shikamkono01
JF-Expert Member
- Mar 26, 2016
- 685
- 2,055
- Thread starter
- #521
OkUsijali kabisa nakutumia tu 😄 hapa kati mambo yamekuwa mengi sana
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
OkUsijali kabisa nakutumia tu 😄 hapa kati mambo yamekuwa mengi sana
Ngoja kuna mambo ya kifamilia niyaweke sawa kwanza then ntakuja naogopa nisije kuweka kisa kikawa episode hazishuki kwa wakati nikawa nashushiwa matusi bure
Ndio uandishi wangu uko hivyo na huo mrejeo rejeo wa sentensi ndio yule msimuliaji alivyokuwa anaweka swaga zake nami akaniathiri,nimeshafanya kazi za kutranscribe ndio maana inakuwa sio tabu kivile kusikiliza na kuandika😂😂Kwahiyo mkuu unasikiliza ndo unaandika,aisee umefanya kazi kubwa sana tena sanaa.
Hongera kuwa na huo moyo aisee
U deserve to be Senior member! UbarikiweNimesoma episode zoote kwa taratibu sana., kuna mambo mengi sana yanayofundisha nimeyapata kutoka kwenye hii simulizi yako., nasema ahsante sana ndugu. Nimkweli siri katika maisha yetu ni muhimuj sana, pesa hubadilisha mwenendo wa mtu ila watu hubadilisha mwenendo wa mtu zaidi.
Ni mtazamo tu wala sijengi chuki!Hadithi hi ilitakiwa iwe na sehemu 10 tu imerefushwaaaa
Ooooh jameeeenyyyyyyyyyyyyyy poleeeeeeDaah kipande cha rojas na yule rafiki yake wa gerezani mpaka machozi yamenitoka alivyokuwa anamwambia rojas kuhusu pesa zake ukweli siku zote mchungu na unauma sana
Mkasa wa kusisimua wa Rojaz katika kipindi cha sitasahau cha radio free africa
Sehemu ya 11
Moyo wangu unatunza siri na moja kati ya vitu nilimuahidi huyu kaka kule gerezani ni kuhusiana na kutunza siri,niliifanya siri hii kuwa ya sisi wawili peke yetu na yeye akiniambia "nimekupa siri ya maisha yangu sijawahi kumpa mtu yoyote hii siri mahali nimetunza pesa sikuwahi kumwambia mtu na ndio maana kile kijumba watu hupita na pengine wengine uenda kufanya shughuli zao uko na hawajawahi kujua chini ya ardhi ziko pesa nyingi,mimi nikamuahidi ya kwamba nitaitunza siri hii lakini kaka amezungumza nami katika lugha ya urafikiya undugu kabisa,nasikia moyoni mwangu angalau niweze kusema nae jambo,nikamwambia kaka "kuna vitu ni vigumu sana hata kusema,naogopa hata kusema" kaka akanambia "ni kitu gani mdogo wangu kama ni cha hatari niko tayari hata mimi kuingia kukusaidia sitamani kukuona unapata matatizo,unajua" nikamwambia "kaka najua" nikaketi na kaka na nikamwambia "hii ni siri,ni siri ambayo sijawahi kutaka kumwambia mtu yoyote yule" kaka akanambia "hata mimi ntaifanya kuwa siri kwa sababu wewe mdogo wangu umetaka iwe siri,niambie" ndipo nilipoanza kumwambia kaka ila nilimwambia kwa uchache sikumueleza kwa upana kama safari ya huyo mtu na mimi ilipoanzia,nilimwambia "kaka ni kweli nina pesa,unaona nafanya maendeleo haya unaona ninavyoagiza magari,unaona jinsi nimefungua biashara yaani kufungua duka la jumla na nimeweka pale kiasi cha milioni ishirini,ni kweli nina pesa lakini kaka hizo pesa si zangu,ni pesa za mtu na huyo mtu amekuwa anatamani kufanya makubwa sana lakini yeye amekosa hiyo bahati ya kuishi maisha ambayo mimi naishi ya uhuru" kaka anakanambia "una maanisha nini,ni nini ambacho unamaanisha? Ni mtu gani ambaye kakosa uhuru,ni vitu gani unazungumza,nikamwambia "kuna mtu amenipa majukumu ya kumfanyia vitu vyake kwakuwa yeye hawezi kufanya hivyo" akanambia "ni nani huyo na kiasi gani cha pesa akupe hata uweze kuagiza magari mengi kiasi hiki na hizo pesa unaweka wapi mwisho wa siku uweze utahatarisha maisha yako na hizo pesa unazijua amezitoa wapi? Kaka alinihoji kwa kuonesha kunijali sana na ni kweli kaka ananijali sana,nikamwambia "mtu huyu yuko gerezani kaka" kaka akashangaa sana "yupo gerezani? Sasa mtu yupo gerezani anawezaje kukupa wewe pesa? Nikamwambia "kaka ni stori ndefu sana ila elewa niko na pesa ila si za kwangu,mtu huyo yuko gerezani anatumikia kifungo na ameniomba nimsaidie kufanya hivi vitu nikiwa uraiani,kwahiyo nimechukua majukumu yake nafanya vitu ambavyo yeye alitamani kuvifanya ili siku moja akitoka gerezani aone hatua ameshaipiga kuliko pesa kuendelea kukaa sehemu bila kuzalishwa" nakumbuka kaka alinambia "kwahiyo umekaa chini na kunitungia kastori,umenitungia kasimulizi kakusadikika flani hivi,iko kitu kinawezekanaje? Hakuna kitu kama iko unanidanganya" nikamwambia "kaka nilihisi hata nikikwambia hautaweza kuniamini" akanambia "ni nani uko gerezani,ni nani ambaye awe na pesa hizi akupe wewe,hana ndugu? Hana watu wa karibu akupe wewe?
Nikamwambia "kaka huyu ni mtu ambaye yuko gerezani ana muda kidogo lakini ndugu zake walimtelekeza uko gerezani,hakuna watu wamekuwa wakienda kumwangalia hata kumtia moyo,hakumuona mv wa kumpa hilo jukumu,kipindi mimi naenda gerezani na nikaanza kuwa na urafiki naye ndio kipindi aliniamini nakuniona ni mtu mwema na akaniomba kama naweza kuwa mwaminifu kwake,ndicho kaka kilichotokea" kaka akaniuliza "ndio mwenye wale watoto uliokuwa ukijipa stress? Nikamwambia "ndio kaka" kaka akaanza kuamini katika nnachokisema baada ya kuendelea kumwambia lakini kaka aliyashangaa sana haya maelezo ambayo mimi namwambia nakumbuka sikutaka kumuweka kaka kiundani zaidi niliongea hayo tu kwa uchache,aliniuliza "pesa ziko wapi? Nikamwambia "kaka siwezi kukwambia" akasema "mimi ni kaka yako" nikamwambia "kaka naweza kukwambia vyote lakini nilimwambia mtu huyo sitasema kwa sababu ni maelekezo yake aliyonipa,kama nilivyokwambia kaka hizi pesa si za kwangu ila yeye aliniruhusu nifungue duka,lile duka la nafaka ni la kwangu lakini kuhusu magari sio ya kwangu,hivi vitu vingi sio vya kwangu"
Nilimueleza kaka yangu kwa upendo kabisa kwa sababu huyu ni kaka yangu na niko nae karibu sana katika mahangaiko yangu,katika mateso yangu kwa mfano kipindi kile nimekwenda gerezani ni kaka ndio alinipigania mpaka hatua ya mwisho akunyamaza,hakutulia mpaka alipoona mimi mdogo wake nimeachiwa huru kwahiyo yupo na mimi siku zote kwahiyo naamini nimemwambia kaka yangu naamini nimemwambia mtu sahihi,nilishea na kaka hayo na kaka alizidi kuniuliza maswali lakini sikujibu yote kwa sababu sikutaka kuzungumza kila kitu,aliniuliza "sasa ulipataje hizo pesa,alizihifadhi wapi?" Hayo yote aliniuliza lakini sikusema.
Baada ya kumwambia kaka hayo maneno nakumbuka niliporejea nyumbani nilisikia moyo wangu unauma sana,nilisikia moyo wangu unapatwa na uchungu kwanini nimesema,nilijilaumu kwanini kinywa changu kimezungumza siri ambayo nimeitunza kwa ahadi kuwa nitaitunza na sitaisema,mbona naumia hivi nami naona nimemwambia mtu sahihi,mbona nimemueleza kaka yangu kwanini nasikia hivi vibaya? Sikulala mpaka asubuhi,ushawahi kufanya jambo alafu ukawa unajilaumu kwanini unafanya? Mimi nilisikia hatia ndani yangu kwanini nimemwambia kaka,kama ningenyamaza kwani nini kingetokea,angenifanya nini? Niliona nimekosea,sikutakiwj kufanya hivyo.
