watu ambao pengine wangekula mlo mmoja au kesho labda wangekula mlo mmoja au wangeangaika kwenda kuombaomba lakini mimi kwa mchele kidogo,kwa mafuta nimewastili siku mbili tatu watapata chakula kizuri,nilirudi kwa furaha na nikalala usingizi mzuri sana.

Pilikapilika ziliendelea na huku nikiendelea kumuelezea kaka kile kinachoendelea kuhusiana na mimi kwenda kuwatembelea hawa watoto,nilienda tena kuwatembelea hawa watoto,na nikaenda tena,nakumbuka nilienda kama mara tano kwenda kuwatembelea hawa watoto na kila ninapoenda kile nilichobarikiwa naenda kuwapelekea,sasa wameshanizoea na huyu mama alishanizoea hata siku moja alishaniambia "wewe ni rafiki wa baba ...(akitaja jina la mtoto wake) ina maana mmejuliana gerezani,unamjua mtu huyu?" Nikamwambia "sitaki kujua chochote ninachojua ni mtu mwema,tulipokuwa gerezani tumeishi vizuri na hili ni ombi lake kwangu na kwa sababu mimi nipo uraiani hawa wamekuwa kama wadogo zangu"
Muda ukaenda baada ya kuwatembelea hawa watoto na nikaona sasa ni wakati wa kwenda gerezani kumsalimia ndugu yangu,ameshakuwa ndugu yangu angalaunimpashe jinsi mambo yanavyoenda uko uraiani na jinsi watoto wake wanavyoendelea vizuri na maisha yanaendelea,nilipofika gerezani awamu hii na kupata nafasi ya kuzungumza na huyu kaka ambaye mimi nilimkuta gerezani na kumuacha uko viko vitu aliniambia nilishangaa sana!




Itaendelea!
Kazi yako ni njema, hongera kwa hilo
 
Bro Kama wewe ndo ulikua ukiihadithia hii simulizi radio free na mzee mzima sky Walker hongera Sana, na wewe kwangu umekua kiigizo chema kabisa katika kuwatendea wema watu wasio na hatia, naikumbuka ile beat iliokua inaplay background wakati wa simulizi, nlikua najitahidi Sana Kila jumapili niwe pembeni ya redio. Ni miongoni mwa vipindi Bora kabisa vya redio kuwahi kutokea hapa Tanzania, nasubiri simulizi ya kuitafuta kwa madiba na Mambo ya "makina"
 
Back
Top Bottom