Mkasa wa kweli, kuhusu visa vya kushangaza nilivyokutana navyo katika kazi za Udalali

Mkasa wa kweli, kuhusu visa vya kushangaza nilivyokutana navyo katika kazi za Udalali

EPS 12

Nilifika kwa Judy sikumkuta Nyumbani, nikampigai simu yangu wala hajapokea, nikamwambia Tu kwamba Nipo kwako uko wapi? Nilikaa wee wala hakujibu nikaamua niondoke nikajipange nikamalizane na Kesi yangu.

Jumatatu asubuhi nilimpitia Masai tukaenda hadi staki shari pale, tulipofika Tukaambiwa subirini tulikaa hadi saa sita wakaniambia Niondoke wakinihitaji watanipia simu muda wowote.

Tuliondoka na pale nilijisemea Jeni sitamtafuta tena maana balaa lote limeletwa nay eye, Kunishirikisha mambo yake na jamaa yake.

Nilienda Kinyrezi na Masai tukapitia sehemu kuna bar Fulani hivi ipo karibu na stand hii mpya ya Kinyerezi, tukala hapo vitu mdogo mdogo huku tunapeana mbinu za kumalizana na jamaa, na ushauri ulikuwa nimtafute niongee naye nje ya polisi maana hata polisi walitushauri hivyo hivyo.

Baada ya amzungumzo mafupi Tuliagana, nikamtafuta judy lakini hata hivyo hakupokea simu nikajua huyu bado ana hasira Hivyo atanitafuta tu akishanimisi.


Huku nyuma bado nilikuwa napiga mishe na Idris lile wazo lake, nililipeleka Kijiweni nikawasilisha mada pale nikawaambia wazee kuna Jamaa anataka kupelekewa Moto ni mwanaume, hivyo anatafuta Kijana wa Kumpelekea moto.

Jamaa walicheka sana wakaniambia kwamba Huko ninakoelekea Ni kubaya mno waliponda sana tukaachana hadi nikajuta kwani nimepeleka amda ya kijinga hivyo .

Wakati natoka mshikaji wangu huyu Tumwite Juma alikuwa ana saloon yake mitaa Fulani sio mbali na kijiweni, akaniambia hilo dili amelipenda sana nimuonyeshe picha ya huyo mtu.

Chap nikafungua simu nikamuonyesha na akaniambia pale nimevunga tu ila hayo mambo ya akwaida kabisa, tukakubaliana nimfichie siri yake, Kisha baadae nikamuunganisha na jamaa wakaendelea Kuchati wanavyojua.

Idris alikuwa ameniambia nisimpe detail zake kabisa maana alikuwa ni mtumishi kweNye taasisi muhimu hivyo ingeweza kumchafulia.

Jamaa walikubalina makubaliano yao, ila mara kwa mara Jamaa alikuwa ananiambia anamfi..ia kwa Gar yake au wakati mwingine wanaenda Club anamfi…ia nyuma ya Club.

Ila kwa Dar ushoga upo kwa kiwango kikubwa sana na unafanywa na watu wakubwa mno hasa vigogo na baadhi ya watumishi wa Dini, wafanyabaishara na watu wa kawaida.

Kuna uchafu mwingi sana unafanyika kwenye Bar hizi kubwa watu wanapelekewa moto sana, na mtu anakuwa ana familia kabisa ila na yeye anapelekewa moto tena wakati mwingine na vijana wadogo tu.

Nasema hivyo kwa sababu Yule mshikaji wangu juma Baada ya yeye kumuunganisha na Idris nilikuwa namdadisi kianina alikuwa ananipa Codes mying sana maeneo anakowapata kwenye bara wanazokaa nilikuwa nazijua kabisa.

Serikali ikitaka kudhibiti hii tabia inakuwa ni ngumu sana maana wanaotakiwa kudhibiti ndio wadau wakubwa wa hizo mambo.

Kwa upande wake Idris alinishukuru sana, alikuwa ananitoa sana kwa kunipa dili ndogo ndogo, ilifika wakati sasa hadi kwenye hizo mambo za kumpelekea hao wadau nikawa nimezoea kuna maeneo ya hatari alikuwa ananituma nikamchukulie na nilikuwa naenda kama kawaida.

HIKI NI KITU AMBACHO NAKIJUTIA SANA Umasikini unaweza ukajikuta unafanya biashara yoyote ili upate hela tama ni mbaya sana. Ilikuwa ananiachia gari naenda kumchukulia basha kwenye hayo maeneo wanakopatikana. Na wale wadau niliokuwa naenda kuwachukua nao wakawa wamenizoea so wakawa wananiambia niwe nawaunganisha an wadau (Wanaitana B na T b ni anayepigw na T anayepiga) Ila kuna wengine wako kote kote.

Hiki ni kisa ambacho kamwe sitakisahau na kilinishangaza sana kuona namna watu walivyokosa maadili, jinsi jamii ilivyoharibik.

Na ile ni kazi ya laana baada ya kuanza kudalalia hizo mambo na kanisani nilianza kuacha kwendahata nguvu ya kuomba iliapungua kuna jinsi ambavyo nilikuwa naona nina hatia kuwaunganisha watu na hao wafi..aji.

Japo nilipiga sana hela aana inahusisha vigogo wenye hela sijui inahusishwa na imani za kishirikina au vipi hilo sijui.

Ni kitu amabcho hata leo ukinipa Billioni moja siwezi kukuunganisha na hao watu kabisa. Ni kisa ambacho kimeacha kumbumbuku mbaya sana ndani yangu.



KWA UPANDE MWINGINE, Jeni alikuja kunitafuta baada ya kutoka polisi baada ya siku mbili hivi, nikataka nisipokee ila akaniomba sana nionane nae ana amzungumzo muhimu na mimi, ila nikamwambia hilo haliwezekani.

Ila baada ya kunishawishi na kuniaminisha wkamba hakuna chochote kibaya nilimuomba Masai niende nae lakini pia tukutane sehemu ambayo ina usalama wa kutosha.