Lakini unajua neno linapotamkwa linakuwa lishatamkwa unakuwa hauna namna yoyote yakuweza kulifuta tayari linakuwa lishatamkwa,nakumbuka kulipopambazuka na siku mpya kuingia kaka alinitumia meseji ikisema Rojas nataka tuongee,naomba nije nyumbani kwako tuzungumze,nilikuwa na ratiba za mishe zangu za hapa na pale lakini kaka yangu namheshimu sana na kama anasema ana jambo anataka kuja nyumbani litakuwa ni muhimu sana,nikamwambia kaka sawa na kaka alikuja nyumbani akanambia "mdogo wangu sijalala usiku kwa maneno uliyoniambia nimekosa usingizi,sijajua uko katika hatari kwa kiasi gani sijui lakini tu kwa experience yangu ya maisha,kwa maisha mimi nimeishi,mimi ni kaka yako najua vitu vingi,napata mashaka sana,nasikia kukosa amani sana kuhusiana na kile umenieleza jana lakini kuna kitu nimesikia amani nacho ndani ya moyo kwa sababu umesema huyo mtu yuko gerezani na hajawahi kumwambia mtu yoyote kuhusiana na hizo pesa,sasa mdogo wangu mimi najambo nataka kukwambia,mtu yupo gerezani na pesa unazo wewe uraiani unajua anatoka lini? Sikujua kaka kwanini ananiuliza maswali kama haya tena akiwa siriasi kweli amefunga safari tuje tuzungumze kuhusiana na hili na nikamwambia "kaka, sijui labda kuna neema itakuja ya yeye kutoka au pengine hiyo neema isipotokea uenda maisha yake yote akamaliza gerezani" "kwani amefungwa kifungo cha maisha? Nikamwambia "kaka kesi ya huyo mtu ilikuwa ngumu sana kwa maelezo ambayo nimepata,alinambia ni miaka 30 lakini nikaja nikagundua yule mtu amefungwa maisha" akasema "amewezaje kukudanganya wakati ni rahisi tu kujua miaka ya mtu" nikamwambia "unamaanisha nini? Akasema "mimi naweza kuifanya hiyo kazi nikajua miaka yake ambayo anatumikia uko gerezani,yaani tujue miaka yake ni mingapi,ni wa kutoka au siwakutoka kwa sababu hapo tupate uhakika" sasa nikawa najiuliza kwanini kaka azungumze hivyo,nikamwambia "yanini kuyajua hayo kwa sababu mimi nimemshauri kitu kwa sababu anazo pesa nyingi alizitafuta katika nafasi yake akiwa uraiani na pesa inanguvu nami nilimshauri ikiwezekana sehemu ya pesa yake ebu atumie uenda akaupata uhuru kwa nguvu akarudi huku uraiani kama ni rushwa au namna yoyote ile itakavyowezekana" nakumbuka kaka akanambia "wewe umshauri maneno kama hayo kwanini? Nikamwambia "kaka ni mtu mwema tu" akanambia "unajua hizi pesa amezitoa wapi? Nikamwambia "hajawahi kunieleza wapi alipozitoa" akanambia "hawa ndio watakuwa watu ambao ni wahujumu uchumi" nikamwambia "unamaanisha nini? Akanambia "kuna watu ambao walijilimbikizia pesa lakini kuna nyakati kuna msako uwa unapita na watu uhofia kuhusiana na hizo pesa kwa sababu hawaziweki benki wanaogopa,watu wengi kumekuwa na historia walikuwa wakichimbia pesa ardhini,vipi hizi pesa hakukwambia ukazichukue ardhini?
Nikashtuka,nikamwambia "kaka kwanini tunazungumza haya na wakati tulishazungumza jana na tumeshamaliza kwa sababu niliona nikushirikishe kaka yangu" akasema "ah umenishirikisha ila wewe bado mdogo hujui vitu vingi mimi ni kaka yako,sasa mimi ni kaka yako mimi najua maisha na najua vitu vingi,unajua ni kwanini huyu mtu kakutafuta wewe? Kwanini uwe wewe ushawahi kujiuliza? Hana watu ambao ameshawahi kufanya nao dili? Hawapo? Kwanini iwe wewe? Unajua kwanini? Nikamwambia "ndio najua" akaniuliza "unajua nini? Nikamwambia "najua kwakuwa tulikuwa marafiki,tuliishi kwa furaha na akaona mimi ni mtu ambaye sina shida yoyote" akasema "sio kweli,iko sababu nyuma ya huyo mtu kukutafuta wewe" sasa mimi kweli uenda kaka yangu ana upeo mpana na akili nyingi kuliko mimi siwezi kataa,sasa mimi namuuliza kaka "kwa sababu zipi? Anasema "si unaona hujajua kwanini akutafute wewe,ngoja nikwambie mdogo wangu mitego ya pesa ni mikubwa sana,waweza pesa itumia leo pesa isiyo halali inaweza ikakuletea shida hata baada ya miaka 10 baadae inaweza ikakuhukumu,ikawa kitanzi kwako,ikatesa moyo wako na maisha yako na ndugu zako" nikamwambia "unamaanisha nini" akasema "pesa hiyo siyo halali,hiyo pesa ni pesa haramu na amefanya hivyo ili siku hukumu ikija ikukute wewe na yeye akiwa pembeni ametulia" nikamwambia "sasa litampata vipi mtu aliye gerezani" nakumbuka kaka akanambia "ndio maana nakwambia wewe bado mdogo,uelewa wako bado mdogo haujajua kuchanganua mambo,usalama wako Rojas ni kukata kila connection ya wewe na huyo mtu wa gerezani na kukata connection na majukumu yote aliyokupatia na hizi pesa zisiwe chini yake,ziwe ni pesa zako sijui kama unanielewa? Kaka alinambia maneno hayo tena ni siku ya pili tu yaani nimemwambia jana na leo ananiamkia asubuhi kumepambazuka kaka anakuja na ujumbe kama huu,nikamwambia "kaka mimi Rojas siwezi kufanya kitu kama hicho,siwezi kufanya kama hivyo,siwezi kutumia pesa isiyo ya kwangu kuifanya ya kwangu siwezi,siwezi kaka kufanya hivyo,ahadi niliyompa mtu huyu nitaitimiza siku zote siwezi kuikengeuka hata kiku kimoja maana nimetafuta pesa katika nyakati zote sikuwahi kupata kwanini nimsaliti mtu ambaye amekuwa mwaminifu kwangu ambaye ameamua kunitunuku na kunitoa katika umaskini nakunipa maisha mengine,kwanini kaka unazungumza maisha ya ushetani hivyo" nakumbuka kaka akacheka na akasema "ushetani? Mdogo wangu kweli hauyajui maisha? Nazungumza mambo ya maana wewe unasema ushetani mimi nazungumza ushetani?" Kiukweli sikupenda kabisa kauli za kaka kabisa na nikamwambia "ndio maana moyo wangu umekosa amani kabisa kukushirikisha,hukustahili kunambia maneno haya tena ikiwa mapema kama hivi" akanambia "nakwambia mapema kwakuwa wewe hujui,wewe bado mdogo hujui kadri unavyozidi kwenda gerezani,wewe si kila siku uwa unaenda gerezani mwisho wa siku utastukiwa,huyu mtu bado anafatiliwa kule gerezani usihisi watu wametulia kumfatilia nisikilize mimi ninachosema" kaka akanambia "huyu ni mhujumu uchumi hawezi kukwambia na mimi ndio nakwambia sasa kwa sababu najua haya mambo ziko nyakati hata wewe ulikuwa bado mdogo kuna watu walifanya hujuma,walihujumu uchumi hawa watu walifanya namna nyingi hawajaacha kufatilia siku mpaka anapokufa ndio huyo mtu ndio wanaacha hivi ninakwambia we si uwa unaenda si una route za kwenda? Unavyoenda watu wameshachora ramani,kuna mtu ana dot dot alikuwa gerezani ametoka lakini anaendeleza ukaribu na huyu mtu,mdogo wangu sasa hivi unakamatwa,unakamatwa na unaniingiza kwenye matatizo kata hiyo connection haraka sana usiende gerezani unakamatwa na ninavyozungumza hivi na pengine si siku nyingi kutoka leo na umezungumza kwangu kwa sababu Mungu hataki upate matatizo"
Kaka anaendelea kunambia vitu yaani mimi naenda gerezani kila siku sikuwahi kuwaza hata siku moja kuwa hizi route za kwenda gerezani ninazofanya labda zinaweza zikawa na ishara yoyote lakini kaka anasema huyu mtu bado yuko kwenye uangalizi kwani amehukumiwa lakini haimaanishi kwamba ameachiwa,huyu bado anafatiliwa yuko kwenye uangalizi.
Toka kaka amezungumza siku ile alinipa hofu,nilianza kuwa nahofu moyoni mwangu kwa maneno kaka aliyoniambia,nakumbuka kama baada ya siku mbili toka siku zile tumezungumza na nikamkatalia kaka akaja na akanambia kitu cha ajabu sana,mimi nilizungumza na kaka na sikuwa nimemtaja mtu kwa majina yake ambaye ndiye yuko gerezani,ambaye ndiye amenipa hili dili na mimi nafanya hivi katika mazingira na sikumuweka kaka kiuwazi sana,kaka alinijia na jina kamili,jina kamili la yule ndugu kule gerezani[emoji23] na akanambia alikuwa gereza flani na akapelekwa gereza flani,yaani amemjua sasa kuliko hata mimi,kuliko mimi ambaye nafanya nae kazi katika mfumo ambao nimekuambia na akanambia uwa naenda gerezani mara ngapi (akanipa idadi),niliogopa sana na nikamuuliza "kaka umeyajuaje yote haya" akasema "nimejua kwakuwa mimi ni mkubwa kwako,mimi ni kaka yako,najua mambo kuliko wewe,hivi unajua kuna watu pale gerezani kila unapoenda kumtembelea uwa wanarekodi? Unajua wewe mpaka sasa hivi inawezekana umeshaanza kufatiliwa mpaka unavyoondoka asubuhi mpaka jioni shughuli zako unavyofanya na watu unaoongea nao,unajua iko kitu?" Niliogopa sana na kaka akasema "uko unatazamwa mdogo wangu,watu wanakufatilia" nikamuuliza "kaka umejuaje,umeyajuaje haya?" Kwa sababu kaka yangu ni mtu wa kawaida tu,ni mtu wa kawaida kusema amjue hadi mfungwa hivyo mimi nilivyomueleza hadi apate connection na kujua mimi nilienda siku flani na siku flani huyo ni mtu wa namna gani,si unaona unaogopa,unajua hii sentensi ninayokwambia maana yake nini,maana yake yule mtu ni kweli siku zimepita ila bado anaendelea kufatiliwa na amemtafuta mtu mdhaifu mdogo ili isiwe rahisi mtu yoyote kujua lakini mambo yashajulikana,unajua uko katika hatari kwa kiasi gani? Unajua?
