Mkasa wa kweli, kuhusu visa vya kushangaza nilivyokutana navyo katika kazi za Udalali

Mkasa wa kweli, kuhusu visa vya kushangaza nilivyokutana navyo katika kazi za Udalali

DALALI MKUU

JF-Expert Member
Joined
May 7, 2022
Posts
2,011
Reaction score
4,705
EPS 1

Heshima Kwenu Wakuu,

Niliwaahidi Kwamba Nitawaletea Mkasa Kuhusu safari au Hekaheka zangu nilizozipata wakati nafanya Shughuli zangu za Udalali Jiji la Dar es salaam na maeneo ya jirani.

Mwaka 2017 Nilitoka kwenye wilaya Niliyokuwa Ninaishi nikaamua Kuhami Jiji La Dar es salaam kwenda Kufanya Kazi zangu binafsi nikiamini Kwamba nitatoboa Kimaisha, Nilikuja Dar es salaam baada ya kufanya akzi maeneno tofauti tofauti Mkoa wa Kilimanjaro.

Nilipofika Dar maisha Yalikuwa magumu sana kwakweli, kuna sehemu nilipata Kazi nilikuwa nalipwa 40k kwa wiki haikuwa inatosha Chochote, Lakini kazi Pia ilikuwa na mateso sana. Nilikuwa nafanya kazi kwenye Kampuni Fulani Binafsi inajihusisha na Masuala ya Matangazo ilikuwa ni kazi ya mteso sana, nilikuwa naingia kazini Asubuhi saa moja natoka saa 12 Jioni.

Nikitoka nakuwa nimechoka sana kiasi kwamba siwezi hata Kufanya shughuli nyingine na mshahara ndio huo kwa wiki unalipwa elfu arobaini tu ukitoa hapo nauli na hela ya kula kwa wiki unabaki na deni au ukijibana sana useme ule mlo mmoja tu unabaki na elfu Kumi.

Kodi nilikuwa nalipa eldu thelathini kwa mwezi maji elfu kumi umeme elfu Kumi jumla Kodi kwa mwezi ni elfu hamsini na kila wiki nikijibana sana kwa mwezi nakuwa na Akiba ya Elfu arobaini yaani kila iki elfu Kumi.

Hapo nilipokuwa nakaa ilifika wakati kodi ikaisha nikawa sina hata Mia mbovu akiba yote nilikuwa nimeitumia kutokana matatizo yaliyojitokeza, Mwenye nyumbaalikuwa haelewi Kitu zaidi ya kutaka hela yake.Yule mzee alinisumbua sana nikaongea nae Anivumilie akanipa Muda wa wiki nikaanza kupiga Bei vitu vyangu vya ndani ila kupata wateja ndio ikawa shida sana, kila nikinidai Mitandaoni hakuna mteja zaidi watacoment watu wanaulizia Uko wapi na bei gani tu.

Aisee nilichanagnyikiwa sana Wakuu Wiki ikakata nikapata ile hela ya wiki Elfu arobain nikakusanya kusanya kwa wadau nilikuwa naapiga Vizinga nikapata elfu sabini nikampa mwenye nyumba ili inayobaki nitamlipa.

Kuna watu ana Roho mbaya sana Yule Mzee akaniambia hapokei Kodi hata kama Imebaki Buku Hapokei na kama siwezi kumpa hela yake nijiandae kuhama nikatafute Chumba sehemu Nyingine.

Pale pale akaanza Kupiga simu anamtafuta Dalali ili amtafutie mpangaji mwingine, Hela yangu ameikataa nilirudi ndani nikawaza sana mambo mengi mno nilipiga simu kwa wadau lakini kila ninayemkopa ananielezea matatizo yake makubwa zaidi nikaamua kuachana nao.

Nikiwa ndani Yule Mzee nikamsikia anaongea na watu anamuonyesha Chumba Changu na wanakubaliana bei afu anamwambia Kuna mtu ndnai ila nitamwmabia afungue uingie ndani ukiangalie.
 
EPSOD 2

Basi Jamaa wakaja wakanigongea wanataka kuingia ndani waangalie Chumba, Nilimuia sana nikajua kabisa Leo hapa nadhalilika, maana nachukia sana watu baki kuingia chumbani kwangu.

Nikapata wazo nikafunga mlango nikatoka nje nikamuambia hata kama ananidai kwa sababu sijahama Siruhusu mtu aingie Chumbani kangu anipe muda nitafute nyumba nyingine nihamie ila kwa akati huo sihitaji Usumbufu wake.

