Mkasa wa kweli, kuhusu visa vya kushangaza nilivyokutana navyo katika kazi za Udalali

Mkasa wa kweli, kuhusu visa vya kushangaza nilivyokutana navyo katika kazi za Udalali

Oya mwanetu huyo juddy apewe maua yake na ukitaka kumuoa basi kuna mchango wako kwangu mzee.

Mie kama mwenyekiti wa jumuia ya WANAUME jamiiforum nitaongea na katibu, muweka hazina na wanachama wote kwa ujumla tumjadili juddy na adhabu gani upewe ukimbadilika baada ya kuoiga pesa.
 
Oya mwanetu huyo juddy apewe maua yake na ukitaka kumuoa basi kuna mchango wako kwangu mzee.

Mie kama mwenyekiti wa jumuia ya WANAUME jamiiforum nitaongea na katibu, muweka hazina na wanachama wote kwa ujumla tumjadili juddy na adhabu gani upewe ukimbadilika baada ya kuoiga pesa.
Akimbadilikia Judy Ni laana amejitafutia.
 
EPS 7

Simu za Udalali zikaanza Kuita, ila tataizo nilikuwa sina uzoefu w akumpanga mteja, nikawa namtafuta Masai ila masai kanishauri nikipata mteja nimungnishe nae ili iwe Rahisi, namimi nikafanya hivyo.

Mteja wa kwanza Tulipata dada mmoja yeye alitaka Nyumba nzima maeneo ya Mbezi, jamaa akampanga mbezi hamna ila kimara anaweza kupata kodi ilikuwa laki 250 kw Mwezi Yule dada alikuja kucheki siku ya kwanza akaridhikaila akasema atakuja na mume wake.

Basi akatupa service charge elfu ishirini, Masai akaniambia kwa sababu ndio unaanza chukua yote nipe buku ya bajaji tu.

Baada ya siku mbili hivi Yule dada akasema mume wake anakuja kuiona na kama atakubali watalipia, nikmpa amsai taarifa tukaenda kukutana nae jioni hivi kama saa Moja jioni wakaicheki wakakubali, masai akamvutia waya Bosi akamwambia aende steshenari Fulani hivi akachukue hapo mkataba, yeye yupo njiani anakuja kumkabidhi.

Wakacheki mkataba, wakasainisha wakapewa Account maana walisema wanalipa kwa njia ya CRDB, wakafanya malipo na sisi walituwekea TIGOPESA.

Nikagawana na Masai ila amsai akaniambia nimpe laki moja mimi nichukue laki na nusu , Daah nikaanza kuona Mwanga wa amisha mapya ndani ya wiki tu nimepata laki moja na nusu niaksema sasa haya ndio maisha.

Dili moja tu mzigo mrefu unapatikana,,Nikaenda na Masai tukaenda sehemu tukaagiza mchemsho na bia safari tukapiga na story nyingi ambazo zilikuwa zinanipa uzoefu.

Majira ya saa tano hivi tukaagana yeye akaenda mbezi mimi nikaenda zangu maghetoni, usiku huo nilikuwa na furaha sana nikampigia Judy nikamwambia namna ambavyo dili zimeanza kusoma na mzigo niliopiga.

Judy alinipongeza sana akanitia sana moyo, Judy kwenye kutia moyo utafikiri mnyaki.

Tuliongea mengi sana na kubwa aliniambia atakuja kunitembelea aone makazi mapya, tukapanga weekend aje maghetoni kufanya uzinduzi.

Baada ya hapo ilikuwa kila siku usiku lazima Nipost Kwenye magroup ya whatsap na Facebook, insta bado nilikuwa sina wadau, Ilikuwa ukiniunga kwenye Group tu bila kujali lina husu nini mimi usiku napost na asubuhi na Posti huko huko kwenye magroup ili mradi nipate wateja.

Ikawa ndio utaratibu wangu na kazi yangu kwa wakati huo, nilienda hivyo na baada ya mwezi nilikuwa tayari nimeshaanza kujulikana maana Masai alikuwa annipa sana mashavu na kunikutanisha na mabosi.

Kwa mwezi ule wa kwanza nilipata wateja kama wanne Hivi, lakini nakumbuka niliweka akiba laki tatu kwa mwezi huo mmoja.

Siku moja Yule dada niliyemtafutia Chumba Huyu tumwite Jeni, alinitafuta kwa simu

Jeni: Mambo dalali

Dalali : Niko salama, unaendeleaje mazingira hapo umeyapenda?

Jeni: Mazingira mazuri kwa kweli pana utulivu asante sana.

Dalali: Sawa sawa, asante kwa mrejesho.