Niko hapa kaka yako nataka nikusaidie,nataka nikusaidie,utapata matatizo upigwe kifungo cha maisha,kwanini hajatumia ndugu zake,kwanini akutumie wewe? Maneno ya kaka yalizidi kuniogopesha na labda kutokana na umri wangu sielewi lakini niliogopa,naogopa kwenda gerezani,sitaki kwenda tena uko.
ITAENDELEA!
Sawa mkuuNgoja kuna mambo ya kifamilia niyaweke sawa kwanza then ntakuja naogopa nisije kuweka kisa kikawa episode hazishuki kwa wakati nikawa nashushiwa matusi bure
Aiseee, hatariMkasa wa kusisimua wa Rojaz katika kipindi cha sitasahau cha radio free africa
Sehemu ya 12
Hofu,hofu,hofu,kiukweli hofu ilinivaa na nikamwambia kaka "mimi sijui hizi taarifa umezipata wapi,inawezeka nipo katika hatari lakini mimi nipo tayari kuipokea hiyo hatari kwani siwezi kuvunja makubaliano tuliyokubaliana na yule mtu,siwezi kufanya hivyo hata siku moja,mimi ntakuwa mtu wa ajabu sana" na kaka amesema amenitumia mimi kwa makusudi kwanza ni kijana mdogo ni vigumu mtu kugundua kama amekutumia wewe na amekataa kutumia ndugu zake kwa sababu hataki kuweka ndugu zake kwenye matatizo ila anakutumia wewe awanufaishe ndugu zake" nilikataa na hata nilipopata muda wa kuwa mwenyewe niliyakataa maneno ya kaka,niliyakataa alafu nikajisikia kuugua ndani kwanini nimeyazungumza kwa sababu nilikuwa na amani kabla sijazungumza,nilifanya mishe zangu kwa amani kabla sijatoa siri hii,kaka aliendelea kunisumbua toka nilipomueleza kuhusu zile pesa,kaka alinisumbua sana alitaka tuonane huku akinitumia meseji za vitisho na hasa kaka alichokuwa ananitishia ni kwamba mimi nafatiliwa kwa sababu ya movement ambazo nimekuwa nazo kule gerezani,hofu ya kwenda gerezani ikaingia kwangu na nikajikuta nahofia kwenda tena gerezani,nilikuwa katika msongo mkali wa maisha yangu.
Nilitoka na kwenda kwa watoto wa mshkaji wangu,nilienda kuwatizama watoto kwani mpaka sasa hivi ilipofikia wanaishi katika mazingira mazuri kwa sababu nilishawatoa kule walipokuwa wakikaa mwanzo,sasa wanakaa pazuri,wanasoma pazuri na mama yao ana majukumu ya kazi pia,nilipoenda kuwatembelea walifurahi kwani sasa mimi nimekuwa moja kati ya majawabu kwenye maisha yao,wananihesabu sasa mimi ni ndugu,ni anko mzuri,niliona kama ni watu ambao naweza nikakaa nao nikajisikia nafuu kutokana na msongo wa mawazo nilioupata ghafla,kwa muda ambao nilikaa na hawa watoto walizungumza na mimi kwa upendo sana kwa mfano huyo mkubwa alisema "anko nashukuru sana nafikiri bila wewe sijui tungekuwa katika mazingira gani lakini umetufanya tunaishi katika nyumba nzuri,umekuwa kama malaika kwangu,mdogo wangu na hata mama,sasa hivi hatupiganii chakula kwani tunakula vizuri na tunakula tunachokitaka,nashukuru sana" huyu mkubwa alinambia maneno haya.
Moyoni mwangu naona nafanya kitu kilicho kizuri kwa sababu watoto hawa walikuwa katika mazingira yasiyo mazuri hata nyumba waliyokuwa wakiishi na sasa wana furaha ina maana sasa watasoma vizuri kwakuwa ada inalipwa kwa wakati,nilitumia muda mrefu kukaa hapa na nakumbuka nikiwa hapa kaka alinipigia simu na nikapokea,kaka aliniuliza "uko wapi" nikamwambia "nipo tu kwenye mizunguko ya hapa na pale" akanambia "usiwe ukawa umeenda uko gerezani" nikamwambia "hamna"" akanambia basi njoo tuonane tuongee maana sasa hivi naona unanikwepa,ukiongea na mimi kwenye simu unakuwa kama hutaki,nilipita ofisini kwako pale,mbona kama sikuelewi elewi sasa hivi" nikamwambia "kaka niko na majukumu hapa nafanya nikitoka nitakutafuta" akasema "sama kuna jambo la msingi nataka tuongee" nikamwambia "sawa".
Baada ya kuona yatosha kukaa hapo nikaondoka na kumtafuta kaka,kaka alinambia "utanikwepa mpaka lini,mimi ni kaka yako,hauwezi kunikwepa kwani damu ni nzito ndugu yangu,utanikwepa mpaka lini" nikamwambia "kaka naomba tuwe na mipaka,najua unanionea huruma sana na haupendi nipate matatizo yoyote yale lakini kaka siwezi kukata connection yoyote na mtu yule,nilimuapia mbele ya Mungu na maswali unayoniuliza sina majibu yake na kuna vitu nilikuambia siwezi kukwambia na nakusisitizia siwezi kukwambia,sijui alipopata pesa na hajawahi kunambia alipozipata ninachojua ni pesa halali na zinasaidia watu kwa namna moja au nyingine kwani wenye uhitaji wanapata mahitaji hilo ndio latosha na mimi wajibu wangu ni kutimiza kile ambacho angekitimiza yeye kama angekuwa uraiani,sijaona kosa langu na kama kutakuwa na hukumu mimi nipo tayari kwa kuhukumiwa lakini si kwenda kinyume na makubaliano na yule mtu,adhabu yangu itakuwa ni kubwa sana,moto wangu utakuwa ni wa kuni zilizochochewa sana,siwezi kufanya hivyo kwani naona unajisumbua sana kwa kutumia maneno mengi ya kuniogopesha,niko tayari na kama kuna watu wananifatilia acha wanifatilie nitawajibu majibu ambayo naamini wanastahili kuyapata" kaka akashangaa na majibu yangu na akanambia "huyo mtu ni bora kuliko ndugu yako wa damu? Nikamjibu "ndugu si kuzaliwa tumbo moja tu,ndugu anaweza zaliwa tu katika maisha ya mtu na sio lazima mtoke ukoo mmoja,mtu huyu amenifanya mimi kuwa ndugu yake na ameweza kunieleza mambo ambayo hakuweza kumueleza hata ndugu zake na amenieleza mimi,kaka umesema vyema kwanini anieleze mimi,ameniamini kwa udogo wangu,ameamini kwenye utu nilio nao ndani yangu,unajua kaka mimi ni mtu wa haki na nimekuwa mtu ambaye sipendi kutamani vya mtu mwengine,sijatamani vitu vyake,waweza kuona kama niko katika utumwa lakini mimi sioni kama utumwa kwa sababu ni kweli pesa ni za kwake si za kwangu" kaka akanambia "utakuja kustuka umechelewa sana,huu ni ujinga,yaani wewe akili zako bado changa,mjinga wewe,hujielewi na hauelewi ninachokisema" tulizozana na kaka na kunipa maneno yakunicrush lakini sikujali wala nini,sitaki kuyafata wala kuyaweka moyoni anayoniambia,yeye amepata wapi jina atajua mwenyewe japo iliniogopesha sana kwakuwa mimi sikumtajia majina ya yule mtu.
Niliendelea na maisha yangu huku maswali yakiwa mengi sana,wanajamaa wakawa wanaulizana,yaani mfano hapo mtaani kwenu kuna mshkaji unamjua ile kiundani yaani kindakindaki na hata mzunguko wake wa pesa alafu ghafla anaibuka na kufanya mambo makubwa hadi kuagiza magari,anafungua mabiashara na unasikia taarifa zake za mambo yake ya fedha hapo lazima watu wahoji,amepata wapi pesa zote hizo,tunamjua mtu huyu alikuwa fukara wa kutupa imekuwaje leo? Kwa kupitia mimi nimeamini pesa zinaweza kumfikia yoyote kwa njia yoyote kwani kwangu zimekuja katika mazingira ambayo sikuyatarajia.