Masai alinitahadharisha sana ila akaniambia tumwambie tukutane mbezi mwisho ila akifika pale tuchukue usafiri tuende malamba huko ndani ndani kuna Bar ya kiaina tu ipo malamba msikitini inaitwa Kilimani ili tukakae hapo tuongee, itakuwa salama sana.

Basi tulifanya hivyo tulipofika pale nilimwmabia amsai asikae mbali sana na eneo hilo akakaa kwneye meza ipo karibu na sehemu ya kuingilia , muda wote nilikuwa nimekunja sana sura yaani kama sitaki utani tena maana nilikuwa naona kabisa jela inanichungulia.

Nilimwambia muda wangu nimchache sana hivyo nenda kwenye point moja kwa moja hasa kwanini ulinihusisha mimi kwenye masuala yenu ?

Jeni akaniangalia akaona kabisa nipo siriazi sana na sihitaji utani, lakini pia hakuwahi kunizoea kuwa an staili hiyo.

Alijua hapa nimeshakasirika na hivyo sihitaji utani kabisa.

Kwanza akaniambia hayo tutayaongea baadae Kidogo ila ana habari nyingine njema alitaka anishirikishe na habari yenyewe ni kwamba baada ya kufanya ile Program ya Maombi niliyompa kwa mara ya kwanza Ameanza kuona siku zake maana alikuwa amekaa karibu miaka mitatu (hayo ni kwa mujibu wa maelezo yake) na tayari ka mara ya kwanza ameona siku zake.

Moyo wangu ulilipuka Paap nilisikia furaha ya ajabu mno (kwa wale waombaji wanajua wanapoomba au kuomwombea mtu Mungu akijibu kuna furaha unaipata)

Japo nilikuwa na hasira nilishindwa Kujizuia kabisa nikajikuta naanza kutabasam na Kumpa Mungu utukufu nikijua kwamba kwa sehemu angalau amepata mwanga maana ni jambo lililokuwa linampa shida sana.

Nilimwambia kama Mungu amejibu hili amini kwamba ni dalili za Kufungua pia uzazi kwako endelea Kumuamini Mungu.

Alinishukuru ila nikamwabia Sifa na utukufu anastahili Mungu peke yake.

Ila nikamwmabia hili tutazungumza baadae maana tayari limepita sasa twende kwenye jambo lililotokea maana linaninyima Amani kabisa na sielewi ilikuwaje mimi nikaingizwa na nikaonekana mimi namzunguka jamaa ake.

Akaanza Kuniomba Msamaha kwanza “Dalali mkuu nisamehe sana mshikaji wangu, yaani mimi nilikuwa mara nyingi ukija namwambia kwamba nipo na wewe, lakini pia mambo mengi nilikuwa anmshirikisha mimi sikuona shida kabisa maana ni mtu wangu”

“Ila baada ya kuanza Kugombana gombana akawa ana hisia Kwamba wewe ndio unatoka na mimi, na majirani pia walimwambia huwa unakuja nyumbani, lakini unapokuja ofisini kufanya kazi pale akaunganisha hayo matukio akajua kabisa unahusika”

“sasa ile siku kabla ya Tukio kutokea nilikuwa naongea na simu muda mrefu alikuwa anpiga anaambiwa Iko bize nikamwmabia nilikuwa naongea na wewe”

Alinielezea mchongo mzima kulikuwa na mambo mengi sana ila alimwmabia Hao watu wako lazima mimi nitadili ano.

Kuhusu huyo anayetaka kumuoa aliniambaia alishawahi kumshirikisha, lakini pia hata walipogombana alimwmabia tena kwamba Yeye anataka kuolewa hivyo inabidi wasahau kila mtu akatengeneze familia yake.

Ila jamaa alitaka kumharibia so alikuwa anatafuta namba ya Brown ili amchimbe biti japo hakuweza kuipata yangu ndio ilikuwa rahisi na alikuwa na uhakika nimemla mchepuko wake.

Lakini pia aliniambia amewatuma marafiki zake wakaongee nae ili amwachie aendelee na harakati zake za ndoa.

Wanawake wanatakiwa kujifunza jambo hasa kuingia kwenye mahusiano na mume wa mtu itakuja kukutesa sana pale unapofikia wakati unaamua wewe kuwa na Familia yako, wanaume ni wabinafsi wao wanaangalia tu mambo yao hata jali kuhusiana na Future yako

Lakini pia wanaume inabidi michepuko ikipata mtu wa Kumuoa umwache mwenzio aende tu maana kama dini yako hairuhusu huyo hutaweza kumuoa wewe.



Kwa upande wa Judy mawasiliano bado yalikuwa magumu mno ila pale ilikuwa ni karibu sana na anapoishi tulikaa na Masai pale msikitini tukala vitu sana hadi saa nne usiku, nikamsindiiza sehemu masai akachukue Ugoro kwa jamaa mmoja anitwa masai pia anakaa aeneo yale yale ana kakibanda kampekana na bar moja inaitwa LITE PUB AU KIBOZONE. Kipindi hicho kibozone ilikuwa haipo.

Baada ya hapo ilibidi niende tena wka Judy nikajue hatma yangu kama tumeachana au vipi.

Nilifika nikamgongea akauliza nani? Dalali mkuu

Kwa sababu pale kulikuwa na watu hakutaka kuleta mzozo aliniambia tu nisubiri nakuja, alitoka amevalia Ki traki na Kisweta cha njano kilikua kimezichora sana Chuchu zake na tama ya kifisi ikaanza kuniingia.

Alifungua na kufunga yaani alijua naweza kuzama ndani akaniambia tusogee hapo mbele tuongee.

Tulipofika umbali kama mita hamsini hivi akaniambia Mimi sihitaji Fujo kabisa ndio maana nimekuja huko wala sitaki Ugomvi, naomba Uondoke sina kitu chochote naweza Kuongea na wewe nimekuvumilia sana hubadiliki kila siku ni matukio tu.