Jeni: Asante dalali uje ututembelee maana hapa hawaai watu wengi nakuwa mpweka sana

Dalali: Nitakuja huko napita sana ila sikutaka kukusumbua.

Jeni: Poa.

Tuliongea mambo mengi sana ila kwa ufupi yalikuwa kwa mtiririko huo.

Kazi za Udalali huwa hatufuti namba ya mteja.



Kazi ziliendelea na Judy alikuwa ankuja sana maghetoni kunitembelea hadi akapozoea na vihela vikawa vimeanza kuingia ingia na mabosi wananitafuta wenyewe niwauzie vitu vyao.

Nikabadili ghetto likawa na muonekano tofauti lakini chumba nikaanza kukiona Kidogo na hakina hadhi tena ya Mimi DALALI MKUU kukaa hapo kwanza ni uswahilini sana. Maskini akipata…………

Jeni nilikuwa na wasiliana nae sana na katika Maongezi yetu akaniambia Kwamba yeye hajaolewa Yule jamaa aliyekuja anye ni mchepuko wake maana yeye ameoa. Pia akaniambia anafanya Kazi kwenye Kampuni moja hivi ya Mawakili yeye ni sekretari.

Lakini pia alinisimulia kuhusu changamoto alizokuwa za Mahusiano yake ikiwemo kukosa mtoto kwa muda mrefu japo anatamani sana.

Nilimtia moyo lakini kwenye mambo ya Kiroho niko vizuri kidogo nikamuombea nikaahidi kwamba nitaendelea Kumuweka kwenye maombi na nitaenda kwao niwe namuombea.

Alifurahi sana sasa mazoea yakazidi ikawa kila akiamka lazima anicheki kwa whatsap, au apige usiku video call yaani akanizoea sana na akawa huru kunieleza vitu vingi sana.

Na mimi nikawa najitahidi sana maana nilikuwa mlokole Mlevi, na yeye ilionekana alinizoea zaidi baada ya kumdanganya nimeokoka na ni mwana maombi (Huko nyuma nimekulia kwenye maisha ya dini sana na ni mtu wa maombi licha ya kuwa mlevi)

Jumapili moja niliamua niende kwake nikamtembelee kwake, nilivaa Kaunda suti yangu moja ya Kilokole alinishonea Judy, Niliwaka kama Pastor kabisa.



Nilienda nikamkuta amekaa sndani mwenyewe na akanihakikishia kwamba usalama upo Jamaa yake Jumapili huwa haendi kule maana anatoka na familia yake OUT, mimi dalali kichwani mawazo yangu yalikuwa yakifisi kabisa nikasema nikifika tu naomba Tunda kilokole na alzima nimle.

Nilifika nikamkuta sebuleni kibarazani amekaa anachezea simu yake

Dalali Mkuu: Habari Jeni! Mambo vipi?

Jeni: Poa sana Dalali Mkuu! Karibu sana.

Dalali Mkuu: Asante sana,

Jeni: Ubize san, leo hatimaye umekuja

Dalali Mkuu: Kweli kazi zinanibana sana kazi zetu hizi hazina ratiba uanweza kupanda daladala ukapigiwa simu na mteja umepeleke site

Jeni: Hehe

Baada ya mazungumzo mafupi nikajumuika nae tukaendelea na stori za hapa na pale.

Kisha akaniambia Karibu ukae ndani maana nje huku tukiongea tu majirani wote wanasikia huko.

Akatangulia ndani lakini mawazo yangu yote nilisema leo simwachi, nikimuacha atanione mnyonge sana hapa Nipige mzigo niachane nae mchepuko wa watu huyu.

Ndani tulipoingia sikutaka Kumwachia pumzi nilianza na stori za Uchokozi nikimtania alivyo mzuri, akaishia kusema tu anapenda utani wangu na amneno yangu.

Nikapna time ianenda nikamsogelea alipokaa, alikuwa amekaa kwenye Kisofa hivi, nikamshika Begani alafu nikamwangalia Usoni, nikaona sura yake inabadilika kwa kasi sana.
 
EPS 8.

Niliona sura yake imebadilika ghafla, alishtuka ila ilionekana kama hajafurahia kitendo hicho, na mimi nikabadili Gia angani, nikamwmabia Fungamacho nikuombee Niondoke akaanza kutabasamu.

Alicheka akaniambia umenishtua sana nilifikiri unataka kunibaka.

Nikamwmabia kama ningekubaka ungefanyaje wakati umenikaribisha ndani mwenyewe, aliishia kucheka cheka tu na mimi nikaamua kubadili mazungumzo.

Nilikaa pale hadi saaa tatu nikala pale Chakula cha Jioni nikaagana nae, nikaondoka.