Nasikia ndani yangu kumtembelea mshkaji,nasikia sana lakini kwa sababu nilipatwa na hofu nikajikuta siendi na nikaendelea kutulia na kuendelea kuchonga mipango mingine zaidi na zaidi,ninapoona kuna sehemu ya kuwekeza nafanya hivyo na nilielezwa kuna eneo la madini na watu walinipa maelezo kwa undani zaidi na nikaambiwa ukitupa pesa yako uko hautapoteza hivyo nikakata shauri kusafiri kabisa kwenda uko ambako ndiko kunafanyika hiyo biashara ili kujiridhisha,nilienda na nilikaa takribani mwezi mmoja.,kwa huo mwezi wote sikuwa najishughulisha na chochote zaidi ya hayo masuala ya madini lakini nikiwa napata mrejesho kwa biashara zangu nyingine kujua maendeleo yake na nashukuru Mungu kwenye magari kulienda poa kwakuwa niliwapa watu sahihi,watu waaminifu na wenye kujielewa,chombo cha moto usipokuwa na watu sahihi tegemea majanga na kwakuwa mimi nimetokea katika mambo ya magari haikuwa tabu kwangu kupata watu hao na niliwawekea kiwango rafiki ili wote mimi na wao asiumie yoyote kati yetu,sote tunufaike na hata wao walipokuwa wakinihoji kuhusu pesa zangu niliwajibu "usiniulize maswali mengi sana hata wewe majira yatakujia na utapata pesa kikubwa fanya kazi kwa uaminifu" hayo ndio yalikuwa majibu yangu,sasa naitwa bosi na mambo kiukweli yalibadilika sana kwangu,nilitazama biashara ya madini na nikapata elimu ya biashara hii nikaona iko powerful,nikaona nina sababu ya mimi kutupa kete huku kwa jinsi ambavyo niliiona,kwa jinsi ambavyo nilituliza akili yangu,sina elimu kubwa lakini nina utulivu sana wa akili na katika neema ya pesa niliyopata huwezi amini nilichanganyikiwa siku nimeziona zile pesa,nilipata mshtuko (hata wewe waweza kukutana nayo hiyo hali)ukifikiria wingi wake na tena zinakuja kuwa za kwako wewe ndio mmiliki lakini namshukuru Mungu katika hali ya kupata pesa na kuwehuka nilipowehuka mara ya kwanza lakini sikuwahi kutumia pesa katika mambo yasiyo sahihi,mimi ni kijana nikweli,wa kijiweni ni kweli lakini sikuwahi kujiingiza katika makundi ya ulevi na vitu kama hivyo,pesa yangu inatoka kwa ajili ya kufanya kitu sahihi na sio kufuja.
Nilipokamilisha lililonipeleka kule machimboni nikarejea zangu na nyakati hizo kaka aliendelea kunijafuta lakini wakati mwingine nilimfungia tu vioo kwakuwa alivyokuwa anazidi kuniambia nikawa naona kama napokea vitu ambavyo vinaharibu akili yangu lakini ni kaka yangu unajua siwezi kumkwepa siwezi kumfukuza siwezi kumkataa kwahiyo tulikutana niliporejea akanambia" vipi mwenzetu unasafiri unaenda mkoa kienyejienyeji tu" nikamwambia "kaka niko busy sana,niko busy sana" akasema "busy unamtumikia mtu? Yaani nguvu zako,akili zako mdogo wangu tena Mungu amekubariki una kipaji,una kipaji cha biashara unajua,mimi ndio najua hiyo siri kama hujui ndio maana watu wanakutumia,yule mtu atakuja kufight siku anatoka gerezani" nikamwambia "kaka mbona wewe unazungumza vitu vingi,umenitajia majina ya huyo mtu,umenambia hawezi kutoka atafia gerezani mara unaniambia siku atatoka je nielewe lipi" akasema "wewe ndio unaelewa zaidi,wewe si ndio unataka kumfaitia atoke" nikamwambia "kaka nisamehe mimi niliyekueleza ukweli" akasema "sio hivydn mdogo wangu,sio hivyo mimi nimekuja hapa tuzungumze jambo" nikamwambia "kaka sitaki kuzungumza jambo lolote,unaharibu sana akili yangu nakuomba kama kuna mengine yakuzungumza tofauti na ya yule sawa"
Nakumbuka kaka maneno alizidi kuzungumza na mimi lakini zaidi kaka aliniambia "nina shida na pesa" na mimi kaka akiniambia ana shida na pesa wala sioni ugumu moyo wangu kumpa pesa,nilimuuliza "kaka una shida na kiasi gani cha pesa" aliniambia ana shida ya milioni mbili ya kitanzania na nikamwambia "sawa kesho utapitia pale dukani kwangu" yaani pale kwenye duka langu la nafaka,akasema "sawa,tupate muda wa kuzungumza mdogo wangu acha kutumika tu,unatumika tu na mtu kwa sababu gani wakati unaweza kujisimamia mwenyewe" nikamwambia "kaka sawa na ninakuelewa unachosema lakini nakushukuru kwa ushauri" Kiukweli ingawa nilikuwa na woga kwa maneno ya kaka lakini toka nimerejea kutoka kule machimboni hamu ya kwenda kumtembelea mshkaji ilinishika sana,nilijiambia ngoja niende kwani sina namna na nakumbuka nilienda gerezani na nikapata chance ya kumuona na ujue sijaja siku nyingi,mshkaji alifurahi kuniona lakini akanambia "Rojas mbona tena umepotea? Nikamjibu "kwani napaswa kuwa nakuja mara kwa mara kiasi hicho? Akanambia "kwanini Rojas unanijibu hivyo bwana ? Mimi ni ndugu yako na wewe si nimekuambia ndio barua yangu wakunijulisha watoto wangu wanaendeleaje,nitapata wapi taarifa ya kujua maendeleo yao,je wanaishi mazingira gani? Sina chochote kutoka kwako zaidi ya kunieleza kuhusu hali ya watoto wangu" nikamwambia "unisamehe bure nina mambo nimekuwa nikiyafatilia na yamekuwa yananikeep busy" akasema "najua lakini nipe taarifa za watoto" nilimpa picha za watoto ambazo nilipiga nao nyakati flani nilipokuwa nimeenda kuwaona,alifurahi sana,kiukweli alifurahi sana,akanambia "mbona Rojas huna raha? Huna raha nakuona" nikamwambia "mimi nina raha tu,ninakufurahia kwa sababu una furaha" akasema "vipi kuna kitu hakiko sawa?
Nikamwambia "kila kitu kiko sawa" nikamuuliza "haujatamani kutoka hapa na siku moja kuwa huru? Akanambia "hakuna mtu hatamani kuwa uraiani" nikamwambia "unazo pesa za kutosha kwanini tusipiganie utoke gerezani,kuna faida gani ya **** na pesa zimehifadhiwa mahali zaidi ya kufanya kitu cha thamani ya wewe kuwa huru,unajua uhuru ni bora kuliko pesa? Akanambia "Rojas sentensi hii unaizungumza mara nyingi kwa sababu una moyo wa ajabu sana wewe mtu,najua unatamani nitoke lakini Rojas ni ngumu sana kunielewa" nikamwambia "niambie tu mimi nitakuelewa kwanini tusipiganie katika hili" akaniambia "Rojas nafurahi umekuja kwa sababu kuna kitu nataka nikwambie cha msingi sana" nikamwambia "ni cha tofauti na chochote ambacho umewahi kuniambia? Akaniambia "inawezekana,naona unanisisitiza sana kuhusu hili,nitakwambia,nitakwambia sababu" nikiwa hapa ananambia jambo mtu huyu.
Mtu huyu aliniambia "Rojas kwa mfano leo umekuja,nashukuru sana lakini kuna shida kidogo naomba ustop kuja hapa" niliposikia maneno haya nilishtuka sana na nikamwambia "kwanini? "Yaani Rojas kuna vitu vingi sana,kuna vitu vingi hadi nahisi kuchanganyikiwa" nikamwambia naomba aniambie ukitilia maanani kaka ameshaniambia hiyo sentensi,hivi vitu anavyoniambia pengine kweli kaka vitu anazungumza labda vina ukweli,nikamwambia "kwanini unashindwa kuniambia,niambie" akaniambia "kuna mtu yoyote ambaye ulishawahi kuzungumza nae chochote kuhusu mimi? Nikamwambia "hapana" akaniuliza "ni kweli Rojas? Nikamwambia "ni kweli" "mimi ni ndugu yako Rojas nieleze tu" nikamwambia "hapana,hapana kabisa" akanambia "nakuamini,hata mimi nilipopata hizo hisia nikakataa hizo hisia,nilisema hapana kwanza ni mapema sana,namjua Rojas hawezi kutoa siri yetu kwa mtu yoyote yule" nikamwambia "kwani kuna nini,kuna kitu gani mbona unanipa wasiwasi,kuna nini? Akasema "usije hapa,naomba uwaangalie watoto wangu kwa uaminifu kama tulivyokubaliana,najua una vingi umeplan kufanya,naomba ukavifanye na mimi niko pamoja na wewe" nikamwambia "unamaanisha nini? Akanambia "namaanisha niko gerezani lakini nipo uraiani pia macho yangu yanakutazama Rojas" nikamwambia "unamaanisha nini mbona unaniambia sentensi kama hiyo" akasema "sisi ni marafiki,sisi ni ndugu Rojas na kama muda wote nakuwaza si ina maana nakuwa pamoja na wewe,ndani yangu hisia zangu ziko sana kwako kwahiyo muda mwingi nakufikiria" nikamwambia "sawa,sasa nitumie muda gani kukb ndio nije nikuone" akasema "itapendeza kama miezi sita bila kuja kuniona na mimi nakutakia mafanikio na usisahau kwenda kumtembelea tena yule dada (yaani yule mwanamke wake)naomba utimize ahadi yako" nikamwambia "naomba uniambie kitu" akasema "sina cha kukuambia kwa sababu kama ungekuwa umemwambia mtu siri yetu ningekwambia lakini kwa sababu haujamwambia mtu yoyote sina hata sababu ya kukwambia kwani haina maana" nikamwambia "nambie" akasema "haujamwambia yoyote kwanini nikueleze haya" yaani moyoni natamani kumwambia nisamehe niliteleza nilimwambia kaka,naogopa nawezaje kusema wakati nilimuahidi ahadi hii kubwa kuwa sitatoa siri,nimekuwa dhahifu nimetoa siri nikazidi kumsisitiza "niambie,niambie,niambie" akaniambia "haujamwambia mtu yoyote kuwa na amani haya yote ntayamaliza mimi mwenyewe nenda tu,nenda tu Rojas usiwe na wasiwasi" nikamwambia "sasa kuna mazungumzo nataka tuongee kuhusiana na biashara" akasema "yote,yote hayo kayafanye vizuri usije,usije huku kabisa" nilitishika na maneno ambayo alinambia huyu ndugu na mimi nashindwa kumwambia ukweli wa mambo jinsi ulivyo.