Unafanya mambo wazi kabisa hujali kama naumia wala nini, unanitafuta ukiwa na shida zake, yaani ukihitaji ngoneo unanitafuta popote ukishamaliza haja zako unaenda kwa Malaya zako.

Maisha ya aina hiyo siyataki mimi, dharau zako zimenichosha kwa kweli.

Mimi muda huo nilikuwa namsikiliza tu sikutaka kabisa Kumjibu

Akaongea sana maneno ya kuumiza sana mengi ikiwa ni hisia zake tu za kusadikika nyingine ilikuwa ni kweli ila sikutaka kumkatisha lengo langu aongee yote amalize yote kabisa.

Aliongea sana hadi machozi yakawa yanamtoka mimi kimya nilisema ngoja nimuache ateme nyongo ili amalize hasira zake.

Baada ya kuongea alianza Kuondoka nikamshika mkono chapu nikamwmabia subiri uanenda wapi, akaniambia mimi nimeshamaliza na siwezi kuongea tena na wewe na naomba hapa usifike tena wala usinitafute tena.

Nilimsihi sana anisikilize nilimwmabia naomba dakika tano tu kama ulivyoongea wewe na Mimi niongee kisha ufanye maamuzi yako.

"Judy, napenda kuanza kwa kukiri kwamba nimekosea sana kwa mambo mengi. Najua nimevnja imani yako na kuvunja moyo wako,nimkekuuiza sana na kwa hilo ninaomba msamaha sana asee. Sikukusudia kukuumiza, na najuta sana kwa kile nilichokifanya. Naomba unipe nafasi ya nikuelezee kilichotokea Ijumaa. Nakupenda sana na nina amini utanielewa.

Nilipiga hapo maneno kama dakika tatu hivi nikaona ameshusha pumzi muda huo tulikua tumesimama. Tukasogea sehemu tukaaa sasa nikaanza kumpanga kilichotokea nikamsimulia Tukio zima ila hakuamini

Nikamuonyesha na Mgongoni Virungu nilivyopigwa maana kuna vialama vilibakia, nikampigia na Masai akaeleza akaamini ni kweli. Lakini pia nilimwambai siku ya Kurudi nitaenda nae ili aamini ni kweli.

Nilimwmabia sikutaka kumwambia nipo polisi ningemshtua sana hivyo lengo langu halikuwa baya.

Alionekana kuniamini na mimi nikaanza kumkandia umenihumu bila kujua kinachoendelea kwanini? Akaanza kujiona kwamba yeye ndio amekosea sasa akataka kuomba msamaha nikamwambia usijali yameisha.

Nikatumia mwanya ule ule kumshawishi sasa Tuende Nyumbani, aliweka pingamzii ila baadae akaniambia aende akaweke mambo sawa kwanza ghetto kwake. Muda huo ilikuwa ni kama saa sita Hivi na mitaa ya kule wka wakati huo kunakuwa kumepoa sana.



Alienda hakuchukua mud asana tulianza safari ya kutafuta usafiri ila ilikuwa ngumu so ikabidi tuchukue Pikpiki hadi mbezi kisha mbezi ndio tuchukue boda boda nyingine ya kunifikisha Nyumbani.



Bada ya kufika home na Kuoga Nilimsogeza kitandani sikutaka Kupoteza Muda hiyo siku kabisa niliusogeza mdomo karibu na mdomo wake na taratibu nilianza kupata denda. . Niliinyonya midomo yake mizuri taratibu naye hakuwa mbali kunipa ushirikiano kwa ufundi mkubwa



Ulimi wake ulikuwa unazunguka tu na kuvinjari ndani yamdomo taratibu huku akitoa miguno ile na sauti ambazo hazieleweki ambayo ilikuwa inaniongezea sana hamu ya kutaka kuingia katika mchezo moja kwa moja ila niliona bado ni mapema lazima zoezi liendelee kwanza



Wakati zoezi la denda linaendelea mikono pia haikuwa mbali na kifua chake kabisa na kushika sehemu ya juu zaidi ya Maembe yake ambayo muda huo yalikuwa yamekuwa na U Fulani hivi kama cha Under 18.



Muda huo ndio miguno na kunena kwa Lugha za malaika zilikuwa zinashika kasi kwa upande wake.



niliendelea kupapasa kifua huku nikiziminya minya embe hizo kwa namna ambazo ni kama mtu alikuwa anachagua kama ndizi zimeiva au bado.



Kila nilipokuwa nikiminya ndivyo miguno yake pia ilivyokuwa inaongezeka Kila hatua ndio alikuwa anakolea na Kuongeza kelele za hapa na pale Yaani ilikuwa kama ndio mara ya Kwanza tunakutana



Siku hii alikuwa anatoa ushirikiano sana. mkono wake alikuwa naye anautembeza na Kufanya ziara kwenye baadhi ya maeneo Muhimu

Namimi nikaamua kubadili uelekeo na kumuweka mkao ambao ungeniwezesha kuchezea vizuri ikulu yake kwa kutumia mashine yangu.



Baada ya zoezi hilo na mazoezi mengine niliona tayari ameshalowa kweli kwlei na Yupo tayari kuanza mbio za matrathon

Na yeye aliishika amshine yangu kwa ustadi sana akaanza kuchomeka mwenyewe kunako asee Ilikuwa ni game moja tafu sana Ilichezwa kwa muda sana baada ya mbio zile Tulikuwa Hoi na muda umeshaenda sana, Usiku huo Ulikuwa wa Furaha na Yeye niliona kabisa amefurahia show na alisahau yote ya huko nyuma yaani ilikuwa kama ndio tunaanza upya.