Nikampa Option ya pili kama anataka Kuingia aje na Mjumbe au mwenyekiti wa serikali za mitaa, tofauti na hapo sitaki usumbufu nikafunga mlango nikasepa zangu, nikaenda bar moja ipo Kibaha kwa mbonde karibu nauwanja wa Mpira ile hela ya Kodi aliyoikataa nikaagiza zangu Konyagi nikaanza Kutuliza mawazo yangu huku na enjoy Music Mzuri na Kuangalia viuno vya watoto wazuri.

Nilikunywa Nyagi hadi usiku Mrefu sana nikaona kwa hiyo siku nisirudi magetoni nikatafuta Guest ya Bei Chee nikaenda kulala hapo, nikaupa mwili likizo kwa muda. Asubuhi nilirudi maghetoni nikavaa nikaenda zangu Job, nilimkuta Yule mwenye nyumba ila sikumsalimia nilimpita kihuni.

Sasa ile siku nilikaa kazini lakin nilikuwa na mawazo sana, nikaanza kujutia namna nilivyoitumia ile hela yangu ya kodi imeshapungua nab ado deni liko pale pale, mawazo yalinivuruga sana, kila mtu alikona nilivyokuwa na mawazo waliniuliza sana ila sikutaka Kumshirikisha mtu yeyote. Huwa sina kawaida ya kumueleza mtu shida zangu kabisa. (Hata wazazi na hapo home siaambia maana nilitaka home sikuaga na hadi sasa hawajui hata niko wapi hii ni stoy nyingine huenda nikaielezea kama nitaona umuhimu katikati ya hiki kisa.)

Baada ya kuwaza sana nikaomba Ruhusa pale nikaondoka magetoni ili angala nikawaze nikiwa nipo mwenyewe huenda nikapata wazo la maana,ila sasa ile nafika Nyumbani nikakuta Mlangoni wamepiga kufuli kubwa JUU YA Kufuli yangu Asee niliishiwa nguvu kabisa.
 
EPS 3

Nikacheki nikaona hapa imeshakuwamajanga na sina namna ya Kuepuekana nayo tena ishakuwa balaa, nikaona hapa cha kufanya niiingie mtaani nikajitafute. Swali nitaenda kulala wapi maana hata ndugu zangu walio Dar sikutaka kabisa nikutane nao wala niende kuishi kwao. Niliwakataa ndugu zangu wote kuna msala Fulani hivi walinifanyia nikaamua kuwakataa nifanye mambo yangu.

Niliwaza nikienda mtaani nitakuwa nalala wapi, nikaondoka nilikuwa naishi Kibaha, nikaenda mbezi mwisho kule nilikuwa nimechoka sna na mfukoni nimebaki na Elfu arobainio tu. Nikaenda kwenye vile vibanda umiza vya mbezi niakkutana na wadau nikanunua Konyagi Kubwa kuna jmaa alikuwa Pembeni yangu pale ikabidi nimshirikishe baadhi ya vitu ili nione kama naweza pata msaada.

Huyu jamaa Tumpe Jina la Masai, masai akaniambia yeye ni dalali akanielezea namna anavyopiga Dili zake, namna anavyokutana na mabosi wenye nyumba, viwanja au biashara kisha wanamkabidhi awatafutie wateja.

Tulienda Kula konyagi pale Mdogo mdogo huku ananisumulia namna alivyo anza kazi hiyo, nikavutiwa sana ila ikabidi nimuelezee pia hali ninayopitia kwa wakati ule nimekwama Kodi ila nikamuambia nina kitanda, Godoro na Tv SONY zile za Chogo za zamani sina vitu vingi anitafutie mteja wa pamoja anipe hela nilipe kodi pale na Inayobaki nikaanzie maisha mengine niachane na ile kazi ya Kutengeneza matangazo.

Akaniambia Kuna jamaa anasehemu ya kununua na kuuza vitu used ila nimkabidhi akishauza ananipa hela, ila nikamwambia Pale siwezi kuingia ndani kuvitoa hadi nilipe kodi ya Yule Mzee.

Akanipa wazo la Kufanya tuende kwa jamaa yake kama atakubali Tuende nae alipie kwanza hiyo ya Kodi kisha nimkabidhi hivyo vitu avipeleke ofisini kwake.
 