Itaendelea!
Nimejikia kulia na wakati huo huo nimetabasamu, nawaza wanangu siku nimetangulalia mapema mbele za haki wakiwa bado hawajaona hata mwanga wa elimu, wataishije huku nyuma.MKASA WA KUSISIMUA WA ROJAZ:
katika kipindi cha sitasahau cha radio free Africa
Part 3
Maisha ya pale kituo cha polisi yalikuwa ni ya muda mfupi kwani utaratibu wa kimahakama ukafika na nikatakiwa kupelekwa gerezani wakati suala langu likiendelea kupatiwa ufumbuzi,wakati nikiwa gerezani kuna kaka mmoja tulitokea kujenga ukaribu wa kiurafiki nae na akawa msaada mkubwa kwangu katika mambo mengi yaliyokuwa yakinikabili,siku moja katika maisha yetu ya gerezani nikiwa na huyu kaka alinambia "kila nikikutizama macho yako nakuona ni mtu mwema sana" nikamuuliza "mimi?akaendelea "yaani hata wale watu wabobevu wa kufanya uchunguzi,watu ambao ukijitetea wanaona auhusiki ndio wanakubana lakini nakuona ni mtu mwema kabisa"
Nikamjibu "sijui,lakini mimi sipendi ubaya na mtu na napenda amani katika harakati zangu za kila siku" akaendelea "unajua uwa nawatizama watu wengi sana hapa lakini katika wengi sijaona mtu mwema kama wewe" nikamuuliza "mimi?" Akasema "ndio sijaona mtu kama wewe humu,wewe ni mtu mwema na kama haujajua basi siku moja utakapopata neema ya kutoka hapa utajua kama wewe ni mtu mwema itambue hiyo na iishi hiyo kwa sababu una upekee wako" nikahisi ni maneno ya faraja tu ananambia yakunitia moyo,kunisahaulisha tabu zangu na kunifanya nifurahi na kujiona ni wa pekee hata kama niko katika mazingira magumu na vitu kama lakini aliendelea kuniambia anamaanisha kwa kile anachokiongea,nakumbuka nilimuuliza "kwanini wewe uko hapa? Kwani wewe si mtu mwema?" Akanambia "hata nikikuambia hautaweza kuniamini lakini mimi natofautiana na wewe,angalia macho yangu yalivyo je una uwezo wa kumtambua mtu tabia zake,hisia zake na kile kilichopo ndani yake? Nikamwambia "hapana sina huo uwezo" akanambia "basi mimi ninao huo uwezo ila sikuutumia vizuri nikiwa uraiani,mimi sifanani na wewe,wewe umekuja kwa njia ambazo si za haki yaani umekuja kwa sababu kuna watu wamefanya mambo mabaya wamekuingiza na wewe lakini mimi ni tofauti na wewe" nikamwambia "utofauti wa mimi na wewe ni upi? Akasema "ni stori ndefu sana huwa sipendi kuzungumza lakini kiufupi niko hapa natumikia kile ambacho nilistahili,siku nyingine ntakueleza lakini siko hapa kwa makosa hakuna mtu amenisingizia,maisha yangu ya uraiani mwenendo wangu ndi ulionipeleka mimi kuwa"
Nilitamani kujua alifanya kitu gani kilichopelekea hadi yeye kuwa anastahili kutumikia kifungo anachokitumikia,alinambia "niko hapa gerezani natumikia miaka yangu 30 na mpaka kesi yangu inasomwa nimeshakaa miaka mingi" nikamuuliza "umekaa miaka mingapi?" Akanambia "sikuvunji moyo wakati mwingine kuna kesi uendeshaji wake uwa unachelewa kwani kabla ya kufikia hukumu unaweza kujikuta umekaa hata miaka 5" nikamuuliza "hivi mimi naweza kukaa hapa muda mrefu?" Akanambia "inategemea na jinsi kesi inavyoendeshwa,kadri kesi inavyoendeshwa uenda uchunguzi zaidi ukaitajika hivyo kupelekea kuchukua muda lakini nakuombea sana mdogo wangu kesi yako isichukue muda mrefu na uachiwe huru" huyu kaka tulikuwa tunazungumza sana na kiukweli alinijenga sana katika mazingira yale nakunipa matumaini.
Siku zikiwa zimepita siku moja huyu kaka aliniita na tukawa tunazungumza na alinambia"unajua kama ninao ndugu zangu lakini toka nimepata haya matatizo wamenitelekeza na kunisusa huku,huwezi amini kati yao wakati nikiwa uraiani nilijitolea sana katika kuwasaidia hata katika vitu ambavyo havikuwa na faida kwangu niliwapiga tafu lakini kwakuwa mimi nimekamatwa hakuna hata anayetaka kunisogelea wakihisi pengine nao wanaweza kuhusishwa na mimi lakini licha ya hivyo hata ilipotoka hukumu hakuna aliyesogea,wameniacha" nikamwambia "ni sehemu ya maisha,je hakuna hata mmoja aliyekuja kukuona? Akanambia "ninaye mtu ambaye yeye hajawahi kuniacha,uwa namimi katika mazingira yoyote yale hata niwe ndani na hauwezi amini yeye uniletea mahitaji toka siku siku ile ya kwanza nimekamatwa" nikamuuliza "ni wazazi wako? Ni mtu gani huyo?" Akanambia ni girl friend wake (mchumba wake) ndio ambaye hajawahi kumuacha toka siku ile amekamatwa,nikamwambia kuwa alibahatika kumpata mtu sahihi sana,akanambia anahisi anaweza kuchoka nami nikamjibu kama ana upendo wa kweli hatoweza kuchoka na akanijibu "sijui,nina watoto pia yupo mwanamke ambaye nilipata nae watoto,watoto wangu wana uhitaji sana lakini mimi baba ambaye nilikuwa nikipambana katika njia mbalimbali leo nipo hapa,watoto wangu hawako katika mazingira salama na huyu mwanamke kila anapokuja kuniona aachi kunipa lawama na sasa amekuwa ni mwanamke wakuhangaika hovyo na wanaume,sielewi hatima ya watoto wangu,nilizungumza na ndugu yangu lakini ndio hivyo wameniacha peke yangu" kiukweli maelezo yake yalinisikitisha sana na hasa aliponielezea juu ya wanae maumivu yaliutanda moyo wangu,alinambia kuwa uraiani alikuwa anapambana sana,anapambana kwelikweli kwa ajili ya watoto wake lakini kwakuwa yupo jela hatoweza tena kuwapambania,kiukweli nikazidi kuumia kwa maneno yake nikamwambia "pole sana ndugu yangu,umenigusa sana,najua ukiwa hapa kule nje kila kitu chako kinakuwa kimesimama na kama ulivyonitia moyo kwenye maswaibu yangu nami nakutia moyo,tutatoka siku moja tutatoka" akasema "ni kweli natambua ni kweli"
Siku zikawa zinaenda na tukawa tunashea mengi katika mazungumzo yetu ya kila siku na kuna siku mfungwa mmoja aliniambia naona uko na urafiki na mtu flani (akimtaja yule mfungwa ambaye uwa napigana nae stori)nami nikamjibu ndio kwani amekuwa kama kaka,kama mshkaji na mfariji ndio tunabadilishana mawazo akanambia jamaa ana miaka mingi huyo kwani sote tutatoka na tutamuacha humo humo na akakazia huyo anafia humo humo gerezani,kiukweli sikumtilia maanani kwani kama ni miaka ambayo tayari imeshatamkwa mfano atatumikia miaka 30 si atatumikia miaka husika kwanini aonekane kama atafia huku? Sentensi gani hizi?