Siku yetu iliisha kwa furaha na ikawa ndio mwanzo mpya tena.
DALALI MKUU
Screenshot_20240630-104622.jpg
Screenshot_20240630-104622.jpg
Screenshot_20240630-104622.jpg
 
EPS 14

N.B Udalali niliacha kuna sehemu nilipata ajira nafanya hapo tangu mwezi wanne mwaka Huu lakini hata hivyo nilikuwa nimeshaacha. Sasa hivi nafanya mara chache sana inapobidi. Nimeweka sawa ili kupunguza maswali.

Kama wewe ni mpangaji au ulishawahi Kununua nyumba kwa watu au kiwanja bila shaka ulishawahi Kukutana na kisa cha Ushirikina hasa Uchawi kwenye Shughuli zako.

Miongoni mwa visa nilivyokutana navyo katika pilikapilika pilika za Udalali ni kazi hii Kuhusishwa na vitendo vya Ushirikina.

Kabla sijaingia kwenye udalali nilikuwa nafikiri kwamba Wenye nyumba ni washirikina sana kumbe visa Vingine vinafanywa na baadhi ya madalali wasiokuwa na maadili.

Kuna visa vingi sana vya watu kufanya Ushirikina asee.

Kisa kimojawapo siku moja Tupo bar na dalali mmoja anaitwa Rama, wakati huo ndio nilikua Nimeshakaa sana kwenye udalali lakini tukawa tuna share Experience za kazi zetu.

Nlimwambia rama Ilivyo ngumu Kumshawishi mteja hadi akubaliane na kazi yako

Rama akaniambia tatizo lako wewe Ni wale wa “MUNGU NISAIDIE” kutoboa ni ngumu sana lazima utembee kidogo kwa wazee.

Aliniambia kwamba madalali wengi wana wa wini wateja kwa sababu ya ushirikina.

Alinisimulia namna ilivyo kwamba ili uweze kupata mteja na hata kumbadilisha akili aache chaguo lake na akubaliane na chagu lako sio kazi rahisi.

Hivyo kuna Bibi ambaye wanamtumia yupo Kihesa Iringa anatoa dawa ya mvuto ambayo ukiitumia ukimshawishi mteja hata nyumba ambayo ipo bondeni anakubali hata kama nyumba aliyokuwa anahitaji yenye sifa Fulani, unaweza kumbadilisha

Huyo bibi wa Kihesa anakupa dawa ambayo ni kama kimzizi ambacho unatakiwa kukiweka mfuko wa nyuma wa suruali yako kila siku unapoenda kwenye mishe mishe zako au kama una kiofisi kuna kidawa anakupa unakiweka kwenye droo unachanganya anhela nyingine zinaitahela tu na watu.

Sikutaka kumbishia maana lengo langu ilikuwa nimsikilize tu ila mimi huwa simaini hayo mambo japo yapo ila sitaki kuyategemea kabisa madhara yake ni makubwa mkuu wala usiyatamani.

Sasa akaniambia kwamba yeye anacho kizizi akiongea na mteja yeyote lazima atakubali tu hata kama alihitaji nyumba Ubungo atampanga atampa ya Kimara au mbezi na atakubali.

Lakini pia unaweza ukawa unahitaji nyumba au kiwanja na mtu akakupeleka abondeni kabisa, au jirani na dampo au sehemu yenye makelele kama bar au kule wanakouza K, unajikuta uekubaliana nae na kulipia ukishalipia ndio akili zinaanza kukufunguka kumbe dawa yenyewe ndio inakuvuta.

Siku ukimkuta mtu amepanga vingunguti machinjoni na ni mtu mwenye akili timamu au amepanga mabondeni mvua ikinyesha tu anaingia ankutoka akiwa anogelea usije kushangaa ujue ni ushirikina unafanya kazi nah ii ni kazi inayofanywa na madalali njaa.

Rama alinaimbia wengine wanachanjiwa dawa kwenye Uume, wanapeleka majina yao kwa waganga kisha wanafanya wanachojua wanakuchanjia dawa kwenye Uboo au shingoni., huyo akikushawishi huchomoki mzee.

Kisa kingine cha Ushirikina hiki nilisimuliwa na Dalali Tumwite Tall wa Tabata Segerea yeye aliniambia sasa hivi dalali mkuu una connection sana na mabosi mpumbaze mmoja uanze kuzifaidi Kodi usikubali kukaa kizembe.

Iko hivi kuna mzee mmoja wa malamba mawili Mwisho, Alikua ndio mtaalam wa hayo mambo ilikuwa ukimkabidhi funguo tu na hauishi hapo anafanya ushirikina wa kukupeperusha anakufanya unasahau kabisa nyumba yako utakumbuka lakini kila ukipanga kwenda unaahirisha, mzee alikuwa anpanga anakula kodi tu kila mwezi na mwenye nyumba hajui chochote kinachoendelea.

Huyu mzee alikuwa an nyumba yake Malamba mawili Alikuwa anaiuza kwa taarifa za watu wa karibu ni kwamba alishawahi kuiuza kwa watu kadhaa alafu wakishalipia anabaki nayo.

Sasa yeye alikuwa na dawa zake alikuwa akishakuuzia nyumba unafanya malipo na anakuambia umpe wiki moja ahamie kwenye nyumba yake nyingine ila ukishalipia hutarudi tena huko na wala hutakumbuka mzee anaendelea kula hela na nyumba anabaki nayo.

Inasemekana yeye watu walikuja kugundua siri kuna jamaa alitaka kununua nyumba hiyo majirani wakamtonya kuhusu hilo swala mnunuzi akasema sasa huu ndio utakuwa mwisho wake. Jamaa akanunua nyumba wakafuata michakato yote kisha akampa hela yake akaondoka mzee akasemaapew siku tatu ahamishe vitu. Usiku akatengeneza dawa zake kama kawaida akafanya ya kufanya, Kesho yake asubuh mnunuzi akarudi akammabia ulichofanya umeshashindwa hama leo leo na ndio ikawa mwisho wa ufalme wa Yule mzee baada ya kuumbuliwa, Kumbe jamaa alikuwa amejipanga sana kiroho alikuwa na kinga zake za kichawi uwezo ukazidiana.

