SHUKRANI SANA:
Ndugu zangu nawashukuru nyote kwa kutumia muda wenu kusoma mkasa huu wa Rojas na hapa ndio hitimisho lake,tukutane tena katika mkasa mwingine siku nyingine kwani haikuwa jambo rahisi ukizingatia kutoa maneno katika mfumo wa sauti kuleta katika mfumo wa maandishi kulileta changamoto kidogo ili kuweza kuifanya hadithi ibaki na mvuto wake ule ule,kuna baadhi ya maeneo ilinilazimu kuongeza nyama ili kuweza kuleta muunganiko kwani upande wa audio kulikuwa ama kukatikakatika,kukosekana kipande kirefu au episode kutosikika kwa zaidi ya dakika 10 hapo ikanibidi nijiongeze.
Mkasa huu umenipa mzuka wa kufanya kazi nyingine na nyingine na kama kuna mtu kati yetu anakifahamu kisa chochote kilicho katika mfumo wa sauti na akapendezwa tukilete jukwaani asiwe mchoyo aniPM nami ntatimiza wajibu wangu kama mwana jukwaa,mbarikiwe sana!