Siku zilikwenda na kwenda,safari za kwenda na kurudi mahakamani hazikuisha na mara zote nilizokuwa nikisimamishwa kizimbani nilikuwa naeleza ukweli na lile nililokuwa nalijua tu,sikuwa napindapinda katika maelezo yangu,sikuwa na mengi yakuyaeleza kwakuwa yangu ni machache kwani nilielezea stori toka nimekutana na huyu kaka hadi kufikia kunifundisha udereva,umiliki wake wa gari na hata kuhusu yule abiria ukutanaji nae ulivyokuwa na kama ujuavyo jela nilipata vijiupeo kutoka kwa wabobevu wa sheria ambao walininoa namna ya kuongea kuwa lipi lakuepuka kuliongea,lipi lakulisema na kadhalika maana mahakamani kuna maswali yamitego ni muhimu kusimamia kile unachokiongea na kiwe cha kweli kwani niliamini ukweli ndio utakaoniweka huru!
Nakumbuka siku moja kaka alikuja kunitembelea gerezani na akanambia "mdogo wangu uko katika mazingira mazuri kabisa katika kesi hii na upelelezi unavyoendelea unaonesha hauhusiki kabisa kwahiyo wakati wowote waweza kuachiwa huru,huenda mara ijayo utakapoenda mahakamani yawezekana usirudi tena huku gerezani" nikamuuliza "ni kweli usemayo kaka?" Akasema "ndio" nikajawa na matumaini na furaha sana kwa maelezo haya ya kaka,kuna siku yule kaka mule jela alinambia "naona mwenendo wa kesi yako si mbaya na matumaini ya kutoka yanazidi kuchanua sana hongera sana" nikamwambia "kaka kuna siku ntaenda mahakamani na sitarudi tena huku" akanijibu "ni kweli na mimi nimefatilia huo ni ukweli kabisa,naomba nikuulize najua utatoka na utakapotoka na kwenda uraiani unaweza kunisaidia kitu?" Nikamjibu "ndio" akasema "ntashukuru sana utakaponisaidia katika hili jambo,naomba unisaidie ntakupa maelekezo naomba ukawasalimie watoto wangu" nikamwambia "kaka hakuna shida" akaongezea "na pia ntafurahi sana kama utapata fulsa yakuweza kwenda kumsalimia na mchumba wangu" nikamjibu "nitafanya hivyo pia kaka" akanambia "naomba tuwe ndugu,unajua ndugu sio lazima muwe mmezaliwa tumbo moja,unajua wako ndugu sasa hivi hata wakija nimekuwa siwaamini tena lakini moyo wangu nimejikuta nakuamini sana wewe,sijawahi kukuona enzi nikiwa uraiani tumekuja kukutana gerezani lakini mimi naamini kukutana kwetu Mungu amepanga tena amepanga tukutane katika mazingira kama haya,hivi unajua waweza kukutana na mtu sahihi hata ukiwa gerezani?" Mi nikacheka kwa hayo maneno yake nikamuuliza "mtu sahihi gerezani? Mtu gani awe sahihi mazingira kama haya?" Akanambia "mimi naweza kuwa mtu sahihi sanj kwako na nikawa mtu mwema kwako,jua nimekuona kuwa wewe ni mtu mwema tafadhali nakuomba nawe unirejeshee huo wema ntakaokupa" yale maneno aliyokuwa akinambia sikuwa nayaelewa alikuwa anamaanisha kitu gani,msisitizo wa maneno haya kwangu uliendelea mara kwa mara mpaka siku naenda mahakamani,nakumbuka siku hiyo sasa ndio naenda mahakamani kabla hatujatolewa nje kupandishwa karandinga alinambia "unakumbuka maneno niliyokuwa nikikwambia mara kwa mara ? Unaweza haya maneno ukayafanyia kazi?
Nikamwambia "kaka wala usiwaze kwani undugu si lazima kuzaliwa tumbo moja,tunakutana katika mazingira yoyote alafu tunatokea kuelewana,nakuahidi kaka kama nilivyokwambia nitaenda kuwasalimia watoto na nitaenda kumsalimia mchumba wako,na nikuahidi mimi ni kijana na kama Mungu atanipa neema ya kutoka nitaenda kupambana,nitaenda kupambana na napenda nikuahidi kitu kimoja nitaenda kuwatembelea watoto wako na chochote nitakachobarikiwa sitawasahau kwani najua wewe baba yao uliyekuwa ukipambana kwa ajili yao umekwama humu" akaniuliza "kweli? Kweli unasema? kweli Rojaz unaniahidi kitu kama hiki? Ndio maana niliona,macho yangu yaliona na moyo wangu ukavutika kuzungumza na wewe,wewe ni mtu mwema" kiukweli ninaikumbuka sana siku hiyo kwani alikuja akanikumbatia huku machozi yakindondoka na kunipigapiga mgongoni akanambia "aisante sana mdogo wangu,asante nakutegemea kwani hakuna mtu yoyote ambaye ameweza kuniahidi hivi kama wewe,sijawahi kupata rafiki mwema hivi kwani kuna mshkaji nilikuwa nae hapa karibu kweli lakini toka ametoka hajawahi kurudi tena kunitembelea,hakuwahi hata kwenda kuwatembelea wanangu,Rojaz kumbuka ahadi unayonipa mdogo wangu" nikamwambia "kaka amini ninachokwambia,sitasahau" mimi niliondoka na nikaweka hiyo ahadi kwenye kichwa changu,muda wa kwenda mahakamani ulipofika tukapandishwa kuelekea uko na kesi ilisomwa na mheshimiwa akangurumisha kesi na mwishowe hakimu akatamka kuwa kuanzia muda huo niko huru,kiukweli kutokana na kuwa sikuhusika sikustuka sana kwa uamuzi ule uliotolewa kwani nilijua ni suala la muda tu ili kuweza kuujua ukweli halisi,jela nilikaa kama mwaka mzima hadi kufikia hii siku ya kuachiwa huru na katika kesi iliyokuwa ikinikabili tulikuwa wengi na wengine waliendelea na kesi mbele,ndugu zangu walifusahi sana kwa ndwtgu yao kuwa huru na kujumuika nao tena uraiani,kaka akanambia "sheria zipo kwa ajili ya kutenda haki walimdhuru huyo kijana watabainika tu, sheria itawakamata na kuwahukumu" kwahiyo mimi nilitoka gerezani na kurudi uraiani hakika ilikuwa ni furaha sana kwetu sisi na nilpata somo kubwa kuwa ni vyema kuwa na tahadhari katika shughuli tunazofanya
Itaendelea!
Nimejikia kulia na wakati huo huo nimetabasamu, nawaza wanangu siku nimetangulalia mapema mbele za haki wakiwa bado hawajaona hata mwanga wa elimu, wataishije huku nyuma.
Sent from my itel S11 using JamiiForums mobile app
Duh Mambo ni fire yanMkasa wa kusisimua wa Rojaz katika kipindi cha sitasahau cha radio free africa
sdhemu ya 5
Katika maisha yangu ya kila siku nimekuwa ni mtu wa kujali sana matatizo ya jamii inayonizunguka na wanajamii kwa kiasi kikubwa walinifahamu hivyo kwahiyo nilivyokutana na huyu mtu gerezani na jinsi alivyokuwa nami kama kaka nimebeba hiyo roho yakuwa sehemu ya kwenda kumtembelea yeye mwenyewe na pia kuwatembelea watoto wake,huyu mtu yupo ndani lakini muda wote akili yake ipo uraiani anawawaza sana watoto wake,anawawaza sana wapo katika mazingira gani kwa sababu anajua mwanamke ambaye amepata nae hawa watoto akili yake kidogo haina utulivu,nakumbuka awamu hii nilipoenda nilienda kumpasha kuhusiana na maendeleo ya watoto wake kuwa wanaendelea vizuri na kumpasha habari nyingine nyingi nilizokuwa nazo kuhusu uraiani na harakati ambazo nimekuwa nazo huku nikimtia moyo huyu ndugu yangu kuwa asikate tamaa mambo yatakaa sawa wala asiwaze sana ajue tu familia yake inaendelea vizuri,katika mengi ambayo nilimueleza ya huku uraiani alinambia "nakuamini,nakuamini sana" nikamwambia "asante" akanambia "unajua niko huku gerezani ni muda sasa na sijawahi kukutana na mtu amenipa matumaini kama wewe,unajua niko huku gerezani toka yule mtoto wangu mdogo akiwa bado ni kichanga" nikamwambia "nakuelewa,nakuelewa" akasema "unajua ndugu zangu wamejua nimepotea huku,nimeishia huku sijawa na mtu wa kumuamini naomba nikuamini" nikamwambia "karibu na uwe na amani" baada ya maneno haya alinishukuru sana.
Shukrani ilikuwa ni sehemu ya utaratibu wake kila tulipokuwa tukiongea na hata siku hii aliponishukuru sikuona kama ni jambo jipya kwakuwa amekuwa akiniambia mara kwa mara,akaendelea kunambia "toka ndani ya moyo wangu nimetokea kukubeba na kukupenda zaidi ya ndugu,naomba nikushirikishe jambo ambalo sijawahi kumshirikisha mtu yoyote katika maisha yangu,naomba nikushirikishe jambo ambalo nilikuwa nilifanye nikiwa uraiani lakini sikubahatika kulifanya" nikamuuliza "ni jambo gani" akanambia "linahitaji uaminifu baina ya mimi na wewe" nikamwambia "haina shida,haina shida" akanambia "basi nenda kajifikirie" nikamwambia "niambie tu wewe niambie lakini naweza kukusaidia kama si jambo baya" akanambia "wala si jambo baya" nikamwambia "sawa nieleze tu" nilimlazimisha anieleze kwa sababu nitakuja tena huku lini,lini ntakuja kwa sababu nami sasa hivi nimekuwa ni mtu ambaye napambana na mishemishe zangu unajua,akanambia "sawa,nataka nikubadilishie maisha yako" nikatabasamu,nikamwambia "mimi? Unibadilishie maisha mimi?" Akasema "ndio,kwani mimi nikiwa gerezani nashindwa kubadilisha maisha ya mtu mmoja uraiani?