Kwa ambao wanasema uchawi haupo nawashangaa sana, ndio maana tunaomba Mungu kila siku ili atuepushe na hayo mambo.

Tall akaa ananishauri na mimi niitumie hiyo dawa kupeperusha mabosi angalu na mimi nipate nyumba moja niwe nalia kivulini jasho la mtu hiyo siku nilicheka sana nikaona sasa hii kazi sio. Sikuwahi kujaribu kabisa hilo jambo japo alinipa shuhuda nyingi sana.

Kuna mama nyumba moja ilikuwa kibaha ni Apartment nzuri sana, lakini kila wapangaji walikuwa wakikaa pale miezi sita wanaondoka wengine hata hawamalizi hata hiyo sita wanaondoka.

Kuna Familia moja walipanga hapo ilikuwa ikifika kila siku usiku wanasikia watu wanacheka sebuleni wakichungulia ahwaoni mtu.

Kuna watu walikuwa wakilala kuna mapaka yanalia kweli kweli nje ya nyumba yanatoa sauti za ajabu sana, wakati mwingine wakitoka wakirudi wanaona kama matone ya damu mlangoni lakini walikuwa hawaelwi kabisa ni nini kinafanyika.

Mwanzoni walifikiri kwamba labda ni ugeni mawazo na woga ndio unawafanya wanasikia hivyo.

Na aliyekuwa akisikia mara nyingi ilikuwa ni mke wa jamaa sasa siku wamekaa sebuleni TV ikawa inajiwasha na kujizima alafu inatokea kama sauti ya vicheko hivi vya kukera.

Walikuwa wamekaa sebeleni wote woga uliwaingia sasa la mwanaume alikausha kwamba sio uchawi kuna hitilafu baadae kweli ikatulia na wakasahau.

Vile visa vikazidi sasasiku hadi siku nyumba akawa haikaliki kuna wakati walikuwa wanasikia pia kama watu wanarusha mawe kwneye mabati lakini wakauliza majirani wanasema wao hawakusikia.

Majini yakawa yanawavamia usiku yanawanyonga sana jamaa akaona visa vimezidi wakati mwingine wanalala kitandani wakiamka wanajikuta wamelala chini sebuleni tena wakiwa watupu.

Jamaa ilibidi aanze kutafuta ushauri kwa wadau wake wakamwambia atumie dawa za kienyeji mara maji ya upako lakini wapi mateso yakawa ni makubwa sana usiku ni heka heka hakuna kulala. Mwisho wa siku jamaa ikabidi ashauriane na mke wake ahame na stori zikasambaa mtaani mwneye nyumba ni mshirikina na ndani kwake kuna majini.

Ila mwenye nyumba alikuwa ansikia akafikiri majirani wanamzushia au hawampendi kwa hiyo mambo ya Kiswahili wanasambaza kwa watu ili nyumba yake wapangaji wasidumu.

Taarifa zilisambaa sana hivyo akaaamu na yeye kufanya tafiti zake za tiba huko kwa wataalam ndio wapiga Ramli wakamtaji jina la mtu Fulani hivi kumbe ndio alikuwa dalali wake anayemletea wateja.

Kwanini dalali alifanya vile, kwa sababu ile nyumba ilikuwa ni nzuri na watu wanavutiwa nayo na kodi yake ilikuwa sio ndogo na kila akileta mteja anpewa kamisheni yake.

Hivyo kuna madawa alikuwa amesindika huko ili wapangaji wasiwe wana dumu wahame apelike wengine apige hela tu kirahisi, maana unaambiwa kuna wapangaji wengine walikuwa Wanaka hata wiki tu na kodi wanasamehe wanasema wamepata mchongo mkoani wanahama kumbe wamekimbia mbilinge mbilinge za majini.

Baadae waganga walikuja kutoa hayo mazindiko na nyumba kwa sasa sijui ikoje il naamini iko vizuri.

Hivi ni visa ambavyo kwenye udalali nilikutana navyo, Wenye nyumba na wapangaji umakini unahitaji Kama una Sali Sali sana ombea eneo lako kabla ya kuhamia, Wakristo wanafanya maombi yao ya kuteka na kumiliki sijui maombi ya vita n.k ili uweze kuishi vizuri, washirikina wanaweka pia mamlaka zao.

Kwenye uuzaji wa viwanja dalali akifika kwenye uwanja wako ukimpa kazi lakini akigundua unataka kumzunguka au kumpa mtu mwingine unaweza kuuza hicho kiwanja hata laki na kisipate mteja hadi yeye aamue.

Unaweza kuuza kiwanja hicho kwa mwaka mzima kila mteja akija munakubaliana bei anakubali kulipa akiondoka hata simu hapokei tena.

Hiki ni kisa kingine tena kwenye udalali na ni matukio ya kweli sio ya kusadikika. Nitarudi kuhitimisha kesho muda kama huu.
 
EPS 14

N.B Udalali niliacha kuna sehemu nilipata ajira nafanya hapo tangu mwezi wanne mwaka Huu lakini hata hivyo nilikuwa nimeshaacha. Sasa hivi nafanya mara chache sana inapobidi. Nimeweka sawa ili kupunguza maswali.

Kama wewe ni mpangaji au ulishawahi Kununua nyumba kwa watu au kiwanja bila shaka ulishawahi Kukutana na kisa cha Ushirikina hasa Uchawi kwenye Shughuli zako.

Miongoni mwa visa nilivyokutana navyo katika pilikapilika pilika za Udalali ni kazi hii Kuhusishwa na vitendo vya Ushirikina.

Kabla sijaingia kwenye udalali nilikuwa nafikiri kwamba Wenye nyumba ni washirikina sana kumbe visa Vingine vinafanywa na baadhi ya madalali wasiokuwa na maadili.

Kuna visa vingi sana vya watu kufanya Ushirikina asee.