Kama kawaida nikapitia Chimbo nikapiga safari zangu kadhaa nikaenda Nyumbani Kulala.

Nilianza Kumpigia Judy kwanza maana tangu mchana sijawasiliana nae na sms zake sikuweza kuzijibu, tukapnga mambo mengi ya maisha yetu mustakabali wangu akaniuliza kama naenelea kutafuta kazi au nimerizika na kazi ya udalali, wakati naongea nae naona Jeni nae anapiga kwa Fujo sana.

Sikupokea niliongea na Judy tukaagana nikampigia sasa Jeni nimsikilize.

Alianza kuniambia kwamba amefurahi sana nilivyoenda kwake, akaniuliza kama nina mahusiano yoyote nikamdanganya kwa sasa sina akaniambia hana usingizi kabisa yupo tu mwenyewe akaniambia anatamani tena ingelala kabisa.

Urafiki wetu uliendelea kukua kwa kasi ya 5G akaanza kunipa Dili ananiunganisha na marafiki zake,wanaohitaji nyumba na viwanja.

Matukio menginenayaruka maana hayana maana.

Alininunganisha na jaMaa Fulani hivi walikuwa wanatafuta sehemu ya kuweka amshine ya Kufyatulia Tofali nikamtafutia huyo Jamaa alikuwa ni kibosile wa taaisisi Fulani ipo karibu na BOT.

Yule mwamba Tumuite Idris,Idris nilimtafutia sehemu ya tofali akapata maeneo ya Huko njia ya Goba, akanipa ya udalali ilikuwa laki mbili ila alinitumia Laki tatu nay a kutolea.

Idris alinikubali sana, akawa ananipa dili ndogo ndogo ananitumahata akiwa na ishu ndogo tu ananiambia nitafutie Bodaboda, au nikamuulizie vitu au bidhaa Fulani nikawa Napata sana hela. Kwa idris kwa wiki tu nilikuwa Napata hadi laki mbili maana alinifanya kama mesenja wake.

Kikubwa alisema mimi ni mwaminifu sana, Na anapenda sana Uchapakazi wangu na uchapu.

Alikuwa akinishirikisha vitu Vingi sana sana akawa sasa rafiki yangu anaiita tunaenda kula bata Jioni maeneo tofauti tofauti.

Nilikula sana bata na viwanja huko na kukutana na mabosi ambao nilipata connection nyingi.

Simu moja tunatoka Tegeta akaniambia anisogeza hadi mbezi mwisho Tulipofika pale ndio alinishangaza sana na Hiki ndio kisa cha Kwanza kwenye kazi yangu ya Udalali.

Tulipofika katika ya Goba njia nne na njia panda ya tegeta A kuna sehem kuna sheli kwa Juu yake, Jamaa akaniambia nataka nikuambie Kitu Ufanye ukiweza nakupa utajiri.

Akaniambi nina Kondomu hapa nisugue yaani nimfi…. Goli moja maana anataka kwenda kwa Mke wake Akaniambia akma siwezi kuna sehemu alinielekeza niende hapo kwa madai yake kuna mashoga nikamtafutie hapo mtu na alionekana yupo serious sana. DAAH nilishangaa sana nikamuuliza tena kama sijamsikia hivi. Niliona amenidharau sana nilikasirika mno yani
 
Eps 9

Nikamchana nikamwambia hilo dili siwezi kwa kweli, akanimbia twende tukifika unashuka unamuelekeza kwa gari nilimkatalia kabisa nikamwamabia hiyo ni ngumu sana.

Nikamwambia niache hapa niondoke tu ukiwa na dili nyingine utanipa lakini kwa Hii hapana, akanisogeza hadi mbezi kwa msuguri akaniacha hapo. Nikaeleka home nikiwa na mwazo sana kwanza ni mtu mwenye status Kubwa sana katika jamii, ana familia alafu ni mtu wa ibada sana swala zote tano. HIKI NI KISA CHA KWANZA Cha ajabu nilichokutana nacho baadae huko mbele nitakuja kuelezea nikiona kuna sababu ya kufanya hivyo.



Basi baada ya Kuchana na Idris kama kawaida kabla ya kurudi home lazima nipitie sehemu nipate safari au konyagi ndio ilikuwa ratiba yangu ya kila siku.

Kwa uapnde wa kazi nilikuwa nimeshaaminika sana na connection nikawa sasa sifanyi tena za kupanga nyumba na viwanja tu Nikawa sasa natafuta an Masoko ya bidhaa mbalimbali. Nilikuwa natafutia makampuni tender kwenye taasisi za umma na serikali so nikawa maisha yamebadilika kwa kweli.