Nikacheka na nikamwambia "hata sikuelewi unamaanisha" akasema "namaanisha ninachokisema,unakumbuka nilikwambia umekuja gerezani kwa ajili yangu?" Nikatabasamu na kumwambia "unajua sikuelewi unachosema" akasema "utanielewa" katika harakati zangu nilitamani maisha mazuri,nilitamani maisha mazuri,maisha bora lakini sikuweza kutimiza ndoto zangu najikuta niko katika maisha ambayo sikuwahi kuwaza kama nitaishia uko lakini pengine maisha yangu naweza nikamalizia uko,sijui ni neema gani yaweza ikaja kwangu na nikatoka,nikamwambia "kwanini unasema hivyo,kwanini unasema hivyo na wakati haya mambo tumeshakaa na tukayazungumza unatumikia kifungo chako na kina miaka tajwa" akasema "hauwezi kuelewa,elewa hili ninalosema nataka kukubadilishia maisha yako na ulikuja gerezani kwa ajili yangu" alinambia nirudi nyumbani na niendelee na harakati zangu na nije tena,nikamwambia "unaniweka njia panda sana mshkaji wangu sielewi hata unachomaanisha,hivi mtu aliyeko gerezani anawezaje kumbadilishia maisha mtu niliyeko uraiani? Ambapo mimi napiga mishemishe,napambana na maisha,ujue gerezani mtu unakaa tu,unakaa tu unawezaje kubadilisha maisha yangu mtu namna hiyo?" Alinambia tutangea na kunisisitiza nisiache kwenda kuwatizama watoto wake nami nikamwambia "usiwaze kuhusu hilo na uwe na amani tu ujue umepata mdogo wako ambaye yupo pamoja nawe hata kama uko gerezani uko pamoja na mimi,usiendelee kunung'unika kuhusu ndugu zako ambao wanaona wewe umeishia huku gerezani Mungu ana njia zake za kuinua ndugu basi ujue na mimi Mungu ameniinua niwe ndugu yako,nitafanya hayo kwa moyo wangu wa dhati" nilimwambia hayo na baada ya muda niliondoka zangu lakini niliyawaza maneno aliyonambia,mtu huyu ni mfungwa tu,mfungwa tu wa kawaida na katika nafasi nilipoingia hapa gerezani na nilipokuwa ninaishi hapa nilimuona ni mfungwa tu ambaye ni mtu mbabe mbabe kwa sababu sio mtu wa kuonewaonewa unajua maisha ya uko kuna watu wababe,watu ambao wana nguvu zao yaani yeye hakuwa mtu wa kuonewa na alikuwa mtu wa kutetea wengine kiufupi nilimuona ni mtu mwema kwa muda wote niliopata nafasi yakuwa nae gerezani lakini kwa habari yakunibadilishia maisha kiukweli ni kitu chakuchekesha unajua yaani nilikuwa nikicheka tu.
Nilirudi uraiani na maisha yalikuwa yanaendelea nilikuwa nikiendelea kupiga mishe zangu kwa sababu sasa hivi si haba japo sijapata gari rasmi napiga tu mishe za udeiwaka japo si haba napata chochote,toka nimetoka kule gerezani ulipita kama mwezi na nikapata nafasi ya kwenda kuwatembelea tena wale watoto,nilienda kuwacheki na kuwapelekea vizagazaga kidogo sawa na kipato changu ambacho napata,wakanambia "anko umekuja tena?" Hii sentensi huyu mtoto alikuwa anapenda kuniambia hivi nami nikamuuliza "ulidhani sitakuja tena? Akanambia "nilidhani hautokuja tena" nikamuuliza "kwanini?kwanini unawaza hivyo? Nilishawaeleza mimi ni anko wenu ambaye nitakuwa nakuja mara nyingi sana,mnaendeleaje?" Lakini pia niliwapelekea mahitaji ya hapa na pale kwa ajili ya shule na walifurahi sana na huyu mama sasa kishajua kama nakuja kwa ajili ya kuwatembelea watoto kwa ajili ya rafiki yangu ambaye alikuwa ni mtu wake ambaye hawako tena kwenye mahusiano kwa sababu wao wenyewe wanazijua,nilizungumza na watoto lakini pia nilizungumza na huyu mama na kikubwa nilimwambia "kwanini siku usitenge muda wa kwenda kumuangalia mwenzio gerezani" kwa mara ya kwanza nazungumza na huyu mama sentensi kama hiyo akasema "mimi nikapoteze muda wangu kudili na mtu aliyeniharibia maisha yangu? Nikamwambia "ujue watu ukosea lakini na watu hujirekebisha,unajua watu hujirekebisha sana wakiwa gerezani? Watu wanabadilisha nienendo yao na inawezekana alipokuwa uraiani hakuwa mtu mwema lakini kule ameshabadilika" akasema "hawezi kubadilika yule mtu,hawezi kubadilika yule mpaka mwisho wa dunia,hawezi kubadilika,mbaya yule kuliko unavyodhani na nashangaa unaangaika kumsaidia mtu yuko gerezani na ataozea uko,nakuangalia tu nione hatua zako zitaishia wapi" aliniambia hayo maneno yakunivunja moyo nami nakumbuka nilimwambia "mtu anaweza kuwa mbaya kiasi gani yaani hadi asiweze kuonewa huruma na kwenda kutembelewa" alinambia "mwanaume mbaya sana amenipotezea maisha yangu na kunipotezea muda,ebu tazama wakati mimi niko nae kumbe yuko na mwanamke tena amekwenda hadi kumtambulisha kwao naye ameshakwenda kutambulishwa hadi kwa huyo mwanamke na wako katika hatua flani za uchumba lakini mimi huku kashanipa tena ujauzito,amenifanya nimeishi maisha magumu sana ya ajabu,namchukia sana na siwezi kunyanyua mguu wangu kwenda kumtizama shetani kama yule hata siku moja" yaani mtu huyu anavyotafiriwa unaona si mtu mwema na kuna sentensi ambazo nimekutana nazo nikiwa gerezani "huyu mtu uko nae karibu kivipi? kama hatafsiriwi kwa wema lakini kiundani kwanini mtu huyu si mwema lakini yeye mwenyewe anasema yupo anatumikia kifungo kwa sababu yeye mwenyewe amestahili wala hajaonewa na yoyote,ni malipo ya madhambi yake,nilimsikiliza huyu mama maneno na hasira zake lakini mimi sio yaliyonileta,hata kama baba yao ni mbaya hawa watoto sio wabaya kwahiyo ntazidi kuja kuwaona pale ntakapopata nafasi hata kama navunjwa moyo na mama yao nitajipa moyo kwa sababu nimewapenda hawa watoto nitakuja tena na tena kuwatizama.
Niliaga na kwenda kuendelea na mishe zangu na maisha yangu yakawa yanasonga mbele na siku zikasogea ikapita kama miezi mitatu niko na mishe zangu sikupata nafasi ya kwenda kuwatizama wale watoto wala sikwenda kule gerezani niko na mambo yangu naendelea,nakumbuka siku moja nikasikia kuwiwa sana kwenda kuwatembelea wale watoto,nilienda lakini nilimkosa huyu mama,nilipouliza kwa majirani nikaambiwa yule mtoto mdogo anaumwa,anaumwa sana na amelazwa,kwahiyo nikafatilia hadi kujua wamelazwa wapi,nikaenda kwenye hiyo hospitali na nikamkuta yule mama pamoja na baadhi ya ndugu zake wakiwa katika hali yakumuangaikia mtoto walisema amepata amoeba sijui nini mambo ya watoto basi nami nikawatia moyo nikasema "nilikuja kuwaona na isitoshe mambo yamekuwa ni kukimbizana muda umepita sana sijaja" huyu mama akasema"nilijua hautakuja tena unadhani utakuwa unakuja kutuangalia kila siku kwa maagizo ya huyo mtu ambaye yuko gerezani ambaye atafia uko gerezani" nikamwambia "siji kwa sababu ya rafiki yangu wa kule gerezani,nakuja kwasababu nimeshakuwa na urafiki na hawa watoto" aliniangalia tu huyu mama lakini hali ya mtoto haikuwa mbaya sana basi nami kwakuwa nilipata taarifa ya mtoto kuumwa nikawa nakuja hadi pale aliporuhusiwa na kurudi nyumbani nami nikaendelea na mishe zangu lakini nilitafuta muda siku hiyo nikajisikia tu nikaenda gerezani kwenda kumtizama mshkaji,kweli nilipata nafasi ya kuzungumza nae,nilimpelekea sabuni na vitu vichache vichache na akanambia "mbona umechelewa sana kuja mshkaji wangu?