EPS 4

Tulienda kwa Yule jamaa tukaongea nae ila jamaa akasema biashara ni ngumu hiyo hela hawezi kuipata kwa haraka labda nisubirie Kidogo kwa siku mbili au tatu,Jamaa alinivunja moyo kabisa nikaona kama mkosi hivi.

Nikapata wazo nikamwambia Yule masai tuende kibaha kwa sababu hela anayonidai Yule mzee ni ya kodi ya miezi inayofuata kwa maana ya kwamba miezi niliyokaa nimeshalipia nikamwambiatwende nikamwmabie sitokaa tena anifungulie nichukue vitu vyangu niondoke.Kama nilivyoeleza ndio nilikuwa naanza maisha hivyo hata vitu havikuwa vingi sana ilikuwa ni vicahache sana hata kwenye bajaji unachukua tu

Muda ulikuwa umeenda sana Masai akaniambia kuna dili zake anafuatilia kama inawezekana kesho yake ndio tuende kibaha, nilikuwa sina jinsi ya kumkatalia maana hata nilikuwa simlipi zaidi ya Konyagi yangu na fegi kadhaa alizovuta.

Nikaagana na Juma sasa Mawazo yakaanza kunijia nitaenda kulala wapi? Nitarudi vipi home na akiba inazidi kupungua tu na nikikaa kizembeinaisha kabisa.

Nikachek mfukoni nilikuwa nimebaki na Elfu kumi na nane tu nikaenda mbezi kuna Kigesti fulani kipo karibu na maeneo ya Lubumbashi nikaulizia wakaniambia pale kulala ni elfu Kumi ila kwa muda ule hawatoi kulala labda tu showtme, Kulala ni kuanzia saa tano usiku. Nikaulizia pale kuna jamaa kaniambia niende barabara ya malamba kuna Guest inaanzia chumba Elfu tano akanielekeza nikapanda bajaji nikaenda.

Wakati nikiwa pale Gesti kuna Demu mmoja akanipigia ni Demu angu wa kibaha, akanimbai amepita ile mitaa na amekutana na Mzee mwenye nyumba akamwambia kila kitu na Usumbufu ninaompa kuhusu kulipa Kodi yake. (Yule mzee anamfahamu demu wangu maana alikuwa ankuja sana pale)

Yule manzi Tumpe jina la Judy. akaniambia anaweza kunikopea hela kwa rafiki yake ili nimalizane na Yule mzee ila nikamwmabia nia yangu ya kuhama ule kibaha na kuacha ile kazi ili nikatafute maisha Dar.

Tuliongea sana na Judy na baadae akakubalina na maamuzi yangu. Nikazima simu kabisa nikalala muda huo ni kama saa nne hivi Usiku.
 
EPS 5.

Asubuhi niliamka kama saa nne hivi baada ya kuja kugongew na dada wa Gesti akaniambia muda umeisha, nikamwambia anipe dakika chache nioge. Nikawasha simu nikaenda kuoga Nikarudi nikakuta sms kibao moja ilikuwa ya TIGOPESA nimewekewa laki nne, na Judy nilikua amenitumia sms kibao akiniuliza kwanini nimezima simu na ameniwekea hela.

Sikumjibu nilivaa nguo nikamkabidhi chumba nikatafuta wakala nikatoa ile hela, yaani nilikuwa nafanya haraka nawaza kwamba Judy anaweza kuirudisha.

Baadae nikamtafuta nikamshukuru na kumwambia mawazo yalinizidi na uchovu hivyo nilizima ili nipate muda wa kulala,uzuri mmoja Judy alikua mwelewa sana.

Huyu Judy ni Dada fulani hivi mzuri wa wastani ni mchaga, alikuwa anafanya kazi ya Ufundi Nguo ila alikuwa ni mpambanaji sana na alitokea kunipenda sana na hasa shughuli ambazo nilikuwa nafanya nilikuwa namuonyesha Picha ambazo natengeneza,matangazo ya sauti na video alikuwa anpenda snaa kazi zangu. Na kilichomvutia zaidi ni utundu wangu kwenye Computer na simu.

Hata simu za marafiki zake alikua ananiomba niwe nawarekebisha kwenye masuala ya setting za kawaida kwa watu wengi hawajui hata ku update whatsap. TUSHIE HAPA NITAKUJA KUWAELEZEA ZAIDI KUHUSU MAISHA YANGU NA JUDY.