Muda huo niliamua kumhamisha Judy kibaha ili niwe karibu nae, sio kumuoa, Nilimtafutia sehemu akaweka ofisi yake ya kushonea Nguo maeneo ya njia ya Kinyerezi, Judy alikuwa na bidii sana katika kazi zake,.

Niliona ni vyema nikamlipa fadhila kwa namna alivyokuwa akinijali sana kipindi nasota.

Judy alikuwa ananipenda sana na siku zote alikuwa ananikumbushia suala la Kwenda kujitambulisha kwao ili nifahamike lakini pia wazazi watupe Baraka za kuanza maisha.

Hilo suala lilikuwa linanikera sana nikaona Sasa anataka kulazimisha ndoa nikawa nampanga sana uzuri nikimpanga alikuwa ananielewa.

Alikuwa anapambana sana kwenye kazi yake kuna wanafunzi pia alikuwa anawafundisha pale na wateja walikuwa wanamkubali sana maana alikuwa anjua kushona nguo za kiume na kike mitindo karibu yote alikuwa anpiga sana hela.

Siku moja aliniambia amekusanya ana akiba ya karibu million tatu ananishauri niongezee nikanunue kiwanja, ila nilimkatalia maana kuna dalili nilikuwa naziona nikasema nisije kumuumiza akaumia zaidi.

WAKUU MIO SIO MWANDISHI MZURI, ILA KWA LEO NAISHIA HAPA KUNA MATUKIO MANNE TU NDIO NITAYAZUNGUMZIA KWA UPANA WAKE JUMATATU.

NITAANDIKA KWA KIFUPI EPS KAMA TANO TU ALAFU TUMALZIE
 
Eps 9

Nikamchana nikamwambia hilo dili siwezi kwa kweli, akanimbia twende tukifika unashuka unamuelekeza kwa gari nilimkatalia kabisa nikamwamabia hiyo ni ngumu sana.

Nikamwambia niache hapa niondoke tu ukiwa na dili nyingine utanipa lakini kwa Hii hapana, akanisogeza hadi mbezi kwa msuguri akaniacha hapo. Nikaeleka home nikiwa na mwazo sana kwanza ni mtu mwenye status Kubwa sana katika jamii, ana familia alafu ni mtu wa ibada sana swala zote tano. HIKI NI KISA CHA KWANZA Cha ajabu nilichokutana nacho baadae huko mbele nitakuja kuelezea nikiona kuna sababu ya kufanya hivyo.



Basi baada ya Kuchana na Idris kama kawaida kabla ya kurudi home lazima nipitie sehemu nipate safari au konyagi ndio ilikuwa ratiba yangu ya kila siku.

Kwa uapnde wa kazi nilikuwa nimeshaaminika sana na connection nikawa sasa sifanyi tena za kupanga nyumba na viwanja tu Nikawa sasa natafuta an Masoko ya bidhaa mbalimbali. Nilikuwa natafutia makampuni tender kwenye taasisi za umma na serikali so nikawa maisha yamebadilika kwa kweli.

Muda huo niliamua kumhamisha Judy kibaha ili niwe karibu nae, sio kumuoa, Nilimtafutia sehemu akaweka ofisi yake ya kushonea Nguo maeneo ya njia ya Kinyerezi, Judy alikuwa na bidii sana katika kazi zake,.

Niliona ni vyema nikamlipa fadhila kwa namna alivyokuwa akinijali sana kipindi nasota.

Judy alikuwa ananipenda sana na siku zote alikuwa ananikumbushia suala la Kwenda kujitambulisha kwao ili nifahamike lakini pia wazazi watupe Baraka za kuanza maisha.

Hilo suala lilikuwa linanikera sana nikaona Sasa anataka kulazimisha ndoa nikawa nampanga sana uzuri nikimpanga alikuwa ananielewa.

Alikuwa anapambana sana kwenye kazi yake kuna wanafunzi pia alikuwa anawafundisha pale na wateja walikuwa wanamkubali sana maana alikuwa anjua kushona nguo za kiume na kike mitindo karibu yote alikuwa anpiga sana hela.

Siku moja aliniambia amekusanya ana akiba ya karibu million tatu ananishauri niongezee nikanunue kiwanja, ila nilimkatalia maana kuna dalili nilikuwa naziona nikasema nisije kumuumiza akaumia zaidi.

WAKUU MIO SIO MWANDISHI MZURI, ILA KWA LEO NAISHIA HAPA KUNA MATUKIO MANNE TU NDIO NITAYAZUNGUMZIA KWA UPANA WAKE JUMATATU.

NITAANDIKA KWA KIFUPI EPS KAMA TANO TU ALAFU TUMALZIE
Jitahidi umalizie hata Kama ni usiku mkuu.
 
Back
Top Bottom