Nikamwambia "kwanini? Akanambia "mbona nilikwambia uje tuzungumze" nikamjibu "unajua mambo uko uraiani ni kupambana sana,mambo yamekuwa mengi mshkaji wangu unisamehe bure ila nilipata nafasi nilikwenda kuwatizama watoto nikakuta mtoto wako anaumwa" akasema "nini tena? Ina maana taarifa hana,hana mtu wakumpelekea taarifa,yaani watu walishamkataa yaani yuko tu huku hana taarifa zozote lakini nikamwambia usiwaze kwani anaendelea vizuri kwa sababu alipatiwa matibabu nami nilikuwa naendaenda pale kwakweli anaendelea vizuri mpaka ameruhusiwa amerejea nyumbani,yaani mtoto anaendelea vizuri kabisa wala usiwaze" akanambia "aisee nashukuru sana,nashukuru sana ndugu yangu,nakushukuru mno na asante sana kwa vitu ambavyo umeniletea" nikamwambia "wala usijali,karibu" akasema "najua moyo wako iko siku utachoka kuja kunitembelea,najua utachoka na hautakuja tena" nikamwambia "sijui,lakini ndugu yangu nikuahidi pale nitakapopata nafasi nitakuwa ninakuja" akasema "lakini naomba tuendelee na mazungumzo yetu ya siku ile tulipoishia " nikamwambia "nakusikia" akanambia "tuliishia pale nilipokwambia nataka kubadirisha maisha yako" nikamwambia "nakumbuka" akanambia "hujaiwaza hiyo sentensi? Nikamwambia "sijaiwaza chochote,kwasababu unaweza wewe kunibadilishia maisha wakati wewe mwenyewe umekosa uhuru na upo tu unafanya kazi za humu ndani,unawezaje kunibadilishia maisha mimi ambaye niko uraiani na nina mwanya wakubadilisha maisha yangu mimi mwenyewe" akasema "ni kweli umesema vyema lakini mimi nimekaa hapa ni kwa sababu nimekosa uhuru wakufanya kitu lakini natamani nifanye kitu nikiwa uraiani" nikamwambia "utawezaje sasa? Akanambia "nataka wewe ukafanye" nikacheka,nikamwambia "kufanya nini? Akanambia "ninao utajiri" nikacheka yaani ni mambo yakuchekesha,nikamwambia "yaani wewe unao utajiri wewe? Akasema "hakuma mtu anajua kama mimi nina utajiri mwingi" nikamwambia "eeh niambie kuhusu utajiri wako" akanambia "hii ni siri nazungumza na wewe na sijawahi kuzungumza na mtu yoyote,natamani uwe rafiki yangu,ndugu wangu wa damu,sina mwingine wa kumuamini moyo wangu umesukumwa na wewe na hata nilipokuwa gerezani nilikuwa nikiomba Mungu usiku na mchana anipe mtu ambaye si ndugu moja na mimi lakini akamfanye awe ndugu yangu,akatimize ndoto zangu uraiani,hivi unajua ni kama vitu visivyoeleweka" nikamwambia "haya nambie,nambie kuhusu utajiri wako" akanambia "ninazo pesa nyingi zakuweza kubadilisha maisha yako,nyingi hata zakuweza kubadilisha maisha ya familia yako lakini niahidi hautawaacha watoto wangu,utawabeba nakuwatunza na kuwalea,utawasomesha,utamsaidia na mama yao,utamsaidia na msichana wangu lakini niahidi,niahidi kitu kimoja,hautamgusa yule mwanamke,utamuacha ataolewa na mtu mwingine,mimi sitaweza kumuoa lakini wewe usimuoe,aolewe na mtu mwingine na msaidie akiwa na matatizo"
Mimi ninayasikia haya,unajua ni kama mambo yasiyoeleweka narudia tena kwa sababu mtu anawezaje kunambia maneno hayo,ananipima? Tunazungumzia habari za pesa ambazo niko huku napambania kweli na udeiwaka mtu ananambia nina utajiri,niliyasikia haya maneno kutoka kwa kaka huyu ambaye tulikutana gerezani na kuishi kama familia na leo ninapoelezwa haya mambo ya pesa na utajiri na mfungwa aliyepo gerezani ananiambia nimuahidi kwanza sikuamini,niamini vipi,niamini vipi kirahisi? Kwanza nikabaki nikitabasamu kwa sababu nimekuwa nikitabasamu hivyo na akanambia "mimi sikutanii na siko kwa ajili ya matani na mimi nilisogea na kuzungumza na wewe toka ulipofika na nikakutana na wewe,nilikuja kwa sababu ya kusudi maalum ili unikamilishie ndoto zangu,wafanye watoto wangu kuwa bora,waishi katika nyumba nzuri,wafanye watoto wangu kuwa watu wa thamani,mama yao pia,sikwambii sana kuhusu ndugu zangu endapo ukiguswa waweza fanya hivyo lakini huu utajiri nakupa wewe,nakutunuku wewe" sasa mfungwa aliyeko
gerezani anawezaje kuwa na pesa,"pesa ziko wapi? Nakumbuka nikamwambia "unanambia mambo mazito yaani sijawahi hata kusikia mtu aliyeko gerezani anaweza kumpa utajiri mtu aliyeko uraiani,basi mimi naweza nikawa nimebahatika ila ndugu yangu nashukuru sana ila huo utajiri sidhani kama mimi nafaa kuupata,naogopa sana vitu hatarishi katika maisha yangu,natamani kufanya vitu vya halali tena vya haki,sitaki matatizo katika maisha yangu,umeniona nimetumikia kwa muda gani hapa gerezani ilihali sijatenda lolote,maisha yangu yalirudi nyuma sana,harakati zangu nilizokuwa nazo zikarudishwa nyuma,unataka na mimi niishie gerezani kama wewe?
Inaonekana maisha yako uraiani hayakuwa mema wewe mwenyewe umesoa unatumikia kile ambacho wewe umestahili kutumikia je unataka na mimi niyaishi maisha ambayo wewe umeyaishi yakakufanya hadi uje gerezani? Akasema "hapana,sio kweli,sio kweli na haijalishi kwa sababu mimi nilikuwa mbaya basi na pesa yangu itakuwa mbaya,unajua nini mimi natamani kufanya,natamani pesa yangu ikafanye mambo mazuri mema" nikamwambia "pesa yenyewe iko wapi? Tunazungumza,tunazungumza nini kwani? Yaani pesa iko wapi unayozungumza wewe? Akanambia "pesa ipo na nataka uniahidi katika mambo niliyokwambia kwa sababu ukitoka hapa unaenda kuchukua pesa kwahiyo ahadi yangu inabidi unipe leo na ahadi yangu nataka uape mbele ya Mungu ya kwamba unaniahidi hata kama mimi kesho nitaondoka ahadi yako kwa Mungu isimame na ikuhukumu kama utaenda kinyume na hayo,mimi nataka kukupa utajiri leo,leo nakupa utajiri,niahidi,najua hauwezi niahidi kwa maandishi lakini kwa kinywa chako niahidi ,niahidi utatunza ahadi hiyo mpaka pale mwisho wa safari ya maisha yako" nikamwambia "kaka we usiongee sana we nambie" akasema "siwezi kuzungumza zaidi ya nilichosema niahidi utawatunza watoto wangu" nikamwambia "ndio nakuahidi nitafanya hivyo" niahidi utamtunza mama wa watoto wangu yaani wale watoto mama yao" nikamwambia ndio nakuahidi, "niahidi utamsaidia mwanamke niliyempenda na kutamani kuishi nae nikiwa uraiani,mwanamke wa ndoto zangu" nikamwambia "ndio" "lakini niahidi huyo mwanamke hautamfanya kuwa mwanamke wako,utamuhudumia na kumsaidia na atakwenda kuolewa na mwanaume anayemtaka yeye lakini sio wewe" nikamwambia "ndio" akasema niapie mbele za Mungu,mimi niko gerezani sasa namjua Mungu,najua mtu ukiapa mbele za Mungu hiyo inasimama kweli" nikamwambia "mbona unanipa vifungu vigumu hivyo kwanini tuape Mungu hapa?
Akasema "niapie mbele za Mungu" haya yalikuwa ni mazungumzo na huyu mtu ambaye amenambia atanipa pesa na hizo pesa ziko wapi? Ananipa katika mazingira gani? Anasema anataka kunipa utajiri abadilishe maisha yangu!
Itaendelea!
Karibu sana
Nini maana ya story sasa, yan masimulizi, ulitaka aanze nikafukua pesa, nikala bata japo sikuwasahau watoto nikamtelekeza jamaa, akaja akafa bana na story ikaishia hapostory nzuri sana
lakini mbona maneno yanarudiwarudiwa sana?
Ubarikiwe dada mihela kama yote!Nini maana ya story sasa, yan masimulizi, ulitaka aanze nikafukua pesa, nikala bata japo sikuwasahau watoto nikamtelekeza jamaa, akaja akafa bana na story ikaishia hapo
Sent from my itel S11 using JamiiForums mobile app
Nadhani ule ujumbe aliopewa na mshkaji kuwa ni yeye mwenyewe akiamua kuwasaidia au vyovyote ni juu yake kwani yeye wamemtelekeza tu kule gerezaniNashukuru story imeishia kwenye furaha, niliwaza utajir wote utaisha na kuanza kuwa ombaomba, ashukuriwe Mungu, kingine nasikitika sijaona sehem amewasaidia shangaz kule kijijini.
Sent from my itel S11 using JamiiForums mobile app
Sasa kama Rojaz hakufirisika,,,mbona dk za mwisho alikuwa anauza mitumba jjini MwanzaNadhani ule ujumbe aliopewa na mshkaji kuwa ni yeye mwenyewe akiamua kuwasaidia au vyovyote ni juu yake kwani yeye wamemtelekeza tu kule gerezani