B
aada ya kuongea na Judy nilitafuta kijiwe nikapate soup nitoe hangover maana ilikuwa inangangania mbaya. Wakati nakunywa chai Masai akanipigia kunikumbusha ule mpango ila nikamwmabia nimebadili maamuzi siuzi ten, anitafutie Chumba cha bei poa maeneo ya karibu na mbezi, akaniambia kuna chumba cha 25 kipo mbezi kwa msuguri.

Nikakiangalie na kama kipo sawa, nilipie nihamie na aknaimbia ya udalali nitamtoa tu elfu kumi maana tumeshakuwa marafiki.

Tulienda kukicheki kilikuwa kizuri kwa uchumi wangu maana kilikuwa ni kipya lakini kimekamilika kwa kila kitu.

Tukalipa tukaondoka nikaenda mbezi nikahamisha vitu nikahamia siku ile ile.
 
EPS 6.

Nikawa tayari nimeacha kazi Rasmi na nimehama kibaha na nimehamia Rasmi Jiji la Dar es salaam mbezi kwa Msuguri.

Maisha mapya yakaanza na vichenji chenji kwneye ile hela ya Judy zilikuwa zimebaki nilikuwa nina jiko dogo la gesi, hivyo nikaenda kununua mahitaji ya ndani ili nijipange upya nijue namna ya kupambana na maisha.

Nikaendelea kukaa pale lakini story ya Masai ya udalali ilinivutia sana nikasema sasa hii ndio kazi ninayotaka nikafanye. Nilikuwa nampigia mara kwa mara masai na kuonana nae lengo anionyeshe njia maana aliniambia kwa kauznia nikipata wateja nimwambie maana kuna nyumba kadhaa na viwanja amevishikilia.

Baada ya wiki hivi nikaanza kutengeneza Posters nakuziweka mitandaoni ili nipate wateja angalu wa kauznia nipate uzoefu.

Kweli baada ya kupost simu zikawa zinaanza kuita ASEE.

HAPO SASA NDIO SAFARI YANGU RASMI YA UDALALI IKAANZA, sasa kwenye hiki kisa au story nitakuelezea matukio ya kufurahisha, ya kusikitisha, dili haramu, dili za ajabu na mambo ya kushangaza ambayo nilikutana nayo. Lengo langu ni ujifunze Mambo mbalimbli ambayo madalai wankutana nayo, namna ya kupambana na changamoto za maisha bila kukataa tamaa, hela inavyoweza kumbadilishia malaika kwa shetani,na mambo mengine mengi.

Baada ya utangulizi huu nitaanz Rasmi Jumatatu hii kushusha vyuma.
 
EPS 6.

Nikawa tayari nimeacha kazi Rasmi na nimehama kibaha na nimehamia Rasmi Jiji la Dar es salaam mbezi kwa Msuguri.

Maisha mapya yakaanza na vichenji chenji kwneye ile hela ya Judy zilikuwa zimebaki nilikuwa nina jiko dogo la gesi, hivyo nikaenda kununua mahitaji ya ndani ili nijipange upya nijue namna ya kupambana na maisha.

Nikaendelea kukaa pale lakini story ya Masai ya udalali ilinivutia sana nikasema sasa hii ndio kazi ninayotaka nikafanye. Nilikuwa nampigia mara kwa mara masai na kuonana nae lengo anionyeshe njia maana aliniambia kwa kauznia nikipata wateja nimwambie maana kuna nyumba kadhaa na viwanja amevishikilia.

Baada ya wiki hivi nikaanza kutengeneza Posters nakuziweka mitandaoni ili nipate wateja angalu wa kauznia nipate uzoefu.

Kweli baada ya kupost simu zikawa zinaanza kuita ASEE.

HAPO SASA NDIO SAFARI YANGU RASMI YA UDALALI IKAANZA, sasa kwenye hiki kisa au story nitakuelezea matukio ya kufurahisha, ya kusikitisha, dili haramu, dili za ajabu na mambo ya kushangaza ambayo nilikutana nayo. Lengo langu ni ujifunze Mambo mbalimbli ambayo madalai wankutana nayo, namna ya kupambana na changamoto za maisha bila kukataa tamaa, hela inavyoweza kumbadilishia malaika kwa shetani,na mambo mengine mengi.

Baada ya utangulizi huu nitaanz Rasmi Jumatatu hii kushusha vyuma.
Duuuuh. Kama inavutia hivi
 
Back
Top Bottom