Kisa kimojawapo siku moja Tupo bar na dalali mmoja anaitwa Rama, wakati huo ndio nilikua Nimeshakaa sana kwenye udalali lakini tukawa tuna share Experience za kazi zetu.

Nlimwambia rama Ilivyo ngumu Kumshawishi mteja hadi akubaliane na kazi yako

Rama akaniambia tatizo lako wewe Ni wale wa “MUNGU NISAIDIE” kutoboa ni ngumu sana lazima utembee kidogo kwa wazee.

Aliniambia kwamba madalali wengi wana wa wini wateja kwa sababu ya ushirikina.

Alinisimulia namna ilivyo kwamba ili uweze kupata mteja na hata kumbadilisha akili aache chaguo lake na akubaliane na chagu lako sio kazi rahisi.

Hivyo kuna Bibi ambaye wanamtumia yupo Kihesa Iringa anatoa dawa ya mvuto ambayo ukiitumia ukimshawishi mteja hata nyumba ambayo ipo bondeni anakubali hata kama nyumba aliyokuwa anahitaji yenye sifa Fulani, unaweza kumbadilisha

Huyo bibi wa Kihesa anakupa dawa ambayo ni kama kimzizi ambacho unatakiwa kukiweka mfuko wa nyuma wa suruali yako kila siku unapoenda kwenye mishe mishe zako au kama una kiofisi kuna kidawa anakupa unakiweka kwenye droo unachanganya anhela nyingine zinaitahela tu na watu.

Sikutaka kumbishia maana lengo langu ilikuwa nimsikilize tu ila mimi huwa simaini hayo mambo japo yapo ila sitaki kuyategemea kabisa madhara yake ni makubwa mkuu wala usiyatamani.

Sasa akaniambia kwamba yeye anacho kizizi akiongea na mteja yeyote lazima atakubali tu hata kama alihitaji nyumba Ubungo atampanga atampa ya Kimara au mbezi na atakubali.

Lakini pia unaweza ukawa unahitaji nyumba au kiwanja na mtu akakupeleka abondeni kabisa, au jirani na dampo au sehemu yenye makelele kama bar au kule wanakouza K, unajikuta uekubaliana nae na kulipia ukishalipia ndio akili zinaanza kukufunguka kumbe dawa yenyewe ndio inakuvuta.

Siku ukimkuta mtu amepanga vingunguti machinjoni na ni mtu mwenye akili timamu au amepanga mabondeni mvua ikinyesha tu anaingia ankutoka akiwa anogelea usije kushangaa ujue ni ushirikina unafanya kazi nah ii ni kazi inayofanywa na madalali njaa.

Rama alinaimbia wengine wanachanjiwa dawa kwenye Uume, wanapeleka majina yao kwa waganga kisha wanafanya wanachojua wanakuchanjia dawa kwenye Uboo au shingoni., huyo akikushawishi huchomoki mzee.

Kisa kingine cha Ushirikina hiki nilisimuliwa na Dalali Tumwite Tall wa Tabata Segerea yeye aliniambia sasa hivi dalali mkuu una connection sana na mabosi mpumbaze mmoja uanze kuzifaidi Kodi usikubali kukaa kizembe.

Iko hivi kuna mzee mmoja wa malamba mawili Mwisho, Alikua ndio mtaalam wa hayo mambo ilikuwa ukimkabidhi funguo tu na hauishi hapo anafanya ushirikina wa kukupeperusha anakufanya unasahau kabisa nyumba yako utakumbuka lakini kila ukipanga kwenda unaahirisha, mzee alikuwa anpanga anakula kodi tu kila mwezi na mwenye nyumba hajui chochote kinachoendelea.

Huyu mzee alikuwa an nyumba yake Malamba mawili Alikuwa anaiuza kwa taarifa za watu wa karibu ni kwamba alishawahi kuiuza kwa watu kadhaa alafu wakishalipia anabaki nayo.

Sasa yeye alikuwa na dawa zake alikuwa akishakuuzia nyumba unafanya malipo na anakuambia umpe wiki moja ahamie kwenye nyumba yake nyingine ila ukishalipia hutarudi tena huko na wala hutakumbuka mzee anaendelea kula hela na nyumba anabaki nayo.

Inasemekana yeye watu walikuja kugundua siri kuna jamaa alitaka kununua nyumba hiyo majirani wakamtonya kuhusu hilo swala mnunuzi akasema sasa huu ndio utakuwa mwisho wake. Jamaa akanunua nyumba wakafuata michakato yote kisha akampa hela yake akaondoka mzee akasemaapew siku tatu ahamishe vitu. Usiku akatengeneza dawa zake kama kawaida akafanya ya kufanya, Kesho yake asubuh mnunuzi akarudi akammabia ulichofanya umeshashindwa hama leo leo na ndio ikawa mwisho wa ufalme wa Yule mzee baada ya kuumbuliwa, Kumbe jamaa alikuwa amejipanga sana kiroho alikuwa na kinga zake za kichawi uwezo ukazidiana.

Kwa ambao wanasema uchawi haupo nawashangaa sana, ndio maana tunaomba Mungu kila siku ili atuepushe na hayo mambo.

Tall akaa ananishauri na mimi niitumie hiyo dawa kupeperusha mabosi angalu na mimi nipate nyumba moja niwe nalia kivulini jasho la mtu hiyo siku nilicheka sana nikaona sasa hii kazi sio. Sikuwahi kujaribu kabisa hilo jambo japo alinipa shuhuda nyingi sana.

Kuna mama nyumba moja ilikuwa kibaha ni Apartment nzuri sana, lakini kila wapangaji walikuwa wakikaa pale miezi sita wanaondoka wengine hata hawamalizi hata hiyo sita wanaondoka.

Kuna Familia moja walipanga hapo ilikuwa ikifika kila siku usiku wanasikia watu wanacheka sebuleni wakichungulia ahwaoni mtu.

Kuna watu walikuwa wakilala kuna mapaka yanalia kweli kweli nje ya nyumba yanatoa sauti za ajabu sana, wakati mwingine wakitoka wakirudi wanaona kama matone ya damu mlangoni lakini walikuwa hawaelwi kabisa ni nini kinafanyika.

Mwanzoni walifikiri kwamba labda ni ugeni mawazo na woga ndio unawafanya wanasikia hivyo.

Na aliyekuwa akisikia mara nyingi ilikuwa ni mke wa jamaa sasa siku wamekaa sebuleni TV ikawa inajiwasha na kujizima alafu inatokea kama sauti ya vicheko hivi vya kukera.

Walikuwa wamekaa sebeleni wote woga uliwaingia sasa la mwanaume alikausha kwamba sio uchawi kuna hitilafu baadae kweli ikatulia na wakasahau.

Vile visa vikazidi sasasiku hadi siku nyumba akawa haikaliki kuna wakati walikuwa wanasikia pia kama watu wanarusha mawe kwneye mabati lakini wakauliza majirani wanasema wao hawakusikia.

Majini yakawa yanawavamia usiku yanawanyonga sana jamaa akaona visa vimezidi wakati mwingine wanalala kitandani wakiamka wanajikuta wamelala chini sebuleni tena wakiwa watupu.

Jamaa ilibidi aanze kutafuta ushauri kwa wadau wake wakamwambia atumie dawa za kienyeji mara maji ya upako lakini wapi mateso yakawa ni makubwa sana usiku ni heka heka hakuna kulala. Mwisho wa siku jamaa ikabidi ashauriane na mke wake ahame na stori zikasambaa mtaani mwneye nyumba ni mshirikina na ndani kwake kuna majini.

Ila mwenye nyumba alikuwa ansikia akafikiri majirani wanamzushia au hawampendi kwa hiyo mambo ya Kiswahili wanasambaza kwa watu ili nyumba yake wapangaji wasidumu.

Taarifa zilisambaa sana hivyo akaaamu na yeye kufanya tafiti zake za tiba huko kwa wataalam ndio wapiga Ramli wakamtaji jina la mtu Fulani hivi kumbe ndio alikuwa dalali wake anayemletea wateja.

Kwanini dalali alifanya vile, kwa sababu ile nyumba ilikuwa ni nzuri na watu wanavutiwa nayo na kodi yake ilikuwa sio ndogo na kila akileta mteja anpewa kamisheni yake.

Hivyo kuna madawa alikuwa amesindika huko ili wapangaji wasiwe wana dumu wahame apelike wengine apige hela tu kirahisi, maana unaambiwa kuna wapangaji wengine walikuwa Wanaka hata wiki tu na kodi wanasamehe wanasema wamepata mchongo mkoani wanahama kumbe wamekimbia mbilinge mbilinge za majini.

Baadae waganga walikuja kutoa hayo mazindiko na nyumba kwa sasa sijui ikoje il naamini iko vizuri.

Hivi ni visa ambavyo kwenye udalali nilikutana navyo, Wenye nyumba na wapangaji umakini unahitaji Kama una Sali Sali sana ombea eneo lako kabla ya kuhamia, Wakristo wanafanya maombi yao ya kuteka na kumiliki sijui maombi ya vita n.k ili uweze kuishi vizuri, washirikina wanaweka pia mamlaka zao.

Kwenye uuzaji wa viwanja dalali akifika kwenye uwanja wako ukimpa kazi lakini akigundua unataka kumzunguka au kumpa mtu mwingine unaweza kuuza hicho kiwanja hata laki na kisipate mteja hadi yeye aamue.

Unaweza kuuza kiwanja hicho kwa mwaka mzima kila mteja akija munakubaliana bei anakubali kulipa akiondoka hata simu hapokei tena.

Hiki ni kisa kingine tena kwenye udalali na ni matukio ya kweli sio ya kusadikika. Nitarudi kuhitimisha kesho muda kama huu.
..
 
EPS 15

Baada ya kumalzia baadhi ya Visa kama nilivyowaambia kwenye Epsd za huko juu nilipewa Kesi ya kutishia Kuua kwa sababu ya Kuwa karibu sana na miongoni mwa wateja wangu wa mwanzo kabisa kwenye Udalali,Jeni.

Kesi nilikuwa naenda lakini wakanishauri nimalizane na mchepuko wa Jeni, ili mambo yasiwe mengi. Nilimtafuta Mchepuko wa Jeni nikaongea nae akakubali ila akaniambia nitafute hela nikafute hiyo kesi polisi. Nilimkubalia lakini sikufanya hivyo ahdi leo.

Jeni baada ya kuona mchepuo anamnganagania sana na anatamani ndoa, walienda kushirikisha marafiki zake wakaongea nae Mwamba ikabidi wakubaliane yaishe ili amruhusu mwenzie aolewe maana yeye hana namna anayoweza kufanya.

Jeni alikuja akapata mimba na alifurahi sana maana kwenye maisha yake hakutegemea kama ingewezekana tena maana kwa maelezo yake alikuwa amehangaika sana bila mafaniko, alinishukuru sana kwa maombi namna ambavyo tulishirikana aliahidi zawadi kubwa sana na kwa wakati huo kuna zawadi alinipa hii haina haja ya kuiandika.

Mwaka alikuja kuolewa akamfuata jamaa yake Huko kilndi Tanga wakaendelea na maisha yao na sasa ana watoto wawili.

Mwaka 2019 mwishoni Nilikuja Kupata pia mtoto nilizaa na Judy lakini hatukuoana, hivyo ilibidi wakati wa ujauzito alipokaribia kujifungua alirudi kwao na hata baada ya kujifungua alikaa sana, mimi nilikuwa naendela kuwasiliana nae kama kawaida na kumpa mahitaji yote Muhimu ya Mtoto.

Na mwaka huo pia niliacha shughuli za udalali kuna Dili ambalo Jeni alinipa kuna Company moja hivi nilikuwa naenda kwa ajili ya Kuandaa Tender Documentes na Ishu nyingine zinazohusiana na Tender mbalimbali lakini pia kwenye masuala ya IT ila jukumu langu kubwa lilikuwa ni IT nilipiga hapo kazi sana kwa Muda mrefu hivi.

Hadi siku niliyokuja kupata matatizo makubwa kwenye hiyo kazi nikaja nikafukuzwa kuna ishu ilitokea ya udanganyifu na mimi nikahusishwa moja kwa moja nikafukuzwa nakumbuka hicho kisa nilikisumilia huku miaka ya nyuma

Siwezi kusahau siku niliyofukuzwa kazi nikiwa baa

baada ya hapo nikajichanganya kwenye Company nyingine nikapata kazi kwenye Taasisi Fulani nikawa mkuu wa Kitengo cha Masoko nilifanya kazi pale na ilikuwa ni kazi ya Kusafiri sana nah ii ndio iliyonibadilisha kabisa, maana ilikuwa na Hel asana ile kazi.

Wakati huo Judy alisharudi dar tukaamua tusihi hivyo bila ndoa rasmi ya kisheria/kidini na mtoto alishakuwa mkubwa kabisa na hapo matukio ya usaliti asee yalikuwa yananitokea sana.

Alikuwa ananifuma sana na matukio ya usaliti, maana ile akzi ilikuwa inanikutanisha na watu wengi sana na wengi wao ni wanawake warembo na mimi ndio ilikuwa ugonjwa wangu

Ulevi ndio ilikuwa moja ya sifa yangu kuu Kuna bara za kimara huko, mbezi, na Goba hadi leo nimeacha vimeo vya madeni lakini pia nimeacha huko umaarufu wa Totozi na kulewa chakari.

Matukio yalipozidiana Judy yalimshinda maana tulikuwa hatuna hata watu wa maana wa kutusuluhisha, nilikuwa najitetea sana lakini mwisho wa siku aliamua Tuachane akaendelee na maisha yake.

Tuliahana na wala sikujali kabisa lakini mara kwa mara nilikuwa nawasiliana nae kwa ajili ya mtoto.

Ile kazi ilikuja kuingiliwa na mambo mengi biashara ikayumba wateja wakapungua maana mkoani watu walikuwa wameshaishtukia wauzaji wakawa wengi sana hivyo nikaachana nayo.

Baada ya kuachana nay o mwaka 2023 mwezi wa kwanza maisha yakabadilika sana akiba nikaanza kutumia kiba kidogo niliyokuwa nayo hadi zikaisha.

Jamaa yangu alikuwa kasulu akanipa mchongo wa biashara ya kulangua mazao, tulikuwa tunanunua nafaka kasulu na maeneo mengine ya Kigoma huko hadi katavi ile biashara ilikuwa ni ngumu sana maana kuna wateja tulikuwa tunawatumia mzigo huko dar lakini wakishapata mzigo wanaanza kuzingua malipo.

Lakini pia kupata hasara za mara kwa mara jamaa yangu kwa sababu alikuwa mwenyeji alikuwa ananipa sana hela hadi mwisho wa siku mtaji ukakata.

Nikaachana nae nikahamia Kigoma mjini kuna hela niliuza kiwanja Dar kama Million tatu hivi nikawekeza kwenye biashara ya vinywaji, nyie Kigoma iskieni tu mtaji ulikata ndani ya muda mfupi sana.



Umasiki ukaanza kuninyeemelea nilipigwa sana Uchumi Mkuu, ulinipiga kweli kweli nikawa mlevi tu nashinda vijiweni na kupiga dili za fasta hasa za ufundi kwenye IT lakini kipato kilikuwa kidogo sana kutokana na hali ya kigoma hakuna mtu anaweza kukupa hela ya maana sana sana elfu kumi au kumi na tano.



Maisha yakanipa kwlei nikaw amlevi tu sasa wa zile Pombe za Bei rahisi kunaambayo ilikuwa inaitwa Shimwa ndio ilikuwa pombe yangu, nikaacha na kwenda ibadani kabisa hata maombi nikawa sifanyi tena maana niliona kama dunia imeshanielemea.

Watu wangu wa dar ndio nilikuwa nawapiga vizinga na Jeni mara kwa maraa alikuwa ananiwezesha kama nimekwama sana japo nilikuwa naogopa sana maisha yakuomba omba tena hela ndogo ndogo

Ilifika wakati iakwa hata nakaa wiki bila Kuoga yaani wala kubadili nguo mimi ni kunywa tu asubuhi hadi jioni.

Usiombe maisha yakupige utakumbuka kila kitu, niliahidi kupambana kwa kila nguvu lakini niliamua kurudi Dar mwaka huu mwezi wa kwanza

Nilitafuta akzi sana hata huku JF niliomba mchongo sana ila watu wana ku PM unampa na namba unajieleza wee kisha anakupotezea.

Mtu anaandika tangazo la kazi ukimcheki anakumbia nakurudia, ilikuwa inaniumiza san asana.

Wakati huo nikiwa dar natafuta Kazi na wakati huo huo nilikuwa nishanza kurudisha majeshi pia kwa Judy kwa ajili ya kuomba tuyamalize ili Turudiane maana sasa hata hela ya kula ilikuwa ishanza kunipa chenga.

Marafiki wengi ukwa na shida ndio utawajua, jamaa zangu nilikuwa nimeshawapiga vizinga hadi nikaogopa.

Tumaini lilikuwa limebaki kwa Judy tu na niliona nitafute suluhu kwanza bila hivyo naweza kukata moto.

Wakati natafuta suluhu na Judy pia nilikuwa natafuta kazi kwa udi na uvumba.

NITARUDI SAA TISA KUMALIZIA WAKUU, NIMEJITAHIDI KUANDIKA KWA KIFUPI ILI NISIWACHOSHE MAANA NILIJARIBU SANA KUSIMULIA KWA MTIRIKO MZURI NIKASHINDWA
 
Back
Top Bottom